Sipendekezi arudi kwenye ramani hiyo kwani naamini ameshiriki au kushirikishwa moja ya migogoro mibaya zaidi ya ardhi iliyowaumiza watu wengi na uharibifu wa mali zao eneo ambalo Ana maslahi nalo,iwe ni moja kwa moja,au kwa kushirikishwa kwa manufaa yake,ama wakati akiwa mkuu wa wilaya kinondoni,au akiwa mkuu wa mkoa dsm,hata kushindwa kujitokeza kwenye mgogoro ule au hata tu kusema neno.I do remember Paul Makonda wa awamu ya nne, akiwa UVCCM na badae DC-Kinondoni na Mjumbe wa Bunge la Katiba, alikuwa promising young politician wa taifa letu.
Lakini ilipoingia awamu ya tano, sijui alilishwa nini huyu kijana, sijui km ni u-RC ndio ulimlewesha, sijui allitaka kucopy style ya uongozi ya mteuzi wake, he was a different Makonda from that we used to know. Majority ya WanaDaresalaam walimchukia kutokana na kupenda sifa na kutojali maoni ya wananchi.
Alikuja na campaingn kadha wa kadha zisizo na kichwa wala miguu, alidharau viongozi wenzake kisa tu yeye alikuwa karibu sana na mteuzi kuliko wenzie lakini mwisho wa siku mteuzi wake na yeye akamuona hana maana na akaachana nae.
Leo jina lake lililokuwa halikosekani kwenye vyombo vya habari kila siku halisikiki tena, kifupi ndugu yangu hayupo tena kwenye ramani za siasa nchini. Atafanya juhudi za kurudi tu no matter what but endapo atarudi kwenye ramani za siasa nchini mwambieni awe Makonda wa Awamu ya nne sio yule wa awamu ya tano
Kazi iendelee.