Makonda kabla ya kuudanganya umma kuhusu punguzo la bei ya nguo, tueleze kuhusu punguzo la kodi za nyumba kama ulivyoagiza

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,296
217,297
Ikiwa kama watanzania wanaweza kudanganywa na mtu mmoja kama mazombie na bado wakakaa kimya , basi hii itakuwa bahati mbaya sana .

Paulo Makonda ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alitoa amri kwa wenye nyumba kuwapunguzia kodi wapangaji wao kutokana na ugumu wa maisha uliosababishwa na janga la corona , kwa bahati mbaya hakuna hata mmoja aliyemsikiliza , si chama chake cha CCM chenye wapangaji kibao kwenye majengo yake wala wenye nyumba waliomsikiliza , Kwa kifupi ni kwamba alipuuzwa , hii ni kwa sababu lengo la porojo zake hizo ilikuwa kujitafutia umaarufu wa kisiasa .

Kama hiyo haitoshi amewafuata tena " mazombie " na porojo za punguzo la 80% kwa maduka ya nguo ! , sasa hoja yangu ni kwamba kabla ya huu upuuzi mwingine atuambie lile punguzo la kodi za nyumba liishia wapi ?

Watanzania siyo wajinga sana - Magufuli .
 
Ikiwa kama watanzania wanaweza kudanganywa na mtu mmoja kama mazombie na bado wakakaa kimya , basi hii itakuwa bahati mbaya sana .

Paulo Makonda ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alitoa amri kwa wenye nyumba kuwapunguzia kodi wapangaji wao kutokana na ugumu wa maisha uliosababishwa na janga la corona , kwa bahati mbaya hakuna hata mmoja aliyemsikiliza , si chama chake cha ccm chenye wapangaji kibao kwenye majengo yake wala wenye nyumba waliomsikiliza , Kwa kifupi ni kwamba alipuuzwa , hii ni kwa sababu lengo la porojo zake hizo ilikuwa kujitafutia umaarufu wa kisiasa .

Kama hiyo haitoshi amewafuata tena " mazombie " na porojo za punguzo la 80% kwa maduka ya nguo ! , sasa hoja yangu ni kwamba lile punguzo la kodi liishia wapi ?

Watanzania siyo wajinga sana - Magufuli .

Maana nataka kujua kama yule muuza mitumba wangu anajua hizo discount ili niende
 
Chadema lipieni jengo mapewa ruzuku na kuchukua laki saba za wabunge msitegemee msaada wa makonda kupambana na kodi ya jengo lenu la ufipa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom