Baba duu Magezi
Member
- Feb 3, 2019
- 11
- 15
Mtandao wa Tigo umekuwa mtandao wa ajabu sana. Yaani saizi wana-program ya ovyo sana ukinunua salio kupitia Tigo pesa, pesa iliyokuwa kwenye acc ya Tigo pesa unakatwa haijalishi hata kama umenunua kifurushi kwa salio la kawaida. Naamini watu wa Sheria mpo humu mtalizungumza suala hili kwa Lugha ya ki-Sheria.
Ni sawa sababu mnadai pesa yenu, lakini kwenye technique za kibiashara mna feli sana. Sababu
1. Mnafanya service yenu kuwa ya gharama sana kwa wateja wenu kitu kinachofanya Vodacom akutandike kila siku sokoni. Mfano mimi mlikuwa mnanidai 3500/= Nimelipa pia nikaongeza vocha ya 3000/= nyingine ili niweze kujiunga kifurushi maana yake hapo nimetumia 6,500/= mnaona Mteja wenu Mlivyo mpatia gharama kubwa.
2. Customer care wanna-midomo michafu sana halafu ukipeleka lalamiko wana kucheka punde unakatiwa simu.
3. MB’s pia mnachakachua tena sana tu. Kweli mnatuogopesha wateja wenu
Niwaambie tu nilikuwa loyal customer wenu ila enough wazee.
WADAU WENGINE WENYE MALALAMIKO HAYA
Vodacom:
Nilikia najiunga vifurushi vya Tigo muda si mrefu,khe!kuangalia menu naona wamepandisha gharama kwa 100% na kupunguza huduma.
Ndio nikageukia vifurushi vya TTCL(laini ninayo),nikaona kwa robo ya gharama ya TTCL unapata huduma mara 2 zaidi kwa Tigo.
Waungwana na wapenda maendeleo wote naomba tuhamie TTCL haraka iwezekanavyo.....nina uhakika hata hapo ofisi ya Tigo makao makuu wote watakua wanatumia TTCL .
1.vifurushi vya TTCL vya wikiView attachment 1686635
2.Vifurushi vya Tigo vya wiki
View attachment 1686650
Leo nilikuwa najaribu kujiunga kifurushi cha internet mwezi kutoka Tigo, ambapo nilikuwa napata GB 7 kwa sh 10,000/=
Ila kwasasa hiyo Sh 10,000/= napewa GB 2.5
Kwa uchumi huu wa kati tunaelekea wapi?
Ni muda sasa wa kuanza kuhama huu mtandao, maana vifurushi vya data kutoka tigo havishikiki kabisaaa.
Mtandao gani kwa sasa una nafuu kuliko Zantel?
Nimeona niandike hili juu ya wizi wa kampuni ya (TIGO) kwenye vifurushi vyao, haijarishi ni kifurushi cha dakika au ni cha sms au internet,
Wamekuwa wakipandisha vifurushi vyao bila kujali hali halisi ya maisha tuliyonayo
Jana nimejaribu kununua kifurushi cha internet
ambacho nimezoea kununua cha Tsh 3000 gb 2 kwa wk
Nimekuta kimepunguzwa gb1 na kubakia gb 1 kwa tsh 3000 nimeshindwa kununua kifurushi hicho bado najiuliza nihamie kampuni gani yenye unafuu wa vifurushi tofauti na hawa wezi @tigo_tz
View attachment 1688193
pia soma > Malalamiko mbalimbali kuhusu mabadiliko ya vifurushi yaliyofanywa na mtandao wa Tigo kwa mwaka 2020Nina laini za mitandao yote inayopatikana kwenye mazingira yangu lakini cha ajabu nazunguka tu humohumo hakuna mwenye nafuu
TTCL walikuja moto ila ikawa kifurushi hakifanyi kazi mpaka kinaexpire (yaani ukituma sms haiendi au unafungua data internet haifunction labda kwa mara chache tu)
Zantel nao wako vizuri lakini dakika unaweza kushangaa tu paap! zimeisha. saa zingine una kifurushi ila wanakata vocha yako bila sababu na ukipiga customer care unakutana na majibu yaleyale ya kukaririshwa darasani
Airtel kwa kachenji kadogo ti utapata bonge la kifurushi (hasa internet) ila ndo utajua mwenyewe utaenda kuipata wapi access ya mtandao
Tigo ndo hata sijui nianzie wapi maana kila uozo ni wao. Kifurushi cha kawaida kabisa lakini kinagawanywa dk nyingine kwa ajili ya usiku tu (yaani unalazimishwa kupiga simu usiku) wakati hii tumezoea inawekwa kwenye vifurushi vile vingine vya ziada kama ofa nk
Halotel nao ndo walewale
Voda kama kawaida yao wao ni wazee wa ghali
Basi nimejikuta nahama mtandao fulani kwa muda tu mara huko kwingine wakileta ujinga nakuja kuurudia tena.
Lakini kuna mtandao mmoja katika hiyo nimeapa sitakaa nije kurudi tena!