Malawi tuonesheni mfano

GAGL

JF-Expert Member
Aug 5, 2010
390
391
Gazeti la jana la Mwananchi la jana, liliripoti kuwa wiki ijayo kutakuwa na maandamano makubwa kukamilisha mpango wa kumuondoa Rais Mutharika madarakani kwa nguvu ya umma. Nafurahia hatua hii kwa kuwa naamini itatuambukiza na sisi pia kuchukua hatua kwa viongozi ambao kiukweli hakuna wanachofanya kutuondolea hali ngumu ya maisha. Hali ya serikali yetu na mwenendo wake, imetufanya wengine tuathirike kisaikolojia kwa kweli.
 
Baada ya Mutharika anafuata Kikwete amini usiamini nitatoa sababu baadae.
 
tatizo lenu mnafikir kila mapinduzi ni faida..wengine wamenunuliwa na vibaraka..
Waambie hao vibaraka waje Tanzania watununue na sisi naona wanafaida kama waliwanunua wahuni wa Misri na Libya na Tunisia na Malawi kwanini isiwe Tanzania kwani sisi ni exceptional.
 
Waambie hao vibaraka waje Tanzania watununue na sisi naona wanafaida kama waliwanunua wahuni wa Misri na Libya na Tunisia na Malawi kwanini isiwe Tanzania kwani sisi ni exceptional.

well said mkuu
 
Waambie hao vibaraka waje Tanzania watununue na sisi naona wanafaida kama waliwanunua wahuni wa Misri na Libya na Tunisia na Malawi kwanini isiwe Tanzania kwani sisi ni exceptional.

Wameanza kuwanunua chademu..lakini nchi yetu tunajua namna ya kuwadhibiti kabla hamjaleta athari kubwa.
 
Waambie hao vibaraka waje Tanzania watununue na sisi naona wanafaida kama waliwanunua wahuni wa Misri na Libya na Tunisia na Malawi kwanini isiwe Tanzania kwani sisi ni exceptional.
<br />
<br />
kama Wahuni wanafanya mapinduzi tunawakaribisha waje na kwetu watununue.
 
Gazeti la jana la Mwananchi la jana, liliripoti kuwa wiki ijayo kutakuwa na maandamano makubwa kukamilisha mpango wa kumuondoa Rais Mutharika madarakani kwa nguvu ya umma. Nafurahia hatua hii kwa kuwa naamini itatuambukiza na sisi pia kuchukua hatua kwa viongozi ambao kiukweli hakuna wanachofanya kutuondolea hali ngumu ya maisha. Hali ya serikali yetu na mwenendo wake, imetufanya wengine tuathirike kisaikolojia kwa kweli.

Chama ambacho hakiwezi kushindana kwenye uchaguzi na badala yake kinaota kupata madaraka kwa njia za mkato na haramu ni chama cha kigaidi, chama cha kihaini na hakina sifa ya kuendelea kuwepo kwenye ushindani wa kisiasa!
 
tatizo lenu mnafikir kila mapinduzi ni faida..wengine wamenunuliwa na vibaraka..
<br />
<br />
malawi inatulisha watanzania sukari,karanga,mbao,ngozi,chai,pamba hivyo wao wana hali bora kuliko tanzania,directly watanzania ilitakiwa tuchukue hatua kabla ya wamalawi!miaka 50 ya uhuru ni bora ya utawala wa mkoloni mjerumani hapa tanganyika
 
Chama ambacho hakiwezi kushindana kwenye uchaguzi na badala yake kinaota kupata madaraka kwa njia za mkato na haramu ni chama cha kigaidi, chama cha kihaini na hakina sifa ya kuendelea kuwepo kwenye ushindani wa kisiasa!
<br />
<br />


Nani amekwambia nguvu ya umma ni chama? Usiwasingizie chadema hayo yatakuwa maamuzi ya wananchi wenyewe!
 
Northen sahara:TUNISIA-MISIRI-LIBYA............ Southen sahara;MALAWI-TANZANIA-UGANDA........................mapinduzi lazima.
 
mwenzako akinyolewa....wewe tia maji. Historia inaonyesha uhuru wa bara la afrika nao ulianza taratibu.
 
Back
Top Bottom