Malawi, Tanzania fail to agree on Lake Nyasa border dispute

Nchini Malawi wanaijua Kiswahili wanafuatilia JF na hat a wenzao walioko hapa Tz engine wakiwa kama Walinzi na watumishi WA nyumbani wamekua bize kuwasiliana NA wenzao nyumbani kwao. sisi tuko bize kulumbana. Ndipo ninapomkumbuka Mwalimu Nyerere.
 
ngoja tuone hiyo september meeting, ila sioni kama kutakuwa na jipya sababu malawi wameshatuweka mtegoni kwa kusema wanasheria wakuu wa serikali wakutane kuupitia mkataba wa 1890, kwa nini wapitie mkataba huo pekee ili hali kila mtu anajua hauipi favour tz kisheria?

Heshima yako mkuu. Ninachokiona hapa ni kuwa Malawi wanatafuta faida fulani kutoka kwa Tanzania, labda mfano kama vile walifanya na Msumbiji walipogawa ziwa kwa Msumbiji wakapewa ardhi na kuachiwa visiwa viwili ambavyo vipo ndani karibu kabisa na ufukwe wa Msumbiji.

Labda Mama Banda anataka reli, access to Mtwara port inajojengwa au concession nyingine kwa kuwa kila mtu anajua na anakubali kuwa kwa kawaida maji yanayopatikana baina ya nchi mbili lazima mpaka uwe kwenye maji. Ufukwe una hali ya kubadilika kwa msimu kwa hivyo mpaka pia utakuwa unabadilika. Pili, ingawa Mjerumani alimkabidhi Mwingereza ziwa lote kupitia makubaliano yao juu ya kisiwa cha Heligoland, wasomi wengi na publications zinazohusu mgogoro wa Ziwa Nyasa conclusion ni kuwa Malawi lazima wakubali kugawa maji yale.

Ukiangalia statement aliyotoa mleta hoja, Membe amenukuliwa kusema solution ni 'negotiated settlement'. Ina maana kuna mambo ya 'mahari' kabla binti Nyasa hajaolewa rasmi na TZ. Tusubiri tuone wanapewa offer gani. Labda free movement of labour ya 'domestic technicians' aka housegirls/shamba boy Masaki na maeneo mengine ...
 
huwezi kuwa fair kwenye hili maana umeshatamka wazi kwamba hawahatuvunjia haki NA Ndege zao kutua Mbambabay walikua NA haki na wanapaswa kwenda kutundika NA Bendera yao kule. Hongera sana Mkuu

Kuna mtu humu kaja na hoja ya kusema waandishi makajanja ndiyo wame-mislead jambo hili. Pamoja na kwaba sikubaliani sana na aliyesema hivyo lakini unavyokuja humu ni kama unaanza jambo jipya wakati tumetuma posts zaidi ya 600 ndai ya wiki mbili kwa hili.

Sasa ona, unakurupuka na suala la ndege kutua Mbamba_Bay ambalo ni la January mwaka huu wakati controversy hii ni ya zaidi ya miaka 50 sasa.


Hebu pitia thread zote ndiyo uje tujiunge behewa moja maana tunashindwa tukujibu nini. Soma walau thread hii: {Click Here}
 
ntasema kidogo juu ya hili

...ni kwamba tanzania inamiliki ziwa hilo kwa asilimia 50 na malawi asilimia 50.. ndipo malawi wakahoji kama tunamiliki ziwa hili kwa 50/50 je msumbiji inamiliki ziwa kwa asilimia ngapi maana sehemu ya ziwa hilo iko pia msumbiji.watanzania walishindwa kujibu. na hili swali liliuzwa pia na chiume waziri wa mambo wa nje wa malawi alipokutana na membe pale serena hoteli mwezi uliopita na membe hakulijibu swali hilo.

kwa kifupi ni kwamba wawakilishi hawakuwa uwezo wa kujenga hoja , maandalizi yalikuwa duni, taarifa a membe bungeni ilileta mkanganyiko mkubwa sana..

Sio sahihi, maana hata wa-Malawi nao wanasema kuwa wanamiliki ziwa hilo hilo kwa asilimia 100. Unadhani hawajui kuwa Msumbiji nayo ipo?. Hii lugha ya 50/50% au 100% inakwendana na context ya mazungumzo yenyewe: (i.e., ukiondoa lile eneo linalomililiwa na Mozambique, then kwa eneo lililobaki wa-Malawi wanasema ni lao lote na sisi tunasema ni nusu kwa nusu...). nadhani somo limeeleweka....:hat:
 
..naona Malawi wanatumia kila opportunity kueleza kwamba wanamiliki 100% ya ziwa nyasa.

..kwa upande mwingine Membe haelezi anacho-negotiate haswa ni kitu gani.

..Membe ameshindwa kueleza haki ya Tanzania ktk ziwa hilo ni ipi. je, ni 50%, 30%, au???!!

Unaonesha hauna umakini wa kusoma na kuelewa, hilo ni tatizo kubwa sana kwa wengi wenye fikra hasi kila wakati.

Soma hiki kipande pekee labda utaacha kutupa madongo yasiyo na muelekeo:

quote_icon.png
By n00b

Nilikuwa Malawi na naomba nitoe maoni yangu hivi:

Kwanza hapa naona watu wanamshambulia Membe wakati timu ilikuwa ni Tibaijuka na timu yake!
 
Nimejaribu ku-attach ule mkataba wa Heligoland Zanzibar ili tuone kama kuna hoja ya msingi kuendelea na majadiliano hayo ya Membe na Chiume. Issue ya mgogoro huu ipo katika article I (2) inaelezea mpaka utakavyokuwa ambapo hakuna shaka sisi kama Watanzania hatuna chetu kwa mujibu wa mkataba huu. Hata hivyo zipo loopholes ambazo tunaweza kuzitumia ili kuu-defeat mkataba huu kwa mfano sehemu ya mwanzo ina maneno haya:

'This treaty temporarily settled colonial disputes between Germany and Great Britain. It recognized Tanganyika as a German colony; in return, the Germans abstained from further encroaching into British Kenya. The agreement ceded Heligoland, an island off the coast of Schleswig-Holstein in the North Sea, to Germany. Because the treaty appeared to abandon German colonial claims to much of east Africa, it unleashed a storm of nationalist protest at home.'

Hapo kwenye nyekundu inaonekana kama ifuatavyo:
(1) Mkataba huu uliondoa migogoro ya kimipaka kati ya Uingereza na Ujerumani kwa muda (temporarily),
(2) Wajerumani walikuwa wakiendelea kuchukua maeneo kutoka koloni la Uingereza liitwalo Kenya; hivyo kwa mujibu wa mkataba huu waliacha kufanya hivyo.

Ni wazi kuwa hapakuwa na mgogoro wowote katika mpaka wa ziwa Nyasa, inawezekana Wajerumani walikuwa wamechukua eneo kubwa kutoka Kenya hatimaye walikubali mpaka wa kusini yaani huko Ziwa Nyasa upite kando kando ya ziwa, hata hivyo mkataba huu ulikuwa ni wa muda tu. Kwa kuunganisha na kijiramani cha German Osta Africa kilichoambatishwa hapa pamoja na ramani za Mwingereza zinazoonesha mpaka ukiwa ndani ya ziwa tunaweza ku-raise doubts kwa mahakama za kimataifa na hatimaye kutupiliwa mbali kwa madai ya Malawi kupitia Heligoland Zanzibar Treaty.

Lengo letu kuu sasa hivi ni kuufanya mkataba wa Heligoland Zanzibar usiwe na nguvu kwa wakati uliopo (kwa sababu huu makataba ndiyo kiini cha madai ya Malawi), tusipopata hoja za kupambana na huo mkataba hilo ziwa litakuwa limeondoka rasmi katika vitabu, ramani, nyaraka zote za Tanzania endapo Malawi watakwenda katika mahakama za kimataifa.

Mimi sio mtalaam wa sheria lakini ninachofahamu mshitakiwa hahitaji kuthibitisha mahakamani kuwa hakutenda kosa bali anatakiwa kuonesha mashaka mbele ya mahakama (to raise doubts) katika ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka ili upande huo wa mashitaka ushindwe kuthibitisha bila kuacha shaka kuwa mshitakiwa alitenda kosa.

AG na timu yako pamoja na wanasheria wote wa nchi hii bila kujali itikadi za kisiasa, unganisheni nguvu tuikomboe nchi yetu pasi na kumwaga damu.

Inawezekana kabisa kukubaliana juu ya mipaka ya Ziwa na wala haitokuwa ni mara ya kwanza. Waingereza hata baada ya treaty hii umeweka hapo juu, walisogeza mpaka hadi kuwa katikati ya Ziwa. Kipindi hiki walikuwa wamepewa trust territory ya Tanganyika. Walitarajia watapata Tanganyika kama colony. Waliponyimwa haki hiyo wakarudisha mpaka ufukweni. Pia kabla ya vita ya kwanza walikubaliana na Wajerumani wale wale kugawa ziwa katikati ila Waingereza wamefuta makubaliano hayo baada ya vita ya pili ya dunia kwa hofu kuwa Wajerumani watajihami na kurudi Africa Mashariki.
Msumbiji imefanya 'negotiated settlement' na kuwapa wamalawi ardhi ili wapate pia eneo la ziwa. Kwa kuwa TZ haina ardhi ya kuuza hivyo labda ni political/ economic concession watafanya ila makubaliano ni lazima.
Ikienda International Court itakuwa hasara kwa Tz kama ulivyosema awali.
 
Kuna mtu humu kaja na hoja ya kusema waandishi makajanja ndiyo wame-mislead jambo hili. Pamoja na kwaba sikubaliani sana na aliyesema hivyo lakini unavyokuja humu ni kama unaanza jambo jipya wakati tumetuma posts zaidi ya 600 ndai ya wiki mbili kwa hili.

Sasa ona, unakurupuka na suala la ndege kutua Mbamba_Bay ambalo ni la January mwaka huu wakati controversy hii ni ya zaidi ya miaka 50 sasa.


Hebu pitia thread zote ndiyo uje tujiunge behewa moja maana tunashindwa tukujibu nini. Soma walau thread hii: {Click Here}

hongera sana. NA sasa manadiliano yamelipuka kwa sababu ya kilichotokea hivi sasa NA ukisoma kauli ya Membe wamezungumzia utafiti WA sasa sio 50yrs back. we we unataka tufumbe macho kutua kwa Ndege wakati Jana suala hill limejadiliwa Lilongwe! hongera sana NA jitahidi utafanikiwa
 
Mpaka baina ya Tanzania na mawawi upo katikati, haina maana tuna share ziwa Malawi nusu kwa nusu maana sehemu ya kusini Malawi ina share ziwa hilo la Msumbiji. Makubaliano ua mda baina ya Ujarumani na Uingereza hauwezi kupoteza Uzalendo wenu kwa nchi yetu na haki yenu kwa kuhofia vita wakati haijawahi kutokea treaty baina ya tanzania na Malawi.

Kuna ujinga unatumiwa hapa kusema mbona hatukudai toka zamani wakishindw akuelewa kwamba Afrika ilitawaliwa zaidi ya miaka 500 kabla hatujadai Uhuru wetu. Sasa unaweza kweli kusema hatukuwa na haki ya kudai Uhuru kwa sababu tulitawaliwa miaka 500 pasipo kudai Uhuru?.

Harakati zinaanza leo baada ya kutokea umuhimu wa kuondokana na adha hii maana hata sisi wenyewe hapa hatukujua how serious Malawi wamelichukua swala hili wakitumia Heligoland treaty. Na wala sii sisi pekee, nchi nyingi duniani zina dispute ktk maeneo ya mipaka yake ambazo hadi kesho wanafanya mazungumzo ama wamefikia kupigana vita...
 
Unaonesha hauna umakini wa kusoma na kuelewa, hilo ni tatizo kubwa sana kwa wengi wenye fikra hasi kila wakati.

Soma hiki kipande pekee labda utaacha kutupa madongo yasiyo na muelekeo:

Zomba,

..ninachojaribu kusema ni kwamba wenzetu wa Malawi wako very clear kuhusu msimamo wao, na zaidi waziri wao wa mambo ya nje anawa-update mara kwa mara wananchi wake kuhusu nini kinachoendelea.

..kwa upande wa Tanzania wananchi hatupewi habari za kutosha. badala yake tunaishia ku-speculate tu, na kuchakura-chakura kila mahali ili mradi tujue nini kinaendelea.

..kuna wana JF wametafuta habari toka facebook, wengine wanadai walikuwepo Malawi lakini wanatumia pseudoname hapa JF.

..masuala kama haya yanapaswa kuzungumziwa na waziri wetu wa mambo ya nje, au msemaji wake, kupitia vyombo RASMI VYA HABARI.
 
Kuna thread imepotea ghafla kabla sijapata nafasi ya kuisoma ikiwa na heading "JK aenda Malawi"
 
Hatutaki ufisadi wa kuwaibia wenzetu ziwa ambalo mkataba unasema si letu.
Nikupateje,

..kwa mtizamo wako unafikiri wa-Tanzania wa-negotiate kitu gani katika mgogoro huu?

..kwa mtizamo wako ni ushahidi au hoja zipi zinaweza kutupatia ushindi au muafaka wenye manufaa kwa wa-Tanzania??
 
Last edited by a moderator:
.. Bila kujali mkataba wa wakoloni unasemaje, haiingii akilini kuwa mpaka uwe kwenye ukingo wa ziwa upande wa Tanzania! Werevu tunaweza tukakubali iwe hivyo, lakini maji ya ziwa "lao" yakimomonyoa udongo wa Tanzania tunaingia vitani! Yaani, wahakikishe maji yao hayamomonyoi udongo wetu. Kama unaona huu ni kama uchizi,basi hata kudai ziwa lote ni la Malawi ni uchizi!
 
Hofu yangu pia ni jinsi Mheshimiwa mkuu wa nchi yetu alivyolichukulia swala hili kama jambo rahisi la kucheka na kulihusisha na upinzani. Last time nilimsikia mwenyewe akisema kuwa mgogoro huo unavumishwa na wanasiasa wa upinzani upande wa Tanzania akiwaita wauchu wa madaraka ! wale maadui zetu ni kitu kimoja, wako united, nahisi watatudharau sana kwa utengano wetu.
 
Namkubali sana Patrick Rutabanzibwa ni moja ya makatibu wakuu wenye uwezo pote alipopita mawaziri wanapata naye tabu sana hasa wanapoleta siasa kwenye utendaji.Kwa hili la Malawi inawezekana atakuwa aliwajengea msingi mawaziri kabla hawajakutana unless wasingekuwa na cha kuongea
 
Ndugu zangu, nalazimika kurudia ku-post yale aliyowahi kuyazungumza former PM Kawawa ktk Bunge la tanganyika mwaka 1963. Mwana jamvi mwenzetu, Nikupateje, aliwahi ku-post hapa. Bahati mbaya wapo wanaoamini kuwa uzalendo ni kung'ang'ania msimamo hata kama ni msimamo usiyohaki na hivyo wapo walioishia kumtukana na kumkejeli wakidai siyo Mtanzania. Binafsi nilimuunga mkono kwani naamini uzalendo ni pamoja na kuacha ushabiki na ku-argue objectively haswa inapokuja ktk hoja serious kama hii. Naamini uzelendo ni kuhakikisha nchi yangu Tanzania inaendelea kupata heshima yake kimataifa kwasababu inaheshimu international treaties. Naamini kuwa uzalendo ni pamoja na kuwashauri viongozi wangu ili wasiitumbukize nchi yangu katika vita kwa kung'ang'ania mitazamo 'fake'. Uzalendo ni pamoja na kutoa habari zaukweli badala ya kuwadanganya watanzania wenzangu kuwa Presentation ya jopo la watanzania ktk mazungumzo ya kule Malawi ilikuwa bomba kiasi cha kustahili PhD wakati ile ya wamalawi ilistahili Certificate kama ambavyo alipata ku-post kwenye FB page yake balozi watanzania kule malawi hata kama yeye alistahili kuwa mwanadiplomasia na wakwanza kuheshimu ukweli kuwa mazungumzo hayo yalitakiwa yawe ya siri.

Prime Minister, Rashidi Kawawa, made three points: (i) that no part of Lake Nyasa fell within German East Africa; (ii) that since the boundary had not been altered by Britain after the assumption of the mandate, the Prime Minister's statement of 30 November 1961 did not apply; and (iii) that whatever the disadvantages to Tanganyika, the Government could not contemplate negotiations with either the Central African Federal Authorities in Salisbury or with Britain. 'If there are to be negotiations on this question', he concluded, 'they must be with the Government of Nyasaland itself and must wait the attainment by Nyasaland of full Independence.

Kinachozungumzwa hapo juu katika point ya pili kinatokana na kauli ya PM Nyerere ya 30 Novemba 1961 ambapo Mwalimu alitoa muelekeo wa sera za nchi huru ya Tanganyika ambapo alisema kuwa Tanganyika ingeendelea kuheshimu makubaliano yaliyofanywa na wakoloni kwa miaka miwili zaidi baada ya kupata uhuru.

Hii maana yake ni kuwa kiongozi wa juu wa Tanganyika aliwahi kukili kuwa Tanzania hatuna chetu katika ziwa lile na kwamba ishu hii si miongoni mwa mikataba ambayo Tanganyika huru ingeendelea kuiheshimum kwa miaka miwili zaidi mara baada ya uhuru. Hii maana yake ni kwamba Mkataba wa Heligoland ni valid mpaka leo kwani haukuwa miongoni mwa mikataba ambayo Tanganyika huru ingeiheshimu kwa kipindi cha miaka miwili tu.

 
Kuna mtu humu kaja na hoja ya kusema waandishi makajanja ndiyo wame-mislead jambo hili. Pamoja na kwaba sikubaliani sana na aliyesema hivyo lakini unavyokuja humu ni kama unaanza jambo jipya wakati tumetuma posts zaidi ya 600 ndai ya wiki mbili kwa hili.

Sasa ona, unakurupuka na suala la ndege kutua Mbamba_Bay ambalo ni la January mwaka huu wakati controversy hii ni ya zaidi ya miaka 50 sasa.


Hebu pitia thread zote ndiyo uje tujiunge behewa moja maana tunashindwa tukujibu nini. Soma walau thread hii: {Click Here}

Mkuu kwani wewe ni Mmalawi? Maana sikuelewi elewi!
 
Ndugu zangu,...

....Prime Minister, Rashidi Kawawa, made three points: (i) that no part of Lake Nyasa fell within German East Africa; (ii) that since the boundary had not been altered by Britain after the assumption of the mandate, the Prime Minister's statement of 30November 1961 did not apply; and (iii) that whatever the disadvantages to Tanganyika, the Government could not contemplate negotiations with either the Central African Federal Authorities in Salisbury or with Britain. 'If there are to be negotiations on this question', he concluded, 'they must be with the Government of Nyasaland itself and must wait the attainment by Nyasaland of full Independence.

Kinachozungumzwa hapo juu katika point ya pili kinatokana na kauli ya PM Nyerere ya 30 Novemba 1961 ambapo Mwalimu alitoa muelekeo wa sera za nchi huru ya Tanganyika ambapo alisema kuwa Tanganyika ingeendelea kuheshimu makubaliano yaliyofanywa na wakoloni kwa miaka miwili zaidi baada ya kupata uhuru.

Hii maana yake ni kuwa kiongozi wa juu wa Tanganyika aliwahi kukili kuwa Tanzania hatuna chetu katika ziwa lile na kwamba ishu hii si miongoni mwa mikataba ambayo Tanganyika huru ingeendelea kuiheshimum kwa miaka miwili zaidi mara baada ya uhuru. Hii maana yake ni kwamba Mkataba wa Heligoland ni valid mpaka leo kwani haukuwa miongoni mwa mikataba ambayo Tanganyika huru ingeiheshimu kwa kipindi cha miaka miwili tu.


Hapo nilipo-underline ndio tulipo kwa sasa, Nyasaland ilishapata uhuru wake. Kitu cha muhimu na cha kutia matumaini ni kwmba suala la umiliki wetu wa sehemu ya ziwa Nyasa lilitambulika na kupewa umuhimu tangu siku ya kwanza ya kupata uhuru wetu.

Hiyo Heligoland yao haikutumia common sense na nina amini kuwa ndio msimamo wetu. Malawi itapata shida sana ikiendelea kung'ang'ani ziwa lote upande wetu na wao wanatambua hilo, kwa kifupi wameshatambua kuwa ni jambo gumu sana kiutekelezaji/haiwezekani.
 
Mkuu kwani wewe ni Mmalawi? Maana sikuelewi elewi!

Huyo ni M-Malawi mbona alishajipambanua siku nyingi?

Mlioko Dar Lifuatilieni hilo Bwabw lililotoroka nchini kwao kutuletea ushog.. huku kwetu! Yaani najisikia kichefuchefu ninaposoma post za huyu Bwabw...!!!!
 
Back
Top Bottom