Malawi: Tunapinga Tanzania kupeleka Meli Ziwa Nyasa (Malawi).

Nchi ya Malawi imepinga na kulalamika kuhusiana na kusudio la Tanzania kupeleka meli mbili za abiria katika ziwa Nyasa na kudai, kitendo cha kufanya hivyo kitaadhiri na kutishia mazungumuzo yanayotafuta suruhisho la muda mrefu ili kulimaliza mzozo wa ziwa Nyasa (malawi) uliodumu kwa muda mrefu. Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Efraimu Chiume alikaririwa jumamosi akisema, kwamba viongozi wa juu wa serikali ya Tanzania walisikika hadharani wakisema kwamba serikali ina mpango wa kununua meli sita na mbili zitapelekwa ziwa Malawi kusaidia kuondoa tatizo la usafiri. Waziri Chiume alidai mpango wa kupeleka meli ziwa Nyasa (malawi) umekuja katika hali ambayo siyo mwafaka ikichukuliwa kuwa mazungumzo yalikuwa yanaendelea bila matatizo. . . . . Mwaka jana serikali ya Malawi iliiruhusu kampuni ya Kiingereza inayoitwa Surestream Petroleum kuanza kutafuta mafuta. Habari kwa hisani ya Reuters.
Heshima yako mkuu, sina shaka unajua makao makuu ya REUTERS yako wapi na ni Kampuni ya akina nani; hilo tu ndilo litakupa picha kamili ni kitu gani kinaendelea behind the SCENE. Hivi hii kampuni ya Kiingereza (Surestream Petroleum) bado inaendelea na utafiti wake wa mafuta katika Ziwa Nyasa au walitii AMRI ya Serikali ya TANZANIA?
 
[B]Hili swala linahitaji zaidi ya uwezo wa kidiplomasia kulimaliza kwa amani pamoja na kwamba nasikia kuna kelele za watu hapa wanataka tuende vitani bila kujua kama hatutapigana na Malawi bali na wadau wa malighafi za Malawi.[/QUOTE][/B]

What do you mean by "zaidi ya uwezo wa kidiplomasia?" Maana diplomasia inaposhindwa kutatua tatizo, usuluhishi unachofuata ni kwa shuruti. Kilichopo hapa ni agenda ya chini ya Wamalawi wakishirikiana na hao wazungu. Sasa nani wa kulinda maslahi ya Watanzania?
 
Heshima yako mkuu, sina shaka unajua makao makuu ya REUTERS yako wapi na ni Kampuni ya akina nani; hilo tu ndilo litakupa picha kamili ni kitu gani kinaendelea behind the SCENE. Hivi hii kampuni ya Kiingereza (Surestream Petroleum) bado inaendelea na utafiti wake wa mafuta katika Ziwa Nyasa au walitii AMRI ya Serikali ya TANZANIA?
Heshima kwako pia mkuu.

Hawa watu wa Reading UK (Surestream Petroleum) walisimamisha kwanza shughuli zao katika eneo lenye dispute mpaka hapo kitakapoeleweka.

Mpaka hapo viongozi wetu watakapo jifunza jinsi ya kufanya kazi na Wazungu, hasa Waingereza ndipo nchi zetu zitakapo ondokana na hii migogoro ya ndani na nje kila mara ambayo mara nyingi niya kupikwa na Wazungu (Waingereza).

Let's wait and see huyu Mama Banda anataka nini kwa kupitia hawa wazungu?.
 
mama joyce banda kuna kitu unataka tu .. acha tumalizane na M23 ... alafu tutakugeukia weye .. kama unataka iwe hivyo itakuwa tu.... tulirudisha order uganda , comoro .. hako kaziwa ndani ya siku 5 linakuwa letu lote hata nusu hutopata ...

mama subiri mazungumzo acha mdomo ...
 
Back
Top Bottom