benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,503
- 2,980
Tarehe 7 mwezi Aprili 2022, kwa mara nyingine tena Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina LM kupitia Chaneli ya Mtandao wa YouTube ya Dar24 alijitokeza hadharani kuishambulia Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe Rais, Samia Suluhu Hassan (SSH) kwa kivuli cha kumshambulia Waziri wa Nishati January Makamba (JM) kwa kile alichokieleza kuwa JM ni mhujumu uchumi ambaye amekuwa akienda kinyume na maagizo ya Rais Samia. Je hii ni bahati mbaya? Unadhani LM amekurupuka?
Kabla hatujasonga mbele sana nikumbushe tu kuwa LM aliwahi kuhudumu kama Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira wakati huo Waziri akiwa ni JM na Makamu wa Rais akiwa ni SSH na mambo hayakwenda sawasawa baina yao sababu LM alihisi kuwa hapewi nafasi ya kusikilizwa sana na SSH na hii ni kutokana na mchango wako kuwa mdogo katika mambo ya Muungano na Mazingira.
Lakini kwa kuwa LM alikuwa anatoka ukanda mmoja na Hayati JPM yeye alikuwa akienda kushtaki kwa "Baba" na alihakikishiwa kuwa kila kitu kitakuwa sawa na hatimaye akapewa Uwaziri wa Mifugo na Uvuvi na JM akavuliwa Uwaziri jambo lililopelekea dharau kushamiri kati yake na JM lakini pia kati yake na SSH akiamini kuwa hana nguvu yoyote bali mwenye nguvu ni JPM pekee.
Muda ukasonga tukapata msiba na leo hii tuko hapa LM ni Mbunge wa kawaida tu, JM ni Waziri wa Nishati, SSH ndiye Rais na Amiri Jeshi Mkuu, na ile iliyokuwa ikiitwa SG karibu yote haina Mamlaka ya kutisha tena.
Sasa SG wameona jiko lina majivu kwa juu hivyo wanatikisa ili kujua chini kuna moto kiasi gani, ili wajue kama utawachoma au wanaweza kuuzima. SG bado wana ndoto za kumuweka Rais wako katika uchaguzi ujao wa 2025, bado hawajaamini kuwa wamepoteza nguvu kabisa na mipango yao ya kidikteta imezimika kama mshumaa uliomwagiwa maji, bado wanachokonoa waone nguvu ya Rais.
KWANINI INASEMWA MPINA AMEMSHAMBULIA RAIS NA SIO WAZIRI
Mpina anagusia agizo la kuondolewa kwa tozo ya Shilingi 100 akisema Waziri alimdanganya Mheshimiwa Rais. Ukirudi katika taarifa toka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu iliyosainiwa Jafar Haniu ya tarehe 05 Oktoba 2021 ilieleza kuwa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ameelekeza kupunguzwa kwa tozo kwenye mafuta zenye thamani ya Shilingi Bilioni 102 kwa mwaka. Rais aliagiza ufanyike haraka mchakato wa kupeleka marekebisho ya Sheria bungeni endapo zipo sheria zinazohitaji mabadiliko ili kukabiliana na kupanda kwa bei ya mafuta (BOFYA HAPA KUSOMA BARUA HIZO).
KAMA MHESHIMIWA RAIS NDIYE ALITOA AGIZO NA LEO HII MPINA ANATOKA HADHARANI KUMKOSOA WAZIRI KWA MAAGIZO ALIYOTOA RAIS NI WAZI KUWA WAZIRI HAPO NI KIVULI TU, ANAYESHAMBULIWA NI RAIS NA MPINA AMETANGULIZWA TU KAMA CHAMBO ILI KUONA RAIS ATACHUKUA HATUA GANI
Baada ya kelele za Mpina Jana (11 April 2022) ameibuka aliyekuwa RC wa Dar es Salaam Paul C. Makonda akieleza kuwa kuna wanaotaka kumtoa uhai kwa mambo aliyoyafanya akiwa madarakani.
Sote tunafahamu aliyoyafanya Makonda, hakuna haja ya kuyarudia, sote tunafahamu furaha alizoleta kwa wananchi lakini tunafahamu machungu machozi na maumivu aliyosababishia Watanzania na pia tunafahamu yeye pia (Makonda) ni mhanga wa SG, hivyo baada ya karata ya kwanza ya Mpina kutoka sasa wamekuja na karata ya pili ambayo ni Makonda. Bado wanapima kuona Rais na Serikali vitachukua hatua gani.
Na hii ni mbinu ya kuirudisha nyuma Serikali kuwachukulia hatua za kisheria wanaostahili, mimi ninamini Rais Samia ni Imara na atasimama kidete kwa maslahi ya nchi, hatoyumbishwa na SG au yeyote na kama kuna anayepaswa kuelekea Segerea kwa makosa aliyoyafanya huko nyuma basi sheria ifuate mkondo wake. SG watulie dawa iwaingie, ule wakati wa kuongoza nchi kwa mkono wa chuma umekwisha, kulialia na kutafuta huruma ya wananchi hakutowarejesha madarakani au kuwapeusha na mkono wa sheria, kwa Serikali hii ya Mama hakuna jiwe litabaki juu ya jiwe lingine, wote tutarudi kwenye mstari
Kabla hatujasonga mbele sana nikumbushe tu kuwa LM aliwahi kuhudumu kama Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira wakati huo Waziri akiwa ni JM na Makamu wa Rais akiwa ni SSH na mambo hayakwenda sawasawa baina yao sababu LM alihisi kuwa hapewi nafasi ya kusikilizwa sana na SSH na hii ni kutokana na mchango wako kuwa mdogo katika mambo ya Muungano na Mazingira.
Lakini kwa kuwa LM alikuwa anatoka ukanda mmoja na Hayati JPM yeye alikuwa akienda kushtaki kwa "Baba" na alihakikishiwa kuwa kila kitu kitakuwa sawa na hatimaye akapewa Uwaziri wa Mifugo na Uvuvi na JM akavuliwa Uwaziri jambo lililopelekea dharau kushamiri kati yake na JM lakini pia kati yake na SSH akiamini kuwa hana nguvu yoyote bali mwenye nguvu ni JPM pekee.
Muda ukasonga tukapata msiba na leo hii tuko hapa LM ni Mbunge wa kawaida tu, JM ni Waziri wa Nishati, SSH ndiye Rais na Amiri Jeshi Mkuu, na ile iliyokuwa ikiitwa SG karibu yote haina Mamlaka ya kutisha tena.
Sasa SG wameona jiko lina majivu kwa juu hivyo wanatikisa ili kujua chini kuna moto kiasi gani, ili wajue kama utawachoma au wanaweza kuuzima. SG bado wana ndoto za kumuweka Rais wako katika uchaguzi ujao wa 2025, bado hawajaamini kuwa wamepoteza nguvu kabisa na mipango yao ya kidikteta imezimika kama mshumaa uliomwagiwa maji, bado wanachokonoa waone nguvu ya Rais.
KWANINI INASEMWA MPINA AMEMSHAMBULIA RAIS NA SIO WAZIRI
Mpina anagusia agizo la kuondolewa kwa tozo ya Shilingi 100 akisema Waziri alimdanganya Mheshimiwa Rais. Ukirudi katika taarifa toka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu iliyosainiwa Jafar Haniu ya tarehe 05 Oktoba 2021 ilieleza kuwa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ameelekeza kupunguzwa kwa tozo kwenye mafuta zenye thamani ya Shilingi Bilioni 102 kwa mwaka. Rais aliagiza ufanyike haraka mchakato wa kupeleka marekebisho ya Sheria bungeni endapo zipo sheria zinazohitaji mabadiliko ili kukabiliana na kupanda kwa bei ya mafuta (BOFYA HAPA KUSOMA BARUA HIZO).
KAMA MHESHIMIWA RAIS NDIYE ALITOA AGIZO NA LEO HII MPINA ANATOKA HADHARANI KUMKOSOA WAZIRI KWA MAAGIZO ALIYOTOA RAIS NI WAZI KUWA WAZIRI HAPO NI KIVULI TU, ANAYESHAMBULIWA NI RAIS NA MPINA AMETANGULIZWA TU KAMA CHAMBO ILI KUONA RAIS ATACHUKUA HATUA GANI
Baada ya kelele za Mpina Jana (11 April 2022) ameibuka aliyekuwa RC wa Dar es Salaam Paul C. Makonda akieleza kuwa kuna wanaotaka kumtoa uhai kwa mambo aliyoyafanya akiwa madarakani.
Sote tunafahamu aliyoyafanya Makonda, hakuna haja ya kuyarudia, sote tunafahamu furaha alizoleta kwa wananchi lakini tunafahamu machungu machozi na maumivu aliyosababishia Watanzania na pia tunafahamu yeye pia (Makonda) ni mhanga wa SG, hivyo baada ya karata ya kwanza ya Mpina kutoka sasa wamekuja na karata ya pili ambayo ni Makonda. Bado wanapima kuona Rais na Serikali vitachukua hatua gani.
Na hii ni mbinu ya kuirudisha nyuma Serikali kuwachukulia hatua za kisheria wanaostahili, mimi ninamini Rais Samia ni Imara na atasimama kidete kwa maslahi ya nchi, hatoyumbishwa na SG au yeyote na kama kuna anayepaswa kuelekea Segerea kwa makosa aliyoyafanya huko nyuma basi sheria ifuate mkondo wake. SG watulie dawa iwaingie, ule wakati wa kuongoza nchi kwa mkono wa chuma umekwisha, kulialia na kutafuta huruma ya wananchi hakutowarejesha madarakani au kuwapeusha na mkono wa sheria, kwa Serikali hii ya Mama hakuna jiwe litabaki juu ya jiwe lingine, wote tutarudi kwenye mstari