Malawi yakamata yakamata tena watanzania wawili kwa tuhuma kupeleleza

jerrytz

JF-Expert Member
Oct 10, 2012
5,960
4,209
Maafisa wawili wa serikali ya tanzania inaarifiwa kuwa walifika Malawi wiki iliyopita ili kupewa taarifa juu ya Watanzania wanane wanaoshikiriwa na serikali ya Malawi.
Watanzania hao walikamatwa katika mgodi wa madini ya Uranium wa Kayekera eneo la Karonga.

Afisa katika mpaka wa Songwe ndugu Yusufu Shaibu alisema kuwa maafisa hao wa Tanzania ambao ni Daniel Magwaza na John Njirakiza walifanya mahojiano na wana usalama wa serikali ya Malawi kutoka Karonga mpakani hapo.

" Walitaka kufahamu juu ya watu waliokamatwa na makosa yao kutokana na taarifa kwamba watu hao walikuwa wakifanya upelelezi katika eneo la Kayelekera na kwamba inadaiwa walitaka kujua kama Malawi inataka kufanya masuala ya Kinyuklia.." alisema Shaibu.

Watanzania hao wanane bado wapo katika gereza la Mzuzu nchini Malawi na watafikishwa mahakamani kujibu mashtaka.
Taarifa zinasema kuwa Watanzania hao nane walikutwa na kamera.

Source: The Guardian 05 January 2017
 
Idd Amin alianza hivi hivi kuamsha hasira za Mwalimu, mwisho wa siku kilizochomkuta ni kukimbia nchi yake
 
Jamanii nchi hizi masikini hatutaki choko choko wala vita!! Sisi majirani na ndugu tuishi kama ndugu na amani!!! Malawi nchi ndogo sana haiwezi kushindana na Tanzania!! Wataishia kuwa masikini mara 100 zaidi
 
Hivi yule bingwa wa mikwara bado hajatoa kauli yake ,au mikwara haivuki mipaka ?
 
Mtoa mada mada na hilo Gazeti kuna jambo mnalitafuta.....Story nyepesi ukilinganisha na issue ya Kujenga Kinu cha Nyuklia.!!!
 
Makonda aandaliwe, mkoa wa Malawi utamfaa. Waache watujaribu.
 
Magufuli asiliongelee swala la Malawi
ataharibu!
Naunga mkono swala la Malawi magufuli aongee na kikwete mwinyi na mkuu wa majeshi mwamunyange na aliyekuwa mkurugenzi wa usalama wa taifa othman kuhusu hilo swala hao ni maguru kwenye hilo
 
Malawi bwana wanajitekenya wenyewe kulima/kununua mahindi wameshindwa ka nchi kananuka njaa halafu eti kinu cha nyuklia fyuuu labda kinu cha mkono cha kutwanga vitunguu swaumu ba sio kurutubisha nuclear wasahau hatuwezi kuwachunguza kwa kitu amvacho tunajua hawana.
 
Malawi bwana wanajitekenya wenyewe kulima/kununua mahindi wameshindwa ka nchi kananuka njaa halafu eti kinu cha nyuklia fyuuu labda kinu cha mkono cha kutwanga vitunguu swaumu ba sio kurutubisha nuclear wasahau hatuwezi kuwachunguza kwa kitu ambacho tunajua hawana.
 
yani naona wazi wazi kabisa kwamba nyuma ya malawi kuna mtu.. nina hakika kuna mtu nyuma ya hizi choko choko, hivi malawai anaanzia wapi kuivimbia tanzania? wazungu washawalisha sumu ndugu zetu tugombane nao
 
Back
Top Bottom