Makonda: Wakuu wa mikoa tuliwapinga machinga, Magufuli akawaunga mkono, nasi tumewaunga mkono

Nucky Thompson

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
1,817
4,058
Mkuu wa mkoa wa Dar Paul Makonda akiwahutubia machinga Kariakoo amesema ana mpango wa kuwabadilisha kuwa watu wanaomiliki viwanda vidogo badala ya kutembeza bidhaa barabarani kwa kuunda uongozi wa kuwasimamia.

Amesema wakuu wa mikoa walikuwa wakiwapinga machinga ila Rais Magufuli amewaunga mkono na hana jinsi nyingine zaidi ya kuwaunga mkono ila atawabadilisha kuwa wakubwa zaidi ili waachaane na kutembeza bidhaa.

 
Unaunga mkono kitu kimoja ambacho kinatoa sadaka kodi, njia za magari, usafi na mipango miji, kitu chenyewe kinaenda kinyume na mikakati ya wataalamu wa mipango miji.

Wewe na uliyeungana naye siyo wataalamu wa kada husika, wataalamu wapo.
Tukuweke kundi gani?
 
Hizi akili hizi basi tu, yani uwabadili machinga kuwa wamiliki wa viwanda vidogo, kwani machinga ni hao tu waliopo au ni generation nzima? Inaweza kuwa idea nzuri lakini haitakuwa ni kwa lengo la kuwafanya watu wasiwe machinga, akitoka machinga mmoja leo kesho atakuja mwingine. Serikali inatakiwa ifungue fursa nyingi ili watu waondokane na idea ya umachinga, mfumo mgumu wa maisha ndo unafanya vijana wengi wawe machinga, serikali isajili vijana kila mkoa na kuwaweka katika makundi ya vijana 10, kila kundi walete idea ya nini wanataka kufanya, wapewe maeneo ya kufanya shughuli zao,serikali iwe mdhamini kwenye mabank wapewe mikopo, wasimamiwe na wataalamu katika wazo lao, kuwe na viwanda vinavyopokea malighafi zitakazozalishwa na hao wajasiliamali, baada ya muda hutaona kijana anafanya umachinga mjini.
 
Ngoja tutoe koment za mwishomwisho JF maana TCRA wameshaingilia kati kuwa haifuati sheria na kuwa itafungwa hii ni baada ya kukosa kile wanachokitaka.
 
Mkuu wa mkoa wa Dar Paul Makonda akiwahutubia machinga Kariakoo amesema ana mpangon wa kuwabadilisha kuwa watu wanaomiliki viwanda vidogo badala ya kutembeza bidhaa barabarani kwa kuunda uongozi wa kuwasimamia
Amesema wakuu wa mikoa walikuwa wakiwapinga machinga ila Magufuli amewaunga mkono na hana jinsi nyinginer zaidi ya kuwaunga mkono ila atawabadilisha kuwa wakubwa zaidi ili waachaane na kutembeza bidhaa

Angejua chanzo na asili ya machinga kabla hajakurupuka kuropoka
 
Mkuu wa mkoa wa Dar Paul Makonda akiwahutubia machinga Kariakoo amesema ana mpangon wa kuwabadilisha kuwa watu wanaomiliki viwanda vidogo badala ya kutembeza bidhaa barabarani kwa kuunda uongozi wa kuwasimamia
Amesema wakuu wa mikoa walikuwa wakiwapinga machinga ila Magufuli amewaunga mkono na hana jinsi nyinginer zaidi ya kuwaunga mkono ila atawabadilisha kuwa wakubwa zaidi ili waachaane na kutembeza bidhaa
Hii bila ya shaka huenda ikawa statement bora kwa mwaka huu!
 
Mkuu wa mkoa wa Dar Paul Makonda akiwahutubia machinga Kariakoo amesema ana mpangon wa kuwabadilisha kuwa watu wanaomiliki viwanda vidogo badala ya kutembeza bidhaa barabarani kwa kuunda uongozi wa kuwasimamia
Amesema wakuu wa mikoa walikuwa wakiwapinga machinga ila Magufuli amewaunga mkono na hana jinsi nyinginer zaidi ya kuwaunga mkono ila atawabadilisha kuwa wakubwa zaidi ili waachaane na kutembeza bidhaa

Hivi huyu kijana ni ndoto ipi aliwahi kutimiza?
1. Walimu kusafiri bure kwenye daladala / kupewa vitambulisho ...
2. Ombaomba kuondolewa jijini Dar ...
3. Shisha vipi?
.. sasa hili la kuwasaidia wamachinga kumiliki viwanda ...
 
Back
Top Bottom