Samahani mkuu, nilijua nitakukwaza maana kuna watu walijaribu kunitahadhalisha kabla, lakini hayo yalikuwa ni mawazo yangu na nimemnukuu Nyerere maana aliyasema pia kwenye kile kitabu chake cha Hatima ya uongozi.
Na najua Malecela amechaguliwa na watu.
- Unasema kwamba u-DC Tukuyu alichaguliwa na wananchi? Alipoteuliwa kwenda kubwa balozi UN alichaguliwa na wananchi? Unasema alipoteuliwa kuwa waziri EAC alichaguliwa na wananchi? Au alipoteuliwa kuwa waziri wa nje alichaguliwa na wananchi?
- Sasa weka facts, alichaguliwa na wananchi gani, wa jimbo gani au taifa lipi hilo?
- Samahani sana kwa kukukwaza.
Respect.
FMEs!
Na unajua c wote waliochaguliwa walichaguliwa kwa sababu kweli walikuwa ni watumishi wazuri, hapana. Kuna sababu nyingi tu zinazoweza kumfanya mtu achaguliwe hata kama hafai.
Ndio sababu sioni ajabu EL kuwekewa zuria wakati ana tuhuma kubwa za rushwa. Na sintaona ajabu kama wamasai watamchagua tena kuwa mwakilishi wao.
Na sioni ajabu Chenge akipokelewa kama mfalme wa wasukuma wakati wote tunajua nini alichofanya. Na sintaona ajabu kama atarudishwa bungeni na chama chake.
Na sioni ajabu hata rais akichagua fisadi Makamba na kumpa ukatibu mkuu wa chama chenu pamoja na tuhuma za ufisadi alizo nazo.
Nasema sintaona ajabu.
Samahani sana kaka kama nimekukwaza ila hapa nilitoa maoni yangu tu hata kama yanachoma moyo. Tuvumiliane tu.
Cigwiyemisi John Samwel Malecela ni mtu mmoja atakayekumbukwa katika historia ya Tanzania kama kada wa CCM na Waziri Mkuu wa JMT aliyepigana kufa na kupona kuzuia upepo wa mageuzi mwaka 1991. Cigwiyemisi John Samwel Malecela alifikia hatua ya kuwafananisha wanamageuzi na sisimizi wa kusiginwa tu na kufilia mbali.
Kama si kwa Mwalimu kuingilia kati na kusema kuongelea mageuzi si dhambi, hakuna mwana CCM hata mmoja - si kiongozi wala mwananchama (mwenye kadi), aliyebariki mfumo wa vyama vingi. CCM ilijikuta inalazimika kusalimu amri na kukubali mageuzi kutokana na nguvu zilizokuwa nje ya uwezo wake japo kwa shingo upande.
Sera ya ufisadi ndani ya CCM ilianza pale ilipokataa kuridhia kuandikwa kwa katiba mpya iliyoendana na hayo mabadiliko makubwa. Hiyo iliwapa nafasi ya upendeleo maalum katika hatua zote za mwanzo tangu katika usimamizi na uandikishwaji wa vyama vipya. CCM imeendeleza hivyo hivyo ubabe wa kuwa mchezaji na mwamuzi vyote kwa pamoja.
Kote huko Cigwiyemisi John Samwel Malecela alikuwa kamanda muhimu.
- Wakahatamia katiba na kuifanya ajenda yao binafsi - ufisadi namba moja.
- Wakatwaa mali zote zilizochangiwa kwa pamoja -- ufisadi namba mbili.
- Wakafunga milango ya kudai haki na usawa- ufisadi namba tatu.
- Wakateua kada wao kuongoza tume ya uchaguzi - ufisadi namba nne.
- Wakabuni hila chafu chafu za kubaki madarakani - ufisadi namba tano
Na sasa Cigwiyemisi John Samwel Malecela, mzee aliyetakiwa kung'atuka na kuwaachia wajukuu wake ulingo wa siasa anasema mbinu mpya ziko jikoni zinapikwa ! Anayejaribu kutenganisha CCM na hii kasi ya ufisadi tunayoshuhudia sasa hivi ni heri akanunue miwani. Mwana CCM anayedai yeye si fisadi na kuwaelekezea vidole makada wenzake ndani ya CCM ni limbukeni wa kutupwa - and that's a memo !!
huyu mzee bwana!............amesahau kwamba alishataka kuwa USTAADHI kwa tamaa za pesa!
Bwahahahahahahahahahahahahahahah!!!!!!!!huyu mzee bwana!............amesahau kwamba alishataka kuwa USTAADHI kwa tamaa za pesa!
- Sasa nielemishe jinsi kiongozi anayefaa kama Kambarage kuishia kuchagua viongozi wasiofaa, huku akijua hawafai ili walifanyie nini taifa? Kwa hiyo unasema Mwalimu alikuwa akichagua viongozi wasiofaa makusudi just because ana sababu! labda uiseme ni sababu ipi hiyo?
- Eti hizi ni logic au facts? Huwezi kunikwaza bila ya kuwa na facts ya unachokisema, infact unajikwaza mwenyewe so far, au?
Respect.
FMEs!
- Unasema kwamba u-DC Tukuyu alichaguliwa na wananchi? Alipoteuliwa kwenda kubwa balozi UN alichaguliwa na wananchi? Unasema alipoteuliwa kuwa waziri EAC alichaguliwa na wananchi? Au alipoteuliwa kuwa waziri wa nje alichaguliwa na wananchi?
- Sasa weka facts, alichaguliwa na wananchi gani, wa jimbo gani au taifa lipi hilo?
- Samahani sana kwa kukukwaza.
Respect.
- Unasema kwamba u-DC Tukuyu alichaguliwa na wananchi? Alipoteuliwa kwenda kubwa balozi UN alichaguliwa na wananchi? Unasema alipoteuliwa kuwa waziri EAC alichaguliwa na wananchi? Au alipoteuliwa kuwa waziri wa nje alichaguliwa na wananchi?
- Sasa weka facts, alichaguliwa na wananchi gani, wa jimbo gani au taifa lipi hilo?
- Samahani sana kwa kukukwaza.
Respect.
- Kwa nini hakuiba kura za Tarime? Au Kigoma kwa Zitto? Acha kurukia treni mkuu na habari za kusimuliwa na alinacha, tafuta facts mwenyewe kabla ya kukurupuka na lugha za hovyo hovyo ambazo haziwezi kutusaidia taifa mkuu Bwa! ha! ha! tizama unavyojikanyaga kanyaga Ha! ha! ha! Inawezekana haya ya uzee una experience nayo, labda ungetoa definiton kwanza on uzee, maana kama wewe kijana unashindana na Mzee Malecela kila kukicha anakushinda kwenye uchaguzi, then something is wrong na hii theory yako ya uzee, kwani Makamba sio mzee mbona hakushinda Tarime? Kwa nini wazee Makamba na Msekwa hawakuiba kura Tarime?
Mkuu FMES watu hubadilika kutoka wakati mmoja hadi mwingine. Mzee alivyokuwa yaani zile colours alizokuwa nazo at that time Nyerere anamchagua kuwa kiongozi huko kote ulikosema si hizi alizokuwa nazo baada ya Mwalimu.
Huyu huyu alikuwa wa kwanza pamoja na kundi lake kulizika azimio la Arusha.
- Unajua hapa sasa ndipo unafurahisha sana mkuu, umesema Mwalimu alimchagua pamoja na kwamba alijua kuwa sio kiongozi safi, sasa umebadili kwamba alikuwa safi lakini alibadilika, sasa chagua mwenyewe unataka kusimamia hoja ipi kati ya hizo mbili zinazopingana ulizozitoa mwenyewe! Bwa! ha! ha!
- Azimio la Arusha lilizkwa na rais wa jamhuri na mwenyekiti wa CCM, then Mwinyi, lilipozikwa Mwalimu alikuwepo hawakumzunguka walifanya wazi kwenye kikao cha CCM Zanzibar, sio Malecela aliyevunja rekebisha hilo.
Na ni kwa huyu huyu Nyerere alijuta kumuweka kwenye system yake hadi kamtungia kitabu. Ina maana kama Nyerere angepewa nafasi ya kutawala tena nakwambia hata anayozungumza leo asingeweza kusema neno.
- Sawa sawa, sasa simamia tena hoja yako, wakati Mwalimu anampa Mkapa urais na uenyekiti wa CCM, kwa nini alimruhusu Malecela kuwa makamu wake huku tayari akiwa ameandika kitabu chake? Bwa! ha! ha! unaona mambo ya kurukia treni kwa mbele sasa Bwa! ha!
Na unaweza kuona kweli kwamba huyu sasa anaonyesha true colours kwa uoza anaosema leo bila hata haya.
Hivi wizi wa kura na mbinu zingine chafu ni vitu vya kujivunia kwa mtu kama mzee huyu? Au labda tuseme uzee unamfanya mtu apunguze uwezo wa kufikiri kabla ya kusema?
Respect mkuu
Mzee pamoja kwamba huyu mzee ni baba yako , lakini kwa maneni yake haya nadhani anastahili kulaaniwa .Bura nzuri ni kama nyie mtamshauri akae pembeni sasa amesha choka na wenzake kama akina Kingunge wana haribu.Yes Tarime hawakuweza kwa kuwa wanaume walisimama kule .Kote kote alikosimamia aliendesha zoezi wa wizi wa kura si kuiba ma box bali kupora ushindi kwa kusema sisi ni Serikali Tangaza tumeshinda na ikawa hivyo .
Mzee pamoja kwamba huyu mzee ni baba yako , lakini kwa maneni yake haya nadhani anastahili kulaaniwa .Bura nzuri ni kama nyie mtamshauri akae pembeni sasa amesha choka na wenzake kama akina Kingunge wana haribu.Yes Tarime hawakuweza kwa kuwa wanaume walisimama kule .Kote kote alikosimamia aliendesha zoezi wa wizi wa kura si kuiba ma box bali kupora ushindi kwa kusema sisi ni Serikali Tangaza tumeshinda na ikawa hivyo .
Kwa hakika ni mwelekeo mzuri, lakini inafaa wengi wapate ujasiri na kuanza kuzungumza na wazungumze kwenye vile vikao rasmi, ni wakati wa kuachana na zidumu fikra...
"Hawa wanaokitabiria chama mabaya kwenye chaguzi zijazo ni wajumbe wa NEC, wao wana nafasi ya kuingia kwenye vikao na kuyazungumza haya. Inakuwaje leo wazungumzie uchochoroni,"alihoji na kusisitiza: "Sisi vijana wa CCM tunao wajibu wa kukipinga kitendo hiki kwa nguvu zoeti."
Alisema kama suala hilo litaachwa liendelee, watakaoteseka ni vijana ambao wana muda mrefu wa kuendelea kukitumikia chama hicho.
"Ndugu zangu hili ni jambo la kusikitisha sana kuona watu wenye nafasi ndani ya vikao vya halimashauri kuu wakilizungumzia suala hilo uchochoroni kama tutaacha liendelea sisi ndio tutakaotaabika,"alisema Bashe.
yeah naona JIPU LIMEKARIBIA KUIVA!litapasuka sasa hiviHakika sasa wanaanza kuumbuana hadharani sisi yetu macho.
Huwezi mtu ukajitokeza tu na kusema CCM itashindwa, kwa tathmini gani uliyofanya? 'no reserch no right to speak (usizungumze bila utafiti)' nalazimika kuyasema haya kutokana na kauli za baadhi ya wana CCM ambazo zinatia shaka.
Haiwezekani chama kikazungumziwa nje ya chama, hii inaonesha maadili yamekwisha na ukizungumzia huko juu kwa juu inatuonesha kuwa huna mapenzi mema na chama chako na unatia mashaka makubwa.
CCM hatuna shaka na ushindi mwakani, hata bila wao CCM itashinda kwa kuwa haijawa mbaya kiasi hicho na bado inaaminika kwa wananchi wake hivyo tabia za kupaka matope kwa nia ya kupotosha iachwe mara moja.
Kutokana na haya ya upotoshaji unaofanywa nakumbuka kauli ya Mzee wetu Kawawa ( Mzee Rashid Kawawa) ambaye alisema mkiona mmoja wenu ndani ya boti mnayosafiria anatoboa, mtoseni afe peke yake ili ninyi msizame '...hivyo hatuko tayari kubaki na watu hao ndani ya chama
Ufisadi anaozungumzia Malecela kwamba utakisambaratisha chama hicho mwakani ni wa kufikirika kwa sababu mpaka sasa hakuna mwenye ushahidi unaodhihirisha kwamba fulani ni fisadi.
Mimi siwajui hawa mafisadi. Hebu wewe nitajie jina la mtu mmoja ambaye una ushahidi kuwa ni fisadi, siyo kweli ila ni jambo ambalo linakuzwa tu.
Hawa wanaoitwa mafisadi wako wangapi? Mbona hawatajwi? Kuna watu ndani ya chama wamedhamiria kuiangusha CCM huku wakijifanya wanapambana na mafisadi ndani ya chama.
Suala hilo linapozungumzwa hadharani na wanachama wa CCM ni hatari. Hapa wanakichafua chama na ndio wanaosaidia vyama (vya siasa) vya upinzani.
Kama kuna tatizo, lipelekwe kwenye vikao na siyo kwenda kupiga kelele kwenye majukwaa na kukichafua chama machoni pa wananchi.
Namna suala hilo linavyozungumzwa sasa, inaonyesha kana kwamba kuna kundi kubwa la wanaCCM wanaojihusisha na ufisadi, lakini ukweli ni kwamba watuhumiwa wa ufisadi, hawazidi wanne !
Huo ni woga tu. Hakuna kitu kama hicho. Naunga mkono maelezo yaliyotolewa na Katibu wangu Mkuu (Yusuf Makamba) kupitia gezeti lenu (Mwananchi) toleo la leo jana akisema hayo ni mambo ya kufikirika.