Makosa 10 aliyotenda Mungu

Testar

JF-Expert Member
May 30, 2015
7,461
12,215
1.KUMUUMBA SHETANI:
Hili lilikuwa kosa kubwa sana. Makosa yate yamechepuka kutoka hapa. Shetani anawasababishia watu maovu, then Mungu anawahukumu watu dhaifu. Hapa Mungu inambidi amkamate shetani na kumtokomeza ili maovu yaishe, kama wote wanatoshana nguvu basi wasuluhishe ugomvi wao na kupatana ili maisha yawe ya amani.

2.KUISHI MAFICHONI:
Toka enzi na enzi, Mungu amekuwa akiishi mafichoni, kwanini asijitokeze na kujionesha kwa viumbe vyake? Anaishi mafichoni kwani yeye ni Joseph Kony? Hili limepelekea watu wake kudanganywa na manabii wa uongo na kutapeliwa bure. God come from your hidings and reveal yourself to your people.

3.MAFURIKO YA WAKATI WA NUHU:
Mungu alisababisha mafuriko ili kuangamiza watu waovu na kubakiza watu wema, Yes he did, sasa waovu wa leo wametoka wapi? mbona aliuwa watu wengi bila huruma? Kama mafuriko yalikuwa ni suluhisho la maovu, Yesu na mitume walijia nini? It seems he fought effects instead of causes.

4.SAFARI YA WANA WA ISRAELI:
Mungu aliwatoa wana wa Israel kutoka Misri kwa madai ya kuwapa nchi ya ahadi, matokeo yake aliwaamuru wafanye uvamizi wa nchi za watu(mf. waamori, wamoabu na wakanani). Kwanini asingebadilisha jangwa na kuwatengenezea waisraeli nchi yao? mbona Gadaffi aliweza? Imagine waje wapuuzi hapa TZ wachukue nyumba na ardhi kwa madai kwamba wameagizwa na Mungu, ungereact vipi? WE HAVE TO BE FAIR!

5.KUTOTIMIZA AHADI YAKE KWA ABRAHAM:
Mungu alimwambia Abraham kuwa atampatia uzao wa wana wengi kama nyota za angani au mchanga wa pwani. Sasa hivi ukichanganya walio wa Abrahamu na wasiyo wa kwake bado watu hawawezi kuwa sawa na nyota au mchanga wa pwani. Ata ukijumlisha na waliokufa back to Adam. Atatimiza lini hi ahadi? je kuna muda wa kutosha? mbona watumishi wake wanasema Yesu yuu karibu kuja ili kutamatisha nyakati?

6.KUWEPO KWA MZIO(ALLERGY):
Kwanini watu wengi ambao ni wema wana allergy na vitu alivyoumba Mungu? mbona maandiko yanasema kila alichoumba Mungu ni chema? Kwanini aumbe mimea na wanyama wenye sumu kwa watu wake awapendao? au hakujua?

7.MAJANGA ASILIA:
Kama Mungu aliumba dunia ili iwe sehemu ya amani kwa watu wake na wamwabudu yeye, kwanini kuna matetemeko ya nchi, vimbunga na mafuriko. Kwanini anawauwa watu kikatili hivi? au haya nayo tumsingizie shetani?

8.KUUMBA VIUMBE HATARISHI:
Kwanini Mungu aumbe bacteria, virusi, fangasi na viumbe wengine wanaosababisha magonjwa na kifo? Kwanini hawa viumbe wasingefia kwenye yale mafuriko ya Nuhu ili watu wema alio wabakiza waishi kwa amani? Je hawa viumbe hatari Mungu alimwamuru Nuhu awaingize wawili wawili kwenye safina?

9.JEHANAMU NA MOTO WAKE:
Kwanini Mungu aumbe jehanamu kuteketeza waovu? Kwani hajui kusamehe? Kwanini huruma yake ina kikomo kwa shetani? Kama wewe ni mzazi, mwanao akikukosea na hajaomba msamaha, itabadilisha uhalisia kuwa yule sii mwanao? SHETANI PAMOJA NA WAOVU NI KAZI YA MIKONO YAKE, PRODUCTS OF HIS OWN MIND BEFORE CREATED THEM. So aache kuweka vinyongo na kutamani kulipiza kisasi juu ya kazi yake.

10.KASORO KWENYE MWILI WA BINADAMU:
Kwanini pawepo na mabadiliko hasi kwenye jeni za binadamu(mutation)? kwani hakujua hicho ni chanzo cha viwete??? Kidole tumbo(appendix) ni cha kazi gani? mbona hajatoa maelezo namna ya kukitumia? Na chuchu za mwanaume ni za kazi gani?

TO THE RIGHT WING OR THE LEFT WING WE ARE NEITHER, NOT EVEN AT THE MIDDLE....R.I.P MOBUTU!

===================
Nimeona Thread inayojaribu kuonyesha makosa kumi ya Mungu ndo maaana nikachukua hatua Yakinifu kuandika haya..Kwanza Kabisa na Ifaamike Mungu anajua yote na Kazi Yake kamwe haina makosa,ebu Tuanze
(whats a Mistake)? a wrong way of doing something,misguided action,inaccuracy!!!!!!!!
=>Kusema Mungu ana makosa ni sawa na kusema hajakamilika(perfection) Kwaio hana tofauti na sisi Jambo ambalo ni kosa,Lucifer Alitenda Hivi Hivi

1.KUMUUMBA SHETANI
Mungu hakumuumba shetani alimuumba Lucifer ambae alingiwa na wivu due to the status quo of Jesus akataka awe Miongoni mwa utatu mtakatifu eventually ule wivu ukasababisha atende dhambi unayoifanya ya kumkosoa Mungu(Imperfection)

2.KUISHI MAFICHONI
Mungu Hajifichi,dhambi zetu ndo zinathfarakanisha na yeye maana hawezi kukaa na sisi hakika tutakufa awali kulingana na Biblia mbona alikua akihukutana na Adam wakaongea sema tatizo ni pale alipotenda dhambi,Israel walitaka kumuona ILA kabla hajafika walighairi wakasema hawataki tena

3.MAFURIKO
Aim ya mafuriko ni kupunguza maasi na Age generally,sio kuondoa dhambi kabisa maana watu wangeendelea na nyendo zao Mungu alisahaulika kabsa lakini kutokana na UPENDO wake akaamua kuchukua hatua hio baada ya warning ya miaka karibia 500 kweli hata kama wee ni kiazi miaka yote hii
elewi concept tu???

4.SAFARI YA WANA WA ISRAEL
Lord promised abraham kuwa atampa nchi specifically ya CANAAN sio popote tu that was the Point kutimiza ahadi sio Ilimradi nchi tu na nyakati zile struggle Ili kusurvive Ilkua ni suala la kawaida ndo maana hata Israel walipokua wanazingua walichezea mkong'oto tuuu!

5.AHADI YA ABRAHAM
Ivii unajua dunia ina miaka mingapi???mimi mwenyewe sina uhakika lakini uzao wa abraham compared to na Generation ya awali uliongezeka japo hukufikia nyota za angani maana israel walikua wagumu mioyoni kwa sababu Mungu sio dictator hakulazimisha

6.ALLERGY 7.MUTATIONS NA 8.NATURAL CALAMITIES
Hivi vyote ni side effects za dhambi duniani,mwanzoni maisha yalikua Bomba vitabu vingine mpka vinasema adam alipoona Kondoo anakuja na kutoka damu walipokua wanatengenezema mavazi alilia sana,hakuamini kilichotokea maana alikua hajawahi ona alafu Mungu alilaani ardhi na dunia Generally ndo maana haya yote yanatokea,vingine sisi ndio chanzo kutokana na vitu kma ukuaji wa sayansi ya technolojia

10.JEHANAMU
Lengo la Moto sio kukomesha watu na sio kwamba God enjoys this kuprove hapendi ndo maana akamtuma mwanae hata kama tulishakataa mara nyingi,moto una lengo la KUTOKOMEZA DHAMBI Ili dunia ibaki salama tukutane na Mungu kma Ilivyokua awali.Na ingeweza kuwa njia nyingine sio lazima moto lakini akachagua njia hii na kuchomwa sio lazima ni Option making it more Fairer sijui binadamu upewe nini uweze kuona Haya.
 
1.KUMUUMBA SHETANI:
Hili lilikuwa kosa kubwa sana. Makosa yate yamechepuka kutoka hapa.Shetani anawasababishia watu maovu, then Mungu anawahukumu watu dhaifu. Hapa Mungu inambidi amkamate shetani na kumtokomeza ili maovu yaishe, kama wote wanatoshana nguvu basi wasuluhishe ogomvi wao na kupatana ili maisha yawe ya amani.

2.KUISHI MAFICHONI:
Toka enzi na enzi, Mungu amekuwa akiishi mafichoni, kwanini asijitokeze na kujionesha kwa viumbe vyake??? Anaishi mafichoni kwani yeye ni Joseph Kony???..Hili limepelekea watu wake kudanganywa na manabii wa uongo na kutapeliwa bure...God come from your hidings and reveal yourself to your people.

3.MAFURIKO YA WAKATI WA NUHU:
Mungu alisababisha mafuriko ili kuangamiza watu waovu na kubakiza watu wema, Yes he didi..sasa waovu wa leo wametoka wapi??? mbona aliuwa watu wengi bila huruma??? Kama mafuriko yalikuwa ni suluhisho la maovu, Yesu na mitume walijia nini??? It seems he fought effects instead of causes.

4.SAFARI YA WANA WA ISRAELI:
Mungu aliwatoa wana wa Israel kutoka Misri kwa madai ya kuwapa nchi ya ahadi, matokeo yake aliwaamuru wafanye uvamizi wa nchi za watu(mf. waamori, wamoabu na wakanani). Kwanini asingebadilisha jangwa na kuwatengenezea waisraeli nchi yao??? mbona Gadaffi aliweza???.Imagine waje wapuuzi hapa TZ wachukue nyumba na ardhi kwa madai kwamba wameagizwa na Mungu, ungereact vipi???...WE HAVE TO BE FAIR!!!

5.KUTOTIMIZA AHADI YAKE KWA ABRAHAM:
Mungu alimwambia Abraham kuwa atampatia uzao wa wana wengi kama nyota za angani au mchanga wa pwani. Sasa hivi ukichanganya walio wa Abrahamu na wasiyo wa kwake bado watu hawawezi kuwa sawa na nyota au mchanga wa pwani. Ata ukijumlisha na waliokufa back to Adam. Atatimiza lini hi ahadi??? je kuna muda wa kutosha??? mbona watumishi wake wanasema Yesu yuu karibu kuja ili kutamatisha nyakati???

6.KUWEPO KWA MZIO(ALLERGY):
Kwanini watu wengi ambao ni wema wana allergy na vitu alivyoumba Mungu??? mbona maandiko yanasema kila alichoumba Mungu ni chema??? Kwanini aumbe mimea na wanyama wenye sumu kwa watu wake awapendao??? au hakujua???

7.MAJANGA ASILIA:
Kama Mungu aliumba dunia ili iwe sehemu ya amani kwa watu wake na wamwabudu yeye, kwani kuna matetemeko ya nchi, vimbunga na mafuriko....Kwani anawauwa watu kikatili hivi???au haya nayo tumsingizie shetani???

8.KUUMBA VIUMBE HATARISHI:
Kwanini Mungu aumbe bacteria, virusi, fangasi na viumbe wengine wanaosababisha magonjwa na kifo??? Kwanini hawa viumbe wasingefia kwenye yale mafuriko ya Nuhu ili watu wema alio wabakiza waishi kwa amani???.Je hawa viumbe hatari Mungu alimwamuru Nuhu awaingize wawili wawili kwenye safina???

9.JEHANAMU NA MOTO WAKE:
Kwanini Mungu aumbe jehanamu kuteketeza waovu??? Kwani hajui kusamehe???Kwanini huruma yake ina kikomo kwa shetani?. Kama wewe ni mzazi, mwanao akikukosea na hajaomba msamaha, itabadilisha uhalisia kuwa yule sii mwanao??? SHETANI PAMOJA NA WAOVU NI KAZI YA MIKONO YAKE, PRODUCTS OF HIS OWN MIND BEFORE CREATING THEM...So aache kuweka vinyongo na kutamani kulipiza kisasi juu ya kazi yake.

10.KASORO KWENYE MWILI WA BINADAMU:
Kwanini pawepo na mabadiliko hasi kwenye jeni za binadamu(mutation)??? kwani hakujua hicho ni chanzo cha viwete??? Kidole tumbo(appendix) ni cha kazi gani??? mbona hajatoa maelezo namna ya kukitumia??? Na chuchu za mwanaume ni za kazi gani???

TO THE RIGHT WING OR THE LEFT WING WE ARE NEITHER, NOT EVEN AT THE MIDDLE....R.I.P MOBUTU!!!
Dhambi zetu ndiyo chanzo cha laana zote sasa Mwenyezi Mungu kosa lake lipi? Wamlaumu kwa makosa ya wenye viburi na tamaa zisizosikia sheria!
 
Magu alisema wale walioimba 'wana imani na nani sijui' angewatimua wote siku hiyo hiyo... Mimi nasema kama ningelikuwa Mungu pindi tu kidole chako kinabonyeza kitufe cha kupost hapo hapo ningekugeuza senene!!

Unafanya dhihaka kama hizi na bado uko hai! Aisee Mungu ana uvumilivu wa hali ya juu sana... Mwacheni Mungu aitwe Mungu!!
 
Magu alisema wale walioimba 'wana imani na nani sijui' angewatimua wote siku hiyo hiyo... Mimi nasema kama ningelikuwa Mungu pindi tu kidole chako kinabonyeza kitufe cha kupost kupost hapo hapo ningekugeuza senene!!

Unafanya dhihaka kama hizi na bado uko hai! Aisee Mungu ana uvumilivu wa hali ya juu sana... Mwacheni Mungu aitwe Mungu!!
Senene Mbona umempendelea maana ni mtamu kushinda nyama
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom