Makongoro amfungia safari Leticia Nyerere

Hapa tukubali rafiki yangu Makongoro kachemsha. Hata nitakapoongea naye nitamwambia hivyo hivyo. Dalili ninayoiona hapa ni kwamba CCM hawataki kukumbushwa jina la Nyerere kwa sababu hata katika ilani zao hawamkumbuki huyu mwanzilishi wa taifa letu. Sasa inawastua kuwa Leticia, aliyekuwa mkwe wa Nyerere, ambaye amemzalia wajukuu, anaendelea kuwakumbusha watu kuwa Nyerere alikuwepo na hii inawashtua sana CCM. Hakuna mahali Dr Slaa katumia jina la Nyerere au Leticia kujipatia umaarufu lakini naona mgombea wa CCM hajiamini kiasi cha kuomba msaada kutoka mwenyekiti wa CCM wa Musoma ambaye hagombei kiti chochote katika jimbo la Kwimba.
 
ina maana mimi niliyemwita mbuzi wangu nyerere akinisikia atanifunga? huyu ni mwenda wazimu flani tu, hilo halina ubishi hata
nyerere alishakufa na jina lake sasa mzimu tu ndiyo unaoitwa nyerere, hata wewe makongoro una jina la baba yako acha
uasherati na uzinzi wa kinywa chako, unatafuta umaarufu tu huna lolote bwana hebu pisha bwana ebooooo!
 
Makongoro akimpinga huyu Leticia,that is just as it should be,kwa sababu huyu ni mpinzani wake wa kisiasa. Isipokuwa, as far as the Nyerere Family is concerned,mimi napinga hili jambo. Kama Leticia anataka kuwa Mbunge,wa wapi kule,Serengeti?,sisi,Familia ya Nyerere hatuwezi kuwa na sababu ya kupinga au kusema kwamba akichaguliwa itakuwa ni jambo baya kwetu. Yuko mtu mmoja nilisema kuchaguliwa kwake hakuwezi kuifurahisha Familia ya Nyerere. Na huyo mtu hakuwa Leticia. Huyo mtu sasa hivi siwezi kumtaja sasa ,kwa sababu conditions zimekuwa difficult.
No,hata kama timu ya mpira,kwa mfano Young Africans,wakimfukuza mchezaji. Yule mchezaji akiondoka Yanga akienda kwenye timu ya Simba,sidhani kama Yanga watasema,''Msimuajiri huyo.''
Kwa hiyo sisi Familia ya Nyerere hatupingi Leticia kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Serengeti. In fact,sisi Familia ya Nyerere,ni lazima,lazima,lazima tuwe non-partisan,tuwe watu ambao hatujali nani anachaguliwa Rais,nani anachaguliwa Mbunge au nani anachaguliwa diwani.
Again,nasema sipingi Makongoro kumpinga Leticia. In fact,namuunga mkono Makongoro kumpinga Leticia,lakini kama Familia,wa are non-partisan.


ulichokisema hapa hakina mkia wala mguu.. maana hujagusa suala la Leticia kutumia jina la Nyerere. Makongoro hampingi Leticia kama Leticia anampinga kwa sababu anatumia jina la Nyerere, na kwa vile wewe humpingi Makongoro maana yake unakubaliana naye kuwa Leticia aache kutumia jina la Nyerere na kwa namna hiyo Mtanzania mwingine yeyote mwenye jina la Nyerere (kama Stephen Nyerere) hatakiwa kutumia jina hilo kujipatia umaarufu hata kama anazo sababu za kihistoria kufanya hivyo.
 
jamani si kosa njaa jaman mbaya, pamoja na tamaa ya utajiri ndo vya msukuma mpaka anamsaliti shemejie..! wafisi.. si watu wazuri waweza fanya chochote mtaji wao ufanyikiwe basi.
 
[QUOTE=mikela;1086606]MWENYEKTI wa CCM mkoani Mara, Makongoro Nyerere, amemtupia madongo mgombea ubunge wa Jimbo la Kwimba, kupitia tiketi ya Chadema, Leticia Nyerere, kuwa anatumia jina la Nyerere ili kujipatia umaarufu wa kisiasa.
Makongoro pia amemtaka Leticia kuacha mara moja, kutumia jina la ukoo wa Nyerere katika harakati zake za kisiasa kwa kuzingatia kuwa ndoa kati yake na Madaraka Gedfrey Nyerere haipo tena.

Leticia anagombea ubunge wa Jimbo la Kwimba, akichuana na Shanif Hirani Mansoor, anayewania kwa tiketi ya CCM.

Hatua ya Makongoro kumtaka Leticia aache kutumia jina la ukoo wa Nyerere katika shughuli za kisiasa, aliifanya juzi alipokuwa akizungumza katika uzinduzi wa kampeni za CCM, katika Jimbo la Kwimba...

"Huyu anayejiita Leticia Nyerere hasemeshani na Madaraka, achilia mbali hata kusalimiana, sasa anatumiaji jina la ukoo wetu. Angalau mimi naweza kuzungumza naye, ni kweli alikuwa mke wa mdogo wangu na alibahatika kuzaa naye watoto watatu lakini mambo ya ndoa wengi mnayajua, sasa siyo mke wake tena," alifafanua.

Alisema ingawa hataki kuingia kwa undani kuzungumzia mgogoro kuhusu ndoa hiyo, alisema yeye na mkewe Jaji Aisha Nyerere, ndio walikuwa wasimamizi.

Alisema katika ndoa hiyo, hayati Mwalimu Nyerere, alitoa ng'ombe 30.

"Huo ni uongo, ninawaomba wananchi wa Jimbo la Kwimba muuachana naye na kumchagua mgombea wa CCM Shanif Mansoor," alieleza makongoro Nyerere.

Makongoro alidai kuwa wakati wa harusi, yeye alikuwa ofisa wa jeshi na mke wake alikuwa hakimu. …

Kwa upande wake, Mansoor alisema akichaguliwa kuwa mbunge, atamaliza matatizo ya maji, huduma za afya na upungufu wa walimu katika shule za jimbo hilo.[/QUOTE]

MAONI YANGU:
Mbunge aliyemaliza muda wake, Mh B Sakira, aliwahi kulalamikia mchakato wa kura za maoni kuwa rushwa ilitumika na ya kwamba TAKUKURU haikujihusisha na kufuatilia sakata hilo japokuwa ushahidi ulikuwepo wazi. Na aliyeshinda katika kura hizo ni Shanif ambaye ni mtanzania mwenye asili ya india. Shanif Mansoor anaishi jijini Mwanza na ni mfanya biashara.

Mimi nashindwa kuelewa kilichopelekea Mh Makongoro kwenda kumpa support Mansoor…je ni chuki dhidi ya shemeji yake ? au ni pesa (ambazo nadhani anazo za kutosha) au ni shinikizo la chama kumsaidia huyo mfanya biashara aweze kukabiliana na upepo wa upinzani? Sina jibu sahihi, lakiniMakongoro atakuwa ame-miss step kama wasemaji wengine hapo juu walivyosema. Hili jambo linaanza kuibua hoja za uhalali wa baba wa taifa kutumia jina la Nyerere na vilevile yeye mwenyewe (Makongoro) kujiita ni motto wa baba wa taifa. Haya yanamdhalilisha yeye na mama na ukoo mzima.

Siasa ni mchezo mchafu na sasa hivi ukijiingiza kichwakichwa kwenye siasa hakikisha umejikagua vizuri na kunawa uso wako sawasawa, vinginevo unaweza kujichafua sana. Makongoro arudi Mara akatulie. Watu wana hasira na CCM na umasikini katika nchi tajiri.


Hata hivyo kwa maoni yangu sasa hivi wamempa umaarufu zaidi, kwasababu wengine tulikuwa tunadhani ni motto wa Nyerere mwingine kwasababu jina hilo sasa hivi linatumiwa na wengi tu wasio na ukoo na baba wa taifa. Lakini Makongoro ndio ametujulisha kuwa ni shemeji yake na amezaa wajukuu 3 wa nyerere. Ningekuwa mimi ni mwenyeji wa huko ndio ningempa kura yangu huyo mama ikiwa ni pamoja na kumpigia kampeini ya nguvu zzanhu zote.
 
Siasa za Tanzania hizo.
Nyerere ana Makongoro
Mwinyi ana Hussein
Malima ana Adam
Kikwete ana Riz One
Makamba ana January




All are rubbish

Umesahau Karume ana Amani na Ally
moses Nauye ana Nape
Mtei ana mkwewe Freeman Mbowe,teh teh teh.
 
Makongoro angeeleza maneno yaliyo tumiwa na Raticia yanayokinzana na wills za mzee wetu wa taifa, otherwise huyo Kongoro uwezo wake wa kupambanua mambo ni mdogo sana mpaka inaniwia vigumu hicho cheo chake ndani ccm ana-ki manage vp.
 
Madaraka amechakachuliwa akili yake mke wa ndugu yake aliyezaa naye watoto wa tatu anaenda kumnyanyasa kijinsia kwa aina hiyo mbele ya Umma ,anadhani watoto wa ndugu yake watakuwa na heshima naye kweli mtu anaenda kumdhalilisha mama yao mbele ya jamii kwa kuendelea kutumia jina mpaka leo,huu ni utamaduni uliobaki kwa wanawake wengi wa Tanzania ambao waliolewa na wakaachika na waume zao lakini pindi wakiwa wamezaa na hao wanaume wameendelea kutumia majina ya waume zao kwa sababu nyingi tu zikiwemo nyaraka za kikazi,passport na hata elimu huw wanaona taabu tena kwenda mahakamani kuapa na kuanza kugeuza kila kitu.
Kuna wengine maarufu hapa Afrika ambao bado wanatumia majina ya waume zao akiwemo Winnie Mandela na Graca Machelle ambaye ni rafiki wa familia ya Nyerere kwa hiyo Madaraka asimnyanyase huyo mama kisaikolojia na sidhani wananchi watamsikiliza kwa huo ujinga wake.

Hapa tutatakiwa kutumia akili kidogo sana, Huyu Makongoro ni Taira na si vinginevyo, kweli Mke wa Mdogo wako aliyezaa na mdogo wako watoto 3, leo unatoka kifua mbele kumtosa?

Wasukuma si wajinga hata kidogo, Mtaona watakachokifanya, Tusubiri.
 
Wee Makongoro, wewe ni Mwenyekiti wa CCM wa Mara. Hivi Kwimba iko Mara? Hujui hata wilaya za mkoa wako?
 
nashangaa tunapoteza muda mwingi kuujadili ujinga wa mjinga, makongoro kashakongoroka sasa antapatapa, letcia ackate tamaaa
 
Madaraka ni mlevi wa kutupa. Yawezekana kapewa pombe na alikuwa akisema haya under the influence of pombe.
Huyo gabachori aliyemwalika kumpigia debe kitu kafanya nadhani ni kumnunulia viroba, kreti ya bia na akabomoka kama mnavyomsikia.
Achaneni naye.
 
Nilikuwa na hamu ya kumuona huyu Makongoro maana nikiri kuwa kukaa huku Shamba kumeniharibu. Hatimaye nimemuona. Anaonekana kafanana saana na Mama yake.

3.JPG
imaging.ashx


Kulia ni Madaraka Nyerere.

Marehemu baba yangu aliniambia siku moja kuwa "Kama si JKN, mwanangu usingelisoma". Ukweli ni kuwa hiyo iko IN-DIRECT. Hivyo hadi kesho ntakuwa na heshima kubwa saaana kwa JKN. Ila kama Wanafamilia mnaanza kuleta ya kuleta mkitegemea mtapata heshima ya JKN basi mmenoa kama alivyosema Jasusi. Mjiheshimu na nyie mtaheshimiwa. Kwa miaka mingi mmekuwa mmekaa Pembeni na hii imefanya kwa hatua kubwa saana msishambuliwe na watu na hata mnapokosea basi watu walielewa kuwa ni makosa ya kibinadamu. Hili mnalolianza sasa mnaanza kuwa kama Ridhiwan Kikwete ambaye siku baba yake atatoka madarakani, atajuta.

Bahati Nzuri sana kwenu ni kuwa Mnaheshimika kwa jina hilo la JKN na siyo CCM. Ridhiwan na mama yake wamejipa Utawala kwa jila la CCM. Siku ikitokea kama huko Kenya kilichotokea kwamba CCM imekufa, hawa watu watakwenda na maji. JKN mwenyewe alisema kuwa "CCM siyo Mzazi wake". Aliweka mbele NCHI na Watu wake wa Tanzania. Kwake jina sidhani kama lilikuwa muhimu sana kama mnavyotaka kutuambia hapa.

Acheni hilo jina litumike kila sehemu ili JKN aendelee kukumbukwa Tanzania milele kama baba wa Taifa.

Kuna Film inaitwa The 13th Warrior ya mwaka 1999 aliyocheza Antonio Banderas. Kwenye film hii, kuna jamaa anasema kuwa (ntajaribu kutafasiri kwa ninayikumbuka) " ......... Mtu Tajiri ni yule ambaye jina lake litachorwa (kuandikwa) ili vizazi na vizazi vilikumbuke....." Hapa nakumbusha tena ni JILA LA JULIUS KAMBARAGE NYERERE. Hilo jina la NYERERE siyo jina la Julius Kambarage bali ni jina la UKOO. Akina Nyerere mko wengi saaana dunia hii ila MWALIMU JULIUS KAMBARAGE baba wa Taifa la Tanzania, Milele atabaki MMOJA. Na ni huyo tu tutamuheshimu na kumkumbuka Milele Tanzania. Wengine mkitaka heshima na kukumbukwa, Watanzania tupo hapa, wanyongee natumeonewa vya kutosha. Msahau Njaa zenu na anzeni kututetea Watanzania.

Huyu Makongoro kama kweli angelikuwa anataka kupata heshima basi mara alipochaguliwa kuwa Mbunge wa Arusha, angeligangamara na Wana-Arusha na kuleta Chachu ya Maendeleo, leo hii angelikuwa mbali sana. Mbona Dr. Slaa kaweza kuwaamsha Watanzania? Yeye alikuwa wapi kufanya hivyo? Kubeba jina la NYERERE kikweli, lina maana tu pale utakapojitwisha na msalaba wake. Vinginevvyo unabaki tu kuwa kama Steven Nyerere au NJOMBA (Makonde) Juliachi Kambarage Nyerere wa huko Newala, macheza Sindimba na mnywaji mzuri sana wa Mnazi.
 
Ehhhh, msimlaumu Makongoro Peke yake jamani. Inaonekana wako wengi kwenye Familia wanakubaliana naye ila hawataki tu kukubali. Hebu someni maelezo ya Ganesh. Huyu jamaa ANAPINGANA na KUKUBALIANA na Maelezo ya Makongoro. Nafikiri hakutaka mwanzo kujionyesha ila mwisho akajisahau na kumwaga yaliyo moyoni mwake.

Hebu someni tena vizuri hii thread:

Makongoro akimpinga huyu Leticia,that is just as it should be,kwa sababu huyu ni mpinzani wake wa kisiasa. Isipokuwa, as far as the Nyerere Family is concerned,mimi napinga hili jambo. Kama Leticia anataka kuwa Mbunge,wa wapi kule,Serengeti?,sisi,Familia ya Nyerere hatuwezi kuwa na sababu ya kupinga au kusema kwamba akichaguliwa itakuwa ni jambo baya kwetu. Yuko mtu mmoja nilisema kuchaguliwa kwake hakuwezi kuifurahisha Familia ya Nyerere. Na huyo mtu hakuwa Leticia. Huyo mtu sasa hivi siwezi kumtaja sasa ,kwa sababu conditions zimekuwa difficult.
No,hata kama timu ya mpira,kwa mfano Young Africans,wakimfukuza mchezaji. Yule mchezaji akiondoka Yanga akienda kwenye timu ya Simba,sidhani kama Yanga watasema,''Msimuajiri huyo.''
Kwa hiyo sisi Familia ya Nyerere hatupingi Leticia kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Serengeti. In fact,sisi Familia ya Nyerere,ni lazima,lazima,lazima tuwe non-partisan,tuwe watu ambao hatujali nani anachaguliwa Rais,nani anachaguliwa Mbunge au nani anachaguliwa diwani.
Again,nasema sipingi Makongoro kumpinga Leticia. In fact,namuunga mkono Makongoro kumpinga Leticia,lakini kama Familia,wa are non-partisan.
 
mawazo yake yanaonekana kuwa mpauko,fikra zake kuwa mgando,
anasahau kuwa watanzania wa leo si mabwege tena,anatumika pengine kwa kujua au kutokujua na wanasiasa wenye upungufu wa kinga rohoni(ukiro),anamtukana shemeji yake leticia kwa kumwambia aache kulitumia jina la nyerere kwani hana ukoo nao,leticia ni mpambanaji,anakemea mafisadi na vibaraka vyao,makongoro anaumia,anamzuia kulitumia jina la mwalimu, kwa mtu anayethubutu kuenzi fikra za mwl nyerere za kukemea,kuhoji,kudadisi maswala ya msingi,kuweka maslahi ya umma kwanza,tumuulize huyo makongoro,je amewahi hata siku moja kujaribu hata kwa robo tu ujasiri wa mwl?haoni jinsi ccm ilivyopoteza mwelekeo?kweli hii ndiyo ccm ya nyerere?
aache unafiki,ni muda mzuri kwake kuwavaa viongozi waliokifanya chama kilichoasisiwa na baba yake kama yeye anavyopenda itamkwe na si baba wa taifa kilivyogeuka genge la wahuni wachache kwa maslahi yao na amwache
mpambanaji leticia na chadema yake


























































mawazo yake
 



Mara nyingi wazazi waliobahatika kuzaa watoto zaidi ya watano, atatokea mtoto mmoja mwenye tabia zinazofanana na baba, bahati mbaya Mwalimu Nyerere amekosa kabisa mtoto aliyerithi hekima na busara zake, labda inaweza kuja kujitokeza kwa wajukuu.

 
Makongoro Nyerere hana jipya afadhali angenyamaza kuliko kuongea ujinga.Makongoro analitia najisi jina la Nyerere kwa kuongea mambo yanayokwenda kinyume na falsafa ya Mwl Nyerere.Nasikitika sana Mwl kakosa mtoto wa mwenye kipaji chake mwanzo nilidhani Makongoro angebeba mikoba ya Mwl lakini imekuwa tofauti na mawazo yangu na watanzania wengi.
 
Back
Top Bottom