TWisheshagi
Member
- May 2, 2020
- 14
- 209
TUNDU LISSU, huenda akawa ni miongoni mwa wanasiasa wenye bahati kubwa!
Ni mwanasiasa, anayenufaika sana na makosa ya wakubwa! Makosa ya wakubwa kwa kujua au kutokujua, kwa kushauriwa au kutokushauriwa vizuri yameanza kumjenga Tundu Lissu.
Awamu hii ya tano, imejenga marafiki wengi wa kificho na maadui wengi wa kificho. Marafiki wa kificho wa awamu hii ni wale wanaojituma kufanya kazi kwa niaba ya CCM au Serikali.
Lipo kundi jingine la marafiki wa kificho wao wanampenda zaidi Rais Magufuli, kuliko wanavyokipenda Chama cha Mapinduzi(CCM). Hawa wako wengi. Na kwa kipindi hiki, wanaojituma kufanya kila kitu wakidhani wanamnufaisha Rais.
Kwa uzoefu wangu mdogo wa mambo haya, ni kwamba kundi hili hujifanyia mambo yake bila kutumwa na mtu yoyote, wala taasisi yoyote yenye mamlaka. Lakini hutumia nembo au kichaka cha kutumwa ili waweze kuaminika.
Kila awamu ya utawala huwa na kundi kama hili. Tofauti ni kwamba awamu hii imezipiku awamu zote kuwa na makundi nje ya mfumo rasmi yanayoingiza mkenge watu na hata kuharibu taswira ya Rais!
Nitatoa mifano: Wakati wa hamahama za wabunge wa upinzani kwenda CCM, Kuna watu walijituma kufanya kazi hiyo ili kumfurahisha Rais. Haku kuwa na makubaliano maalum, bali wengi walio hama waliingizwa mkenge!
Rais alipewa taarifa kuwa watu hawa wanampenda na kumuunga mkono! Kuna kilio kikubwa huko kwa sasa! Na zahma kubwa linakuja endapo wakubwa wataamua kuwarejesha kwa nguvu wale wote waliokataliwa na Wajumbe. Hapo ndipo makosa ya wakubwa yatakapoanza kumnufaisha Tundu Lisu.
Hotuba za Lissu sasa zinazuiwa na watu ambao wanaojituma. Hawapendi Rais asemwe hata kama yeye binafsi anapenda kusikiliza maoni ya Lissu.
Chombo kikubwa kama ITV kufanya jambo la kijinga na kitoto kama hilo ni matokeo ya kundi hili kujipenyeza kila pahala kwa lengo la kumfurahisha Rais!
Badala ya kumsaidia Rais, Sasa wanamjenga Lissu! Pamoja na ukweli kuwa Tundu Lissu alisikika na kutikisa sana kipindi cha KIKWETE! Lakini katika awamu hii amejiongezea umaarufu maradufu!
Umaarufu wa Tundu Lissu, umeongezeka sana ndani ya siku chache! Wanaopenda kutukana mnakaribishwa, lakini huo ndiyo ukweli mchungu.
Hotuba za Lissu zinatafutwa kwa sababu wanaojituma wanamzimia maiki anapoongea. Naamini, wanaofanya hivi hawatumwi kufanya hivyo, bali wanajituma.
Na kwa sababu hata wakubwa hawakemei wala kukataa vitendo hivyo hadharani, basi wote wanashiriki hatua kwa hatua kumwimarisha Tundu Lisu.
Haiwezekani kama Chama, tufanye kazi kubwa ndani ya Miaka mitano. Tufanye kampeni sisi wenyewe, tuimarishe uchumi wetu, harafu tushindwe kuwa na hoja za kumjibu Tundu Lisu, ambaye hakuwepo nchini kwa muda mrefu mpaka tupate msaada wa watu wanaojituma kuzima maiki za Lissu ili asisikike!
Hapa Kuna tatizo! Makosa yetu wenyewe ndiyo yanamejenga Tundu Lissu.
Wahenge husema: Hata anayerudi nyuma, ana mbele yake anayo kwenda, japokuwa sisi tunaotizama tunaona anaelekea nyuma.
Ndimi Mkulima wa Bamia, Bonde la Mto Simiyu-Magu, Mwanza.
Ni mwanasiasa, anayenufaika sana na makosa ya wakubwa! Makosa ya wakubwa kwa kujua au kutokujua, kwa kushauriwa au kutokushauriwa vizuri yameanza kumjenga Tundu Lissu.
Awamu hii ya tano, imejenga marafiki wengi wa kificho na maadui wengi wa kificho. Marafiki wa kificho wa awamu hii ni wale wanaojituma kufanya kazi kwa niaba ya CCM au Serikali.
Lipo kundi jingine la marafiki wa kificho wao wanampenda zaidi Rais Magufuli, kuliko wanavyokipenda Chama cha Mapinduzi(CCM). Hawa wako wengi. Na kwa kipindi hiki, wanaojituma kufanya kila kitu wakidhani wanamnufaisha Rais.
Kwa uzoefu wangu mdogo wa mambo haya, ni kwamba kundi hili hujifanyia mambo yake bila kutumwa na mtu yoyote, wala taasisi yoyote yenye mamlaka. Lakini hutumia nembo au kichaka cha kutumwa ili waweze kuaminika.
Kila awamu ya utawala huwa na kundi kama hili. Tofauti ni kwamba awamu hii imezipiku awamu zote kuwa na makundi nje ya mfumo rasmi yanayoingiza mkenge watu na hata kuharibu taswira ya Rais!
Nitatoa mifano: Wakati wa hamahama za wabunge wa upinzani kwenda CCM, Kuna watu walijituma kufanya kazi hiyo ili kumfurahisha Rais. Haku kuwa na makubaliano maalum, bali wengi walio hama waliingizwa mkenge!
Rais alipewa taarifa kuwa watu hawa wanampenda na kumuunga mkono! Kuna kilio kikubwa huko kwa sasa! Na zahma kubwa linakuja endapo wakubwa wataamua kuwarejesha kwa nguvu wale wote waliokataliwa na Wajumbe. Hapo ndipo makosa ya wakubwa yatakapoanza kumnufaisha Tundu Lisu.
Hotuba za Lissu sasa zinazuiwa na watu ambao wanaojituma. Hawapendi Rais asemwe hata kama yeye binafsi anapenda kusikiliza maoni ya Lissu.
Chombo kikubwa kama ITV kufanya jambo la kijinga na kitoto kama hilo ni matokeo ya kundi hili kujipenyeza kila pahala kwa lengo la kumfurahisha Rais!
Badala ya kumsaidia Rais, Sasa wanamjenga Lissu! Pamoja na ukweli kuwa Tundu Lissu alisikika na kutikisa sana kipindi cha KIKWETE! Lakini katika awamu hii amejiongezea umaarufu maradufu!
Umaarufu wa Tundu Lissu, umeongezeka sana ndani ya siku chache! Wanaopenda kutukana mnakaribishwa, lakini huo ndiyo ukweli mchungu.
Hotuba za Lissu zinatafutwa kwa sababu wanaojituma wanamzimia maiki anapoongea. Naamini, wanaofanya hivi hawatumwi kufanya hivyo, bali wanajituma.
Na kwa sababu hata wakubwa hawakemei wala kukataa vitendo hivyo hadharani, basi wote wanashiriki hatua kwa hatua kumwimarisha Tundu Lisu.
Haiwezekani kama Chama, tufanye kazi kubwa ndani ya Miaka mitano. Tufanye kampeni sisi wenyewe, tuimarishe uchumi wetu, harafu tushindwe kuwa na hoja za kumjibu Tundu Lisu, ambaye hakuwepo nchini kwa muda mrefu mpaka tupate msaada wa watu wanaojituma kuzima maiki za Lissu ili asisikike!
Hapa Kuna tatizo! Makosa yetu wenyewe ndiyo yanamejenga Tundu Lissu.
Wahenge husema: Hata anayerudi nyuma, ana mbele yake anayo kwenda, japokuwa sisi tunaotizama tunaona anaelekea nyuma.
Ndimi Mkulima wa Bamia, Bonde la Mto Simiyu-Magu, Mwanza.