Makongoro amfungia safari Leticia Nyerere

Madaraka amechakachuliwa akili yake mke wa ndugu yake aliyezaa naye watoto wa tatu anaenda kumnyanyasa kijinsia kwa aina hiyo mbele ya Umma ,anadhani watoto wa ndugu yake watakuwa na heshima naye kweli mtu anaenda kumdhalilisha mama yao mbele ya jamii kwa kuendelea kutumia jina mpaka leo,huu ni utamaduni uliobaki kwa wanawake wengi wa Tanzania ambao waliolewa na wakaachika na waume zao lakini pindi wakiwa wamezaa na hao wanaume wameendelea kutumia majina ya waume zao kwa sababu nyingi tu zikiwemo nyaraka za kikazi,passport na hata elimu huw wanaona taabu tena kwenda mahakamani kuapa na kuanza kugeuza kila kitu.
Kuna wengine maarufu hapa Afrika ambao bado wanatumia majina ya waume zao akiwemo Winnie Mandela na Graca Machelle ambaye ni rafiki wa familia ya Nyerere kwa hiyo Madaraka asimnyanyase huyo mama kisaikolojia na sidhani wananchi watamsikiliza kwa huo ujinga wake.

Mama Zuma aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Afrika Kusini enzi ya Mbeki anaendelea kutumia jina la mumewe ingawa waliachana miongo mingi tu iliyopita!! Huo ni utamaduni wa kiafrika mara mwanamke anapokuwa na watoto na mume wake walioachana!! Makongolo kwahilo kafulia!!
 
Huyu mtu kapata wapi huo ujasiri wa kumuamulia mtu mzima mwingine jina la kutumia wakati ni jina halali? Yaani imepita miaka kumi na mbili ndio anakumbuka kuwa Leticia bado anatumia jina la Nyerere? Na watoto wa Leticia wanaruhusiwa kutumia jina la "babu yao maarufu"?
 
MWENYEKTI wa CCM mkoani Mara, Makongoro Nyerere, amemtupia madongo mgombea ubunge wa Jimbo la Kwimba, kupitia tiketi ya Chadema, Leticia Nyerere, kuwa anatumia jina la Nyerere ili kujipatia umaarufu wa kisiasa.
Makongoro pia amemtaka Leticia kuacha mara moja, kutumia jina la ukoo wa Nyerere katika harakati zake za kisiasa kwa kuzingatia kuwa ndoa kati yake na Madaraka Gedfrey Nyerere haipo tena.

Mwenyekiti huyo wa CCM na Madaraka ni watoto wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Leticia anagombea ubunge wa Jimbo la Kwimba, akichuana na Shanif Hirani Mansoor, anayewania kwa tiketi ya CCM.

Hatua ya Makongoro kumtaka Leticia aache kutumia jina la ukoo wa Nyerere katika shughuli za kisiasa, aliifanya juzi alipokuwa akizungumza katika uzinduzi wa kampeni za CCM, katika Jimbo la Kwimba.

Kampeni hizo zilizinduliwa katika mji mdogo wa Hungumalwa, wilayani Kwimba.

Katika uzinduzi huo, Makongoro alielezea kushangazwa kwake juu ya hatua ya viongozi wa Chadema na Leticia, kutumia jina la ukoo wa Nyerere katika kujinadi kwa wapiga kura.

Alisema hata hivyo kitendo hicho kinacholenga katika kumwezesha mgombea huyo wa Chadema kuchaguliwa, hakitasaidia hata kidogo kushinda katika uchaguzi huo.

Alisisitiza kuwa ni makosa kwa mgombea huyo kutumia jina la ukoo wa Nyerere kujinadi, hasa ikizingatiwa kuwa ndoa baina yake na mdogo wake (Madaraka) haipo tena.

Kwa mujibu wa Makongoro, wanandoa hao walitengana miaka 12 iliyopita baada ya kutofautiana.

"Huyu anayejiita Leticia Nyerere hasemeshani na Madaraka, achilia mbali hata kusalimiana, sasa anatumiaji jina la ukoo wetu. Angalau mimi naweza kuzungumza naye, ni kweli alikuwa mke wa mdogo wangu na alibahatika kuzaa naye watoto watatu lakini mambo ya ndoa wengi mnayajua, sasa siyo mke wake tena," alifafanua.

Alisema ingawa hataki kuingia kwa undani kuzungumzia mgogoro kuhusu ndoa hiyo, alisema yeye na mkewe Jaji Aisha Nyerere, ndio walikuwa wasimamizi.

Alisema katika ndoa hiyo, hayati Mwalimu Nyerere, alitoa ng'ombe 30.

"Huo ni uongo, ninawaomba wananchi wa Jimbo la Kwimba muuachana naye na kumchagua mgombea wa CCM Shanif Mansoor," alieleza makongoro Nyerere.

Makongoro alidai kuwa wakati wa harusi, yeye alikuwa ofisa wa jeshi na mke wake alikuwa hakimu.

Pia alisema mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chadema, Dk. Wilbroad Slaa, amekuwa akimtumia Leticia kama mtaji wa kisiasa katika kuomba kura.

Katika hotuba yake, Makongoro pia alisema Dk Slaa naye anapoteza muda mwingi kuzungumzia ufisadi, wakati jambo hilo limeshashughulikiwa na Serikali ya Awamu ya Nne.

Alisema serikali imeshughulikia jambo hilo, kwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa.

"Ufisadi ni sawa na kibaka, fisadi anaweza kuwa upande wowote, mbona hata kwao wana mafisadi kibao,ufisadi ni tabia ya mtu,CCM iko safi na ndio maana tumekuwa tukiendesha kampeni zetu kwa ustaarabu bila kutumia matusi. Wnanchi msidanganywe na hoja ya ufisadi mwacheni Dk Slaa aendelee kupiga kelele kuhusu ufisadi,",alisema.

Kwa upande wake, Mansoor alisema akichaguliwa kuwa mbunge, atamaliza matatizo ya maji, huduma za afya na upungufu wa walimu katika shule za jimbo hilo.




Namfahamu vizuri Makongoro, sekondari alichapwa viboko alipo jibu swali la nani rais wa Tanzania naye akajibu "Babangu" Wakina nyerere mbona wapo kila mahali Tanzania???????????? Umaarufu wa Baba wa taifa mbona ulileta wa kina nyerere nchi nzima??? kwa mila nyingi za kiafrica watu wengi huweka kumbukumbu zao kutokana na jambo kuu (remarkable ) lilokuwapo kipindi hicho, Leo tangu nyerere kutawazwa ni miaka karibu 50 je ? walioitwa wakina Nyerere leo hawana watoto wenye ubin wa jina hilo????!! je sheria inawazuia kutumia jina??????? ACHENI HIZO.
 
Huyu naye aache kuchemka.

Mbona Tina Turner anatumia jina la Mumwe hadi leo na walishaachana zamani saana na mumewe kufariki.

Mbona Vivian Ndour anatumia jina la NDOUR ingawa walishaachana na mdogo wake Youssour Ndour?

Mifano ipo mingi saaana.

Hapa nawawekea kibao alichotesa watu roho akiwa na Phillip Monteiro:


Chini mwenye nguvu anaweza kuangalia wakati Bibie akiimba kwa jina la Viviane Chidid yaani hapo alikuwa hata bado hajaolewa. Ila pamoja na kuachana, waweza kuona Clip walizoimba pamoja tena na Youssour Ndour na hii imefanya watu wengi wafikiri ni mtu na dada yake wakati ukweli ni kuwa ni mtu na Ex-Shemeji yake. Youssour alikuwa bado Yanki ile mbaaaya yake.

YouTube - Youssou Ndour & Viviane Chidid Seven Second Live
 
Last edited by a moderator:
Hapa makongoro kanoa step; kama ni kweli mama huyu alikuwa ameolewa na mtoto wa Nyerere na katika kipindi cha ndoa yao akawa amebadili jina na kuitwa Leticia Nyerere. bado ana haki ya kutumia jina hilo hata kama wameshatalikiana lasbda kama yeye mwenyewe atataka kubadili tena. Ndiyo maana hata mama yake mzazi Maria Nyerere anaendelea kuitwa hivyo ingawa kwa sasa hivi siyo mke wa Nyerere tena

Kosa ni kama ataendelea kujitambulisha kama mke wa Madaraka, ila kama anajitambulisha kama mtariki wa Madaraka ni haki kabisa.
 
Ex-husband wa Leticia, Madaraka, HAJALALAMIKA. Nini kiherehere cha Makongoro? Mzee, kama umeishiwa hoja, kaa kimya! Angerudi Mwalimu angekuchapa bakora hapo ulipo!
 
Mbona Mama Maria anaitwa Maria Nyerere wakati Ndoa yake na Nyerere haipo tena ( Tena Imetenganishwa na Mungu). Graca Machel pamoja na kuolewa na mandela lakini bado anaendelea kutumia jina hilo hilo! Hapa Mkulu makongoro kweli umetokota
 
Huyu aliwahi kukimbia kulipa bili ya bia pale Fourways ya zamani kule masaki....tukamlipia kwa heshima ya babaye na kwa kuwa alikuwa Anakunywa SAFARI...

Ka vile ulikuwa unanisoma. Na kwa kupenda bia za bure huyooooooooo! basi zake ni pale kaunta. Njaa kali wako wengi huko CCM.
 
Makongoro akimpinga huyu Leticia,that is just as it should be,kwa sababu huyu ni mpinzani wake wa kisiasa. Isipokuwa, as far as the Nyerere Family is concerned,mimi napinga hili jambo. Kama Leticia anataka kuwa Mbunge,wa wapi kule,Serengeti?,sisi,Familia ya Nyerere hatuwezi kuwa na sababu ya kupinga au kusema kwamba akichaguliwa itakuwa ni jambo baya kwetu. Yuko mtu mmoja nilisema kuchaguliwa kwake hakuwezi kuifurahisha Familia ya Nyerere. Na huyo mtu hakuwa Leticia. Huyo mtu sasa hivi siwezi kumtaja sasa ,kwa sababu conditions zimekuwa difficult.
No,hata kama timu ya mpira,kwa mfano Young Africans,wakimfukuza mchezaji. Yule mchezaji akiondoka Yanga akienda kwenye timu ya Simba,sidhani kama Yanga watasema,''Msimuajiri huyo.''
Kwa hiyo sisi Familia ya Nyerere hatupingi Leticia kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Serengeti. In fact,sisi Familia ya Nyerere,ni lazima,lazima,lazima tuwe non-partisan,tuwe watu ambao hatujali nani anachaguliwa Rais,nani anachaguliwa Mbunge au nani anachaguliwa diwani.
Again,nasema sipingi Makongoro kumpinga Leticia. In fact,namuunga mkono Makongoro kumpinga Leticia,lakini kama Familia,wa are non-partisan.
 
Huyu Makongoro kweli kichaa mimi sikutaka kuamini siku zote toka zamani tukikutana. Yaani hii inaonyesha wazi jinsi mtu huyu anavyowatazama wanawake kama chombo cha kutumiwa na kubwagwa anapotaka. Yeye nani kuamua nani anatakiwa kutumia jina la Nyerere na nani hatakiwi?.. Hata kama hakuolewa na Madaraka bado mtu yeyote anaweza badilisha jina lake na kujiita Nyerere maadam amepitia sheria za kubadilisha jina acha mbali huyu mke alozaa watoto wenye kutumia jina la Nyerere kama babu yao.

Ukisha oa na mke akachukua ubini wa jina lako hapo kisheria tayari ni jina lake yeye mhusika ambaye pekee ndiye anaweza kuamua kutolitua tena..
 
Makongoro akimpinga huyu Leticia,that is just as it should be,kwa sababu huyu ni mpinzani wake wa kisiasa. Isipokuwa, as far as the Nyerere Family is concerned,mimi napinga hili jambo. Kama Leticia anataka kuwa Mbunge,wa wapi kule,Serengeti?,sisi,Familia ya Nyerere hatuwezi kuwa na sababu ya kupinga au kusema kwamba akichaguliwa itakuwa ni jambo baya kwetu. Yuko mtu mmoja nilisema kuchaguliwa kwake hakuwezi kuifurahisha Familia ya Nyerere. Na huyo mtu hakuwa Leticia. Huyo mtu sasa hivi siwezi kumtaja sasa ,kwa sababu conditions zimekuwa difficult.
No,hata kama timu ya mpira,kwa mfano Young Africans,wakimfukuza mchezaji. Yule mchezaji akiondoka Yanga akienda kwenye timu ya Simba,sidhani kama Yanga watasema,''Msimuajiri huyo.''
Kwa hiyo sisi Familia ya Nyerere hatupingi Leticia kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Serengeti. In fact,sisi Familia ya Nyerere,ni lazima,lazima,lazima tuwe non-partisan,tuwe watu ambao hatujali nani anachaguliwa Rais,nani anachaguliwa Mbunge au nani anachaguliwa diwani.
Again,nasema sipingi Makongoro kumpinga Leticia. In fact,namuunga mkono Makongoro kumpinga Leticia,lakini kama Familia,wa are non-partisan.

Mkuu Mbona unajichanganya katika maneno yako?
 
Tena kwa mila na desturi za KIZANAKI ndoa huwa hazivunjiki. Kama Leticia kaendelea kuzaa hata baada ya kutengana na Madaraka watoto ni wa Madaraka!

Kuna madai kutoka baadhi ya Wazanaki wanaoijua familia kwamba hata Nyerere mwenyewe si mtoto wa Chifu Burito Nyerere, alipata "uNyerere" kwa style hiyo hiyo, baada ya mama yake kutoka kwa Chifu Burito, lakini kwa mujibu wa mila hii ikabidi aukwae uNyerere tu. Hamna mwanahistoria anayeweza kuchunguza hili Tanzania.

Funny things. Bitter politics. Family dirty laundry tossed open in the air for political expediency.

Haya ndiyo matokeo ya kuwafanya watu waamini kwamba jina la Nyerere lina upako fulani wa kitakatifu.

Watu wameona Nyenyere, nini Nyerere.
 
Siasa za Tanzania hizo.
Nyerere ana Makongoro
Mwinyi ana Hussein
Malima ana Adam
Kikwete ana Riz One
Makamba ana January

All are rubbish

Mhe. Mmakonde,

Umesahau kwamba Kawawa ana Vita
Nnauye ana Nape
Sijaona ana,???......jazia hapo
 
Yaliyofanywa na Makongoro ni unyanyasaji mkubwa kijinsia. Leticia anazo haki zote za kutumia jina la Nyerere kwa sababu alifunga ndoa takatifu katika kanisa Katoliki. Kuingiza mambo ya ndoa ya mtu kwenye mambo ya siasa ni dalili za kufilisika. Mwacheni Leticia ahukumiwe na achaguliwe na wananchi kwa uwezo wake binafsi. Naamini kabisa Mzee Kambarage Nyerere angelikuwa hai wala Makongoro asingethubutu kunyanyua mguu wake kwenda kumchafua shemejiye. Makongoro amejiaibisha sana!

Wakina mama wa tz mko wapi katika hili? wanawake mlio wanaharakati bila kujali vyama vyenu hamuoni huu ni unyanyashaji wa kijinsia? hamuoni kuwa anatengeneza mkakati wa kuwadhalilisha kwa kutumia majina ya waume zenu. Huyu makongoro ana bahati sana amelisema hili akiwa tz ambako wanasisiem hawaguswi kwa maovu wanayowafanyia wananchi wengine!! vinginevyo kama angekuwa yuko afrika ya kusini ,angepigwa mbooko hadharani na kutobolewa macho!!!!
 
Madaraka amechakachuliwa akili yake mke wa ndugu yake aliyezaa naye watoto wa tatu anaenda kumnyanyasa kijinsia kwa aina hiyo mbele ya Umma ,anadhani watoto wa ndugu yake watakuwa na heshima naye kweli mtu anaenda kumdhalilisha mama yao mbele ya jamii kwa kuendelea kutumia jina mpaka leo,huu ni utamaduni uliobaki kwa wanawake wengi wa Tanzania ambao waliolewa na wakaachika na waume zao lakini pindi wakiwa wamezaa na hao wanaume wameendelea kutumia majina ya waume zao kwa sababu nyingi tu zikiwemo nyaraka za kikazi,passport na hata elimu huw wanaona taabu tena kwenda mahakamani kuapa na kuanza kugeuza kila kitu.
Kuna wengine maarufu hapa Afrika ambao bado wanatumia majina ya waume zao akiwemo Winnie Mandela na Graca Machelle ambaye ni rafiki wa familia ya Nyerere kwa hiyo Madaraka asimnyanyase huyo mama kisaikolojia na sidhani wananchi watamsikiliza kwa huo ujinga wake.
FROIDA nikusahihishe kidogo aliyechakachuliwa akili ni Makongoro na si Madaraka kama ulivyoeleza, Madaraka mwenye mke yupo kimya wala ajazungumzia mkewe kugombea ubunge wala kutumia jina la Nyerere hila vuvuzela Makongoro ndio yupo hewani. Wala haelewi kumdhalilisha shemejie ni kuzalilisha watoto wao na nduguye Madaraka. Kweli njaa mbaya na kufulia usiombe Makongoro unadai hadi jina.
 
Katika ukoo wa Nyerere wapo watu wengi mno lakini aliyelibeba jina ni Julius Kambarage Nyerere na kwa mbali mdogo wake Joseph Nyerere lakini tukumbuke hata jina la JULIUS sio la kizanaki bali mwalimu alilichagua wakati anabatizwa. Je waje wenye asili ya jina la Julius walidai maana sio la kiafrika? Pili Makongoro wakati akiwa mbunge wa Arusha Mjini kupitia NCCR MAGEUZI kuna mwanaCCM mashuhuri hivi aliwahi kusema Makongoro sio mtoto wa mwalimu kutokana na mambo yake na kuasi chama, Mwanasiasa huyo alishambuliwa sana ili kulinda heshima ya mama Maria kuwa hana mtoto wa nje ya ndoa, pamoja na matusi na udhalilishwaji huo kichwa maji huyo wa mwalimu akarudi CCM, baada ya wakina MKONO NIMROD kumuhakikishia kumpatia uenyekiti wa CCM mkoa. Makongoro inabidi aelewe kuwa NYERERE ni jina kama MADENGE, NIPASHE, KOMBA, NGURUWE, MCHAMBAWIMA nk. Jina NYERERE limepata umaarufu sababu ya JULIUS KAMBARAGE kuwa kiongozi muadilifu na mfano hadi waTZ tukakubali kumuita baba wa TAIFA. Lakini akumbuke waafrika wanautamaduni wa kuenzi viongozi wanao wapenda kwa kuwapa watoto wao majina ya viongozi hao mf kuna watanzania wengi wanaitwa SAMORA , MANDELA, MUGABE, OSAMA nk. Kimsingi wenye majina hayo wala hawana nasaba na koo husika. hivyo jina ni jina tu. mtu anaweza kuitwa FISI na bado akawa kiongozi mzuri kuliko mtu anayeitwa NYERERE mfano mzuri ni wewe mwenyewe Makongoro ulichemsha katika ubunge Arusha japokuwa ulitumia jina la NYERERE. Wanachi watamchagua au kumkataa LETICIA kwa kupitia sera za chama chake na uwezo wake nasi kwa jina la NYERERE. kama jina la NYERERE ni mtaji basi wewe gombea urais 2015 uone kama utashinda? Tena kumbuka kuweka majina yote muhimu MAKONGORO JULIUS KAMBARAGE BURITO NYERERE wa KIJIJI CHA BUTIHAMA mtoto wa MARIA NYERERE.Acha mambo ya kizamani yakila mtu kujidai anatoka ukoo wa kichifu, au kila baba yeye alikuwa wa kwanza darasani, kumbuka umaarufu wa ukoo wa NYERERE unabebwa na JULIUS KAMBARAGE na si kila mwana Ukoo. Akili, BUSARA na uadilifu ni wa JULIUS KAMBARAGE nasi wakila mwana Ukoo wa Nyerere mbona wewe dk tano mbele na bado ni Nyerere tu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom