Makonda awaponza Star Tv na Sahara Media mbele ya TEF

UAMUZI WA STAR TV NI USALITI KWA TAALUMA YA HABARI
Kwa muda wa wiki moja sasa kampuni ya Sahara Communications Limited, wamiliki wa Star TV na vyombo vingine vya habari kupitia mitandao ya kijamii wanasambaza taarifa kuwa watafanya mahojiano maalum na Mkuu wa Mkoa wa Dar ea Salaam, Paul Makonda, Jumatatu Mei 22, 2017.

Kusudio hilo la Star TV limekuja wakati kiongozi huyo akiwa amefungiwa na vyombo vya habari kwa uamuzi ulioitikiwa kwa pamoja baina ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) na kuungwa mkono na Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Nchini (MOAT) na taasisi nyingine za kihabari nchini. Uamuzi wa kumfungia Makonda uliotangazwa Machi 2017, ilitokana na kiongozi huyo kuvamia Kituo cha Utangazaji cha Clouds Madia, March 17, 2017 akiwa na askari wenye bunduki.

Uvamizi wa Clouds ulikuwa mwendelezo wa matukio ya RC Makonda kudhalilisha wanahabari, kutukana na kutoiheshimu taaluma ya habari. Katika tamko hilo, Makonda tulimpa masharti mepesi kurejesha uhusiano na tasnia ya habari, ambayo ni kuomba radhi waandishi wa habari kwa tukio la Clouds na matukio mengine kwa ujumla wake kama sehemu ya uungwana wa Kitanzania.

Tulisema katika tamko kwa yeyote atakayeshirikiana na Makonda naye tutamhesabu kama adui wa tasnia ya habari nchini. Kwa mantiki hiyo tunasema ikiwa Star TV wameamua kushirikiana na Makonda, basi ni wazi wameamua kwa hiyari yao wenye kujitangaza kama adui wa tasnia ya habari nchini.

Kila Mtanzania anajua jinsi ya kupambana na adui kwa namnaya kujilinda, na tasnia haitasita ku fanya hivyo. Kadhalika hivi sasa TEF tunafuatatilia kwa karibu uhusiano wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na vyombo vya habari kutokana na matukio ya mara kwa mara ya kudhalilisha wanahabari wanapokuwa kazini kwa amri yake. Matukio haya yakiendelea, tutalazimika kupitia uhusiano wa RC Gambo na vyombo vya habari nchini.

Mwisho, tunavipongeza vyombo vya habari, kwa maana ya magazeti, radio, televisheni na mitandao ya kijamii ndani na nje ya nchi kwa kutekeleza uamuzi wa kumfungia RC Paul Makonda kwa uaminifu uadilifu wa hali juu, licha ya vishawishi vya hapa na pale vinavyotolewa na wapambe wake.

Nguvu yetu ipo katika umoja wetu kama wanahabari. Tusiipoteze Mungu ibariki Tanzania.

Deodatusi Balile
Makamu Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania.
Mei 19, 2017
Ni Wendawazimu kupokea hongo kutoka kwa Gwajima ili kumsusia Rc Makonda.
 
UAMUZI WA STAR TV NI USALITI KWA TAALUMA YA HABARI
Kwa muda wa wiki moja sasa kampuni ya Sahara Communications Limited, wamiliki wa Star TV na vyombo vingine vya habari kupitia mitandao ya kijamii wanasambaza taarifa kuwa watafanya mahojiano maalum na Mkuu wa Mkoa wa Dar ea Salaam, Paul Makonda, Jumatatu Mei 22, 2017.

Kusudio hilo la Star TV limekuja wakati kiongozi huyo akiwa amefungiwa na vyombo vya habari kwa uamuzi ulioitikiwa kwa pamoja baina ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) na kuungwa mkono na Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Nchini (MOAT) na taasisi nyingine za kihabari nchini. Uamuzi wa kumfungia Makonda uliotangazwa Machi 2017, ilitokana na kiongozi huyo kuvamia Kituo cha Utangazaji cha Clouds Madia, March 17, 2017 akiwa na askari wenye bunduki.

Uvamizi wa Clouds ulikuwa mwendelezo wa matukio ya RC Makonda kudhalilisha wanahabari, kutukana na kutoiheshimu taaluma ya habari. Katika tamko hilo, Makonda tulimpa masharti mepesi kurejesha uhusiano na tasnia ya habari, ambayo ni kuomba radhi waandishi wa habari kwa tukio la Clouds na matukio mengine kwa ujumla wake kama sehemu ya uungwana wa Kitanzania.

Tulisema katika tamko kwa yeyote atakayeshirikiana na Makonda naye tutamhesabu kama adui wa tasnia ya habari nchini. Kwa mantiki hiyo tunasema ikiwa Star TV wameamua kushirikiana na Makonda, basi ni wazi wameamua kwa hiyari yao wenye kujitangaza kama adui wa tasnia ya habari nchini.

Kila Mtanzania anajua jinsi ya kupambana na adui kwa namnaya kujilinda, na tasnia haitasita ku fanya hivyo. Kadhalika hivi sasa TEF tunafuatatilia kwa karibu uhusiano wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na vyombo vya habari kutokana na matukio ya mara kwa mara ya kudhalilisha wanahabari wanapokuwa kazini kwa amri yake. Matukio haya yakiendelea, tutalazimika kupitia uhusiano wa RC Gambo na vyombo vya habari nchini.

Mwisho, tunavipongeza vyombo vya habari, kwa maana ya magazeti, radio, televisheni na mitandao ya kijamii ndani na nje ya nchi kwa kutekeleza uamuzi wa kumfungia RC Paul Makonda kwa uaminifu uadilifu wa hali juu, licha ya vishawishi vya hapa na pale vinavyotolewa na wapambe wake.

Nguvu yetu ipo katika umoja wetu kama wanahabari. Tusiipoteze Mungu ibariki Tanzania.

Deodatusi Balile
Makamu Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania.
Mei 19, 2017
Ni Upumbavu na Wendawazimu kuandika barua yenye chuki dhidi ya Rc Makonda bila kuthibitisha kama kweli alishiriki kukivamia kituo cha Clouds Fm akiwa na polisi. Kwanini TEF watoe hukumu kabla ya Tume iliyoundwa na Nape kutoa majibu? Star Tv haina wabdishi makanjanja na wana msimamo unaojitegemea. Big up Star tv na viunga vyake.
 
Uhuru wa Habari afu unawapangia wengine wanachotaka kutangaza??

Ivi TEF na UTPC ni Regulatory Body ama ni jukwaa na Club tu?? Wanapata wapi mamlaka ya kuwakataza wezao kupractise taaluma yao kwa uhuru ???

Balile na Meena wanamatatizo na wanatumika vibaya
 
Haya yooooote ni jeuri isiyokuwa na sababu,mtu yeyote anayetetea mambo aliyofanya mpaka vyombo vya habari kumsusia sidhani kama yupo sahihi.wanaompenda na walio karibu yake wamshauri aombe msamaha hata kama ni wakinafiki ili maisha yaendelee vinginevyo hata siasa zake bila wanahabari atakwama tu hata kama siyo leo basi huko mbele ya safari.siasa gani atakayofanya kwa ushirikiano wa Star tv tuuu?ni jambo la muda tuu labda kama anafikiria kutoka kwenye siasa.
Aombe msamaha kwa lipi? ushasikiliza upande wake wa shilingi? na kama hujasikiliza wawezaje kujudge hao wanaotetea? eti mkuu wa mkoa kavamia, upuuzi wa hali ya tangu lini mkuu wa mkoa akavamia eneo lililo ndani ya mipaka ya utawala wake?
 
Nilikua napendekeza hivi; watu wote MAKINI tungeachana kabisa na kuangalia Start TV pamoja na kusikiliza radio yao ya RFA halafu tuone na yeye Dialo atafanyaje?
Wafanya biashara kabla ya kupeleka tangazo la biashara kwenye kituo chochote hua wanafanya utafiti wa kujua hiyo TV na au radio inawasikilizaji kiasi gani so kwa mgomo wetu hu ndio Dialo atakapo jua nani zaidi
 
Acheni kuwapangia watu.au mliwasaidia kununua maspika?
Kama wameamua waacheni.

Issue sio kupangiwa mkuu bali walikabaliana kwa umoja wao kwamba waachane na habari za Bashite baada ya kushindwa kuomba radhi kwa kuvamia Cloud media! Na star tv waliridhia haya makubaliano, sasa sijaona mahali wamepangia. Tatizo wabongo hatujui maana ya "agreement" na hatuziheshimu kabisa. Tumesongwa na njaa hadi akilin, hakuna cha msomi na ambaye hajasoma. Be consistent in whatever you are doing, and this is rational.
 
Issue sio kupangiwa mkuu bali walikabaliana kwa umoja wao kwamba waachane na habari za Bashite baada ya kushindwa kuomba radhi kwa kuvamia Cloud media! Na star tv waliridhia haya makubaliano, sasa sijaona mahali wamepangia. Tatizo wabongo hatujui maana ya "agreement" na hatuziheshimu kabisa. Tumesongwa na njaa hadi akilin, hakuna cha msomi na ambaye hajasoma. Be consistent in whatever you are doing, and this is rational.
Sijaona sababu ya wao kujiingiza kwenye ugomvi na makonda na clouds.wakati hao jamaa walikuwa marafiki.siku wakipatana je?
 
Aombe msamaha kwa lipi? ushasikiliza upande wake wa shilingi? na kama hujasikiliza wawezaje kujudge hao wanaotetea? eti mkuu wa mkoa kavamia, upuuzi wa hali ya tangu lini mkuu wa mkoa akavamia eneo lililo ndani ya mipaka ya utawala wake?
Hata ukisikiliza upande wa pili,
Hana la upande mwingine wa shilingi alikosea kama ambavyo binadamu mwingine yeyote anaweza kukosea,hakikuwa kitu cha kawaida pamoja na kuwa ni ndani ya eneo lake la mipaka ya kiutawala.
 
Mkuu Paskali, yote hayo nayafahamu sana. Lakini kama wamejiwekea utaratibu huo na wanaendesha mambo yao, sioni kama kuna tatizo. Isitoshe issue iliyopo mbele, kwa sasa, sio uhalali wa TEF au MOAT. Issue ni kusalitiana. Labda uniambie kama wahariri wa Startv sio members wa TEF na Startv sio member wa MOAT, lakini kama ni members na vitrip vya mishiko vya TEF huwa wanapokea, na walikubaliana na uamuzi wa kujitenga na Daud Bashite, Startv wanapaswa watekeleze maamuzi ya TEF, na wasipotekeleza TEF hiyo hiyo ya Brela na MOAT hiyo hiyo isiyokuwa na mandate wawashughulikiea wahariri wa Startv na wamiliki wao kwa utaratibu waliojiwekea. Uelewe, kama wahariri wa Startv na Startv wenyewe walijiunga kwenye vyombo hivyo walifanya hivyo baada ya kuona umuhimu wake!

Na jambo la muhimu kulifahamu ni kwamba, hata hiyo TAJA ni kundi la watu tofauti yake na TEF pamoja na MOAT ni muundo wake tu kisheria. Suala lililoko katika mjadala sio suala la kisheria, ni suala la uaminifu. Ni jambo linaloonekana dogo lakini lenye athari kubwa kijamii. Unapokuwa na wamiliki wa vyombo vya habari pamoja na wahariri wao "wasaliti" unatarajia nini?

Naomba unielewe mkuu Paskali. Maoni yangu yanazingatia iwapo tu wahariri wa Startv ni wanachama wa TEF, na Diallo amejiandikisha MOAT na amekuwa akinufaika kama membar wa MOAT.
Mkuu Chabusalu, hili la kukubaliana kisha kugeukana nililizungumza kwa kirefu hapa Media Kususia Habari za Fulani: Jee Tanzania Tuna Independent Media Yenye Jeuri Hiyo?.

Kwenye mambo ya media kuna wamiliki, wahariri, waandishi, watoa habari, watangazaji (advertisers) na walaji wa habari. Very very unfortunately wahariri ambao ndio implementors wa mgomo huo, are not the determinants nini kiandikwe! . Determinants ni wamiliki, na watangazaji wanaoleta pesa za mishahara ya hao wahariri na kugharimia kuiendesha media husika. Editors can't say no to Bashite. Na hili la Star ni mwanzo tuu, wengine wanafuata.

Paskali
 
Mkuu Chabusalu, hili la kukubaliana kisha kugeukana nililizungumza kwa kirefu hapa Media Kususia Habari za Fulani: Jee Tanzania Tuna Independent Media Yenye Jeuri Hiyo?.

Kwenye mambo ya media kuna wamiliki, wahariri, waandishi, watoa habari, watangazaji (advertisers) na walaji wa habari. Very very unfortunately wahariri ambao ndio implementors wa mgomo huo, are not the determinants nini kiandikwe! . Determinants ni wamiliki, na watangazaji wanaoleta pesa za mishahara ya hao wahariri na kugharimia kuiendesha media husika. Editors can't say no to Bashite. Na hili la Star ni mwanzo tuu, wengine wanafuata.

Paskali
Nafahamu yote hayo Paskali. Lakini ni "implementors" wa mgomo na "determinants" wa nini kiandikwe walikubaliana kwa pamoja kumtenga Bashite. Na katika hili mimi bado nawaona Startv wanayo hatia, kwa sababu hata kama "advertisers" na hapa niwe wazi tu-yaani serikali imewa influence, walikuwa na nafasi ya kushawishi MOAT na TEF kupunguza au kumaliza msusio huo kabla ya kuamua kufanya ambacho tafsiri yake ni usaliti. Startv walikuwa na nafasi ya kuwa katikati kwa kuwa wao wamejifungamanisha na serikali, na wangeweka mambo sawa ndani kwa ndani.

Kinachotokea sana ni kibaya zaidi kwa tasnia na Startv. Sisi wengine tunaona Startv wamekula mlungula na tutaendelea kuwaona hivyo hivyo hata milele, na mimi kama mwananchi ambaye natamani kuona media inaheshimika na viongozi wetu wakiwa na adabu kwa kuwa tunawalipa mishahara, baada ya kipindi hicho kurushwa Jumatatu, sitapeleka tangazo langu Startv wala redio Free Africa. Nitaanza kuwachukia mno!
 
Una ushahidi na ulichokiandika (maandishi mekundu) au ndio huo ushabiki wa habari za uzushi wa mitandaoni!

Au utakuja na jibu lako ati Si kazi ya TEF kumpeleka mahakamani Daud Bashite!

Kama kuna ushahidi usio na mashaka uwekeni wazi, kila raia auone na kushinikiza vyombo husika kuchukua hatua.

Kumbuka RC Makonda ni Kiongozi wa juu Kitaifa, hivyo hapaswi kutiliwa mashaka ya aina yoyote, maana CHEO NI DHAMANA.
Uko very low, mkuu. Pumzika tu..
 
Kipindi kinachovuta audience kubwa kwa Star TV and RFA ni pamoja na kipindi cha Kutoka Magazetini!!

Kama ndivyo, endapo Star TV wataendelea na programu yao na Daudi Albert Bashite, basi wamiliki wa vyombo vya habari wapige marufuku magazeti yao kusomwa na Star TV na RFA. Aidha, wakataze waandishi wao kushiriki mijadala ya kila asubuhi inayoendeshwa na Star TV ambayo mara kwa mara huwa inaalika watu wa media zingine.
Kweli wakizUia magazeti yao kusomwa star t✓ watakuwa wamewakomoa
waache wakimbie na bashite ambaye hatachelewa kuwageukia, hahaha
 
Aombe msamaha kwa lipi? ushasikiliza upande wake wa shilingi? na kama hujasikiliza wawezaje kujudge hao wanaotetea? eti mkuu wa mkoa kavamia, upuuzi wa hali ya tangu lini mkuu wa mkoa akavamia eneo lililo ndani ya mipaka ya utawala wake?
Rudia kusoma ulichoandika, upumzike halafu urudie tena? Aliyekudanganya kwamba mkuu wa mkoa anaweza akaingia hata chumbani kwako wakati wowote bila utaratibu maalum ni nani? Hivi mkuu wa mkoa kwako ni Mungu? Hata mnayemtetea wakati mwingine anawapuuza sana!
 
Uhuru wa Habari afu unawapangia wengine wanachotaka kutangaza??

Ivi TEF na UTPC ni Regulatory Body ama ni jukwaa na Club tu?? Wanapata wapi mamlaka ya kuwakataza wezao kupractise taaluma yao kwa uhuru ???

Balile na Meena wanamatatizo na wanatumika vibaya
Hivi watu mnakula maharage gani? nani kawaambia TEF wamezuia wenzao kupractise taaluma yao kwa uhuru? Ni wapi TEF wamewapangia wengine wanachotaka kutangaza? Issue iliyopo ni kuwepo kwa usaliti dhidi ya maamuzi yaliyofikiwa kwa pamoja baina ya TEF, MOAT na clubs. Jamaa zako wa Startv hawajazuiwa, wala TEF hawana mamlaka ya kuwazuia, ila wanaweza kuwatenga, basi! Sasa hapa kitu gani kinasukuma kudai Balile na Meena wanatumika? Unaweza kuthibitisha au ni mahaba tu?
 
Back
Top Bottom