Makusanyo ya TRA ya Julai - September 2018/2019 yapanda maradufu: Yakusanya 3,840,000,000,000/-

Wale wanaochukia jitihada za awamu ya tano nina uhakika watachukizwa na habari hii pia.

Wakwanza akiwa ni yule muheshimiwa mshirikina wa Kigoma Ujiji na Domo Kaya aliyepo kwenye matibabu Ubeligiji.
 
Mamlaka ya Mapato nchini TRA, imetoa taarifa ya ukusanyaji wa mapato yake ya quarter ya kwanza ya Mwaka wa Fedha 2018/2019, ambayo imeonyesha makusanyo ya shilingi Trilioni 3.84, sawa na asilimia 5.3% ya mwaka 2017/2018 ambako makusanyo yalikuwa ni trilioni 3.65.
TRA imewashukuru walipakodi wote ambao wameendelea kulipa kodi zao kwa hiari na kwa wakati na kuwahimiza wale ambao bado wanasuasua kujitokeza kulipa kodi hizo kwa wakati. TRA imewataka wenye changamoto mbalimbali kufika katika Ofisi za TRA mikoani na wilayani kuonana na mameneja wao.

View attachment 891163

Ni tatizo la uwezo wa kujua kusoma namba na kuzitafsiri kwa maneno, pole ndg yangu rudi skuli upya na uwasikilize walimu wako uache tabia ya kupiga chabo wakati wa mitihani
 
Tatizo mmeweka Sheria za Twakimu zinabana kuchambua takwimu za serikali kukosa hizo Sheria Zitto angetuambia Ukweli.
 
Mamlaka ya Mapato nchini TRA, imetoa taarifa ya ukusanyaji wa mapato yake ya quarter ya kwanza ya Mwaka wa Fedha 2018/2019, ambayo imeonyesha makusanyo ya shilingi Trilioni 3.84, sawa na asilimia 5.3% ya mwaka 2017/2018 ambako makusanyo yalikuwa ni trilioni 3.65
View attachment 891163


Ambayo ni sawa na "zaidi" ya asilimia 5.3%. Tuzingatie, tuwe makini kutumia lugha sahihi. Tuna wataalamu wa kutosha.

"Zaidi" ni neno muhimu hapa. Otherwise the statement doesn't make any sense.
 
Mamlaka ya Mapato nchini TRA, imetoa taarifa ya ukusanyaji wa mapato yake ya quarter ya kwanza ya Mwaka wa Fedha 2018/2019, ambayo imeonyesha makusanyo ya shilingi Trilioni 3.84, sawa na asilimia 5.3% ya mwaka 2017/2018 ambako makusanyo yalikuwa ni trilioni 3.65.

TRA imewashukuru walipakodi wote ambao wameendelea kulipa kodi zao kwa hiari na kwa wakati na kuwahimiza wale ambao bado wanasuasua kujitokeza kulipa kodi hizo kwa wakati.

TRA imewataka wenye changamoto mbalimbali kufika katika Ofisi za TRA mikoani na wilayani kuonana na mameneja wao.

View attachment 891163
hata mkisema mmekisanya trillion 400, nani atabisha, say anything you like! trillion 1,000 zimekusanywa Salary Slip
 
Hawa TRA na BOT wangekuwa wanatoa detailed statistics kuliko hii final figure ingependeza.
Tunataka tupate indication ya growth kwenye kila sekta mfano kilimo, uvuvi, imports, exports, biashara za ndani, uzalishaji viwandani nk.
 
Mleta mada nawe umetia kachumbari hiyo taarifa ni kweli kuna ongezeko lakini kusema maradufu siyo kweli maana difference ni 0.19 kati ya 3.84 na 3.65 maradufu ingekuwa na sense kama tungekuwa na difference ya kuanzia at least 1.5 hivi

Ila bado wanapaswa kupongezwa japo hata kwa hicho kidogo walichofanikiwa ila sasa watafute namna kidogo hizo hela zirudi kwenye mzunguko ili kuchochea zaidi ukuaji wa uchumi na kuongeza purchasing power ya watu wakifanya hivyo mapato yataongezeka ila hii contractionary method yao ina athari sana maana hali zetu wananchi mbaya
 
Mamlaka ya Mapato nchini TRA, imetoa taarifa ya ukusanyaji wa mapato yake ya quarter ya kwanza ya Mwaka wa Fedha 2018/2019, ambayo imeonyesha makusanyo ya shilingi Trilioni 3.84, sawa na asilimia 5.3% ya mwaka 2017/2018 ambako makusanyo yalikuwa ni trilioni 3.65.

TRA imewashukuru walipakodi wote ambao wameendelea kulipa kodi zao kwa hiari na kwa wakati na kuwahimiza wale ambao bado wanasuasua kujitokeza kulipa kodi hizo kwa wakati.

TRA imewataka wenye changamoto mbalimbali kufika katika Ofisi za TRA mikoani na wilayani kuonana na mameneja wao.

View attachment 891163
Jifunze kwanza kuandika kiswahili...marafufu ndo nini wew jinga kubwa?Shida ni kukimbilia sit kushabikia mithili ya zombiz!!
 
sasa wanatuletea takwimu ili sisi tusemeje??
siku hiz ukisema waongo unawekwa jera. wanataka tuitikie kama tuko ibadani ! ujinga huu kuna kipindi tutakua tunaukwepa kama sio sisi waasisi
 
Tangu iwekwe ile sheria ya takwimu, ni vigumu sana kuamini usahihi wa taarifa za serikali na vyombo vyake. Hakuna anayeweza kuhoji wala kuhakikii.
 
Hii habari yote ni upuuzi mtupu.

Aliyesema kuwa mapato yameongezeka maradufu yaelekea hata kiswahili hajui. Mapato yaliyoongezeka ni kidogo sana ambayo wala hata hayaendani na ukuaji wa uchumi ambao tuliambiwa ni 7%. Kama uchumi unakuwa kwa 7%, inakuwaje mapato yaongezeke (revenue difference not revenue growth rate) kwa 5% tu? Na hiyo 5% ni ongezeko wala siyo ukuaji.

Kwa vyovyote, ina maana ukuaji wa makusanyo ya serikali ni chini ya 2.5%. Hapa lazima kuna eneo tunadanganywa. Haiwezekani ukuaji wa uchumi 7%, ukuaji wa makusanyo ya kodi chini ya 2.5%!

Kwa wasiojua maana ya maradufu:

Ufafanuzi wa maradufu katika Kiswahili

maradufu

KIVUMISHI1

mara mbili ya kitu kingine k.v. kwa ukubwa, ujazo, thamani, nguvu au idadi.
 
Back
Top Bottom