Makosa ya Wazazi kurithisha watoto elimu iliyopitwa na wakati huzaa watu wasiojiamini na tegemezi

Jukumu la elimu bora ni la Mzazi mwenyewe kuchagua aina ya elimu. kuendeleza elimu hii ya kikoloni ya kusoma kumaliza miaka au kubadilika kuwekeza kwenye elimu ya utambuzi na uvumbuzi yenye kumjengea mtoto kujiamini

Nipo Dodoma kwa sasa kutafuta PhD kama alama na sio kama uwezo

Wakati huo wenzangu wazazi wao wakiwasisitiza watoto wao wasome mambo ya Forced labour, Trigonometric, Integration by parts. Economics na Uhasibu

Mimi mzazi wangu alinipiga marufuku kusoma mambo hayo bali alininunulia Computer za kizamani sana zenye kutumia Floppy disk sio kama hizi za sasa za CD na Flash Disk

Kwa utu uzima wangu huu sikuwahi peleka watoto wangu Form five na Six hata Mimi sikuwahi soma form five na Six kwani mzazi hakunipitisha kwenye mfumo huo wa elimu na hata Yeye mzazi wangu mmoja wapo hakupitia mfumo huo wa Form five na Six

Miaka miwili ya Form five na Form Six iliniwezesha kufanya mambo kwa vitendo kama kujifunza kuagiza mizigo toka nje, Uwasilishwaji wa document muhimu kama vibali vya kuagiza bidhaa na uwezo wa kuunda Application tofauti

Coding Language ndio elimu ambayo mzazi alinifundisha kwa wakati huo, Niliharibu computer nyingi sana utotoni nikitaka kujua ndani ya computer kuna kitu gani tofauti na Radio au TV ambazo mara nyingi nilijua ndani kuna vitu gani

Coding language ndio kitu pekee nilikitumia kama fimbo ya kuchapia na kuweka mambo sawa kabla ya siasa, Watoto wangu wapo step moja mbele ya mimi hasa kwenye teknolojia

Wazazi smart baadhi Nawapongeza sana watoto wao wanapata hii elimu ya coding shule ya msingi kwa sasa. lakini kwa sasa coding imepitwa na wakati kidogo

Kwanini Mimi na wanangu tupo hapa Udom kwa sasa? Lengo letu ni PhD lakini kilichotuleta ni kuna vijana walipata tuzo kwenye mambo ya computer hasa kwenye "Hacking na Cyber Security" na ni wanafunzi wa kutoka Udom ndaki ya teknolojia hapa UDOM, Tunaamini kama hawa watoto wa wakulima wasio na vifaa na wana elimu ya kata wanajua vitu hivi basi moja kwa moja wana kitu cha ziada ambacho Mimi na wanangu hatuna au tunaweza ongeza nguvu nasi tukapata kitu kipya cha Uelekeo wa wajukuu zetu

Uelekeo wa Dunia sasa kwa wajukuu zetu hapa nyumbani ni Artificial Intelligence( AI). Tunajitahidi kuwekeza kwa watoto wa wanangu mambo ya AI na sio coding sana

Gharama ni kubwa sana sana kwenye haya mambo ya AI bali hatukati tamaa kwani hata Mimi mzazi hakukata tamaa juu yangu wala mimi sikukata tamaa kwa hawa vijana wangu nilionao hapa Dodoma kwa muda
Mambo ya Blockchain watu wanayojisumbua sana sasa ni mambo ambayo miaka ile ya dunia nyeusi akina Professor Mwandosya na baadhi kama Mathew luhanga walijifunza huko ulaya ufanyaji kazi yake na utengenezaji wake, Sorry Prof Mwandosya amestaafu na elimu yake wakati vijana kwanza hawaelewi hata maana ya Blockchain na wanaogopa kuwekeza huko

Artificial Intelligence( AI) ndio inatumika kwenye mambo yote kwa sasa ukiacha bara giza kama Tanzania, Upasuaji sasa umeanza kutumia Robots

Ni muda muafaka wa wazazi wenyewe kufanya maamuzi magumu ya kufundisha watoto mambo ya maisha na teknolojia na sio kupeleka kwenda kujifunza mambo yasiyo na msingi kwenye ulimwengu wa sasa

Nini maana ya mtoto kusoma Grade 1 mpaka Darasa la saba, Kuna kitu gani anaondoka nacho shule kwa miaka hiyo saba, Wazazi badilikeni

Wazazi wenye watoto wadogo bado mna muda wa kufundisha watoto mambo ya msingi kwenye teknolojia

Mwezi huu Desemba zaidi ya wanavyuo elfu tatu wamemaliza vyuo vikuu, Je kwa miaka minne au mitatu wamepata kitu gani cha maisha yao au ndio mambo ya Debit Cash and Credit Motor vehicle a/c

Tuwarithishe watoto wetu elimu yenye msingi mkuu na tuachane na elimu hii ya kusoma soma tu ili kumaliza miaka kadhaa

Kuna tofauti gani kati ya mwanachuo aliyemaliza chuo na mtu aliyeamua kutokusoma kabisa na akafanya biashara au akawa mwanasiasa na mbunge?

Tukiweka siasa pembeni kuna mambo ni jukumu la Mzazi mwenyewe na sio Serikali
Upo sahihi sana, kitu kimenishangaza kidogo una degrade kusoma coding, coding ndio foundation ya computer science, computer engineering, AI,..lazima watoto wajifunze coding language before anything else, hata Steve Jobs Ali stress umuhimu wa coding kwa kila mmarekani.
 
Sawa, Mkuu.

Nafikiri hukutakiwa kufika mbali. Ungeenda moja kwa moja sehemu iliyokusudia.

Wazee wako na wanao kutokusoma advance, sidhani kama ilikuwa na toka.

Nasikia hapo Dodoma wanatoa ph.D za mchongo. Kila la heri.
 
Sawa, Mkuu.

Nafikiri hukutakiwa kufika mbali. Ungeenda moja kwa moja sehemu iliyokusudia.

Wazee wako na wanao kutokusoma advance, sidhani kama ilikuwa na toka.

Nasikia hapo Dodoma wanatoa ph.D za mchongo. Kila la heri.
Hata ccm tunashinda kwa mbinu
 
Jaribu kujifunza mambo mapya unafahamu maana ya coding au Blockchain au AI?

Nina uhakika wewe hujui kitu na mbumbu kwenye mambo hayo

Huyo ni mwana ccm wa Oxford school of Economics na Mkinga kamili wa Makete

Anafahamu anachokifanya na kukiongea

Punguza hasira na Povu, Mambo ya vasco da Gama au Forced labor yana msaada gani?
Sikujua idadi ya wajinga (ignorants) ni kubwa hivi! Coding, blockachain and AI si mambo hata nimesema hayafai, nimeuliza tu kama kila mtu anapaswa kuyajua. Uko saihi kuwa sijui mambo hayo lakini niko sahihi kuwa siyahitaji kufanya ninachofanya katika maisha yangu na ndio maana nikauliza kama kila mtu anapaswa kuyafahamu.

Wewe pia ni mpumbavu (fool). Huyu kuwa mwanaCC au amesoma Oxford school of economics na ni mkinga au sio na anatoka Makete au kwingine ni mambo ambayo hayahusiani na arguments zangu. Waweza kuwa unamfahamu mleta mada personally, sidhani una uwezo wa kuthibitisha unafahamu anachofahamu na kukiongea. Jiwekee mipaka katika kutambua watu ili waache kukuwakilisha kama bendera fuata upepo. Wewe na wewe hamjaweza hata kuelezea mpaka sasa uhusiano wa hiyo coding, blockchain au AI na kujitegemea na kutojiamini. Go back to my points and address them. Hakuna sehemu nimeandika mambo ya Vasco da Gama au forced labour!! Stay focused when making learned argument.

I am a proud product of Warwick School of Business. And so what??? Narudia tena, wewe na mleta mada hamna soft skills!! Wala sio hasira, niko focused and straightforward - ndicho mnastahili. Na wewe unabaki kuwa irrelevant kwa sababu unashabikia tu anachosema na unajua hutakuwa anachotaka uwe au unachotamani. Mie ninasubiri uvumbuzi wake mpya katika eneo la AI atakapohitimu. Kujua AI ni nini haitoshi, kutumia AI ndio jambo la maana zaidi!!
 
Hivi tuna Centres of Research zenye vifaa vya kutosha?
Kuna vitu huwa nashindwaga kuelewa kwa elimu yetu.
 
Hivi tuna Centres of Research zenye vifaa vya kutosha?
Kuna vitu huwa nashindwaga kuelewa kwa elimu yetu.
Elimu yetu bado ina changamoto kubwa sana kuanzia kwenye muundo mpaka mahitaji. Elimu yetu haileti uvumbuzi! Hata wa vitu vidogo vidogo kabisa!! Lakini suluhisho lake sio elimu ya robotics, coding, blockchain wala AI PEKEE.

Kwangu mimi, ni lazima elimu itoke kuwa ya kila mtu kuipata ikawe ya kila mwenye kipaji kuendelezwa!! Elimu sio ufunguo wa maisha, kipaji ni.
 
Screenshot_20211216-074325~2.png
 
Kwa mambo yote uliyoandika sasa yamewekwa kwenye Artifial intelligence

Sheria zote na kesi zote zilizoamuliwa na calculations zote za possibility ya new Case zipo kwenye AI

Huwezi kwepa AI, Uwe Dakatari au Muhasibu mambo yote sasa ni AI

Miaka kadhaa ijayo hizi kazi za udaktari na sheria zitafanywa na AI

Facebook kama kampuni mpya ya Meta alishaanza kuwekeza huko na yupo hatua za mwisho

Mambo ya manual ndio kwaheri
Gussie, una hoja ya kupumbavu (hili sio tusi, ni kisifa cha hoja yako). Kuna uwezekano mkubwa sana uko ignorant si kwa jambo hili tu, bali mengi sana. AI is not a profession but a vehicle to make things EASIER na QUICKER huku ikipunguza makosa kwa sababu iko na consistency katika repetitive happenings!!

Bado unahitaji daktari kujua AI 'inapaswa' kufanya nini. Bado unahitaji design engineer kujua AI inapaswa kufanya nini. AI sio teknolojia ya ufahamu, ni teknojia ya utendaji/ufanyaji. AI system itafanya moja ya "possibilities". Ni hizo possibilities ndio zinazofanya professions mbali mbali ziendelee kuwepo.

Hujui AI zaidi ya kujua long form yake kuwa ni Artificial Intelligence na kuwa Meta wataanza kuitumia!! Kutakuwa na AI katika kila profession, inawezekana. Ambacho hakiwezekani ni kuwa AI systems hazitahitaji wabobezi katika fani husika. Na kama mleta mada, unakwepa kwa makusudi kuzungumzia jinsi AI inavoweza kukufanya usiwe tegemezi na mwenye kujiamini. Pathetic!!
 
Jukumu la elimu bora ni la Mzazi mwenyewe kuchagua aina ya elimu. kuendeleza elimu hii ya kikoloni ya kusoma kumaliza miaka au kubadilika kuwekeza kwenye elimu ya utambuzi na uvumbuzi yenye kumjengea mtoto kujiamini

Nipo Dodoma kwa sasa kutafuta PhD kama alama na sio kama uwezo

Wakati huo wenzangu wazazi wao wakiwasisitiza watoto wao wasome mambo ya Forced labour, Trigonometric, Integration by parts. Economics na Uhasibu

Mimi mzazi wangu alinipiga marufuku kusoma mambo hayo bali alininunulia Computer za kizamani sana zenye kutumia Floppy disk sio kama hizi za sasa za CD na Flash Disk

Kwa utu uzima wangu huu sikuwahi peleka watoto wangu Form five na Six hata Mimi sikuwahi soma form five na Six kwani mzazi hakunipitisha kwenye mfumo huo wa elimu na hata Yeye mzazi wangu mmoja wapo hakupitia mfumo huo wa Form five na Six

Miaka miwili ya Form five na Form Six iliniwezesha kufanya mambo kwa vitendo kama kujifunza kuagiza mizigo toka nje, Uwasilishwaji wa document muhimu kama vibali vya kuagiza bidhaa na uwezo wa kuunda Application tofauti

Coding Language ndio elimu ambayo mzazi alinifundisha kwa wakati huo, Niliharibu computer nyingi sana utotoni nikitaka kujua ndani ya computer kuna kitu gani tofauti na Radio au TV ambazo mara nyingi nilijua ndani kuna vitu gani

Coding language ndio kitu pekee nilikitumia kama fimbo ya kuchapia na kuweka mambo sawa kabla ya siasa, Watoto wangu wapo step moja mbele ya mimi hasa kwenye teknolojia

Wazazi smart baadhi Nawapongeza sana watoto wao wanapata hii elimu ya coding shule ya msingi kwa sasa. lakini kwa sasa coding imepitwa na wakati kidogo

Kwanini Mimi na wanangu tupo hapa Udom kwa sasa? Lengo letu ni PhD lakini kilichotuleta ni kuna vijana walipata tuzo kwenye mambo ya computer hasa kwenye "Hacking na Cyber Security" na ni wanafunzi wa kutoka Udom ndaki ya teknolojia hapa UDOM, Tunaamini kama hawa watoto wa wakulima wasio na vifaa na wana elimu ya kata wanajua vitu hivi basi moja kwa moja wana kitu cha ziada ambacho Mimi na wanangu hatuna au tunaweza ongeza nguvu nasi tukapata kitu kipya cha Uelekeo wa wajukuu zetu

Uelekeo wa Dunia sasa kwa wajukuu zetu hapa nyumbani ni Artificial Intelligence( AI). Tunajitahidi kuwekeza kwa watoto wa wanangu mambo ya AI na sio coding sana

Gharama ni kubwa sana sana kwenye haya mambo ya AI bali hatukati tamaa kwani hata Mimi mzazi hakukata tamaa juu yangu wala mimi sikukata tamaa kwa hawa vijana wangu nilionao hapa Dodoma kwa muda
Mambo ya Blockchain watu wanayojisumbua sana sasa ni mambo ambayo miaka ile ya dunia nyeusi akina Professor Mwandosya na baadhi kama Mathew luhanga walijifunza huko ulaya ufanyaji kazi yake na utengenezaji wake, Sorry Prof Mwandosya amestaafu na elimu yake wakati vijana kwanza hawaelewi hata maana ya Blockchain na wanaogopa kuwekeza huko

Artificial Intelligence( AI) ndio inatumika kwenye mambo yote kwa sasa ukiacha bara giza kama Tanzania, Upasuaji sasa umeanza kutumia Robots

Ni muda muafaka wa wazazi wenyewe kufanya maamuzi magumu ya kufundisha watoto mambo ya maisha na teknolojia na sio kupeleka kwenda kujifunza mambo yasiyo na msingi kwenye ulimwengu wa sasa

Nini maana ya mtoto kusoma Grade 1 mpaka Darasa la saba, Kuna kitu gani anaondoka nacho shule kwa miaka hiyo saba, Wazazi badilikeni

Wazazi wenye watoto wadogo bado mna muda wa kufundisha watoto mambo ya msingi kwenye teknolojia

Mwezi huu Desemba zaidi ya wanavyuo elfu tatu wamemaliza vyuo vikuu, Je kwa miaka minne au mitatu wamepata kitu gani cha maisha yao au ndio mambo ya Debit Cash and Credit Motor vehicle a/c

Tuwarithishe watoto wetu elimu yenye msingi mkuu na tuachane na elimu hii ya kusoma soma tu ili kumaliza miaka kadhaa

Kuna tofauti gani kati ya mwanachuo aliyemaliza chuo na mtu aliyeamua kutokusoma kabisa na akafanya biashara au akawa mwanasiasa na mbunge?

Tukiweka siasa pembeni kuna mambo ni jukumu la Mzazi mwenyewe na sio Serikali
Mzazi wako, Wewe na wanao bado hamjajielewa. Kuna vitu mnahitaji kuvijua lkn mnashindwa mtavijuaje.

Yes, mimi wanangu tunapoelekea, sitamani wasome elimu ambazo wamalizapo, wanatembea na bahasha kuomba kazi. Natamani wasome vitu real ambavyo wakimaliza, wavifanye, viwape ajira wao na watu wengine.

Tanzania ni maskini sababu fursa za kiuchumi tulizonazo hatujazitumia hata kwa theluthi tu. Na hii yote ni sababu ya elimu isiyohusu mazingira yetu.

Mtu kama mimi nimesoma sociology. Zaidi ya kuwaza cdo, hr, au mashirika, sina ninachoweza. Kifupi badala ya kusoma kufuta ujinga, mimi nimesoma kuongeza ujinga.

Mates wangu wa 1999 standard 7, waliojitambua leo hii, wana uchumi imara na wanaendesha maisha bila kuhofia kesho. Mimi mshahara ukikata tu, nakuwa kibaka
 
Moja ya nyuzi za kipumbavu kabisa kusoma katika miezi ya karibuni. Na sitaki mleta uzi unielewe vibaya. Nimechukulia uzi wako kama mambo mawili. Moja, umepata nafasi ya kujidai kuanzia kwa wazazi wako, wewe mwenyewe na hata watoto wako. Nitawaacha wazazi wako na watoto wako, nitajikita kwako! Pili, unasema unatafuta PhD kama ndio lengo ikiwa ni pamoja na kujifunza na kuongeza kwa ajili ya wajukuu zako. Umekiri mwenyewe hapa kuwa kwako PhD ni "prestige" ya labda uko wenu ili kuonesha kuanzia wazazi wako kuwa "form five na six" sio ngazi ya muhimu katika mfumo wa elimu. Nitakukumbusha yafuatayo:
1. Utakuwa mmoja wa waliosoma lakini sio walioelimika. Lengo la elimu yako ni kwa ajili ya wajukuu zako na sio taaluma husika. Impact yako katika dunia hii itakuwa ndogo sana.

2. Kwa aina na kiwango cha kufikiri, hukupaswa hata kuandika uliyoandika. Sina hakika ulimaanisha tuondoe elimu ya kidato cha tano na sita ili tuwe kama ulivokuwa wewe na wanao. Au ulimaanisha kusema role models wako "hao hackers" nao walipitia njia uliyopitia wewe au walienda form five na six. Na kama walipita vidato hivo, point yako wa form four inakuwa haina maana. Inabaki tu kuwa ni moja ya njia lakini not the best or even the least expensive in terms of both the time and finances. Unashauri waTanzania njia ya form four, niambe hapa ni chuo gani kinatoa degree kwa mwanafunzi anayetoka form four hapa nchini. Au unasema wamalize form four halafu wasome diploma kisha degree??

3. Kwa kushindwa kufahamu kuwa professions hutegemeana - hustahili hata kusoma kwa kiwango cha PhD. Unataka wote wasome AI. Nani awe mwanasheria, engineer, daktari, nk??

4. Mada yako ina maneno "tegemezi" na "wasiojiamini" katika kichwa cha habari. Kuna sehemu yoyote umeoanisha elimu yako au wazazi wako na watoto wako na kujiamini kwenu au kutokuwa tegemezi? Kujiamini ni nini hasa au tegemezi ni nini katika context ya elimu yenu? Kuwa watu waliosoma AI ndio wanaojitegemea au kujiamini na wengine si hivo? Au waliosoma form six ni tegemezi na wasiojiamini??

Wewe ni kiwakilishi cha watu wasiohitajika katika sehemu yoyote hapa duniani. Wale wasiotambua kuwa jamii ni "interdependent" na kuwa jamii inahitaji "kila mtu na anachojua". Huna soft skills, na hii itakufanya usiwe na uwezo hata wa kuchanganua mambo. Soft skills ni kitu muhimu kuliko hata hiyo PhD unayotafuta - na ninasikitika kuwa utakuwa "msomi" badala ya "aliyeelimika". Bado hujatambua mazingira yako na hivo huwezi kupambana nayo!!

What a waste of energy!!
Nakubaliana na wewe. Lkn kutegemeana kwenye professions lzm kuwe balanced. Moja ya sababu kwa nini kuna ujinga mwingi kwenye jamii zetu, ni matokeo ya kuwa na taaluma zisizodhibitiwa. Mfano unasoma sheria lengo uwe mwanasheria. Lkn unamaliza unakaa miaka mingi hujapata kazi yoyote ya sheria. Huoni ni kupoteza muda?

Mfano taaluma ambazo ni practical, ndizo ziwe na watu wengi, then hizi nyingine wawe wachache. Tunapenda uvivu sana na kula bila kufanya kazi
 
Jaribu kujifunza mambo mapya unafahamu maana ya coding au Blockchain au AI?

Nina uhakika wewe hujui kitu na mbumbu kwenye mambo hayo

Huyo ni mwana ccm wa Oxford school of Economics na Mkinga kamili wa Makete

Anafahamu anachokifanya na kukiongea

Punguza hasira na Povu, Mambo ya vasco da Gama au Forced labor yana msaada gani?
Huyu anavitu anahitaji lkn hajui atavipata wapi. Angalia walimu wake, nini wamefanya? Kwa nini apoteze muda kusoma PhD wakati anajua haitomsaidia bali status? Waliofanikiwa kwenye technology, hawana PhD, ni kujituma na kijaribu kufanya vitu.

Aache uoga, yeye akaendeleze kile anachoamini, udom hatokipata. Huko anasomea ujinga zaidi
 
Hua nashindwa kuwaelewa watu wanaolaumu mfumo wa elimu, haswa kwenye swala la uvumbuzi, kitu wasichielewa hawa wanaobeza mfumo wa elimu ni kwamba uvumbuzi haufundishwi popote pale uvumbuzi husababishwa na udadisi alionao binadamu...
Ndiyo maana nasema mleta hoja ni mwoga wa maisha, kuna vitu anahitaji kuvijua lkn hajui atavijuaje, matokeo yake anaenda kusoma PhD. Ujinga mtupu
 
Back
Top Bottom