- baadhi ya wasichana huyaelekeza macho yao kwa wanaume matajiri wakisahau kuwa hakuna mtu aliyezaliwa na utajiri bali hata masikini wa leo anaweza kuwa tajiri baadae.
- baadhi ya wasichana wanapenda na kutamani kuwa na wanaumme wazuri sana kuliko wote amabao hawapo.
- baadhi ya wasichana hawajishughulishi kabisa na kujiweka katika hali ya kuvutia wakiamini kwamba mungu atawaletea tu. Hata wawe na tabia nzuri au mbaya.
- baadhi ya wasichana wakivishwa pete na baadae kutelekezwa na kuachwa huamini kuwa wanaume wote duniani hawafai tena na huwachukia wanaume wote.
- baadhi ya wasichana wanajifanya ni wa daraja la juu sana na mwishowe hufanya kiburi na hatimae wanaume wanawakwepa.
- baadhi ya wasichana wana tatizo la kutokujiamini na wanawaogopa wanaume kupita kiasi.
- baadhi ya wasichana wanapenda kuolewa na watu wa kabila lao au watu kutoka kijiji kimoja ambayo , ambapo pale mahala wanapoishi kwa sasa huwa vigumu kupatikana !!!