Makosa Matatu ya Salum Mayanga na Hatma ya Stars

Baba Kiki

JF-Expert Member
May 31, 2012
1,544
940
Salum Mayanga ni kocha ambaye amekonga mioyo ya Watanzania kwa muda mfupi kutokana na kuunda Taifa Stars mpya ya vijana wadogo wenye vipaji vikubwa na ari ya kucheza soka. Amebadilisha mfumo kutoka ule wa kubutuabutua hadi kuweka mpira chini kwa pasi nyingi na kucheza kwa kushambulia zaidi. Kifupi binafsi nimetokea kuwa shabiki wake, japo katika mechi 3 alizosimamia Tiafa Stars amenifanya hofu niliyokuwa nayo baada ya mechi zile mbili za kirafiki dhidi ya Botswana na Burundi ithibitike leo. Pamoja na mpira kuwa na matokeo 3 sikuzote lakini sare ya leo ya Taifa Stars vs Lesotho imechangiwa kwa kiasi kikubwa na makosa makubwa matatu aliyofanya Salum Mayanga kama kocha.

1. UPANGAJI MBOVU WA KIKOSI

Nimekuwa nikishangaa sana Taifa Stars kucheza bila kuwa na mchezaji au mfumo wa kumchezesha Samatta. Tangu alipotoka Haruna Moshi Boban, tumekuwa hatuna mshambuliaji mzuri wa pili ili anayeweza kupangua ngome au kupiga pasi za kuifungua defence ya timu pinzani na kutoa pasi za magoli kwa Samatta. Ajibu angeweza kufanya hili lakini bado anakaa sana na mpira bila sababu, lakini yeye ni afadhali kuliko wengine. Navutiwa sana na Kichuya akicheza kulia kama anavyotumika akiwa Simba na alivyokuwa Mtibwa. Wanapangwa Mao Mkami na Muzamiri Yahaya lakini wote licha ya commitment zao kuwa kubwa, hawalainishi mipira ndio maana inabidi Samatta atumie muda mwingi kukaa na mpira atoe pasi kisha awahi mbele yeye mwenyewe kutafuta nafasi za kufunga! Mayanga jaribu kuwachezesha Mao, Muzamir na mmoja kati ya Ndemla au Sureboy halafu ushambuliaji waache Samatta na Mbaraka na winga mmoja tu kati ya Kichuya na Msuva.

2. KUCHELEWA KUBADILISHA MBINU ZA MCHEZO

Mayanga umeona kabisa Taifa Stars ilikuwa ikitawala mchezo lakini bila kutengezea nafasi za kutosha. Ulimwengu aliyecheza leo sio yule tunayemjua, Msuva alipoteza uelekeo toka mwanzo wa mchezo na idara ya kiungo ilizidiwa idadi na maarifa na kiungo cha Lesotho. Timu imecheza mfumo huohuo hadi zaidi ya dkk 75 huku ikiwa imedhibitiwa kabisa eneo la kiungo lakini Mayanga hakuonesha ile urge ya kulazimisha ushindi. Ajabu ni kuwa Majanga amesubiri hadi karibia dkk za mwisho wa mchezo kufanya mabadiliko tena yasiyokuwa ya kiufundi kabisa. Alitoa winga akaingiza winga, akatoa kiungo akaingiza kiungo, akatoa mshambuliaji akaongeza mshambuliaji! Kimsingi kwa jinsi Lesotho ilivyokuwa inacheza kwa kukaba njia alipaswa kuondoa winga mmoja mapema kabisa kati ya Kichuya na Msuva na kuingiza kiungo aina ya Salumu Abubakari au Said Ndemla ili idadi na pia kuongeza ubunifu eneo la katikati ya uwanja. Pia Mayanga anajua silaha ya Msuva ni kasi maana si mpigaji chenga mzuri, alipaswa kupanua uwanja ili kutengeneza nafasi za yeye kukimbia na kupiga krosi-pasi. Msuva leo hajatengeza nafasi hata moja, kitu ambacho ni habari mbaya mno. Ulimwengu alikuwa mzito kiasi, na Lesohto wanakasi kutokana na maumbile yao, Mbaraka Yusufu alipaswa kuingia mapema zaidi.

Mayanga ongeza ufanisi wa kikosi chako kwa kufanya Msuva na Kichuya wagombanie namba, wasicheze pamoja. Ule utofauti wao unaweza kuleta kitu kipya ndani ya mechi kwa mfano anapoanza mmoja na baadae akaingia mwingine inaweza kuleta utofauti mkubwa.

3. KUKAA KIMYA MUDA WOTE WA MCHEZO

Mayanga ni kocha mwenye uwezo mkubwa ila uko too quite, too passive! Ukikaa umekaa utadhani unasimamia timu iliyosheheni professionals! Kama Zidane anaweza kusimama kuwaelekeza wachezaji aina ya Christiano Ronaldo na Ramos, itakuwa Taifa Stars? Defence imefanya makosa mengi sana ya kujirudia, hadi hatimaye wakafungwa goli wewe ukiwa umekaa tu. Kwa Taifa Stars hii na wachezaji wa Kitanzania kwa ujumla subiri majanga zaidi kama utaendelea na utamaduni huo. Wanahitaji kukumbushwa mara kwa mara na wakati mwingine kuwapanga kabisa na hata kufoka. Hakuna kocha yoyote makini ataona walinzi wake wanarudia makosa yaleyale yeye akiwa amekaa ansubiri eti half time!

Sina nia ya kukupangia, lakini hii timu ni yetu sote, so pokea hii feedback. Tukishindwa mwaka huu basi tena
 
Salum Mayanga ni kocha ambaye amekonga mioyo ya Watanzania kwa muda mfupi kutokana na kuunda Taifa Stars mpya ya vijana wadogo wenye vipaji vikubwa na ari ya kucheza soka. Amebadilisha mfumo kutoka ule wa kubutuabutua hadi kuweka mpira chini kwa pasi nyingi na kucheza kwa kushambulia zaidi. Kifupi binafsi nimetokea kuwa shabiki wake, japo katika mechi 3 alizosimamia Tiafa Stars amenifanya hofu niliyokuwa nayo baada ya mechi zile mbili za kirafiki dhidi ya Botswana na Burundi ithibitike leo. Pamoja na mpira kuwa na matokeo 3 sikuzote lakini sare ya leo ya Taifa Stars vs Lesotho imechangiwa kwa kiasi kikubwa na makosa makubwa matatu aliyofanya Salum Mayanga kama kocha.

1. UPANGAJI MBOVU WA KIKOSI

Nimekuwa nikishangaa sana Taifa Stars kucheza bila kuwa na mchezaji au mfumo wa kumchezesha Samatta. Tangu alipotoka Haruna Moshi Boban, tumekuwa hatuna mshambuliaji mzuri wa pili ili anayeweza kupangua ngome au kupiga pasi za kuifungua defence ya timu pinzani na kutoa pasi za magoli kwa Samatta. Ajibu angeweza kufanya hili lakini bado anakaa sana na mpira bila sababu, lakini yeye ni afadhali kuliko wengine. Navutiwa sana na Kichuya akicheza kulia kama anavyotumika akiwa Simba na alivyokuwa Mtibwa. Wanapangwa Mao Mkami na Muzamiri Yahaya lakini wote licha ya commitment zao kuwa kubwa, hawalainishi mipira ndio maana inabidi Samatta atumie muda mwingi kukaa na mpira atoe pasi kisha awahi mbele yeye mwenyewe kutafuta nafasi za kufunga! Mayanga jaribu kuwachezesha Mao, Muzamir na mmoja kati ya Ndemla au Sureboy halafu ushambuliaji waache Samatta na Mbaraka na winga mmoja tu kati ya Kichuya na Msuva.

2. KUCHELEWA KUBADILISHA MBINU ZA MCHEZO

Mayanga umeona kabisa Taifa Stars ilikuwa ikitawala mchezo lakini bila kutengezea nafasi za kutosha. Ulimwengu aliyecheza leo sio yule tunayemjua, Msuva alipoteza uelekeo toka mwanzo wa mchezo na idara ya kiungo ilizidiwa idadi na maarifa na kiungo cha Lesotho. Timu imecheza mfumo huohuo hadi zaidi ya dkk 75 huku ikiwa imedhibitiwa kabisa eneo la kiungo lakini Mayanga hakuonesha ile urge ya kulazimisha ushindi. Ajabu ni kuwa Majanga amesubiri hadi karibia dkk za mwisho wa mchezo kufanya mabadiliko tena yasiyokuwa ya kiufundi kabisa. Alitoa winga akaingiza winga, akatoa kiungo akaingiza kiungo, akatoa mshambuliaji akaongeza mshambuliaji! Kimsingi kwa jinsi Lesotho ilivyokuwa inacheza kwa kukaba njia alipaswa kuondoa winga mmoja mapema kabisa kati ya Kichuya na Msuva na kuingiza kiungo aina ya Salumu Abubakari au Said Ndemla ili idadi na pia kuongeza ubunifu eneo la katikati ya uwanja. Pia Mayanga anajua silaha ya Msuva ni kasi maana si mpigaji chenga mzuri, alipaswa kupanua uwanja ili kutengeneza nafasi za yeye kukimbia na kupiga krosi-pasi. Msuva leo hajatengeza nafasi hata moja, kitu ambacho ni habari mbaya mno. Ulimwengu alikuwa mzito kiasi, na Lesohto wanakasi kutokana na maumbile yao, Mbaraka Yusufu alipaswa kuingia mapema zaidi.

Mayanga ongeza ufanisi wa kikosi chako kwa kufanya Msuva na Kichuya wagombanie namba, wasicheze pamoja. Ule utofauti wao unaweza kuleta kitu kipya ndani ya mechi kwa mfano anapoanza mmoja na baadae akaingia mwingine inaweza kuleta utofauti mkubwa.

3. KUKAA KIMYA MUDA WOTE WA MCHEZO

Mayanga ni kocha mwenye uwezo mkubwa ila uko too quite, too passive! Ukikaa umekaa utadhani unasimamia timu iliyosheheni professionals! Kama Zidane anaweza kusimama kuwaelekeza wachezaji aina ya Christiano Ronaldo na Ramos, itakuwa Taifa Stars? Defence imefanya makosa mengi sana ya kujirudia, hadi hatimaye wakafungwa goli wewe ukiwa umekaa tu. Kwa Taifa Stars hii na wachezaji wa Kitanzania kwa ujumla subiri majanga zaidi kama utaendelea na utamaduni huo. Wanahitaji kukumbushwa mara kwa mara na wakati mwingine kuwapanga kabisa na hata kufoka. Hakuna kocha yoyote makini ataona walinzi wake wanarudia makosa yaleyale yeye akiwa amekaa ansubiri eti half time!

Sina nia ya kukupangia, lakini hii timu ni yetu sote, so pokea hii feedback. Tukishindwa mwaka huu basi tena
Sawa sawa
 
Tukupe timu wewe mkuu
Uchambuzi wako ni kama unaonesha mwalimu anamapungufu mengi mno,ni kama tumekata tamaa hivi
 
Hata Hugo Samatta ni WALEWALE TU , sema zari limemkubali, ona vijana Wa Lesotho walivyo MDHIBITI!
 
Umechambua vema sana! Ila mi naamini mfumo na ubovu wa ligi yetu ndo unaopelekea kuwa na timu mbovu ya Taifa . Ligi legelege huzaa timu ya Taifa legelege. Ligi yetu haina ushindani kabisa na imejaa ubabaishaji mkubwa.
Wachezaji wanatoka katika timu zinazoshinda kwa mipango afu unatarajia waje wayashinde mataifa mengine. Muda si mrefu hata Somalia na Sudani Kusini zitaanza kutusumbua! By the way bado tunahitaji kocha kutoka nje ya nchi.
 
Hivyo jani wanatumiaga hawa vijana! Nyuso gani zisizo na soni kwa kubezwa kila mechi na bado mnaona poa tu
!
 
Sio dhambi tukikubali kua hatuwezi jambo fulani alafu tukahamishia nguvu zetu kwenye jambo lingine,mpira umetushinda nahisi tunatafuta matatizo ya moyo kwa nguvu.
 
Hakuna tuendako kwa kocha huyu tuliyenae, in facts tutakuwa wa mwisho katika group hili, Tanzania tuna matatizo gani kichwani? salum namuyanga amecheza mechi zipi za kimataifa duniani hadi tumpatie team yetu? tunajifanya eti ohhh tunatakiwa tuwe na kocha wa ndani sijui ohhh uzalendo tunajidanganya, swala la kuwa na kocha wa ndani na tukafanya vizuri ni kwa nchi chache sana hapa Africa, pengine samatta akicheza katika league bora ulimwenguni akaacha soccer akirudi bongo ndo kidogo tunaweza kumfikilia kuwa kocha, kwa nini hatujiulizi kuwa kina "Benni McCarthy" ambae alicheza katika league za nje hadi kutwaa champions league na mourinho bado ni TV soccer analyzer (DSTV)to South Africa na hawampatii nafasi ya kuwa kocha? kuna mambo mengine DARASA ameshasema hayatakagi ujuaji, hili ndo shida la Tanzania, tuchukueni kocha wazuri kutoka nje tuacheni ujuaji, nimetaza mechi ya Taifa stars na harambee ya Kenya zote zina ujuaji ujuaji hakuna soccer wanalocheza, upuuzi tu, tujifunze walau kutoka Uganda ,the cranes, hawa ndo wanaocheza mpira wa kueleweka EAC. Hatujachelewa, tufukuzeni huyu kocha tulete foreigner haraka asimamie game ijayo, lasivyo hakuna jipya na tunapoteza muda tu hapa kusema tutaqualify hata tukicheza uwanjani 22 halafu team pinzani 9 hatuta qualify. Hivi kweli Tanzania tunashindwa kuchukua kocha wazuri tukawalipa vizuri ili watufundishie hii team? na hivi tuko na waziri mzee basi soccer katika miaka kumi hii ni maumivu , kwani hatujifunzi kwa mkwasa alivyotupotezea muda?, uwezo wa kuwa na kocha wa ndani (mzawa) bado sana, kwa nini drogba /samwel etoe /George weah/wasifundishe team za taifa katika nchi zao na hata uwezo wao pengine ni mkubwa mara mia nane ya salum mamuyanga.
 
Timu lenyewe bovu. Ila tuwe wavumilivu maana hata NIGERIA, IVORY COAST na ZAMBIA Zimepigwa tena zikiwa nyumbani kwao
 
Tff wamrudishe Kim poulsen yule jamaa Ni muumini wa soka la vijana na anambinu,kwa muda aliokaa nchini nna uhakika ameshajua aina ya wachezaji aina ya ligi,na Ni kitu gani watanzania tunataka,nashauri tff wampandishe Kim huyu mayanga awe msaidizi,Ni mkimya sana huyu kocha!!pamoja na hayo mkwasa ndo aliivuruga zaidi taifa stars!!
 
timu apewe mwalimu kashasha. wachezaji wa kimataifa wasiitwe kwani wanasababisha hawa wandani kushindwa kujiamini
 
Tuache kuwatumia wachezaji wa timu kubwa hawana uchungu na Taifa..Malinzi chagueni wachezaji wa timu ndogo wenye maumbo makubwa tukawajaribu COSAFA ....mnategemea vichezaji vidogooo vitashinda vipi...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom