Makonda: Ndoa zote ndani ya mkoa wa Dar es Salaam kusajiliwa

Etwege

JF-Expert Member
Jul 4, 2018
5,661
15,026
Mkuu wa mkoa wa Dares salaam amepania kuanzisha kanzi data ya ndoa zote ndani ya mkoa ili kuwanusuru wanawake wanaotapeliwa kimapenzi na kudanganywa kwamba wataolewa na kuishia kutumika tu bila ndoa.

My take .
Hii idea inaweza kuwa mwiba mchungu mitaa ya ufipa na watakuja kupinga sana kwa sababu ya mwenyekiti wao mpenda totozi( fly to KIA baby)

=====

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam nchini Tanzania, Paul Makonda amesema kuna mpango wa kuanzisha kanzi data ya ndoa zote zilizopo kwenye mkoa wake ili kupunguza utapeli wanaofanyiwa wanawake kwa kudanganywa kuolewa.

pic+makonda.jpg



Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam nchini Tanzania, Paul Makonda amesema kuna mpango wa kuanzisha kanzi data ya ndoa zote zilizopo kwenye mkoa wake ili kupunguza utapeli wanaofanyiwa wanawake kwa kudanganywa kuolewa.

Kanzidata hiyo itahusisha usajili wa ndoa zote ili wanaume waliooa waweze kubainika na kuwanusuru wanawake wasitapeliwe na kuumizwa mioyo kwa kutegemea ndoa.

Makonda amesema pamoja na kanzidata hiyo atatumia mkutano wa SADC kupata uzoefu kutoka kwa nchi nyingine kufahamu namna gani wanakabiliana na utapeli wa aina hiyo.

Mkuu huyo wa mkoa amesema kumekuwepo na malalamiko mengi ya wanawake kuumizwa hivyo wakati umefika wa kuanza kushughulikia.

“Tutaanza kuangalia na kupata uzoefu kwa wenzetu wa SADC ambao kama haya wanashughulikiaje na mkutano ukiisha tutajadiliana kama mkoa tunawezeshaje usajili huo,” amesema

“Kanzidata hii itawasaidia wanawake wasitapeliwe, mtu akitaka kukuoa utaenda mtandaoni na kuangalia taarifa zake, utabaini kama ameoa au la na vilevile itawasaidia hata wanawake ambao wameolewa ili kuzuia waume zao wasioe kwa siri,” ameongeza
 
Mkuu wa mkoa wa Dares salaam amepania kuanzisha kanzi data ya ndoa zote ndani ya mkoa ili kuwanusuru wanawake wanaotapeliwa kimapenzi na kudanganywa kwamba wataolewa na kuishia kutumika tu bila ndoa.

My take .
Hii idea inaweza kuwa mwiba mchungu mitaa ya ufipa na watakuja kupinga sana kwa sababu ya mwenyekiti wao mpenda totozi( fly to KIA baby)
)

kama ni kweli basi takuwa ana nyota ya ndoa.

Hawajifunzi kwa mwenzao Anton Mtaka wa simiyu.jamaa nampendaga bure.amekaa kama waziri wa Maendeleo ya mchi vile.
 
Back
Top Bottom