Makosa ya Karume Kuhusu Muungano!!

Buchanan

JF-Expert Member
May 19, 2009
13,199
1,969
Wakuu,
Mpaka sasa inaonekana kama vile Hayati Julius K. Nyerere ndiye "mkosaji pekee" katika kile kinachodaiwa kuwa ni "UBATILI" wa Muungano! Mwenzake Hayati Karume anaonekana yuko innocent kabisa au labda ni kuogopa ile "dhambi" iliyowahi kutamkwa na Baba wa Taifa mwenyewe kuwa ni "kuogopa kuwaudhi Wazanzibari!"
Kwa maoni yangu mzigo wote wa lawama unatakiwa aubebe Karume, kwa nini?
1. Kwa sababu hakupeleka Hati za Makubaliano Ya Muungano kwenye Baraza la Mapinduzi kuridhiwa! Hili hata hivyo kwangu mimi si tatizo kuhusu UHALALI wa Muungano, kwa kuwa kuridhia sio lazima kusaini, hata kwa "conduct" tu inatosha! Kama wengine mnaamini katika kusaini basi mzigo huo anapaswa aubebe Karume!
Sidhani kama ilikuwa kazi ya Nyerere kuanza kuwahoji Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi kuwa mmeridhia au la, hayo yalikuwa yafanywe na Karume!
2. Karume alipokea cheo cha Makamu wa Kwanza wa Rais hata bila kuridhiwa kwa Hati huko Zanzibar! Sioni hapa kosa la Nyerere liko wapi!
3. Kutwaa Mamlaka ya Zanzibar taratibu. Mamlaka haya hayakutwaliwa bila ridhaa ya Karume na Marais waliofuata. Kila kitu kilifanyika kwa makubaliano na kwa ridhaa ya Karume, Marais waliofuata pamoja na Wazanzibari wote! Sasa haya matusi dhidi ya Baba wa Taifa, Mwl Julius K. Nyerere yanatoka wapi?
4. Kwa kweli kama tumeamua "kufunguka" tuwe wakweli, isionekane kwamba Wazanzibari waliduwaa kama kondoo wakati masuala mbalimbali ya Muungano yanafanyika!
5. Sisemi Karume atukanwe kama alivyofanyiwa Hayati Nyerere la hasha bali lawama zilenge mhusika, kama ni lazima sana kulaumu!
 
Kuna ile dhana kwamba Tanganyika imeimeza Zanzibar, pengine ndiyo sababu lawama zote anaelekezewa Mwl. Nyerere. Inaonekana Mwl ndiye ali play part kubwa sana kumshawishi Mzee Karume kuridhia Muungano.

Lakini jambo la msingi la kujiuliza ni kwa nini Mzee Karume alikubali haraka haraka Muungano hata bila ya kushirikisha baraza la Mapinduzi (kama kweli hakuwashirikisha)

Yawezekana kabisa uwepo wa serikali ya Muungano ulisaidia sana kuyalinda mapinduzi, na kwa hali iliyojionyesha bungeni bmk, lazima Muungano uendelee, vinginevyo hakutakuwa na Zanzibar tunayoiona sasa.

Swali la kujiuliza ni je, ni muungano upi ambao utaihakikishia Zanzibar iendelee kuwepo? Je ni huu wa serikali mbili? Au ni ule wa serikali tatu. Jambo la kushangaza zaidi ni kwamba Watanganyika Inaonekana wanawapenda sana ndugu zao wa Zanzibar kuliko wazanzibar wanavyowapenda Watanganyika maana kwa msisitizo ule ule, "Nje ya Muungano hakuna Zanzibar"

Siku zote mkubwa ni jalala na ndiyl sababu Mwl. Hana budi kulaumiwa na wale wasiopenda muungano.
 
Watu wooote hapa wamebaki kumtupia matusi Mwl. Nyerere huku wakisahau kwamba hati hiyo hakuisaini mwenyewe na wala hakufanya kidikteta km ibavyotafsiriwa. Kila mmoja alikuwa na wajibu wake ktk kufanikisha Muungano huu. Sasa tu'focus kwny kuangalia suluhisho la kero hizi zinazoukabili muungano wetu. LAWAMA HAZIJENGI!!!!
 
Watu wooote hapa wamebaki kumtupia matusi Mwl. Nyerere huku wakisahau kwamba hati hiyo hakuisaini mwenyewe na wala hakufanya kidikteta km ibavyotafsiriwa. Kila mmoja alikuwa na wajibu wake ktk kufanikisha Muungano huu. Sasa tu'focus kwny kuangalia suluhisho la kero hizi zinazoukabili muungano wetu. LAWAMA HAZIJENGI!!!!

Nakubaliana na wewe mkuu, tu-focus ya mbele bila ya kufukua ya nyuma ambayo yatatuharibia zaidi kuliko kutusaidia!
 
Hati ya muungano mbona hata mimi ninayo
hati ya muungano ni katiba ya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo imepitishwa na bunge lenye wabunge wan kutoka tanganyika na zanzibar na kuridhiwa na baraza la wawakilishi.Hiyo ndio hati ya kisheria ya muungano.Zingine zote porojo zikiwemo za mleta mada
 
"Sisi watanganyika, kule sisi wazanzibar. Baada ya hapo itakuja "sisi wa-Unguja, kule sisi Wapemba".

Ndugu Wazanzibar ikiwa sasa hivi mnabaguana waunguja na wapemba kwa sababu ya vyama, je ikitokea Zanzibar ikiwa taifa si mtameguka vipande vipande kama alivyosema Hayati Mwl. Julius Nyerere?

Tafakarini, ila mtoto akililia wembe apatiwe tu, hamna namna. Tutapata chanzo kipya cha mapato kwa pande zote mbili...sukari yao tutalipa kodi, wao kuanzia mkaa, mchanga, umeme nk
 
"Sisi watanganyika, kule sisi wazanzibar. Baada ya hapo itakuja "sisi wa-Unguja, kule sisi Wapemba".

Ndugu Wazanzibar ikiwa sasa hivi mnabaguana waunguja na wapemba kwa sababu ya vyama, je ikitokea Zanzibar ikiwa taifa si mtameguka vipande vipande kama alivyosema Hayati Mwl. Julius Nyerere?

Tafakarini, ila mtoto akililia wembe apatiwe tu, hamna namna. Tutapata chanzo kipya cha mapato kwa pande zote mbili...sukari yao tutalipa kodi, wao kuanzia mkaa, mchanga, umeme nk

Fear mongering at its best!
 
Back
Top Bottom