Makonda awaponza Star Tv na Sahara Media mbele ya TEF

Nafahamu yote hayo Paskali. Lakini ni "implementors" wa mgomo na "determinants" wa nini kiandikwe walikubaliana kwa pamoja kumtenga Bashite. Na katika hili mimi bado nawaona Startv wanayo hatia, kwa sababu hata kama "advertisers" na hapa niwe wazi tu-yaani serikali imewa influence, walikuwa na nafasi ya kushawishi MOAT na TEF kupunguza au kumaliza msusio huo kabla ya kuamua kufanya ambacho tafsiri yake ni usaliti. Startv walikuwa na nafasi ya kuwa katikati kwa kuwa wao wamejifungamanisha na serikali, na wangeweka mambo sawa ndani kwa ndani.

Kinachotokea sana ni kibaya zaidi kwa tasnia na Startv. Sisi wengine tunaona Startv wamekula mlungula na tutaendelea kuwaona hivyo hivyo hata milele, na mimi kama mwananchi ambaye natamani kuona media inaheshimika na viongozi wetu wakiwa na adabu kwa kuwa tunawalipa mishahara, baada ya kipindi hicho kurushwa Jumatatu, sitapeleka tangazo langu Startv wala redio Free Africa. Nitaanza kuwachukia mno!
Mkuu samahani nimepotia conservations zako na Mayala napata picha kuwa kama unachuki na upande wa Makonda badala ya kutafuya fairness itakayokuongoza ktk kuwalaumu Start tv.

Labda nami nikuulize tu hizo adhabu za TEF zimetajwa ktk kanuni gani za miungano yao?

Na je hizo adhabu zina ukomo wa kuanza kutumikia na kumaliza adhabu yako?

Kama adhabu alopewa Makonda haizingatia hayo napenda nikuambie tu hao TET + MOAT waliendeshwa na mihemko ya wenye nguvu ktk vyama vyao bila kujali Principles of natural justice.

Huenda star tv wame review uamuzi wao na kuchukua maamuzi mapya ambayo sioni shida kwa sbb wao ni wanadamu wanapaswa kuwa dynamic.

Ona Gambia walikuwa wanachama wa ICC lkn miezi 3 kabla uchaguzi wao walijitoa uanachama wa ICC sembuse ktk jambo hili la kibiashara mtu aache kuangalia maslahi yake.

Ndio muono wangu huo wakuu Chabusalu + Mayala.
 
Acha u bashite, apigwe bang hadi atakapokufa.
5d470ffe3ca199375a1744105e9669cd.jpg
 
Mkuu samahani nimepotia conservations zako na Mayala napata picha kuwa kama unachuki na upande wa Makonda badala ya kutafuya fairness itakayokuongoza ktk kuwalaumu Start tv.

Labda nami nikuulize tu hizo adhabu za TEF zimetajwa ktk kanuni gani za miungano yao?

Na je hizo adhabu zina ukomo wa kuanza kutumikia na kumaliza adhabu yako?

Kama adhabu alopewa Makonda haizingatia hayo napenda nikuambie tu hao TET + MOAT waliendeshwa na mihemko ya wenye nguvu ktk vyama vyao bila kujali Principles of natural justice.

Huenda star tv wame review uamuzi wao na kuchukua maamuzi mapya ambayo sioni shida kwa sbb wao ni wanadamu wanapaswa kuwa dynamic.

Ona Gambia walikuwa wanachama wa ICC lkn miezi 3 kabla uchaguzi wao walijitoa uanachama wa ICC sembuse ktk jambo hili la kibiashara mtu aache kuangalia maslahi yake.

Ndio muono wangu huo wakuu Chabusalu + Mayala.
Mkuu afnhondya, asante kwa observation yako. Nina mambo machache kurespond. Kwanza, ni kweli sipendi namna ya utendaji kazi wa RC wa Dar. Yapo matukio yaliyonifikisha kwenye hitimisho hilo. Mfano, alivyomdhalilisha yule dada/mama mfanyakazi wa halmashauri ya manispaa Kinondoni, vitendo vyake kwenye Bunge la Katiba ikiwemo "kushiriki kwake kumwokoa Mzee Warioba' pale Blue Pearl, kudhalilisha watu kwenye suala la madawa ya kulevya; etc. Hata hivyo, sina chuki binafsi dhidi ya mtu huyo ambaye anatajwa kwa jina la Makonda aka Bashite. Sina mahali nakutana naye kwa namna yoyote ile kiasi cha kumchukia kama ambavyo andishi lako lilikusudia.

Pili, hili JF hawakuweka sharti kwa wachangiaji kuwa na mtazamo unaofanana mnapojadili jambo. Na ninadhani kutofautiana kimitazamo ndio msingi wa kuanzishwa kwa jukwaa lenyewe. Hivyo basi, mimi na Paskali kutofautiana katika hoja hii it is not a big deal. Ni jambo linalotarajiwa.

Tatu, kuhusu adhabu za TEF kutajwa kwenye kanuni gani, nadhani hapa ni vizuri tukaelewana zaidi. TEF haikuanzishwa kwa ajili kukabiliana na Makonda. TEF ilianzishwa kama kundi lenye kulinda maslahi ya wahariri. Sasa kwamba hakuna kifungu kwenye documents za kuanzishwa kwa TEF haiwaondolei uwezo TEF wa kukutana na kuamua jambo, kama hilo la kusitisha mahusiano na Makonda, kama wanaona kuna sababu za kimantiki za kufanya hivyo. Ni sawa na chama cha waendesha bodaboda cha kijiwe A kuamua kuweka msimamo wa kutompakia mbabe fulani ambaye amekuwa akipanda daladala kisha akifikishwa anakoenda anagoma kulipa nauli kwa sababu tu yeye ni 'mbabe' (huu ni mfano tu, unaweza kuwa usifanane. Nimeutumia kuonyesha kwamba katiba ya waendesha bodaboda hao inaweza isiwe na kifungu kinachowazuia kutompakia 'mbabe' hata kama akiwafanyie ubabe, lakini wao kama wanakikundi wanao uwezo wa kumgomea. Na maamuzi yao yanaheshimika). Kwa mfano huo huo ndio maana unasikia wenye daladala wanagoma; nakadhalika.

Nne, umeuliza je hizo adhabu zina ukomo? Sijui kama unafuatilia hili jambo. Kwa kesi ya Makonda kama umesoma taarifa ya TEF imeweka wazi kabisa kuwa wao waliweka sharti rahisi tu kwamba bwana mkubwa awaombe radhi tu, basi!

Tano, unadai kama adhabu aliyopewa Daud Bashite haikuzingatia hayo uliyoyaona wewe kuwa ni ya "msingi mno" basi TEF na MOAT waliendeshwa na mhemko. Hapa unashangaza kidogo. Yaani watu na kikundi chao wakae chini wafikie uamuzi dhidi ya mtu ambaye wanaona "hajawatendea" vyema, wewe unaibuka unadai walihemka? na kama ni hivyo, Kwanini usiwaone Startv kuwa ndio walihemka kama walishiriki na kubariki uamuzi huo, halafu leo wanawasaliti wenzao?

Sita, unasema huenda Startv wamereview uamuzi ule wa TEF na MOAT+ (vilabu vya mikoani) na kuchukua maamuzi mapya. Hili nimelieleza kwenye post zangu awali. Kwanza sina tatizo na hilo, tatizo litakuwa ni kwa namna gani wamewashirikisha wenzao baada ya kureview. Kwa sababu kama walishiriki pamoja na wenzao kufikia uamuzi kwanini leo wageuke kwa na namna ya usaliti? Wewe huoni hili kuwa lina athari ambayo inagusa jamii pana? Kwamba huoni kama Startv wanahamasiha usaliti katika jamii?

Saba, umetolea mfano wa Gambia kujitoa katika ICC na uamuzi wa Startv ambao katika tafsiri yoyote ile ni usaliti. Sidhani kama mfano huo ulioutoa una fit hapa. Ila kumbuka wahariri wa Startv na wamiliki wa Startv wamekuwa wakinufaika na kuwa kwao wanachama wa TEF na MOAT, hivyo hata kama inajulikana kuwa Startv wako katika mapambano ya kuhakikisha hawafi kabisa hivyo wanaweza kufanya lolote, basi angalau wangelifanya kwa hekima. Nimesema huko nyuma kuwa kwa kuwa wao wamejiegesha upande wa serikali wangeweza kutumia mbinu mbalimbali kushawishi TEF na MOAT ili kwa pamoja waseme basi imetosha muda waliomsusa huyu bosi kubwa wa Dar unatosha, tuanze kufanya naye kazi. Lakini hii njia waliyochagua kuipita haiwezi kuwaacha salama mkuu!
 
Nadhani maelezo yamejitosheleza. Aliyeandika barua hii anaonekana kweli ana weledi wa kutosha katika tasnia ya uandishi wa habari...


Ana weledi kwa kuwa anaandika kama UKIWA wanavyotaka.Star TV wakitangaza nini kitatokea? je wakiungana na waliogoma,wagomaji watamwongezea mauzo ya habari?

Mnalilia uhuru wa habari ila mnataka nyie muwawekee masharti wengine,mnachekesha.Mmegoma mmoja wenu hajaona faida ya mgomo mnaanza kulia.Mmiliki wa Sahara ni Mwenyekiti wa CCM (M) mnatarajia ashiriki ujinga wa kukiumiza chama chake.

Tuungane kuwashawishi wachaga wagome kunywa mbege kwa faida ya Taifa,wakikubali tutamshawishi mmiliki wa Star kuungana na waliogoma.

Vyombo vilivyogoma vingefurahi maana vitapata wateja watakaoikimbia Star,vinginevyo subirini maumivu ya kukimbiwa na wateja wenu endapo Makonda atawashawishi wasikilizaji.
 
Nadhani maelezo yamejitosheleza. Aliyeandika barua hii anaonekana kweli ana weledi wa kutosha katika tasnia ya uandishi wa habari...


Ana weledi kwa kuwa anaandika kama UKIWA wanavyotaka.Star TV wakitangaza nini kitatokea? je wakiungana na waliogoma,wagomaji watamwongezea mauzo ya habari?

Mnalilia uhuru wa habari ila mnataka nyie muwawekee masharti wengine,mnachekesha.Mmegoma mmoja wenu hajaona faida ya mgomo mnaanza kulia.Mmiliki wa Sahara ni Mwenyekiti wa CCM (M) mnatarajia ashiriki ujinga wa kukiumiza chama chake.

Tuungane kuwashawishi wachaga wagome kunywa mbege kwa faida ya Taifa,wakikubali tutamshawishi mmiliki wa Star kuungana na waliogoma.

Vyombo vilivyogoma vingefurahi maana vitapata wateja watakaoikimbia Star,vinginevyo subirini maumivu ya kukimbiwa na wateja wenu endapo Makonda atawashawishi wasikilizaji.
 
Nafahamu yote hayo Paskali. Lakini ni "implementors" wa mgomo na "determinants" wa nini kiandikwe walikubaliana kwa pamoja kumtenga Bashite. Na katika hili mimi bado nawaona Startv wanayo hatia, kwa sababu hata kama "advertisers" na hapa niwe wazi tu-yaani serikali imewa influence, walikuwa na nafasi ya kushawishi MOAT na TEF kupunguza au kumaliza msusio huo kabla ya kuamua kufanya ambacho tafsiri yake ni usaliti. Startv walikuwa na nafasi ya kuwa katikati kwa kuwa wao wamejifungamanisha na serikali, na wangeweka mambo sawa ndani kwa ndani.

Kinachotokea sana ni kibaya zaidi kwa tasnia na Startv. Sisi wengine tunaona Startv wamekula mlungula na tutaendelea kuwaona hivyo hivyo hata milele, na mimi kama mwananchi ambaye natamani kuona media inaheshimika na viongozi wetu wakiwa na adabu kwa kuwa tunawalipa mishahara, baada ya kipindi hicho kurushwa Jumatatu, sitapeleka tangazo langu Startv wala redio Free Africa. Nitaanza kuwachukia mno!
hakuna cha mkungula ,unajua kuwa Balile alipewa hela na wauzaji Wa dawa za kulevya?
 
Nafahamu yote hayo Paskali. Lakini ni "implementors" wa mgomo na "determinants" wa nini kiandikwe walikubaliana kwa pamoja kumtenga Bashite. Na katika hili mimi bado nawaona Startv wanayo hatia, kwa sababu hata kama "advertisers" na hapa niwe wazi tu-yaani serikali imewa influence, walikuwa na nafasi ya kushawishi MOAT na TEF kupunguza au kumaliza msusio huo kabla ya kuamua kufanya ambacho tafsiri yake ni usaliti. Startv walikuwa na nafasi ya kuwa katikati kwa kuwa wao wamejifungamanisha na serikali, na wangeweka mambo sawa ndani kwa ndani.

Kinachotokea sana ni kibaya zaidi kwa tasnia na Startv. Sisi wengine tunaona Startv wamekula mlungula na tutaendelea kuwaona hivyo hivyo hata milele, na mimi kama mwananchi ambaye natamani kuona media inaheshimika na viongozi wetu wakiwa na adabu kwa kuwa tunawalipa mishahara, baada ya kipindi hicho kurushwa Jumatatu, sitapeleka tangazo langu Startv wala redio Free Africa. Nitaanza kuwachukia mno!
hakuna cha mkungula ,unajua kuwa Balile alipewa hela na wauzaji Wa dawa za kulevya?
 
UAMUZI WA STAR TV NI USALITI KWA TAALUMA YA HABARI
Kwa muda wa wiki moja sasa kampuni ya Sahara Communications Limited, wamiliki wa Star TV na vyombo vingine vya habari kupitia mitandao ya kijamii wanasambaza taarifa kuwa watafanya mahojiano maalum na Mkuu wa Mkoa wa Dar ea Salaam, Paul Makonda, Jumatatu Mei 22, 2017.

Kusudio hilo la Star TV limekuja wakati kiongozi huyo akiwa amefungiwa na vyombo vya habari kwa uamuzi ulioitikiwa kwa pamoja baina ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) na kuungwa mkono na Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Nchini (MOAT) na taasisi nyingine za kihabari nchini. Uamuzi wa kumfungia Makonda uliotangazwa Machi 2017, ilitokana na kiongozi huyo kuvamia Kituo cha Utangazaji cha Clouds Madia, March 17, 2017 akiwa na askari wenye bunduki.

Uvamizi wa Clouds ulikuwa mwendelezo wa matukio ya RC Makonda kudhalilisha wanahabari, kutukana na kutoiheshimu taaluma ya habari. Katika tamko hilo, Makonda tulimpa masharti mepesi kurejesha uhusiano na tasnia ya habari, ambayo ni kuomba radhi waandishi wa habari kwa tukio la Clouds na matukio mengine kwa ujumla wake kama sehemu ya uungwana wa Kitanzania.

Tulisema katika tamko kwa yeyote atakayeshirikiana na Makonda naye tutamhesabu kama adui wa tasnia ya habari nchini. Kwa mantiki hiyo tunasema ikiwa Star TV wameamua kushirikiana na Makonda, basi ni wazi wameamua kwa hiyari yao wenye kujitangaza kama adui wa tasnia ya habari nchini.

Kila Mtanzania anajua jinsi ya kupambana na adui kwa namnaya kujilinda, na tasnia haitasita ku fanya hivyo. Kadhalika hivi sasa TEF tunafuatatilia kwa karibu uhusiano wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na vyombo vya habari kutokana na matukio ya mara kwa mara ya kudhalilisha wanahabari wanapokuwa kazini kwa amri yake. Matukio haya yakiendelea, tutalazimika kupitia uhusiano wa RC Gambo na vyombo vya habari nchini.

Mwisho, tunavipongeza vyombo vya habari, kwa maana ya magazeti, radio, televisheni na mitandao ya kijamii ndani na nje ya nchi kwa kutekeleza uamuzi wa kumfungia RC Paul Makonda kwa uaminifu uadilifu wa hali juu, licha ya vishawishi vya hapa na pale vinavyotolewa na wapambe wake.

Nguvu yetu ipo katika umoja wetu kama wanahabari. Tusiipoteze Mungu ibariki Tanzania.

Deodatusi Balile
Makamu Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania.
Mei 19, 2017
kuna tetesi kuwa Balile alipokea in mrungula 14.2ml ngoja niifanyie kazi nitamwaga ushahidi wote hapa.
 
Nafahamu yote hayo Paskali. Lakini ni "implementors" wa mgomo na "determinants" wa nini kiandikwe walikubaliana kwa pamoja kumtenga Bashite. Na katika hili mimi bado nawaona Startv wanayo hatia, kwa sababu hata kama "advertisers" na hapa niwe wazi tu-yaani serikali imewa influence, walikuwa na nafasi ya kushawishi MOAT na TEF kupunguza au kumaliza msusio huo kabla ya kuamua kufanya ambacho tafsiri yake ni usaliti. Startv walikuwa na nafasi ya kuwa katikati kwa kuwa wao wamejifungamanisha na serikali, na wangeweka mambo sawa ndani kwa ndani.

Kinachotokea sana ni kibaya zaidi kwa tasnia na Startv. Sisi wengine tunaona Startv wamekula mlungula na tutaendelea kuwaona hivyo hivyo hata milele, na mimi kama mwananchi ambaye natamani kuona media inaheshimika na viongozi wetu wakiwa na adabu kwa kuwa tunawalipa mishahara, baada ya kipindi hicho kurushwa Jumatatu, sitapeleka tangazo langu Startv wala redio Free Africa. Nitaanza kuwachukia mno!
Mkuu Chabusalu unachokisema ninakielewa fika na hoja zako zote ni za msingi, ila not in Tanzania, hata hao TCRA kuna wakati sii lolote sii chochote.

Wakati wa uchaguzi niliwahi kuhoji matangazo ya kampeni ya CCM tuu pekee kwenye Star TV yanalipiwa na nani?. Sikupata jibu.
Paschal Mayalla: Matangazo ya kumnadi Magufuli Star TV yamelipiwa kiasi gani na CCM?

Ukinisoma hapo utaelewa kwa nini Star TV wamemwalika Bashite!.

Kiukweli kuna wakati kujipendekeza huwa kunalipa maana huchelewi kupewa shavu. Ila pia kuna wakati kujipendekeza kupita kiasi kunakushusha thamani mbele ya jamii.
Star TV wamepima pros na cons, wameamua kuvuta bingo, na kwa taarifa tuu the target sio kumu impress Bashite, bali aliye nyuma ya Bashite.

Paskali
 
Mkuu Chabusalu unachokisema ninakielewa fika na hoja zako zote ni za msingi, ila not in Tanzania, hata hao TCRA kuna wakati sii lolote sii chochote.

Wakati wa uchaguzi niliwahi kuhoji matangazo ya kampeni ya CCM tuu pekee kwenye Star TV yanalipiwa na nani?. Sikupata jibu.
Paschal Mayalla: Matangazo ya kumnadi Magufuli Star TV yamelipiwa kiasi gani na CCM?

Ukinisoma hapo utaelewa kwa nini Star TV wamemwalika Bashite!.

Kiukweli kuna wakati kujipendekeza huwa kunalipa maana huchelewi kupewa shavu. Ila pia kuna wakati kujipendekeza kupita kiasi kunakushusha thamani mbele ya jamii.
Star TV wamepima pros na cons, wameamua kuvuta bingo, na kwa taarifa tuu the target sio kumu impress Bashite, bali aliye nyuma ya Bashite.

Paskali
Nimekupata mkuu Paskali!
 
Mkuu afnhondya, asante kwa observation yako. Nina mambo machache kurespond. Kwanza, ni kweli sipendi namna ya utendaji kazi wa RC wa Dar. Yapo matukio yaliyonifikisha kwenye hitimisho hilo. Mfano, alivyomdhalilisha yule dada/mama mfanyakazi wa halmashauri ya manispaa Kinondoni, vitendo vyake kwenye Bunge la Katiba ikiwemo "kushiriki kwake kumwokoa Mzee Warioba' pale Blue Pearl, kudhalilisha watu kwenye suala la madawa ya kulevya; etc. Hata hivyo, sina chuki binafsi dhidi ya mtu huyo ambaye anatajwa kwa jina la Makonda aka Bashite. Sina mahali nakutana naye kwa namna yoyote ile kiasi cha kumchukia kama ambavyo andishi lako lilikusudia.
!
Mkuu Chabusalu, binadamu tunatofautiana sana kwenye mitazamo, visions, missions, angle of views na kufikia judgement fulani fulani kwenye kuwa judge watu.

Hayo uliyoyaona kama mapungufu ya Bashite kwa upande wako, kwa wengine ni strengths zinazomfanya azidi kung'ara azidi kupaa.

Hebu niangalie mimi nimeona nini kwa mtu huyu.
1. Akiwa DC Kinondoni, niliona haya na nikatoa ushauri huu. Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam

2. Kisha nikapitia maisha yake, alipotoka, na hapa alipo sasa kiasi cha kuweza ku determine ni wapi anakokwenda Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe Walilolikataa Waashi Litafanywa Kuwa Jiwe Kuu la Pembeni

3. Na baada ya kuanza vita vya madawa nikampandisha kule juu kabisa

Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze...

4. Sikuishia hapo, walipomsingizia kufoji nilijitokeza kumtetea
Ndugu, Jamaa na Marafiki, Njooni Tumtetee Makonda Dhidi ya Mapapa Wauza Unga Wanaomzushia...


Paskali
 
Big up TEF, Bashite ameshindwa kudhihirisha hata uungwana wa kitanzania wa kusema maneno matatu tu "I Am Sorry"; simply because ana God father Magogoni basi komaeni mpaka akili japo ya kupandikizwa imrejee!
 
Big up TEF, Bashite ameshindwa kudhihirisha hata uungwana wa kitanzania wa kusema maneno matatu tu "I Am Sorry"; simply because ana God father Magogoni basi komaeni mpaka akili japo ya kupandikizwa imrejee!
Mkuu MTK, ili kusema sorry hatua ya kwanza ni kukubali kosa kuwa umekosea ndipo uombe msamaha.

Bashite hajafanya kosa lolote, kila siku alikuwa anakwenda Clouds na kuna wakati alikuwa anakaa hadi usiku wa manane. Wale makirikiri ni personal body guards wake, anakwenda nao kokote anakwenda. Laiti tungejua ni mara ngapi, Bashite amekwenda Clouds bila taarifa, ndipo tungejua ule haukuwa uvamizi.

Wale vijana walishiriki kwenye kuipanga ile movie, wakakunja mkwanja safi, wakamuahidi Bashite kuwa wangerusha. Walipompigia Mchungaji ili kupata upande wa pili, naye akakata, mkwanja, akampiku dau Bashite kuwa wasirushe.

Huko nyuma Bashite keshamwambia yule godfather wake kuwa waangalie, muda ulipofika watu wazima hao wakatoa macho kodo kwenye TV kuangalia.

Alipoona patupu ndipo hata ungekuwa wewe lazima ungekasirika!. Pale Clouds hakuvamia bali alikwenda kufuata movie yake aliyoigharimia kuitengeneza na kuilipia kuirusha lakini wahuni wale, walivuta tuu fungu na kukaika! .

Laiti baada ya kushikishwa na Mchungaji dau kubwa kuliko la Bashite, ustaarabu ikikuwa ni kumtaarifu Bashite kuwa movie haitachezwa kwa siku hiyo, ili na yeye amjulishe yule aliyemwambia aangalie kuwa movie haitakuwepo.

Hivyo ule sio uvamizi, ilikuwa ni just a follow up tuu ya movie yake.

Paskali
 
Unajua makonda kawekwa na nani?pale?
Vipi huyo aliyemuweka makonda zinaandikwa habari zake hauhaziandikwi?
Na aliyemuweka Makonda na vitisho vyake amemsaidiaje Makonda ili aandikwe???
Hiyo ni nguvu ya umoja imefanya Mkulu ashindwe kumsaidia mpendwa wake.

Nawashauri endeleeni na msimamo wenu ndio salama yenu, star TV ni adui si kwa media pekee bali hata watanzania wapenda haki.
 
Na aliyemuweka Makonda na vitisho vyake amemsaidiaje Makonda ili aandikwe???
Hiyo ni nguvu ya umoja imefanya Mkulu ashindwe kumsaidia mpendwa wake.

Nawashauri endeleeni na msimamo wenu ndio salama yenu, star TV ni adui si kwa media pekee bali hata watanzania wapenda haki.
Pia asipoandikwa magazetini analala njaa?au anapungukiwa kiungo?
 
Kwa mujibu wa mtangazaji Samadu Hasan leo asubuhi katika kipindi cha tuongee siasa kilicho kuwa Live, ametangaza kuwa mahojiano hayo yatafanyika kesho 22/6 bila kutaja muda na kipindi ila amesema "kujua mbivu na mbichi " mahojiano yatakayo ongozwa na mtangazaji Mapuli wa Star Tv.
 
Back
Top Bottom