MAKUBALIANO YA SIRI: JK aahidi kumrudisha Lowassa madarakani

Wadau wanasema kuwa kabla ya kuamua kuchukua tena fomu za kugombea Urais, Jakaya Kikwete alishikwa na hofu kubwa sana na akasita kuchukua uamuzi. Hii ni baada ya kusikia kutoka kwa watu wake wa karibu na vyombo vya dola kuwa Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, Edward Lowassa, anataka kum-challenge Kikwete kwenye kupata nomination ya kugombea Urais 2010 yeye mwenyewe au kwa kuweka mgombea wake mwingine.

Ndipo hapo Kikwete akaamua kumuuliza Lowassa mwenyewe iwapo hizo taarifa ni za kweli. Lowassa akajibu kuwa bado hajafanya uamuzi kama agombee Urais 2010 au la.

Lowassa akamwambia Kikwete ingawa makubaliano yao ya awali ni kuwa Lowassa achukue Urais 2015 baada ya Kikwete kumaliza vipindi viwili, hivi sasa yuko gizani kisiasa baada ya kujiuzulu (political wilderness).

Lowassa's fear is that wanasiasa kama Bernard Membe, Prof. Mark Mwandosya, Dr Hussein Mwinyi, Dr. John Magufuli na Lawrence Masha (ingawa yuko kambi ya Lowassa) watampiku kwa umaarufu ifikapo 2015 hivyo ndoto zake za kuwa Rais zitafifia zaidi.

"Unajua msimamo wangu na malengo yangu (ya kuwa Rais 2015) bado yapo palepale," Lowassa alikaririwa akimwambia Kikwete.

Kikwete akamjibu Lowassa kuwa basi asijali. Akamwambia kuwa kujiuzulu kwako kama PM tutasema ilikuwa ni ajali ya kisiasa tu. Akamuahidi Lowassa kuwa atamshangaza kila mtu na kumrudisha serikalini kwa kishindo baada ya uchaguzi wa 2010.

"Don't worry my friend. I will surprise everybody kwa kukurudisha madarakani ili ujiweke vizuri na uchaguzi wa 2015," JK alikaririwa na wadau akimwambia Lowassa.

Haikuweza kufahamika mara moja ni madaraka gani JK atampa Lowassa ili ajiweke vizuri kumrithi Urais 2015.

Kuna tetesi kuwa JK atampa Lowassa a senior Cabinet post (uwaziri) au kumfanya ndiye Katibu Mkuu mpya wa CCM baada ya Yusuf Makamba ili akikamate chama vizuri kuelekea 2015.

Baada ya mazungumzo na Lowassa, Kikwete ndipo akapata nguvu kwenda Dodoma kuchukua fomu za kugombea Urais kama mgombea pekee wa chama.

Ila bado ana suspicion kuwa kundi la mtandao ndani ya CCM lililokuwa loyal kwa Lowassa na Rostam Aziz linaweza kumfanyizia. Ndiyo maana akamtuma mwanae Ridhwani afanye kazi ya kutafuta wadhamini kwa hofu ya kuwa sabotaged na kuwekewa wadhamini feki na hivyo kuwa disqualified kama candidate.

Narudia tena, hizi ni tetesi tu. Ila inapotokea hali ambapo Rais wa nchi anamhofu ex-PM wake, tena aliye lazimika kujiuzulu kwa kashfa ya ufisadi ina maana kuwa "this country has gone to the dogs" kama Mwalimu Nyerere alivyowahi kutuonya.

Jamani, Lowasa kwani si mtanzania kama walivyo watanzania wengine?. Ina maana hana haki ya msingi ya kugombea uongozi ndani ya Tanzania?.

Tusiwe kama wayahudi waliokuwa wanashangalia na kushabikia kwamba YESU asulubiwe bila kujua hali halisi ya mambo.

Hivi hapa jamvini kuna mtu anaweza kuja na facts kuonesha na kudhibitisha mabaya na machafu ya Lowasa?.

Bila shaka ni wachache sana hapa jamvini wanaojua ukweli kwanini Lowasa alijiuzulu uwaziri mkuu na pia kwanini hakupewa nafasi ya kujieleza mbele ya kamati ya Mwakyembe.

Jamani shilingi ina pande mbili, hivyo kuweza kujua urembo wa shilingi ni hekima kuangalia pande zote.

Wengi mlifurahi sana kuona Lowasa amejiuzulu uwaziri mkuu, lakini mliweza kujiuliza kujiuzulu kwake katika nafasi hiyo kuliwapa faida gani hapa jamvini ama ndani ya Tanzania?. Mnaimba kwamba Lowasa alikuwa ni fisadi, sasa amejiuzulu uwaziri mkuu je ufisadi umekoma ama umeisha ndani ya Tanzania?.
 
Jamani, Lowasa kwani si mtanzania kama walivyo watanzania wengine?. Ina maana hana haki ya msingi ya kugombea uongozi ndani ya Tanzania?.

Tusiwe kama wayahudi waliokuwa wanashangalia na kushabikia kwamba YESU asulubiwe bila kujua hali halisi ya mambo.

Mimi nafikiri tatizo si kwa Lowassa kugombea bali tatizo ni kuanza kuwekeana mikataba ya kilaghai kana kwamba nchi hii ni ya babu yao au ni shamba la bibi yao, huwezi kuanza kampeni za 2015 wakati hata uchaguzi wa 2010 haujamalizika.

Hii inaashiria kuwa kuna "network imejipanga" kuendelea kuwashindilia watanzania vijiti vikavu bila ridhaa yao. Hii hali ni lazima ikemewe kwa nguvu zote. Tanzania ina watu takribani 40M, nina hakika wapo viongozi wazuri kuliko huyu aliyekwisha pata kashfa, ila unapoona mkulu wa nchi anaingia kwenye dili haramu(kama haya yanayosemwa ni kweli) basi ujue nchi inaelekea kusikofaa.

Je huyu Lowassa ana mkataba na mwenyezi mungu wa kumuweka akiwa na afya njema mpaka 2015? Kama anayobasi huu ni wakati wa kuanza kuwaombea mabaya wale wote wenye mawazo kama haya (Kama yanayosemwa ni kweli kuhusu wao)
 
Jamani, Lowasa kwani si mtanzania kama walivyo watanzania wengine?. Ina maana hana haki ya msingi ya kugombea uongozi ndani ya Tanzania?.

Tusiwe kama wayahudi waliokuwa wanashangalia na kushabikia kwamba YESU asulubiwe bila kujua hali halisi ya mambo.

Hivi hapa jamvini kuna mtu anaweza kuja na facts kuonesha na kudhibitisha mabaya na machafu ya Lowasa?.

Bila shaka ni wachache sana hapa jamvini wanaojua ukweli kwanini Lowasa alijiuzulu uwaziri mkuu na pia kwanini hakupewa nafasi ya kujieleza mbele ya kamati ya Mwakyembe.

Jamani shilingi ina pande mbili, hivyo kuweza kujua urembo wa shilingi ni hekima kuangalia pande zote.

Wengi mlifurahi sana kuona Lowasa amejiuzulu uwaziri mkuu, lakini mliweza kujiuliza kujiuzulu kwake katika nafasi hiyo kuliwapa faida gani hapa jamvini ama ndani ya Tanzania?. Mnaimba kwamba Lowasa alikuwa ni fisadi, sasa amejiuzulu uwaziri mkuu je ufisadi umekoma ama umeisha ndani ya Tanzania?.
Kweli Lowassa ni mtanzania na ana haki zote za kugombea uongozi wowote ule, lakini kuwa na haki pekee hakutoshi kumfanya mtu kuwa kiongozi. Uongozi una miiko yake ambayo yeye kaikiuka, pamoja na mambo mengine kiongozi anatakiwa asiwe na doa awe msafi mbele ya macho ya jamii.
 
So inaonekana Lowasa alipo jiuzulu alim cover mtu ,na PM anaweza kumcover nani zaidi ya rais!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kidatu,
Mkuu wangu sasa huu ni Ushabiki.. unashindwa kuiona picha kubwa. Lowassa kujiuzuru kwake ni sawa na mtu mwenye Ukimwi aliyekataa kutembea na wewe baada ya kutuhumiwa ana Ukimwi..Sasa unapouliza watu wamepata faida gani kutotembea na mtuhumiwa itakuwa shida kubwa sana kuzungumzia isipokuwa tunajua maradha ambayo yangetokea kama tunge.....Na hakika hakuna baina yetu anayeweza kuthibitisha maradhi ya mtuhumiwa ikiwa majibu hayatoki kwa daktari lakini huo ushahidi mchache wa watu aliotembea nao na wameondoka inatosha kabisa kutushtua wengine..

Hatumsemi vibaya Lowassa kama sii Mtanzania isipokuwa anapotaka kurudi kuchukua madaraka ndipo swala zima la usalama wetu linapoingia, kwa sababu hataki kujisafisha kwa vipimo vya haki isipokuwa kulonga sana ktk magazeti kwamba anasingiziwa tu.. Ya kina Karamagi na wengineo haya..come clean hawataki.. ati tuthibitishe sijui kitu gani..

Sisi wananchi tulichomwamba Lowassa akapime, asimame mahakamani au bungeni na kujisafisha dhidi ya report ya Mwakyembe, kinyume cha hapo mkuu wangu itakuwa kazi kubwa sana kuwaridhisha wananchi na hakika JK hawezi kabisa kubeba mzoga huu wakati yeye mwenyewe anaishi ktk kujificha..
 
Kidatu,
Mkuu wangu sasa huu ni Ushabiki.. unashindwa kuiona picha kubwa. Lowassa kujiuzuru kwake ni sawa na mtu mwenye Ukimwi aliyekataa kutembea na wewe baada ya kutuhumiwa ana Ukimwi..Sasa unapouliza watu wamepata faida gani kutotembea na mtuhumiwa itakuwa shida kubwa sana kuzungumzia isipokuwa tunajua maradha ambayo yangetokea kama tunge.....Na hakika hakuna baina yetu anayeweza kuthibitisha maradhi ya mtuhumiwa ikiwa majibu hayatoki kwa daktari lakini huo ushahidi mchache wa watu aliotembea nao na wameondoka inatosha kabisa kutushtua wengine..

Hatumsemi vibaya Lowassa kama sii Mtanzania isipokuwa anapotaka kurudi kuchukua madaraka ndipo swala zima la usalama wetu linapoingia, kwa sababu hataki kujisafisha kwa vipimo vya haki isipokuwa kulonga sana ktk magazeti kwamba anasingiziwa tu.. Ya kina Karamagi na wengineo haya..come clean hawataki.. ati tuthibitishe sijui kitu gani..

Sisi wananchi tulichomwamba Lowassa akapime, asimame mahakamani au bungeni na kujisafisha dhidi ya report ya Mwakyembe, kinyume cha hapo mkuu wangu itakuwa kazi kubwa sana kuwaridhisha wananchi na hakika JK hawezi kabisa kubeba mzoga huu wakati yeye mwenyewe anaishi ktk kujificha..

Mkandara,

Sina sababu ya kuwa shabiki wa Lowasa, bali naangalia ukweli katika suala hili.
Kila ukiimbwa wimbo wa ufisadi katika Tanzania basi Lowasa amekuwa ni corus ya kibwagizo. Lakini ukiangalia kwa undani zaidi utaona wazi kwamba Lowasa alikubali kujiuzulu kwa lengo la kuwajibika na wala si ufisadi kama yanavyosemwa hapa Jamvini. Kama waziri mkuu asingeweza kuchukua maamuzi mazito kama yale bila ya kumshirikisha mkuu wake wa kazi. Hapa nina maana ofisi kuu ya nchi ilikuwa inajua bayana kila lililokuwa linaendelea na ilitoa baraka.

Rejea ripoti ya Mwakyembe: - Kuna mengine hatutayasema kwa ajili ya usalama wa nchi. Unafikiri Mwakyembe alikuwa na maana gani?. Elewa kwamba kamati ya Mwakyembe ilikuwa inatoa ripoti ofisi kuu katika kila stage ya uchunguzi inayofikiwa.

Mkandara, ukiisoma vyema repoti hiyo ya Mwakyembe utaona wazi kwamba kulikuwa na kila sababu za msingi za kumwita na kumuuliza maswali Lowasa kwa lengo la kupata ufafanuzi wa kina kwa yale aliyoyatolea maamuzi ama kuyaagiza kufanyika. Kwanini hakupewa nafasi hiyo?. Mawaziri na watu wengine wote waliitwa na walisema wanafanya kazi kwa kushirikiana na ofisi ya waziri mkuu, lakini elewa kwamba na yeye alikuwa na mkuu wake wa kazi aliyekuwa anashirikiana naye katika kufanya kazi hiyo. Huoni kwamba angepewa nafasi ya kuhojiwa tungeyajua mengi?, nani wa kuwajibika katika hili?.
 
Kweli Lowassa ni mtanzania na ana haki zote za kugombea uongozi wowote ule, lakini kuwa na haki pekee hakutoshi kumfanya mtu kuwa kiongozi. Uongozi una miiko yake ambayo yeye kaikiuka, pamoja na mambo mengine kiongozi anatakiwa asiwe na doa awe msafi mbele ya macho ya jamii.

Kama kuna miiko ya uongozi katika Tanzania ya leo, basi hakuna kiongozi hata mmoja anayefaa kuwa katika nafasi hiyo. Miiko ya uongozi katika Tanzania ilikufa mara tu baada ya kifo cha Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
 
Mimi nafikiri tatizo si kwa Lowassa kugombea bali tatizo ni kuanza kuwekeana mikataba ya kilaghai kana kwamba nchi hii ni ya babu yao au ni shamba la bibi yao, huwezi kuanza kampeni za 2015 wakati hata uchaguzi wa 2010 haujamalizika.

Hii inaashiria kuwa kuna "network imejipanga" kuendelea kuwashindilia watanzania vijiti vikavu bila ridhaa yao. Hii hali ni lazima ikemewe kwa nguvu zote. Tanzania ina watu takribani 40M, nina hakika wapo viongozi wazuri kuliko huyu aliyekwisha pata kashfa, ila unapoona mkulu wa nchi anaingia kwenye dili haramu(kama haya yanayosemwa ni kweli) basi ujue nchi inaelekea kusikofaa.

Je huyu Lowassa ana mkataba na mwenyezi mungu wa kumuweka akiwa na afya njema mpaka 2015? Kama anayobasi huu ni wakati wa kuanza kuwaombea mabaya wale wote wenye mawazo kama haya (Kama yanayosemwa ni kweli kuhusu wao)

Mkuu,

Kupanga ni kuchagua, lakini kuchagua si kupanga. Ni nani kati yetu atakayependa kutembea huku kafumba macho?. Unapotembea unaangalia mbele ili kujua na kuona unakokwenda kwa lengo la kujinga vyema.
 
Mkandara.. unasahau kuwa kashfa ya Lowassa na Richmond ilitokea katika miaka miwili ya kwanza ya JK ambapo alikuwa bado anajifunza yeye na utawala wake. Kwa hiyo, ukiangalia utaona kuwa sasa hivi ameshajua cha kufanya na makosa ya Lowassa na wenzie yanaeleweka (kama sehemu ya mafunzo). Binafsi wala sitakuwa na tatizo la EL kurudishwa madarakani, tatizo langu ni hayo madaraka mikononi mwa EL.
 
Mafisadi wenzake wote bado wako madarakani. Kwa nini yeye asirudi? Hakuna unafuu kokote. Sio BUNGE wala MAHAKAMA ambako hakuna mafisadi. Hata ambao machoni tunawaona wana ahueni kama Pinda wanafanyakazi kwa woga na tahadhari kubwa. Sana wanakimbilia Bagamoyo kumfukuza mhasibu wa halmashauri!
 
Huyu mleta hii thread amenishangaza sana, mbona habari hii haionekani kama ni 'tetesi' maana amequote mpaka mazungumzo kati ya JK na EL, sasa hii inakuwaje tetesi kama aliyasikia hayo mazungumzo?
 
WOTE WaNAO MTAKA LOWASSA NI VICHAA. AWAJUI HAKI YAO KIKATIBA, MTU KASHFA KIBAO , ALIPASWA AWE MAGEREZA AU KAPIGWA RISASI ADHARANI WEWE UNAMTETEA NINI? KWELI WATANZANIA ATUFIKIRII, NATAMANI TUNGEKUWA NA UJASIRI WA CHINA.
 
Tunavyozidi kumzungumzia Lowassa na hata kumuota inamaanisha sisi wenyewe ametukaa akilini.Tuna mapenzi naye isipokuwa htunashindwa kuyasema hadharani..JK anaweza kuwa mjinga lakini sidhani kama ni mjijga kiasi cha kumrudisha Lowassa madarakani.

Lowassa almost cost his Presidency na maadam kisha rekebisha mambo, Lowassa will remain where he is kama Mkapa na wengineo.. hao walioko madarakani leo hii wengi wao walikuwa maadui wa Lowassa toka Pinda, Mwanri, Membe hadi makatibu wakuu leo hii mnataka kunambia JK amekuwa kichaka cha kumrudisha Lowassa ambaye mwaka mmoja tu wa Utawala wake ilikuwa scandal baada ya scandal arudi tena madarakani!....

Kumbukeni baraza la mawaziri lote la kwanza lilipitishwa na Lowassa na RA, hivyo bado wapo watu wana imani naye warudi kutawala lakini isiwe sababu ya kumweka meza moja na JK.. Jamaa kisha temwa atafanya kila alifanyalo kamaLowassa kurudi madarakani na hakika washabiki wake wapo wengi tu..

Mzee umesahau chorus yako hapo!
 
Tuanze kuwaongelea watu wenye maadili. Tuachane na Lowassa, alionekana kuwa hafai, akajiuzuru kwa kuwa hafai. Na sasa tumsahau kwa kuwa hatufai. Tuongelee watanzania waadilifu kama Pinda labda, Dr. Migiro; or my God, they arent many eeh?
 
Wadau wanasema kuwa kabla ya kuamua kuchukua tena fomu za kugombea Urais, Jakaya Kikwete alishikwa na hofu kubwa sana na akasita kuchukua uamuzi. Hii ni baada ya kusikia kutoka kwa watu wake wa karibu na vyombo vya dola kuwa Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya Richmond, Edward Lowassa, anataka kum-challenge Kikwete kwenye kupata nomination ya kugombea Urais 2010 yeye mwenyewe au kwa kuweka mgombea wake mwingine.

Ndipo hapo Kikwete akaamua kumuuliza Lowassa mwenyewe iwapo hizo taarifa ni za kweli. Lowassa akajibu kuwa bado hajafanya uamuzi kama agombee Urais 2010 au la.

Lowassa akamwambia Kikwete ingawa makubaliano yao ya awali ni kuwa Lowassa achukue Urais 2015 baada ya Kikwete kumaliza vipindi viwili, hivi sasa yuko gizani kisiasa baada ya kujiuzulu (political wilderness).

Lowassa's fear is that wanasiasa kama Bernard Membe, Prof. Mark Mwandosya, Dr Hussein Mwinyi, Dr. John Magufuli na Lawrence Masha (ingawa yuko kambi ya Lowassa) watampiku kwa umaarufu ifikapo 2015 hivyo ndoto zake za kuwa Rais zitafifia zaidi.

"Unajua msimamo wangu na malengo yangu (ya kuwa Rais 2015) bado yapo palepale," Lowassa alikaririwa akimwambia Kikwete.

Kikwete akamjibu Lowassa kuwa basi asijali. Akamwambia kuwa kujiuzulu kwako kama PM tutasema ilikuwa ni ajali ya kisiasa tu. Akamuahidi Lowassa kuwa atamshangaza kila mtu na kumrudisha serikalini kwa kishindo baada ya uchaguzi wa 2010.

"Don't worry my friend. I will surprise everybody kwa kukurudisha madarakani ili ujiweke vizuri na uchaguzi wa 2015," JK alikaririwa na wadau akimwambia Lowassa.

Haikuweza kufahamika mara moja ni madaraka gani JK atampa Lowassa ili ajiweke vizuri kumrithi Urais 2015.

Kuna tetesi kuwa JK atampa Lowassa a senior Cabinet post (uwaziri) au kumfanya ndiye Katibu Mkuu mpya wa CCM baada ya Yusuf Makamba ili akikamate chama vizuri kuelekea 2015.

Baada ya mazungumzo na Lowassa, Kikwete ndipo akapata nguvu kwenda Dodoma kuchukua fomu za kugombea Urais kama mgombea pekee wa chama.

Ila bado ana suspicion kuwa kundi la mtandao ndani ya CCM lililokuwa loyal kwa Lowassa na Rostam Aziz linaweza kumfanyizia. Ndiyo maana akamtuma mwanae Ridhwani afanye kazi ya kutafuta wadhamini kwa hofu ya kuwa sabotaged na kuwekewa wadhamini feki na hivyo kuwa disqualified kama candidate.

Narudia tena, hizi ni tetesi tu. Ila inapotokea hali ambapo Rais wa nchi anamhofu ex-PM wake, tena aliye lazimika kujiuzulu kwa kashfa ya ufisadi ina maana kuwa "this country has gone to the dogs" kama Mwalimu Nyerere alivyowahi kutuonya.


Mimi ninadhani hizo nihabarikama habari kama habari zingine kwani ninachoweza kufahamu nikwamba maongezi kama hayo aranyingi nifaragha tena ukizingatia nimazungumzo nz mkuu wa nchi!!Hapo hata mlinzi wake anawekwa kando!!Hivyo ni habari hambayo aijitoshelezi kuwekwa bayana katika Jamii Forum!.Huo ndo mtazamo wangu wadau.
 
Una uhakika gani kama atarudi madarakani,watu kama nyie mna ni kera sana yan...hamstahili hata kuishi hapa Tanzania


Sijaona chama cha upinzani TZ cha kumuangusha rais JK KATIKA UCHAGUZI MKUU UJAO.
 
Siku zote EDO amekuwa na sura ya unyonge sana na uwenda anajutia uamuzi wake wa kujiuzulu u-PM. Lakini hata ukimsikiliza katika maelezo yake ya awali siku zile alipojiuzulu, hanaonyesha jinsi gani asivyokubalina na tuhuma dhidi yake. Alikuwa wazi kabisa kuficha hata ukweli iwapi kulikuwa na makubaliano yeyote kati yake na JK kuhusu yeye kuachia ngazi. JK aliliridhirisha hili kinamna siku aliyowaambia watanzania kuwa yaliyomkuta EDOO ilikuwa ni ajali ya kisiasa lakini alimfunika kwa kumtaka asikate tamaa. IPO SIRI KUBWA KATI YA HAWA MASWAHIBA!!!


Edward Lowassa (MB) Akijieleza TVT 2


Edward Lowassa Akijieleza TVT Seh. 1

YouTube - Edward Lowassa Akijieleza TVT Seh. 1
 
Kihalali kwa siasa zao CCM chini ya uongozi wa JK Lowassa anastahili heshima ya kupewa nafasi muhimu katika baraza lijalo la mawaziri.

napendekeza mh JK afikirie kumpatia Mh LOWASSA uwaziri wa elimu na mafunzo ili atekelezee vemaa gurudumu hiloo.

sina tatizo lolote na JK kumpatia uwaziri lowassa serikali ijayoo..na itakuwa ni undumilakuwilii mkubwaa kwa JK kutokumpatia nafasi hiyoo.
 
Back
Top Bottom