Kawe Alumni
JF-Expert Member
- Mar 20, 2019
- 8,685
- 11,988
Sehemu ya kwanza
03.11.2019
Kutoka nje wakati Rais wa jamhuri wa Muungano anahutubia bunge kwa mara ya kwanza hii ilikuwa ni dharau kubwa kwa Kiongozi wa Nchi. Bahati mbaya walikuwa wanatikisa kiberiti huku hawajui namna ya kuzima. Unamfanyia dharau kiongozi wa Nchi Halafu bado unarudi unaomba siasa za kistaarabu! How? Mbona nyie hamkuonyesha ustaarabu mlipotakiwa kuonyesha ustaarabu?
Kuita utendaji wa Rais ni nguvu ya soda. Rais alipoingia madarakani kila hatua alizokuwa akichukua Rais Magufuli wapinzani walikuwa wakibeza kwa dharau kubwa mno ati ni nguvu ya soda. Hapa kwa wabunge wenye maarifa na wenye kuona mbali wangeunga mkono juhudi za Rais, wangemkosoa baada ya kushindwa.
Kubeza Serikali kuhamia Dodoma. Wabunge Wengi walisikika wakimdhihaki Rais kwamba wao hawawezi wakahamia Dodoma watabaki Dar es Salaam, kana kwamba Dodoma hapafai kuishi watu.
Kumwita Rais dikteta huku wakijua sio Kweli, unashangaa mbunge anaita waandishi wa Habari kwa ajili ya kumtukana Rais. Mara Rais dikteta, mara Rais hivi ila ukiangalia Hakuna logical kabisa. Wabunge wenye akili wangekaa chini kuangalia namna gani ya kufanya kazi na Rais mwenye itikadi za uzalendo badala ya kumtukana majukwaani.
Nimefatilia Wabunge wengi duniani sijawahi kuona mbunge anaitisha mkutano kwa ajili ya kumtukana Rais. Hata huko Marekani wanakosema Ndio kitovu cha demokrasia Sijawahi kuona mbunge anamtukana Rais. Nenda Urusi huwezi kusikia mbunge anamtukana Rais. Ila baadhi ya wabunge wa upinzani Tanzania walitaka walifanye hili ni jambo la kawaida.
Wapinzani kupinga maendeleo. Hawa jamaa walikuwa wanasema inakuaje Nchi kubwa kama Tanzania inakosa shirika la ndege wakati Rwanda Nchi dogo inamiliki shirika la ndege. Sasa hivi wanasema ndege za kazi Gani!
Walikuwa wanakesha bungeni kupigia kelele ufisadi na mafisadi. Baada ya Magufuli kuanza kuyashughulikia mafisadi sasa wamebadilika wanasema mafisadi wanateseka mno kukaa gerezani.
Walilamikia madawa ya kulevya yanavyoharibu vijana ila baada ya wauza madawa ya kulevya kuanza kushughulikiwa wakaanza kuwatetea.
Nakumbuka kabla ya 2015 ilikuwa kila baada ya hatua kadhaa unakutana na teja linadondosha mate au linasinzia barabarani lakini Sasa hivi sio rahisi unaweza kukaa hata mwezi bila kukumbana na teja.
03.11.2019
Kutoka nje wakati Rais wa jamhuri wa Muungano anahutubia bunge kwa mara ya kwanza hii ilikuwa ni dharau kubwa kwa Kiongozi wa Nchi. Bahati mbaya walikuwa wanatikisa kiberiti huku hawajui namna ya kuzima. Unamfanyia dharau kiongozi wa Nchi Halafu bado unarudi unaomba siasa za kistaarabu! How? Mbona nyie hamkuonyesha ustaarabu mlipotakiwa kuonyesha ustaarabu?
Kuita utendaji wa Rais ni nguvu ya soda. Rais alipoingia madarakani kila hatua alizokuwa akichukua Rais Magufuli wapinzani walikuwa wakibeza kwa dharau kubwa mno ati ni nguvu ya soda. Hapa kwa wabunge wenye maarifa na wenye kuona mbali wangeunga mkono juhudi za Rais, wangemkosoa baada ya kushindwa.
Kubeza Serikali kuhamia Dodoma. Wabunge Wengi walisikika wakimdhihaki Rais kwamba wao hawawezi wakahamia Dodoma watabaki Dar es Salaam, kana kwamba Dodoma hapafai kuishi watu.
Kumwita Rais dikteta huku wakijua sio Kweli, unashangaa mbunge anaita waandishi wa Habari kwa ajili ya kumtukana Rais. Mara Rais dikteta, mara Rais hivi ila ukiangalia Hakuna logical kabisa. Wabunge wenye akili wangekaa chini kuangalia namna gani ya kufanya kazi na Rais mwenye itikadi za uzalendo badala ya kumtukana majukwaani.
Nimefatilia Wabunge wengi duniani sijawahi kuona mbunge anaitisha mkutano kwa ajili ya kumtukana Rais. Hata huko Marekani wanakosema Ndio kitovu cha demokrasia Sijawahi kuona mbunge anamtukana Rais. Nenda Urusi huwezi kusikia mbunge anamtukana Rais. Ila baadhi ya wabunge wa upinzani Tanzania walitaka walifanye hili ni jambo la kawaida.
Wapinzani kupinga maendeleo. Hawa jamaa walikuwa wanasema inakuaje Nchi kubwa kama Tanzania inakosa shirika la ndege wakati Rwanda Nchi dogo inamiliki shirika la ndege. Sasa hivi wanasema ndege za kazi Gani!
Walikuwa wanakesha bungeni kupigia kelele ufisadi na mafisadi. Baada ya Magufuli kuanza kuyashughulikia mafisadi sasa wamebadilika wanasema mafisadi wanateseka mno kukaa gerezani.
Walilamikia madawa ya kulevya yanavyoharibu vijana ila baada ya wauza madawa ya kulevya kuanza kushughulikiwa wakaanza kuwatetea.
Nakumbuka kabla ya 2015 ilikuwa kila baada ya hatua kadhaa unakutana na teja linadondosha mate au linasinzia barabarani lakini Sasa hivi sio rahisi unaweza kukaa hata mwezi bila kukumbana na teja.