Makweta alikuwa chifu wa kwanza na wa mwisho katika wilaya nne za mkoa wa njombe.

lutondwe

Senior Member
Dec 20, 2010
150
74
Kifo cha Makweta,kimenifikirisha na hakika nimekumbuka kuwa yeye ndiye mtu maarufu kuliko wanasiasa wengi waliopata kutawala katika mkoa wa Iringa na Njombe ikiwamo.Ni huyu Makweta ambaye aliwahi kuwa mbunge wa wilaya zote za mkoa wa Njombe wa sasa pia ni mtu wa pekee toka maeneo yetu aliyeshika uwaziri katika wizara nyingi.Kwa muda mrefu alikuwa mbunge wa eneo lote la Ludewa,Makete,Wanging'ombe na Njombe yote ambayo sasa imezalisha majimbo ya uchaguzi matatu.
Katika historia ya mkoa wa Iringa na Njombe Makweta atabaki kuwa mtu maarufu namba mbili baada ya Chifu Mkwawa aliyekuwa chifu wa wahehe miaka ya 1880s.

Makweta lazima aheshimiwe kwa jitihada zake za kuendeleza maeneo yote ya ukanda wa kusini kwa kuhamasisha upandaji wa miti ya mbao na kuni,ujenzi wa sekondari na mapambano makubwa aliyoongoza dhidi ya ugonjwa wa funza uliowatesa sana watoto wa Njombe hasa maeneo ya Lupembe na Mkambako.

Kwa wale wote wanaozaliwa au kuishi katika maeneo tajwa hapo juu yafaa tushiriki kwa ukaribu katika shughuli za kumsindikiza katika maisha ya amani ya milele.Makweta amekufa mwili lakini mawazo na falsafa zake zitaishi milele.Makweta ulitutoa porini ukatuleta barabarani.We shall always remember you and love you forever.R.I.P JACKY.
 
Now we have the King and Chief Njombe J. Makwetta, albeit posthumously.
 
Huyu si ndiye yeye aliyejaza mashule ya sekondari huko njombe akaziacha wilaya za ludewa na makete zikitegemea hisani ya kupewa nafasi za sekondari kutoka nje ya wilaya zao. Akiwa waziri alifungua shule nyingi ndani ya wilaya ya njombe akiwaacha majirani zake wakililia hisani ya mgao wa serkali. Enzi hizo ilikuwa ukichaguliwa kwenda sekondari toka ludewa au makete ni lazima uwe kichwa kwelikweli maana nafasi zilikuwa finyu kama vile kwenda mbinguni. Huo ndio udhaifu wake unaotokana na ukabila
 
Funza nasikia ni kweli wanawatesa sana watoto na wakaazi wa Njombe,Makete sana tena wenyewe wanangaliana vidole tu wanajua kama umekulia kule ama la!nafikiri ni sababu ya vumbi na baridi...kuoga ni shida,na funza kwa vumbi ndio kwao!
 
Funza nasikia ni kweli wanawatesa sana watoto na wakaazi wa Njombe,Makete sana tena wenyewe wanangaliana vidole tu wanajua kama umekulia kule ama la!nafikiri ni sababu ya vumbi na baridi...kuoga ni shida,na funza kwa vumbi ndio kwao!
 
sipendi kweli hizi sifa za marhemu,mbona kabla hajafa hamjawahi kuandika wasifu wake na kuthamini mchango wake katika taifa hili? ina maana taarifa hizo mmezipata baada ya kifo chake?huu ni unafiki tunaopaswa kuukemea na kutouendeleza mambo hayo,wapeni sifa zao watu wakiwa hai bana
 
Kifo cha Makweta,kimenifikirisha na hakika nimekumbuka kuwa yeye ndiye mtu maarufu kuliko wanasiasa wengi waliopata kutawala katika mkoa wa Iringa na Njombe ikiwamo.Ni huyu Makweta ambaye aliwahi kuwa mbunge wa wilaya zote za mkoa wa Njombe wa sasa pia ni mtu wa pekee toka maeneo yetu aliyeshika uwaziri katika wizara nyingi.Kwa muda mrefu alikuwa mbunge wa eneo lote la Ludewa,Makete,Wanging'ombe na Njombe yote ambayo sasa imezalisha majimbo ya uchaguzi matatu.
Katika historia ya mkoa wa Iringa na Njombe Makweta atabaki kuwa mtu maarufu namba mbili baada ya Chifu Mkwawa aliyekuwa chifu wa wahehe miaka ya 1880s.

Makweta lazima aheshimiwe kwa jitihada zake za kuendeleza maeneo yote ya ukanda wa kusini kwa kuhamasisha upandaji wa miti ya mbao na kuni,ujenzi wa sekondari na mapambano makubwa aliyoongoza dhidi ya ugonjwa wa funza uliowatesa sana watoto wa Njombe hasa maeneo ya Lupembe na Mkambako.

Kwa wale wote wanaozaliwa au kuishi katika maeneo tajwa hapo juu yafaa tushiriki kwa ukaribu katika shughuli za kumsindikiza katika maisha ya amani ya milele.Makweta amekufa mwili lakini mawazo na falsafa zake zitaishi milele.Makweta ulitutoa porini ukatuleta barabarani.We shall always remember you and love you forever.R.I.P JACKY.
Na mimi namkumbuka sana alikuwa mwalimu wangu wa somo la historia shule ya upili (secondary school) Mungu aiweke roho yake peponi.
 
Back
Top Bottom