Makongoro aibuka na kudai mafisadi wako 4 ndani ya CCM

mahanga.jpg


Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk Makongoro Mahanga.

Na Na Leon Bahati

NAIBU Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk Makongoro Mahanga amesema makada wa CCM wanaodai kupambana na ufisadi wanapaswa kudhibitiwa ili wasikivuruge chama kwa kuwa mafisadi ndani ya chama hicho hawazidi wanne.

Akizungumza na gazeti hili jana Mahanga ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, alisema makada hao wasipodhibitiwa watakivuruga chama na kukifanya kipoteze viti vingi vya ubunge kwa wapinzani katika uchaguzi mkuu mwakani, kwa kudhaniwa kimejaa mafisadi.

"Hawa wanaoitwa mafisadi wako wangapi? Mbona hawatajwi?" alihoji Dk Mahanga akibainisha kuwa tathmini yake inaonyesha kuwa kelele zote za ufisadi zinawalenga watu ambao hawazidi wanne ndani ya chama hicho, na kwamba miongoni mwao, tayari wameanza kushughulikiwa.

Alipotakiwa kuwataja hao mafisadi wanne, Mahanga alisema hiyo ni tathmini yake na hakuna haja ya kutaja majina yao kwa vile wanafahamika.

Kwa kauli hiyo, Dk Mahanga anakuwa mtu wa pili ndani ya CCM kupingana na Makamu Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, John Malecela ambaye Ijumaa iliyopita alitoa kauli kutaka mafisadi wadhibitiwe kwa nguvu zote, ili wasikiweke chama katika wakati mgumu kwenye uchaguzi huo. Tayari kauli hiyo imepingwa na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba.

Lakini jana Dk Mahanga alisema ajenda ya ufisadi imekuwa ikitumiwa vibaya na watu ambao wanafikiri wanajijengea mazingira mazuri kisiasa ili washinde ubunge mwakani, lakini hawafikirii kwamba njia wanayoitumia inalenga kuiharibia CCM.

"Kuna watu ndani ya chama wamedhamiria kuiangusha CCM huku wakijifanya wanapambana na mafisadi ndani ya chama," alisema Dk Mahanga jana katika mahojiano na Mwananchi Jumapili na kuongeza:

"Kama wapinzani wangesimama majukwaani wakisema ndani ya CCM kuna mafisadi, hakuna mtu ambaye angeshangaa kwa sababu malengo yao ya kisiasa ni kukichafua chama tawala ili kianguke na wao wachukue nafasi hiyo," alisema Dk Mahanga ambaye pia ni Mbunge wa Ukonga.

"Suala hilo linapozungumzwa hadharani na wanachama wa CCM ni hatari. Hapa wanakichafua chama na ndio wanaosaidia vyama (vya siasa) vya upinzani," alisema.

Naibu waziri alishauri: "Kama kuna tatizo, lipelekwe kwenye vikao na siyo kwenda kupiga kelele kwenye majukwaa na kukichafua chama machoni pa wananchi."

Alipoulizwa kama haoni kulizungumzia suala hilo hadharani kutasaidia kuzuia ufisadi nchini, alisema: "Namna suala hilo linavyozungumzwa sasa, inaonyesha kana kwamba kuna kundi kubwa la wanaCCM wanaojihusisha na ufisadi, lakini ukweli ni kwamba watuhumiwa wa ufisadi, hawazidi wanne."

Kuhusu kuwepo kwa mtandao wa watu ndani ya CCM waliopanga mbinu za makusudi za kuwaangusha wabunge waliopo mstari wa mbele kwenye mapambano dhidi ya ufisadi, Mahanga alisema:

"Huo ni woga tu. Hakuna kitu kama hicho. Naunga mkono maelezo yaliyotolewa na Katibu wangu Mkuu (Yusuf Makamba) kupitia gezeti lenu (Mwananchi) toleo la leo jana akisema hayo ni mambo ya kufikirika," alisema Dk Mahanga.

Alisema kuwa woga huo unatokana na baadhi ya wabunge kuwa na wasiwasi kwamba, wanachama wengine ndani ya CCM wanaweza kuchukua nafasi zao, hivyo kutumia suala la ufisadi kama njia ya kupambana nao.

Alitoa mfano kuwa katika jimbo lake tayari wamejitokeza wana-CCM saba wanaotaka kumrithi, lakini hapigi kelele kwa sababu anajua ni haki yao ya kikatiba na hana wasiwasi na yupo tayari kupambana nao kupitia michakato ya uteuzi ndani ya CCM.

"Hili liko wazi. Hata wengi wao mwaka 2005 kwenye majimbo yao walikuwepo wabunge ambao waliwaondoa na kuchukua nafasi zao," alisema Dk Mahanga.

Alisema hata kama watu wachache wanaodaiwa kuwa ni mafisadi wakifukuzwa ndani ya CCM bado suala la wabunge kupata upinzani ndani ya chama litakuwa pale pale.

Aliwataka wana-CCM wenye nyadhifa mbalimbali kufahamu kuwa wapo wanachama wengi waliokuwa wanazitamani na hata sasa wanazitaka nafasi wanazozishikilia na wakati huo huo wapo wapya wanaojitokeza kuziwania.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Zamani, Cleopa Msuya amesema kwamba msimamo wa serikali kuhusu mafisadi unajulikana na tayari vyombo vyake husika vimeanza kuwashughulikia, hivyo akataka visiingiliwe,viachwe vifanye kazi yake.

"Mimi sina cha kusema juu ya hilo tatizo, tunaandika sana, hebu tuviachie vyombo vya utekelezaji vifanye kazi yake," alisema Msuya ambaye alikuwa waziri mkuu katika utawala wa serikali ya awamu ya kwanza na ya pili.

Fisadi Mkapa, Papa fisadi RA, fisadi Mramba, Fisadi Chenge, Fisadi Karamagi, Fisadi Makamba, Fisadi Lowassa, Fisadi Msabaha and the list goes on. Aaache usanii huyu wa kuturushia Watanzania changa la macho.
 
- Mahanga alimjia juu Muungwana, kwenye kikao cha NEC Butiama kwamba kwa nini Lowassa anasingiziwa mambo ya Richimonduli wakati ukweli ni kwamba hana makosa kabisa, akamtaka Muungwana na CCM tena kwa ukali sana kutoa tamko kali la kumsafisha Lowassa kwamba hana makosa, Muungwana hakujibu.

- Kilichofuatia waziri akahamishiwa wizara maarufu sana kwa wanosubiri kutupwa nje, wa kwanza wizara hiyo alikuwa Mzee wa Kiraracha.

Respect.

FMES!
 
Rev.Kishoka mimi sina la kusema kwa muda huu ila najiuliza huyu jamani dr kwa mitishamba ama doc wa PhD ana Vet ?

Nashukuru kwa swali lako mkuu LUNYUNGU!

Makongoro Phd yake WIZI MTUPU, ni kama ya Kamala, Nchimbi, Nagu na wengine kibao ndani ya Chukua Chako Mapema (CCM).

Hizi Phd zinatolewa na chuo flan online kinaitwa CommomWealth Open University. Ukiwa na US dollar 5,000 (sina uhakika kama imeishapanda) unapewa Phd in a year.

..........Send us copies of your transcripts and we will develop a customized degree plan stating exactly what is needed to complete your doctorate in the shortest time and least cost.

Source:
http://www.commopu.org/commprog.htm

HABARI NDIO HIYO!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Nashukuru kwa swali lako mkuu LUNYUNGU!

Makongoro Phd yake WIZI MTUPU, ni kama ya Kamala, Nchimbi, Nagu na wengine kibao ndani ya Chukua Chako Mapema (CCM).

Hizi Phd zinatolewa na chuo flan online kinaitwa CommomWealth Open University. Ukiwa na US dollar 5,000 (sina uhakika kama imeishapanda) unapewa Phd in a year.

..........Send us copies of your transcripts and we will develop a customized degree plan stating exactly what is needed to complete your doctorate in the shortest time and least cost.

Source:
http://www.commopu.org/commprog.htm

HABARI NDIO HIYO!!!!!!!!!!!!!!!!!!

sasa haya sio majadiliano bali ni taarabu
 
mwenye email yake au simu ya mkononi naomba ampatie haya majina.
Mafisadi ndani ya CCM
mkapa
apson
mboma
chenge
mgonja
rostam
dr idrisa
karamag
lowassa
arthur
mo-Dewji
JK
makamba
londa
naomba muendeleze list halafu apelekewe Dr makongoro ili awatete hao mafisadi ili akisafishe chama chake chenye mayai ya ufisadi, rejea Generali Ulimwengu.

Anapatikana kwenye +255 784 337755 ama mmahanga@parliament.go.tz.
 
ila huwa anajitahidi sana kutetea mafisadi, nasikia alikuwa ktk kikao cha EL pale dodoma kupanga mikakati ya kumsafisha

H O N G E R A S A A N A

Huyu Makongoro, Adam Malima, Masha na Serukamba ndio maboi wakuu wa Lowassa katika mbinu za kumsafisha ili aje aukwae Urais huko mbele.Bahati nzuri wananchi wamekwisha wastukia na wote wamo katika list ya endangered wabunge watakaofyekwa mwakani!
 
kwa kuwa mafisadi ndani ya chama hicho hawazidi wanne.

Hii ni big joke,
Kwahiyo kwakuwa ni wanne tu ni sahihi? Na kama the rest ni clean kwanini wasiwatimue hao wanne waache kuwatia doa badala yake wana wakumbati kwa nguvu zote na garama yoytre ile?

Anasahau kwamba samaki mmoja akioza wote wameoza? Kwa taarifa yake yake ni kwamba kapu la samaki CCM linatoa harufu kali ya uvundo haijalishai wameoza wanne tu, kama wanataka haurufu iishe wawaondoshe hao walo oza, ama wakubali tulitupe kapu zima lenye uvundo!
 
Huyu jamaa ni mjinga kupindukia yaani siamini haya aliyoyasema!


Lazima awe mjinga si kuna taarifa hata chuo alichosoma ni feki! sasa tutegemee nini kama sio pumba tupu!
 
Nashukuru kwa swali lako mkuu LUNYUNGU!

Makongoro Phd yake WIZI MTUPU, ni kama ya Kamala, Nchimbi, Nagu na wengine kibao ndani ya Chukua Chako Mapema (CCM).

Hizi Phd zinatolewa na chuo flan online kinaitwa CommomWealth Open University. Ukiwa na US dollar 5,000 (sina uhakika kama imeishapanda) unapewa Phd in a year.

..........Send us copies of your transcripts and we will develop a customized degree plan stating exactly what is needed to complete your doctorate in the shortest time and least cost.

Source:
http://www.commopu.org/commprog.htm

HABARI NDIO HIYO!!!!!!!!!!!!!!!!!!


Huyu jamaa sio PHD tu bali path yake yote ya elimu ya juu ni mashaka makubwa ,ukiniuliza mimi nitasema jamaa ana diploma ya ifm.

-
 
Date::8/10/2009
Spika achochea moto wa Malecela
sitta%202.jpg

SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta ambaye ameunga mkono mjadala ulioanzishwa na makamu mwenyekiti wa zamani CCM John Malecela kuhusu ufisadi unaoendelea kukitafuna chama.

*ASEMA NCHI INA UFISADI WA KUTISHA, ATABIRI UGUMU KWA WABUNGE 2010

Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi


SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta amejitosa katika mjadala ulioanzishwa na makamu mwenyekiti wa zamani wa CCM, John Malecela, akisema ufisadi nchini umefikia kiwango cha kutisha kutokana na baadhi ya watu, wakiwemo wanasiasa kuwa na utajiri ambao vyanzo vyake havina maelezo.

Wiki iliyopita Malecela alikaririwa na vyombo vya habari akisema kuwa suala la ufisadi litawaweka pabaya wabunge wengi wa CCM kwenye uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2010, huku akisema baadhi ya wabunge wanaweza kupoteza viti vyao kutokana na kutoenda majimboni na kutofuata ilani ya CCM.

Kauli hiyo iliibua mjadala baada ya katibu mkuu wa chama hicho tawala, Yusuf Makamba kumjibu mkongwe huyo akisema haoni mafisadi wala ugumu kwa chama kushinda mwakani, huku Naibu Waziri wa Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk Makongoro Mahanga akiibuka na kusema mafisadi ndani ya CCM ni wanne tu.

Jana Spika Sitta, akizungumza na Mwananchi kwa simu akiwa Entebe, Uganda, alisema ufisadi uliopo sasa nchini unatisha na akatabiri ugumu kwa baadhi ya wabunge kurejea kwenye chombo hicho cha kutunga sheria.

"Ahaa... mimi ninachofahamu suala si kusema kuna mafisadi wanne ndani ya chama au wangapi, tunazungumzia suala zima la kuporomoka kwa maadili ya uongozi," alisema Spika Sitta ambaye zaidi ya wiki moja iliyopita aliomba kuongezewa ulinzi akidai kuwa wapinzani wake wa kisiasa wanamuandama, akiwatuhumu kuwa ni mafisadi.

"Unaponiambia sijui kuna mafisadi wanne sikuelewi. Hivi sasa kuna ufisadi mkubwa, watu wana utajiri wa kutisha ambao maelezo yake hayaeleweki.

"Kwa mwanasiasa wa kawaida kuwa na utajiri wa kutisha, inatia mashaka sana."

Sitta, ambaye alijinadi kuwa bunge lake litakuwa la "kasi na viwango" mara baada ya kuvishwa joho la uspika, alisema kuporomoka kwa maadili ndiko kunakofanya kuwepo mafisadi kuanzia ndani ya chama.

"Hivi sasa hakuna miiko ya uongozi ndiyo maana kuna ufisadi wa kutisha, zamani kulikuwa na miiko ya uongozi," alisisitiza.

Aliongeza: "Kwa mfano, mimi nilikuwa mtumishi wa umma kwa miaka 40, lakini nisingeweza kuwa na utajiri kama baadhi ya watu walivyo, sasa iweje mwanasiasa tu wa kawaida uwe na utajiri wa ajabu?" alihoji.

Alisema hata kama wapo wanasiasa wafanyabiashara, bado kuna mashaka na utajiri wao.

"Unaweza kukuta mtu ana magari ambayo idadi yake inatisha; ana majumba mikoani na fedha za ajabu. Utajiri huu unatoka wapi kwa mtu mwanasiasa tu,"alihoji.

Alisema watu siku hizi wanaangalia haki binafsi badala ya maslahi ya umma, ndiyo maana hata baadhi yao hushiriki katika mikabata mibovu ya kifisadi.

"Mtu anachungulia atapata nini katika mkataba fulani, anasahau kabisa maslahi ya jamii,"alisema Spika Sitta.

Kuhusu kauli nyingine ya Malecela kwamba wabunge wa CCM wanaoishi mijini watakabiliwa na wakati mgumu mwakani, alijibu: "Hilo liko wazi.'

Spika alisema siku zote mbunge awe wa CCM au wa chama cha upinzani ambaye haendi jimboni kwa wapigakura wake, ana wakati mgumu kutetea kiti chake.

"Sijui kama wabunge wa CCM ambao watakabiliwa na ugumu jimboni ni wengi au wachache, lakini mbunge yoyote ambaye hayuko karibu na wapigakura wake mwakani atakuwa katika wakati mgumu," alisisitiza.

Alisema kwa kawaida mbunge anapaswa kuwa karibu na wapigakura wake ili kushiriki katika mambo mbalimbali, yakiwemo ya kijamii.

Alisema kuna mambo ya ndani ambayo wananchi wanaamini mtu pekee wa kumweleza ni mbunge, sasa asipokuwa karibu na wapigakura lazima utapata wakati mgumu tu mwakani.

Kuhusu utekelezaji wa ilani ya chama, alisema: "Hilo kwa sehemu kubwa linapaswa kutekelezwa na serikali na imekuwa ikifanyika hivyo, lakini mbunge lazima ufike jimboni."

Pamoja na mambo mengine, Malecela alisema: "Vita dhidi ya mafisadi ni ngumu kwa sababu ndani ya CCM kuna baadhi ya watu wanaokichafua chama kwa tabia zao za kuungana na mafisadi."

Mzee Malecela aliwasha moto huo wakati tayari kukiwa na mvutano mkubwa ndani ya CCM baina ya kambi inayopambana na ufisadi, ambayo imekuwa ikijionyesha waziwazi na ile inayotuhumiwa kuwa ya ufisadi ambayo vita vyake vinaonekana kuwa vya chinichini. Malecela, mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu ya CCM, alienda mbali zaidi alipoonya baadhi ya wabunge kwa tabia zao za kutokwenda kwenye majimbo yao na kwamba, hawafuati ilani ya uchaguzi ya chama hicho.
 
hujamaa anataka kujifanya yeye mafisadi kawa soma kwenye gazeti kuwa ni wanneeeeeee na wakati wanachama chao cha mafisadi kilianzishwa hotelini na huwa wanakutana yeye ni quit ledaaaaa
 
na bado mtatajana sanaaa mwaka huu!
japo ukweli utabaki ule ule mme wadhurumu watanzania wasio na hatia
sida zote walizonazo watanzania ni kwa ajili yenu!
umaskini wote uliopo hapa ni kwa ajili yenu
kuna wakati huwa natamani kuwachapa viboko wabunge lakini mikono ya sheria inatisha.
kwa sisi ambao kwa sasa tunafanya kazi kijijini zaidi hali ni mbaya mno
umaskini unazidi
na sijui kama mambo yatabadilika
mfano mzuri Chamwino kuna njaa mbaya sana lakini wana siasa wamekaa kimya
watu wanakula mlo mmoja si kwamba ni wavivu hapana mvua hazikunyesha vizuri kwa miaka miwili mfululizo lakin hatulioni hili
kweli hali ni mbaya sana japo kwa uchoyo wa wenzetu na ufisadi tulionao tunasababisha matatizo tusio stahili inauma sana.
nimeapa sintafanya kazi kwenye migodi hata watoe dau kiasi gani sipo tayari
kinachoniuma zaidi watu hawa eti nasikia accounti zao ziko nje kiasi kwamba wanasababisha hata hela walizotuibia zisiweze kutuajiri kwa njia nyingine na matokeo yake wazungu wanazungusha wanavyo taka.
tunaweza kulalamika riba mbona kubwa kuliko ulaya itakuwaje ndogo wakati hatujali vya kwetu
wazungu wa idle cash kwa nini wasikopeshane kwa bei nafuu kwanza hela zenyewe zimewekwa na watu wanaogopa kujulikana kwamba wanazo
amini nawaambia kwa hali ilivyo ipo siku tutachinjana habari ndo hiyo hata kama hatukubali inatia hasira sana
 
Yaani mtu ana PhD simple logic tu inamshinda.

Waziri "Hawa mafisadi mbona mnawaogopa? Si wapo wanne tu, tuwataje"

Muandishi "Wanne, tutajie basi"

Waziri "Aaah, hayo ni mawazo yangu tu, mimi si msemaji wa wananchi"

Hilarious, just hilarious.Somebody should cartoon this and make it the textbook example of hipocrisy and buffoonery.
 
Hivi huyu Mahanga ni mbunge wa wapi vile? Bila shaka kwa kauli hii ameshapoteza kiti chake cha Ubunge 2010. Sidhani kama waTz waliochoshwa na ufisadi wanaweza kumpa tena kura zao mtu mwenye upeo mdogo kama huyu. Lakini hawa ndio mawaziri wetu!
 
.....yule Mweka hazina wa CCM kwenye kesi ya EPA

Sure!
Yule bwana mweka hazina wa sisiemu anaitwa Shabani Maranda

.....namjua Rostam Aziz aliwahi kuwa mweka hazina SISIEMU. Wengine siwakumbuki......

Mkuu, sio Rostam, ni huyo bwana niliyemtaja hapo juu


Kifupi hupaswi kumshangaa Mahanga ila tushangae sisi wana Ukonga tuliemweka madarakani,


Elimu na madarasa yake aliohudhuria hayakutosha kumfuta ujinga, bado ana kiwi cha macho machoni.

Hakika!
Mafisadi ni wale wanaowaweka viongozi wabovu madarakani, Mwakani nitapiga kura katika jimbo la Mahanga , hakika sitampa kura yangu kamwe!
 
Ndani ya serikali ya Tanzania Certificates ni mtaji wa kupatia vyeo. Kwa hiyo wafanyakazi wengi wako busy, siyo kudeliver au kuperfom kazi walizopewa, bali kusaka certificates ili ziwape turufu ya kupaa. Si wote, lakini PHD na Masters nyingi humo serikalini ukizipeleka kwenye private sector zinaflop vibaya mno.

Therefore si ajabu kuwa accademic credentials haziko proportional na analytical au intellectual capacity ya walio wengi. Huyu anayejadiliwa hapa ni representative wa kundi hilo!
 
Makongoro Ni mbunge wangu wa jimbo la Ukonga, huyu bwana vikao vyake vya mikakati alikua anavifanyia pale banana, kuna bar moja maarufu inaitwa ANGELS BAR, au Tarime bar almaarufu kwa Chota, hapa ndipo alipokua anaanzishia mashambulizi na alipata msaada mkubwa wa Wakurya na wajaluo wanaoishi kipunguni.....bado mbinu zake tunazifatilia, ila naamini uchaguzi mkuu ujao atadondoka kama wapinzani wake ndani ya chama watajipanga vizuri, au kama mission ya wapinzani kuchukua majimbo yote ya Dar es salaam itaungwa mkono na umma,

Kifupi hupaswi kumshangaa Mahanga ila tushangae sisi wana Ukonga tuliemweka madarakani,

Elimu na madarasa yake aliohudhuria hayakutosha kumfuta ujinga, bado ana kiwi cha macho machoni.


Mkuu Papa Sam,

Siku hizi amehamisha kijiwe, anafanyia vikao kwenye baa moja imejificha ndani kidogo eneo jipya la makazi linaitwa MONGOLANDEGE almaarufu MONGOLA.

Hiyo maskani mpya inaitwa MPERA PUB. Iko pembeni mwa kibarabara kinachochepuka kushoto mara tu baada ya kuvuka daraja kama unakwenda segerea ukitokea majumba sita.

Ni hivi karibuni tu mwezi wa tano na wa sita alikuwa anakutana na wapambe wake pale wakala nyamachoma na kufungua ze lagaz kwa wingi.Na kampeni zake zimeshaanza tena kwa kasi.Mojawapo ya watu wanaotajwa kutaka kumkabili ni diwani wa kata ya ukonga kijana Jery Slaa.

Sasahivi sio wakurya wote wanomuunga mkono jamaa kama zamani. Kuna siku nilimtembelea rafiki yangu anakaa kipunguni, tukawa tumekaa Ngemo annex(iko banana), tukawa tunapata moja moto moja baridi, kukaibuka malumbano makali sana kati ya wapambe wa Mahanga wanamfanyia kampeni ili arudi mjengoni na wale wanaompinga.Ilikuwa ni wiki moja baada ya kufanya kikao MPERA PUB.

Vilevile kuna habari nilizisikia hapo ngemo siku hiyo kwamba Chadema wanajiandaa kumsimamisha Mwita Mwikwabe Waitara kukabiliana na bw.Mahanga.

Na kama kweli Waitara ana mpango wa kugombea ubunge Ukonga, basi Mahanga anayo kazi pevu, maana potipoti wanasema hawatamuunga mkono mahanga tena! eti bora wampe kura kijana wa nyumbani, mahanga ameshindwa kuwajengea barabara ya lami hadi kitunda, mwanagati, kivule na machimbo kama alivyowaahidi 2005.

ni hayo tu wadau.
 
Back
Top Bottom