Makosa katika maandishi ya lugha ya Kiswahili, kwanini yanashamiri?

Hapo umeelezea makosa ya kimaneno, ila pia kuna makosa ya sentensi, mfano nilikwenda nikamkuta hayupo, Juma huwa anakujaga hapa kila siku, bwana harusi alipokelewa kwa matarumbeta, sijampa kwa sababu nilikuwa sina, naomba nikopeshe elfu tano wakati kumbe hitaji la elfu tano unahitaji wewe.
Naamini 'ga' mwishoni mwa kitenzi yamaanisha kitendekacho mara kwa mara.
 
Ila kosa kubwa ambalo limeota mizizi na juzi nimeliona gazeti moja limetumia ni uridhi badala ya urithi;matumizi ya dhi na thi ni janga la kitaifa
Kwenye magazeti ndio huwa inanisikitisha maana utasema hawana wahariri yaani na matumizi ya lugha za mtaani kwenye shughuli za serikali nayo imeshamiri...kuchomekea kwenye speech ama mazungumzo hakuna shida, shida inakuja pale yale maneno ya mtaani yanayochomekewa kwenye mazungumzo alafu unayakuta kwenye taarifa ya kimaandishi mfano "fyekelea mbali" kwenye taarifa rasmi ya Ikulu iliandikwa kama lugha rasmi vile
 
Kuchanganya 'dh' na 'th' utaona

Kudhibitisha au dhamani.

Ujinga mwingine ni kuyaongezea konsonati majina ya kibantu.
Mfano Lissu badala ya Lisu, Zitto badala ya Zito, Kigwangalla badala ya Kigwangala wajinga.
Kessy na Mchaky vipi?
 
Kuna maneno kwa kweli yanaudhi, sio tu kuyasikia bali hata kuyasoma!

Halafu kuna neno aghalabu! Neno hili watumiaji wengi wa Kiswahili hupindua tafsiri yake, kutoka mara nyingi na kudhani ni (huzani?) ni mara chache!! Aidha, mara nyingi matumizi ya neno "tegemea" huacha ukakasi mwingi nyuma yake.

Yote tisa, donda ndugu lipo kwenye "r" na "l". Inakera sana kuona mtu anatamka au kuandika "naludi saa tano manake mala kwa mala huo ndio muda wangu wa kuludi kazini!"

Tusisahau pia neno saa linapotamkwa au kuandikwa kwa wingi kwamba masaa! Hapa utakuta hata Waandishi wa Habari wakisema "Waziri Mkuu alihutubia kwa masaa matatu!

Nilisahau! Ingawaje maneno yapo mengi mno kiasi kwamba siwezi kuyataja japo robo yake lakini wacha tu nilizungumzie hili neno "aidha."

Watumiaji wengi wa Kiswahili wanalitumia neno "aidha" kama "either" la Kiingereza, wakati tafsiri ya neno "aidha" ni "vile vile", "pia" au neno lolote lenye tafsiri sawa na hayo. Hivyo basi, badala ya kusema mathalani, "natarajia kuhamishiwa aidha Morogoro au Dodoma", hapo ulitakiwa kusema "natarajia kuhamishiwa ama Morogoro au Dodoma!"

Lakini mleta mada, nawe unatakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno. Inaleta ukakasi kuona unaandika maneno zaidi ya thelathini na hakuna kituo pahala popote pale kwenye tungo husika.

Kwavile umehusisha matumizi mabaya ya Kiswahili na uandishi, basi pia tukumbushane uhandishi sahihi ni pamoja na matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno; yaani punctuation.
Kwenye aya ya mwisho ulipaswa kuandika uandishi na sio uhandishi.
Vinginevyo umefafanua vizuri sana.
 
2
Kuchanganya 'dh' na 'th' utaona

Kudhibitisha au dhamani.

Ujinga mwingine ni kuyaongezea konsonati majina ya kibantu.
Mfano Lissu badala ya Lisu, Zitto badala ya Zito, Kigwangalla badala ya Kigwangala wajinga.
2o8 = tuonane
 
Kuna maneno kwa kweli yanaudhi, sio tu kuyasikia bali hata kuyasoma!

Halafu kuna neno aghalabu! Neno hili watumiaji wengi wa Kiswahili hupindua tafsiri yake, kutoka mara nyingi na kudhani ni (huzani?) ni mara chache!! Aidha, mara nyingi matumizi ya neno "tegemea" huacha ukakasi mwingi nyuma yake.

Yote tisa, donda ndugu lipo kwenye "r" na "l". Inakera sana kuona mtu anatamka au kuandika "naludi saa tano manake mala kwa mala huo ndio muda wangu wa kuludi kazini!"

Tusisahau pia neno saa linapotamkwa au kuandikwa kwa wingi kwamba masaa! Hapa utakuta hata Waandishi wa Habari wakisema "Waziri Mkuu alihutubia kwa masaa matatu!

Nilisahau! Ingawaje maneno yapo mengi mno kiasi kwamba siwezi kuyataja japo robo yake lakini wacha tu nilizungumzie hili neno "aidha."

Watumiaji wengi wa Kiswahili wanalitumia neno "aidha" kama "either" la Kiingereza, wakati tafsiri ya neno "aidha" ni "vile vile", "pia" au neno lolote lenye tafsiri sawa na hayo. Hivyo basi, badala ya kusema mathalani, "natarajia kuhamishiwa aidha Morogoro au Dodoma", hapo ulitakiwa kusema "natarajia kuhamishiwa ama Morogoro au Dodoma!"

Lakini mleta mada, nawe unatakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno. Inaleta ukakasi kuona unaandika maneno zaidi ya thelathini na hakuna kituo pahala popote pale kwenye tungo husika.

Kwavile umehusisha matumizi mabaya ya Kiswahili na uandishi, basi pia tukumbushane uhandishi sahihi ni pamoja na matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno; yaani punctuation.
Hivi uhandishi unamaanisha ndiyo nini ?
 
Awez badala ya Hawezi
Ujaacha badala ya Hujaacha
Uendelei badala ya Huendelei

mkuu ni kweli, yaani hiyo kuacha 'h' huwa mpaka nachukia nikiona msg ya namna hiyo. Nimejaribu sana kurekebisha walio karibu nami lakini naona imekuwa ngumu kweli.
 
Kweli kabisa Mzee kifimbocheza.

Hayo pia yanaiharibu lugha yetu.
Pia kuna vijimaneno vya wanawake lakini cha ajabu waweza kukuta mtoto wa kiume anayatumia.
1.Jomon
2.kudamshi

hahahaa bilashaka ulimaanishi maneno kama haya
 
Lazima ujue kutofautisha swaga na andishi rasmi.
Makosa hayo ukiyakuta kwenye kitabu au gazeti huko ndo unaweza kupima ukubwa wa tatizo

Kuna mtu anachanganya r na l au 'a' na 'h', hii si swaga tena bali ni ulemavu katika uandishi. Iwe ni mawasiliano yasiyo rasmi au la, inakera

Kwa kweli nikikutana na kitabu kina shida hizo mbili hapo juu nakitupa...potelea mbali ujumbe uliomo na hela niliyopoteza
Kuna kipindi gazeti la mwananchi lilikuwa na shida hiyo, sijui hakuwa na mhariri.

Na hakuna watu wabishi kama hao walemavu, ukiwakosoa ni ligi
 
Tusisahau pia neno saa linapotamkwa au kuandikwa kwa wingi kwamba masaa! Hapa utakuta hata Waandishi wa Habari wakisema "Waziri Mkuu alihutubia kwa masaa matatu!

Hili neno" masaa " badala ya" saa " nikijaribu kumuelekeza mtu kwa mfano, Dar es salaam kwenda Morogoro ni mwendo wa" saa " 4. Mtu hakuelewi hadi utumie" masaa"4.
 
Habari za asubuhi wana JF?

Kumekuwa na tatizo la kiuandishi kwa watu wengi kuanzia humu JF mpaka kwingineko kote kwenye mitandao ya kijamii mwanzo nilidhani ni kujisahau lakini sasa naona kama imezoeleka na kuonekana kama ni maneno ya kawaida kwenye kiswahili na watu wala hawastuki kuona kama ni makosa,yaani makosa yakirudiwa rudiwa mara nyingi huzoeleka na kuonekana ni usahihi

Naomba nitoe mifano michache ya hayo maneno hapa chini;
Nisamee badala ya Nisamehe
Eshima badala ya Heshima
Asubui badala ya Asubuhi
Mdogo angu badala ya Mdogo wangu
Kiac badala ya kiasi
Awez badala ya Hawezi
Ujaacha badala ya Hujaacha
Uendelei badala ya Huendelei
Utamsikia Mtangazaji anasema Nyimbo hii badala ya kusema wimbo huu

Yako maneno mengi sana yanayopotoshwa na wadau wengi humu ndani,ombi langu tu ndugu zangu tubadilike tuandike maneno kwa usahihi wake kwa sababu humu ndani panapitiwa na wanafunzi kuanzia Shule za Msingi,Sekondari na hata Vyuo wanajifunza nini juu ya tunayoyaandika humu?

Eti hapo ndio tunawadharau Wakenya hawajui Kiswahili hawajui kiswahili wakati sisi wenyewe ndio tunavuruga tu.

Ni hayo tu wadau muwe na Jumapili njema

Asante!
Kuna watanzania wengi sasa hivi wanasema "nyimbo ya" badala ya "wimbo wa". Mpaka watangazaji kwenye maredio, yaani imekuwa ni kama kawaida kusema hivyo wakati ni makosa.
 
hizo ni slang mkuu. kuna lugha rasmi, kuna lugha ya mtaani na kwa sasa mitandao ya kijamii imekuja na utamaduni wake wa jinsi ya kuwasiliana. kuna wakati ukisoma ujumbe mfupi wa simu unaweza usielewe utadhani kilichoandikwa si Kiswahili.
Mkuu, unajua maana ya slang?
 
Kuchanganya 'dh' na 'th' utaona

Kudhibitisha au dhamani.

Ujinga mwingine ni kuyaongezea konsonati majina ya kibantu.
Mfano Lissu badala ya Lisu, Zitto badala ya Zito, Kigwangalla badala ya Kigwangala wajinga.
hapa wao wenye majina haya ndio wamejiongezea
 
Sentensi ipi hapa ni sahihi.

1) Na kula Bia

2)Nakunywa Bia

Nimeona na kusikia wengi wa wasanii hasa Wa muziki Wa kitumia hiyo Namba moja.
 
Kuna maneno kwa kweli yanaudhi, sio tu kuyasikia bali hata kuyasoma!

Halafu kuna neno aghalabu! Neno hili watumiaji wengi wa Kiswahili hupindua tafsiri yake, kutoka mara nyingi na kudhani ni (huzani?) ni mara chache!! Aidha, mara nyingi matumizi ya neno "tegemea" huacha ukakasi mwingi nyuma yake.

Yote tisa, donda ndugu lipo kwenye "r" na "l". Inakera sana kuona mtu anatamka au kuandika "naludi saa tano manake mala kwa mala huo ndio muda wangu wa kuludi kazini!"

Tusisahau pia neno saa linapotamkwa au kuandikwa kwa wingi kwamba masaa! Hapa utakuta hata Waandishi wa Habari wakisema "Waziri Mkuu alihutubia kwa masaa matatu!

Nilisahau! Ingawaje maneno yapo mengi mno kiasi kwamba siwezi kuyataja japo robo yake lakini wacha tu nilizungumzie hili neno "aidha."

Watumiaji wengi wa Kiswahili wanalitumia neno "aidha" kama "either" la Kiingereza, wakati tafsiri ya neno "aidha" ni "vile vile", "pia" au neno lolote lenye tafsiri sawa na hayo. Hivyo basi, badala ya kusema mathalani, "natarajia kuhamishiwa aidha Morogoro au Dodoma", hapo ulitakiwa kusema "natarajia kuhamishiwa ama Morogoro au Dodoma!"

Lakini mleta mada, nawe unatakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno. Inaleta ukakasi kuona unaandika maneno zaidi ya thelathini na hakuna kituo pahala popote pale kwenye tungo husika.

Kwavile umehusisha matumizi mabaya ya Kiswahili na uandishi, basi pia tukumbushane uhandishi sahihi ni pamoja na matumizi sahihi ya utenganishi wa maneno; yaani punctuation.
Mkuu Chige ninaomba msaada wako kuna jamaa yangu mfaransa anajifunza kiswahili. Huwa ananiuliza maswali ya kiufundi nyakati nyingine, ambayo kimsingi ni nje ya taaluma yangu.

Nimeona kwa uchangiaji wako, nikahisi waweza kuwa ni wa msaada. Nina c&p ujumbe chini wa swali husika la huyo mgeni:

Rafiki, I have a question

There is a sentence:
Wanawake niliowaona ni wazuri.
Is that correct?

Siwezi kufaham kwa nini kuna -wa- ndani ya "verb".
There is the relative -o- and I can get that (The women THAT I saw...), but why the repetition of "women" in -wa-?

Why should we repeat the relative -o- and the object -wa- (wanawake)?
 
Back
Top Bottom