Uchaguzi 2020 Makosa ya wakubwa yanavyomnufaisha Tundu Lissu

Nafikiri ITV na vyombo vingine vya mitandaoni siyo wanajipendekeza au wanajituma kumfurahisha JPM.
Kinachotokea hivyo vyombo vinamjua Lissu hachelewi kutoa kauli zinazoweza kupelekea kuwaingiza matatani vyombo usika kwa kurusha matangazo ambayo yanaweza kutafsiriwa kama uchochezi au ya uvunjifu wa sheria kwa mujibu wa leseni za urushaji matangazo. Ngumu kuhariri matangazo yanayorushwa mubashara (live), na Lissu is very unpredictable kwakweli, muda wowote anaweza kurusha maneno makali sana.

Mhariri wa gazeti flani ana kesi ya kujibu mahakamani sababu ya kuchapisha kauli au maneno flani ya Lissu. Kila siku kushinda mahakamani na kuwalipa wanasheria sababu ya kutaka kuwafurahisha watu wa chama flani ni uzembe katika biashara. Mara kadhaa tumesikia vyombo kama Clouds FM wakipigwa faini sababu ya maneno au simulizi flani ya mmoja wa watu walio alikwa kwenye kipindi cha njia panda!!

Kila mtu anajua jinsi TCRA inavyo zilima faini kubwa vyombo vya habari kwa kurusha vitu vinavyo tafsiriwa kama uvunjivu wa sheria na maadili.

ITV na media zote they are playing smarty kama ujuavyo sasa biashara ngumu na faini wanazolipa zinawaumiza zaidi wao kama biashara.

Ukumbuke mwisho wa siku zile ni biashara kama biashara zingine siyo charity organizations.
Chini ya hizi sheria kandamizi za kinyangogo kiukweli lazima wakae karibu na swichi hasa pale MWANAUME LISSU AKIONGEA, hizi sheria za kipuuzi ni za kuongozea ng'ombe na siyo watu na akili zao kama LISSU ndo maana wanapata taabu tangu bwana wa burigi akamate usukani li nchi limekuwa la hovyo hovyo ngoja wanyooshwe na mnyooshaji mh. LISSU keshatia maguu.
 
Nani alimpa Rais watu wa hovyo wasiomshauri vizuri? Huyo aliyempa washauri hao hovyo maelfu kati ya Raia milioni 50 alikosa kuchagua washauri mahili hata 50 tu wamsaidie Rais? Wananchi mtaani wanaona kipenzi chao kinavyodhalilishwa na washauri hovyo, yeye haoni na akawatumbua pamoja na hao wanaompatia hao wasaidizi hovyo? Alipoingia tu madarakani alitumbua washauri wengi aliyowakuta kusafisha nyumba, bado hajagundua alitupa jalalani nafaka akabakiza mabua bila chakula? Katika kupata washauri wazuri akaanza kuteua washauri wake mwenyewe, mbona hali bado vilevile hadi kusababisha teua/tengua ya kila siku?

Tatizo la mzee wa chattle ni misifa, aliteua walevi wa baa kwa hila na sifa alifukuza watu wengi wenye weled na kuweka makanjanja kama yule bwana aliyeruka tikitaka na taulo kule jimboni kigamboni kabla wajumbe hawajamshughulikia, pia kujifanya kuwa ana akili nyingi kisa kukariri idadi ya mayai ya samaki ziwa tanganyika akavuruga nchi.

Njaa ikatamalaki hadi ndani ya ccm, hali ikawa mbaya kila wakati utasikia habari za Bombardia, ndege inakuja kutoka Canada mawaziri wote na makatibu wakuu wanaacha kazi wanaandamana kwenda uwanja wa ndege kuipokea, ushamba uliopitiliza.
 
Eti w
Thread bora kabisa kwa siku ya leo. Hongera sana mleta mada kwa thread hii. Wewe unastahili kuwa kwenye jukwaa hili la great thinkers

Nikiwa bado CCM kabla sijahama niliwai kusema haya. Vyombo vya dola, serikali na mawakala uchwara wa CCM ndiyo waliomjenga Lissu kisiasa.

Hakukuwa na haja ya kumfungulia Lissu Mashtaka ya uchochezi mahakamani. Lile lilikuwa kosa la kwanza, kesi zilimbeba Lissu. Kila akienda Mahakamani waandishi walikuwa wanamfuata na akazidi kusikika na kupendwa zaidi.

Alivyozidi kupendwa wakafanya kosa la pili kumpiga risasi. Hapa ndo walikosea kupindukia kwa sababu vyovyote vile labda angekufa. Kupona kwake hata watu wasiomuamini Mungu wanachukulia kuwa ni miujiza.

Kibaya zaidi hawa watu hawajifunzi kamwe, Lissu karudi mikutano inayomuhusu hawaioneshi, wakionyesha wanamzimia sauti. Haya yanamjenga Lissu kisiasa mara 1000 zaidi.

Kwa jinsi Lissu anavyoonewa mchana kweupe hili linaongeza mapenzi kwake mara 1000 zaidi na tunapoelekea Lissu atakuwa na nguvu hata ya kuwaambia watu waingie mtaani kufanya maandamano na watu wakamsikiliza kweli na wanafanya.

Nilichojifunza ni kuwa Magufuli alitakiwa awe na wasaidizi wenye akili kubwa, busara na hekima sana na kubwa zaidi ndo wawe watu wa kumuelekeza cha kufanya. Ila hakupata hawa watu akapata watu wanaojipendekeza kwake


Tatizo alipata watu wa hovyo wasiomshauri vizuri na matokeo yake Lissu amejengwa vizuri na mwisho lazima amuangushe magufuli
Eti washauli wamekuwa kina polepole na Tid.
 
Alionewa na nani? Huo ni mshahara aliolipwa kwa kuwahadaa wengine waingie kwenye madhila ya maandamano, kumbe yeye anasubiri mabilioni ya EL.

Bado haja pata fundisho. Hotuba zake mara zote ni kuhimiza maandamano.
Maandamano ni haki ya kila raia duniani kote, ni sawa na kwenda mahakamani kutafta haki.Sasa unapomzuia mtu asiende mahakamani kutafta haki yake sina hakika kama utakuwa njema kichwani.
 
Maandamano ni haki ya kila raia duniani kote, ni sawa na kwenda mahakamani kutafta haki.Sasa unapomzuia mtu asiende mahakamani kutafta haki yake sina hakika kama utakuwa njema kichwani.

Baada ya muda si mrefu utasema Ushoga ni haki ya kila rai ulimwenguni. USA wanastrugle wakati huu kuvunja maandamano baada ya kuruhusu uhuru holela.
 
Baada ya muda si mrefu utasema Ushoga ni haki ya kila rai ulimwenguni. USA wanastrugle wakati huu kuvunja maandamano baada ya kuruhusu uhuru holela.
Hata hakimu anastrugle ili kutoa hukumu, kuhusu ushoga usinilishe maneno, kama we kweli ni kidume simama uupige marufuku huo ushoga.
 
TUNDU LISSU, huenda akawa ni miongoni mwa wanasiasa wenye bahati kubwa!

Ni mwanasiasa, anayenufaika sana na makosa ya wakubwa! Makosa ya wakubwa kwa kujua au kutokujua, kwa kushauriwa au kutokushauriwa vizuri yameanza kumjenga Tundu Lissu.

Awamu hii ya tano, imejenga marafiki wengi wa kificho na maadui wengi wa kificho. Marafiki wa kificho wa awamu hii ni wale wanaojituma kufanya kazi kwa niaba ya CCM au Serikali.

Lipo kundi jingine la marafiki wa kificho wao wanampenda zaidi Rais Magufuli, kuliko wanavyokipenda Chama cha Mapinduzi(CCM). Hawa wako wengi. Na kwa kipindi hiki, wanaojituma kufanya kila kitu wakidhani wanamnufaisha Rais.

Kwa uzoefu wangu mdogo wa mambo haya, ni kwamba kundi hili hujifanyia mambo yake bila kutumwa na mtu yoyote, wala taasisi yoyote yenye mamlaka. Lakini hutumia nembo au kichaka cha kutumwa ili waweze kuaminika.

Kila awamu ya utawala huwa na kundi kama hili. Tofauti ni kwamba awamu hii imezipiku awamu zote kuwa na makundi nje ya mfumo rasmi yanayoingiza mkenge watu na hata kuharibu taswira ya Rais!

Nitatoa mifano: Wakati wa hamahama za wabunge wa upinzani kwenda CCM, Kuna watu walijituma kufanya kazi hiyo ili kumfurahisha Rais. Haku kuwa na makubaliano maalum, bali wengi walio hama waliingizwa mkenge!

Rais alipewa taarifa kuwa watu hawa wanampenda na kumuunga mkono! Kuna kilio kikubwa huko kwa sasa! Na zahma kubwa linakuja endapo wakubwa wataamua kuwarejesha kwa nguvu wale wote waliokataliwa na Wajumbe. Hapo ndipo makosa ya wakubwa yatakapoanza kumnufaisha Tundu Lisu.

Hotuba za Lissu sasa zinazuiwa na watu ambao wanaojituma. Hawapendi Rais asemwe hata kama yeye binafsi anapenda kusikiliza maoni ya Lissu.

Chombo kikubwa kama ITV kufanya jambo la kijinga na kitoto kama hilo ni matokeo ya kundi hili kujipenyeza kila pahala kwa lengo la kumfurahisha Rais!

Badala ya kumsaidia Rais, Sasa wanamjenga Lissu! Pamoja na ukweli kuwa Tundu Lissu alisikika na kutikisa sana kipindi cha KIKWETE! Lakini katika awamu hii amejiongezea umaarufu maradufu!

Umaarufu wa Tundu Lissu, umeongezeka sana ndani ya siku chache! Wanaopenda kutukana mnakaribishwa, lakini huo ndiyo ukweli mchungu.

Hotuba za Lissu zinatafutwa kwa sababu wanaojituma wanamzimia maiki anapoongea. Naamini, wanaofanya hivi hawatumwi kufanya hivyo, bali wanajituma.

Na kwa sababu hata wakubwa hawakemei wala kukataa vitendo hivyo hadharani, basi wote wanashiriki hatua kwa hatua kumwimarisha Tundu Lisu.

Haiwezekani kama Chama, tufanye kazi kubwa ndani ya Miaka mitano. Tufanye kampeni sisi wenyewe, tuimarishe uchumi wetu, harafu tushindwe kuwa na hoja za kumjibu Tundu Lisu, ambaye hakuwepo nchini kwa muda mrefu mpaka tupate msaada wa watu wanaojituma kuzima maiki za Lissu ili asisikike!

Hapa Kuna tatizo! Makosa yetu wenyewe ndiyo yanamejenga Tundu Lissu.

Wahenge husema: Hata anayerudi nyuma, ana mbele yake anayo kwenda, japokuwa sisi tunaotizama tunaona anaelekea nyuma.

Ndimi Mkulima wa Bamia, Bonde la Mto Simiyu-Magu, Mwanza.
Aisee umeongea ukweli machungu sana lakini hio ndio hali halisi, huyu Lisu ilivyo ni mwiba machungu sana, fikiria kwamba jamaa walimuaminisha mh kuwa upinzani umekufa lakini ionekanavyo sasa upinzani ni zaidi ya mwaka 2015.
 
Nafikiri ITV na vyombo vingine vya mitandaoni siyo wanajipendekeza au wanajituma kumfurahisha JPM.
Kinachotokea hivyo vyombo vinamjua Lissu hachelewi kutoa kauli zinazoweza kupelekea kuwaingiza matatani vyombo husika kwa kurusha matangazo ambayo yanaweza kutafsiriwa kama uchochezi au ya uvunjifu wa sheria kwa mujibu wa leseni za urushaji matangazo. Ngumu kuhariri matangazo yanayorushwa mubashara (live), na Lissu is very unpredictable kwakweli, muda wowote anaweza kurusha maneno makali sana.

Mhariri wa gazeti flani ana kesi ya kujibu mahakamani sababu ya kuchapisha kauli au maneno flani ya Lissu. Kila siku kushinda mahakamani na kuwalipa wanasheria sababu ya kutaka kuwafurahisha watu wa chama flani ni uzembe katika biashara. Mara kadhaa tumesikia vyombo kama Clouds FM wakipigwa faini sababu ya maneno au simulizi flani ya mmoja wa watu walio alikwa kwenye kipindi cha njia panda!!

Kila mtu anajua jinsi TCRA inavyo zilima faini kubwa vyombo vya habari kwa kurusha vitu vinavyo tafsiriwa kama uvunjivu wa sheria na maadili.

ITV na media zote they are playing smart kama ujuavyo sasa biashara ngumu na faini wanazolipa zinawaumiza zaidi wao kama biashara.

Ukumbuke mwisho wa siku zile ni biashara kama biashara zingine siyo charity organizations.
Ni yeye 2020
 
Na
Kwa wanamtandao, Lissu anaonekana ni nyota iliyowadondokea

Kwa wachambuzi wa siasa na wasomi waliobobea kiufahamu, Lissu si mwanasiasa, wala si mwanaharakati, ila ni mtu anajifanya mjuaji - hajui kama hajui

Kwa wapiga kura, Lissu ni mmoja wa mavuvuzela wa wagombea

Lissu amejimaliza mwenyewe kabla ya kupanda kwenye jukwaa la kampeni, labda abadili kauli zake.
Naona unateseka sana, vumilia tu Lissu awanyooshe waimba mapambio na yesu wao wa chato
 
Back
Top Bottom