Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,196
- 25,516
Kuna aina mbili za viongozi wa mikoa na wilaya wanaowania Ubunge. Wapo wale wanaowania kwenye majimbo ambayo hayako kwenye mikoa au wilaya walizokuwa wakizioongoza. Na wapo wale ambao wanagombea kwenye majimbo ambayo yapo kwenye mikoa na wilaya walizokuwa wakiongoza.
Nawazungumzia waliokuwa wakuu wa mikoa na wilaya. Paul Makonda na Mrisho Gambo ni kati ya wakuu wa mikoa na wilaya wa naowania Ubunge kwenye majimbo yaliyopo kwenye mikoa waliyokuwa wakiiongoza. Makonda anawania Kigamboni ya Dar es Salaam na Gambo anawania Arusha Mjini kule Arusha.
Kwa jinsi walivyokuwa wakijipambanua, kujitangaza na kuonekana kama wachapakazi na watatuzi wa changamoto za wananchi wao huku wakijisifu kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM, ni rahisi kuamini kuwa wana nguvu kubwa ya kuwaunga mkono ndani na nje ya chama chao cha Mapinduzi.
Leo, zoezi la kuchukua, kujaza na kurejesha fomu za kuwania Ubunge ndani ya CCM limekamilika. Sasa unasubiriwa mchakato wa ndani ya chama kuwapata wagombea wa Ubunge katika majimbo husika. Makonda, Gambo na wanaofanana nao kwa jinsi walivyojichora hawapaswi kushindwa.
Kushindwa kwenye majimbo yao, ndani ya chama au kwenye uchaguzi mkuu, itakuwa ni aibu na kituko cha karne. Itawezekanaje 'wachapakazi na watekeleza ilani' kama Makonda na Gambo kushindwa? Kama ni kweli walikuwa wakiwatumikia vyema wananchi, wanapaswa kutunzwa kichama na wananchi wao.
Karibu ukweli utajianika!
Nawazungumzia waliokuwa wakuu wa mikoa na wilaya. Paul Makonda na Mrisho Gambo ni kati ya wakuu wa mikoa na wilaya wa naowania Ubunge kwenye majimbo yaliyopo kwenye mikoa waliyokuwa wakiiongoza. Makonda anawania Kigamboni ya Dar es Salaam na Gambo anawania Arusha Mjini kule Arusha.
Kwa jinsi walivyokuwa wakijipambanua, kujitangaza na kuonekana kama wachapakazi na watatuzi wa changamoto za wananchi wao huku wakijisifu kusimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM, ni rahisi kuamini kuwa wana nguvu kubwa ya kuwaunga mkono ndani na nje ya chama chao cha Mapinduzi.
Leo, zoezi la kuchukua, kujaza na kurejesha fomu za kuwania Ubunge ndani ya CCM limekamilika. Sasa unasubiriwa mchakato wa ndani ya chama kuwapata wagombea wa Ubunge katika majimbo husika. Makonda, Gambo na wanaofanana nao kwa jinsi walivyojichora hawapaswi kushindwa.
Kushindwa kwenye majimbo yao, ndani ya chama au kwenye uchaguzi mkuu, itakuwa ni aibu na kituko cha karne. Itawezekanaje 'wachapakazi na watekeleza ilani' kama Makonda na Gambo kushindwa? Kama ni kweli walikuwa wakiwatumikia vyema wananchi, wanapaswa kutunzwa kichama na wananchi wao.
Karibu ukweli utajianika!