Makonda awaponza Star Tv na Sahara Media mbele ya TEF

UAMUZI WA STAR TV NI USALITI KWA TAALUMA YA HABARI
Kwa muda wa wiki moja sasa kampuni ya Sahara Communications Limited, wamiliki wa Star TV na vyombo vingine vya habari kupitia mitandao ya kijamii wanasambaza taarifa kuwa watafanya mahojiano maalum na Mkuu wa Mkoa wa Dar ea Salaam, Paul Makonda, Jumatatu Mei 22, 2017.

Kusudio hilo la Star TV limekuja wakati kiongozi huyo akiwa amefungiwa na vyombo vya habari kwa uamuzi ulioitikiwa kwa pamoja baina ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) na kuungwa mkono na Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Nchini (MOAT) na taasisi nyingine za kihabari nchini. Uamuzi wa kumfungia Makonda uliotangazwa Machi 2017, ilitokana na kiongozi huyo kuvamia Kituo cha Utangazaji cha Clouds Madia, March 17, 2017 akiwa na askari wenye bunduki.

Uvamizi wa Clouds ulikuwa mwendelezo wa matukio ya RC Makonda kudhalilisha wanahabari, kutukana na kutoiheshimu taaluma ya habari. Katika tamko hilo, Makonda tulimpa masharti mepesi kurejesha uhusiano na tasnia ya habari, ambayo ni kuomba radhi waandishi wa habari kwa tukio la Clouds na matukio mengine kwa ujumla wake kama sehemu ya uungwana wa Kitanzania.

Tulisema katika tamko kwa yeyote atakayeshirikiana na Makonda naye tutamhesabu kama adui wa tasnia ya habari nchini. Kwa mantiki hiyo tunasema ikiwa Star TV wameamua kushirikiana na Makonda, basi ni wazi wameamua kwa hiyari yao wenye kujitangaza kama adui wa tasnia ya habari nchini.

Kila Mtanzania anajua jinsi ya kupambana na adui kwa namnaya kujilinda, na tasnia haitasita ku fanya hivyo. Kadhalika hivi sasa TEF tunafuatatilia kwa karibu uhusiano wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na vyombo vya habari kutokana na matukio ya mara kwa mara ya kudhalilisha wanahabari wanapokuwa kazini kwa amri yake. Matukio haya yakiendelea, tutalazimika kupitia uhusiano wa RC Gambo na vyombo vya habari nchini.

Mwisho, tunavipongeza vyombo vya habari, kwa maana ya magazeti, radio, televisheni na mitandao ya kijamii ndani na nje ya nchi kwa kutekeleza uamuzi wa kumfungia RC Paul Makonda kwa uaminifu uadilifu wa hali juu, licha ya vishawishi vya hapa na pale vinavyotolewa na wapambe wake.

Nguvu yetu ipo katika umoja wetu kama wanahabari. Tusiipoteze Mungu ibariki Tanzania.

Deodatusi Balile
Makamu Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania.
Mei 19, 2017
Mnaminya uhuru wa habari
 
Haya yooooote ni jeuri isiyokuwa na sababu,mtu yeyote anayetetea mambo aliyofanya mpaka vyombo vya habari kumsusia sidhani kama yupo sahihi.wanaompenda na walio karibu yake wamshauri aombe msamaha hata kama ni wakinafiki ili maisha yaendelee vinginevyo hata siasa zake bila wanahabari atakwama tu hata kama siyo leo basi huko mbele ya safari.siasa gani atakayofanya kwa ushirikiano wa Star tv tuuu?ni jambo la muda tuu labda kama anafikiria kutoka kwenye siasa.
 
UAMUZI WA STAR TV NI USALITI KWA TAALUMA YA HABARI
Kwa muda wa wiki moja sasa kampuni ya Sahara Communications Limited, wamiliki wa Star TV na vyombo vingine vya habari kupitia mitandao ya kijamii wanasambaza taarifa kuwa watafanya mahojiano maalum na Mkuu wa Mkoa wa Dar ea Salaam, Paul Makonda, Jumatatu Mei 22, 2017...

Uvamizi wa Clouds ulikuwa mwendelezo wa matukio ya RC Makonda kudhalilisha wanahabari, kutukana na kutoiheshimu taaluma ya habari. ...

Tulisema katika tamko kwa yeyote atakayeshirikiana na Makonda naye tutamhesabu kama adui wa tasnia ya habari nchini. ...

Nguvu yetu ipo katika umoja wetu kama wanahabari. Tusiipoteze Mungu ibariki Tanzania.

Deodatusi Balile
Makamu Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania.
Mei 19, 2017
Deodatusi Balile: popote ulipo, kama taarifa hiyo umeiandaa wewe mwenyewe, tambua kwamba wewe si mwana habari aliyekamilika. Rejea sifa na wajibu wa mwanahabari ambayo ni kuwahabirisha watu katika mazingira yoyote yale, hata ya hatari.

Kama hiyo taarifa inawakilisha tasnia ya habari, ni hakika kwamba Tanzania haina wanahabari bali wachumia tumbo. Mnainajisi tasnia ya habari.

Kipi kinachohatarisha mwanahabari hadi aache kutafuta na kutoa habari, iwapo hata vitani, wanahabari wanakuwepo!

Iwapo, mna ushahidi tosha kuhusu RC Makonda kuvamia CloudsTV (nukuu ya maandishi katika rangi nyekundu), njia sahihi si kususia kuaandika maswala ya RC Makonda, hata yanayohusu ofisi yake (Mkuu wa Mkoa), ila kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. Naamini wanahabari wanao uwezo wa kuchunguza na kukusanya ushahidi wa kutosha, na ndiyo maana wengi hutegemea vyombo vya habari kupata taarifa ya kila tukio na masuala mbalimbali.

Deodatusi Balile: TOA BORITI JICHONI KWAKO KWANZA
 
  • Thanks
Reactions: nao
nilishaachaga kuitazama star tv siku nyiiiingi..kwa hio warushe tu wala sina khabari....naskia mapato yao yameshuka sana tofauti na ilivyokua kabla ya uchaguz. sasa hivi wateja wao wengi tumehamia channel ten na azam tv.
 
Uliyosema yote kuhusu Bashite na Clouds hapo kabla ni ukweli tupu!!! Hata hivyo, twende hatua kwa hatua na unijibu maswali yangu kama ulivyofanay kwa hilo hapo juu:
Mkuu Chige, kwanza asante kwa objectivity yako katika hili, ingawa umesema wewe sii mwandishi wa habari, ila kiukweli kwa maswali haya wewe ni zaidi ya mwandishi!. You have the Intellect ya kuhoji kuliko hata mwandishi, kiukweli if you're not a lawyer, then you should have been one, kwenye cross examinations ungewabananisha kwenye kona hadi hakuna pa kutokea. Maswali yako ni mengi na yote ni ya msingi, hivyo kukutendea haki, nitayajibu yote, I'll leave no stone unturned, ila naomba tuu uwe mvumilivu. Nitakujibu taratibu. Naomba usiulize mengine ili nikimaliza ndipo tuendelee na maswali mengine.
Mosi, kwavile tu alikuwa na ukaribu huo na Clouds, unadhani alikuwa sahihi kutengeneza story ya Gwajima kwa manufaa yake binafsi?! Do you really believe it?
Bashite ni binadamu tuu kama wanadamu wengine. Hii ya kutengeneza movie ya Gwajima, japo sio sahihi ila angetumia msanii wa kweli, lakini kitendo cha kutumia msanii wa kuchonga
Kiukweli huu ni uendawazimu. Huyu ni mwendawazimu, nimesema mwendawazimu sio mtu wa kuadhibiwa bali anapaswa kusaidiwa.
Kuwa Kichaa Sio Mpaka Kuokota Makopo!. Jee Tanzania Tuna Vichaa Wengi Kuliko Tunavyojidhania?!.
Insane Anahitaji Huruma, Kusaidiwa. Sio Kulaumiwa, Kulaaniwa na Kususwa! He Needs Help, Tumsaidieje?
Pili, unaamini alikuwa sahihi kulazimisha kile kipindi kirushwe tofauti na wenyewe ambao hawakuwa tayari kwavile stori ilikuwa haija-balance!!!

TIP: Ushahidi wa kimazingira unaonesha ni kweli Bashite alishinikiza hiyo habari na ndio maana, baada ya kushindikana kurushwa, mtu wa mwanzo kuisambaza ile habari mitandaoni alikuwa ni Le Mutuz.
Kama kutengeneza ile movie ni ukichaa, then kitendo cha Bashite kulazimisha kurusha pia ni ukichaa. Japo aligharimia zoezi zima kwa kutoa mtonyo, aliamini kwa mtonyo ule wangerusha, kumbe wenzake wamevuta huku na kule, hivyo alikwenda kwa hasira ambayo sasa ni hasara.
Swali la tatu: Wewe ukiwa kama Mwanahabari; hivi ni kweli unaamini hatua Bashite kutoka na ile content na kwenda kuisambaza informally ilikuwa ni hatua sahihi inayoweza kuhalalishwa kutokana na ukaribu wake na Clouds?!
ANGALIZO: Hata katika mazingira ya mahusiano ya kawaida ya kati ya mwanadamu mmoja na mwingine; hutokea wakati mwingine watu mkawa mmeshibana kama ilivyokuwa kwa Clouds na Bashite! Na katika hali hiyo mmoja anaweza kujikuta anafanya jambo moja dhidi ya mwenzake huku akiamini anachofanya ni jambo la kawaida tu!!

Pamoja na kudhani hilo ni jambo la kawaida, mwenzako anajikuta amekwazika kweli kweli... tena sana! Na bila ya kupepesa macho, anakwambia wazi kwamba this's not right, UMENIKOSEA kwahiyo nitake radhi!!!!

Hivi kwa muungwana bila kujali ni kama kweli amekosea au hapana, hawezi kuomba radhi kwa sababu tu mwenzake amemkwaza?! Hivi mara zote ambazo huwaga tunawaomba radhi wenzetu tunakuwa tumekosea?
Hatua haikuwa halali. Kama tangu mwanzo ni ubatili, then ubatili huu unabatilisha zoezi lote kwa ujumla wake.
Now tell me, hivi unaamini kabisa, from deep inside your heart, pamoja na yote hayo, Bashite hakuwa na kosa hata kidogo?! Nini kimemfanya asiombe radhi kama alivyotakiwa? Au kwavile yeye ni Mkuu wa Mkoa ndo anadhani hawezi kuomba radhi taasisi zingine?!
Kwa mujibu wa tathmini yangu, Bashite hakuwa na kosa kisheria ila ana kosa kijamii. Kisheria ili kutenda jinai lazima kwanza vitu viwili vifanyike, actus reus (kitendo cha jinai) na mens rea (nia ya kutenda jinai), japo kitendo kimetendeka, jee Bashite alivamia Clouds kwa nia ya kutenda jinai?. Jibu ni no!. Ukiisha mhesabu mtu ni insane, sheria inamsamehe kwa kumuhesabu alikuwa hajui atendalo. Ile kulia kanisani madhabahuni ni uthibitisho tosha this man is insane ila hayuko peke yake!, hata yule mwenzake pia ni insane!. Naomba usiniulize mwenzake yupi!.
Turudi kwa hao Star TV unaosema wanaonewa!!
SWALI: Je, unataka kuniambia Sahara Media sio sehemu ya MOAT, TEF na UTPC?!
SMG ni sehemu ya MOAT, TEF na UTPC by preference only and not obligation. Maelekezo ya TEF sio compulsory kuyafuata kwa sababu sio binding. Unaweza kuyatekeleza na unaweza kuyapuuza na nothing will happen.
Kama sio sehemu ya hizo taasisi, usiende swali linalofuata lakini kama ni sehemu ya MOAT, TEF na UTPC; ni kwa namna gani unasema kwamba Star TV wanaonewa?!
SMG wanaonewa kwa sababu kuna mambo makubwa na mabaya zaidi tasnia hii imetendewa na wahusika hawakuchukuliwa hatua kali hivi. SMG licha ya kuwa ni chombo cha habari it has to survive, MOAT, UTPC na TEF, hakuna hata mmoja anayetoa sentano yake kuisupport SMG, kwa vile Bashite ndiye mwanaye kipenzi anayependezwa naye, he who pays the piper may call the tune ili maisha yaendelee!. SMG wako right kumualika Bashite.
Kama Star TV ni sehemu ya hizo taasisi; do you really believe kwamba Star TV wanaonewa?! Au unaweza kunipa mfano mmoja tu wa media yoyote (achana na TBC) ambayo ilishirikiana na Daudi Albert Bashite lakini pamoja na yote hayoTEF na UTPC hawakutoa tamko?! Mfano wako utasaidia kuonesha double standard ya TEF na UTPC... kwamba, kumbe wapo wengine walioshirikiana na Bashite lakini hakuna tamko lolote lililotolewa dhidi yao?
Double Standards ya TEF sio kwenye hii issue ya Bashite, kwa sababu hicho kinachoitwa uvamizi is not kuwa ni uvamizi kweli bali imekuwa just blown out of proportion na kufanywa a very big deal. Mambo mangapi makubwa mabaya media tumefanyiwa na sijaona TEF wakifanya kitu.
Au kama Star TV na Sahara Media kwa ujumla waliona uamuzi wa TEF & UTPC haukuwa sahihi; kwanini hapo hapo hawakuweka wazi kwamba hawakubaliani na uamuzi huo na hivyo; wao kama wao wataendelea kushirikiana na Bashite?!.
Sio lazima kila uamuzi usiokubaliana nao useme, mambo mengine ni actions tuu speak louder than words.
Kutoka ndani kabisa ya nafsi yako, hivi ni kweli unaamini kabisa kwamba Star TV katika hili wanaonewa?
Kutoka ndani kabisa ya moyo wangu Star TV katika hili wqnaonewa na TEF wamekengeuka!. Journalism ni noble professionals kama udakitari, waandishi hatutakiwi kugoma. Hata wakati wa ule mgomo wa madaktari wengi humu mkawa support, mimi ni miongoni mwa tuliopinga, no matter how bad the situation is, it's un ethical kwa daktari kugoma!, sambamba na mtu wa fire, tanesco, postal na simu etc. Kwenye media ethics nilizosoma mimi, sikumbuki wapi media tuliruhusiwa kugoma, hivyo mgomo wa TEF ni batili! . Acha SMG wapige pesa yao na umma upate habari za uhakika kuhusu Daudi Albert Bashite, mwana Kolomije.
Aidha unasema: Naamini you're smart enough kufahamu nini maana ya double standard!!! Hivi unaweza kuniambia ni double standard ipi iliyofanyika ama dhidi ya Bashite au Star TV?!
Nadhani nimeisha izungumza hii huko nyuma. Alichokifanya Bashite kwenye Clouds media ni nothing compared na Jeshi la Polisi lilichokifanya kwa Daudi Mwangosi. Where were TEF wakati wa kifo cha Mwangosi! . Mara ngapi waandishi tunanyanyaswa, tunadhalilishwa, tunapigwa hadi kuuwawa mbona TEF hawatangazi mgomo?. Bashite ni kichaa fulani amefanya ukichaa wake kwa vichaa wenzie wa Clouds media, tusiingeuze ni national agenda.
Mimi sio mwanahabari lakini hii sio mara yangu ya kwanza kusikia viongozi mbalimbali wakisusiwa hapa nchini!!! Hivi ikiwa wengine walikuwa wanasusiwa huku ukiamini kilichofanyika sasa ni double standard; do I miss something in the real meaning of double standard?!
Kama nilivyosema mwanzo, japo wewe sio mwanahabari but you're far better kuliko wengi wa wanahabari, kama sio mara yako ya kwanza kusikia viongozi wakisusiwa, then you're far better than me, mimi niko kwenye tasnia hii for 27 years, kwa Tangazo la TEF, ndio mara yangu ya kwanza kuona kususa kunatolewa kwa statement na kufuatiwa na statement ya kukazia hukumu!. Huko nyuma media tumekuwa tunasusa kwa kauli tuu na baada ya muda kususa huko kunayeyuka tuu naturally bila kauli zozote za kulaani au kukazia hukumu.
To me this is too much attention and emphasis on a non issue!. Media zetu zenyewe zipo zipo tuu kama hazipo, kwa issue kama ya Bashite na mazagazaga yake, tungekuwa na serious media saa hizi tungekuwa tumeisha mtundika msalabani zamani na anayempa kichwa angeisha adabishwa kwa kitu kinachoitwa non volenti mahakamani!, lakini sisi media yetu kazi yetu ni maneno mingi vitendo sifuri!.
Btw, inawezekana aliyofanya Bashite yote kwako ni sahihi lakini in the eyes of TEF aliyofanya sio sahihi!!! Kwahiyo ulitaka TEF wasichukue hatua dhidi ya Bashite hadi watakapotoa hizo rules of engagement ingawaje hapo kabla wameshawahi kuchukua hatua kama hizo kwa wengine?!
Sijasema alichofanya Bashite ni sahihi, nimesema ule ni ukichaa fulani, hauwezi kuzuiliwa kwa ukichaa mwingine wa TEF
Frankly speaking, please gimme Class 101: The Meaning, Application and Limitations of the phrase Double Standard.
Standards ni rules and procedures za ku deal na situation fulani ambazo zinakuwa applicable whenever such situation arises. Inapotokea jambo kama hilo na kuwa treated differently!, mangapi mabaya yamefanywa kwa media na kubwa kuliko ni kuuwawa kwa Mwangosi, lakini hao TEF wamefanya nini?!.
HITIMISHO: Kwamba wewe utafuatilia kipindi na unawashauri wengine wafanye hivyo wala hauna sababu ya kuhamasisha watu kwa sababu mgogoro ni kati ya Daudi Albert Bashite na vyombo vya habari na key players wao!!! Azimio la TEF na UTPC wala haliwataki wananchi wasishirikiane na Bashite; na isitoshe, wala hawana mamlaka hayo!!! Hata hao members wa TEF na UTPC I bet nao wataangalia kwa sababu, nothing is personal here!!

Hata mimi huenda nikaangalia... na kama atakuwa anaongea mambo ya msingi huenda nikamfuatilia kwa sababu sina mgogoro na Bashite!!! Muhimu ni kama nilivyosema hapo awali.
Asante hiyo Jumatatu tuangalie kisha tukutane humu jukwaani ili tupeana feedback.

Asante

Paskali
 
Hadithi ya kibiblia juu ya usaliti wa Yuda Iskariote bado roho inatenda kazi,lakini kana ketendo kilchofanywa huyo bwana cha kuvamia tena akitumia askari wenye ailaha na kufumbiwa macho,kama kweli wewe ni mcha Mungu hakikuwa kitendo cha kibinadamu wala cha kuchekelewa.
 
Kwa nini unampangia wakati wao wamekubaliana na Star TV?

Mimi na wewe ni walaji tu wa hicho kipindi kwa sababu hatufahamu makubaliano yao.
Je sahara media haikuwepo kwenye makubaliano ya kutompa ushurikiano bashite kama walikuwe na je sahara media sio wanachama kama ni wanachama nisawa na mwanaccm kuto kubaliana na maamuzi ya mabadiliko madogo ya katiba ya sasa
 
Hadithi ya kibiblia juu ya usaliti wa Yuda Iskariote bado roho inatenda kazi,lakini kana kitendo kilchofanywa huyo bwana cha kuvamia tena akitumia askari wenye ailaha na kufumbiwa macho,kama kweli wewe ni mcha Mungu hakikuwa kitendo cha kibinadamu wala cha kuchekelewa.
 
kawaida ya watu wenye akili za ccm bashite kwani hawana jipya ngoja tuone maana mi nasubiri kuona bashite Wa arusha naye tunamfungia hatutaki ujinga
 
Mkuu Chabusalu, kwanza sijasema katazo ni la kijinga, its just not practical! .

Sii wengi wanaojua kuwa TEF na MOAT ni taasisi binafsi kama makampuni binafsi na vimesajiliwa Brela, na hazina mandate kwa sababu vyombo hivi sio statutory media organizations na bonafide, representatives za waandishi, hivyo uamuzi wake sio binding. Chombo statutory kama Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania ni TAJA, Tanzania Journalist Association. Taasisi ya Media inayotambulika rasmi ni Baraza la Habari Tanzania, Media Council, MCT ambalo kwa sheria mpya linakufa na sio TEF sio MOAT!. Hivi ni vikundi tuu vya watu.

Paskali
Mkuu Paskali, yote hayo nayafahamu sana. Lakini kama wamejiwekea utaratibu huo na wanaendesha mambo yao, sioni kama kuna tatizo. Isitoshe issue iliyopo mbele, kwa sasa, sio uhalali wa TEF au MOAT. Issue ni kusalitiana. Labda uniambie kama wahariri wa Startv sio members wa TEF na Startv sio member wa MOAT, lakini kama ni members na vitrip vya mishiko vya TEF huwa wanapokea, na walikubaliana na uamuzi wa kujitenga na Daud Bashite, Startv wanapaswa watekeleze maamuzi ya TEF, na wasipotekeleza TEF hiyo hiyo ya Brela na MOAT hiyo hiyo isiyokuwa na mandate wawashughulikiea wahariri wa Startv na wamiliki wao kwa utaratibu waliojiwekea. Uelewe, kama wahariri wa Startv na Startv wenyewe walijiunga kwenye vyombo hivyo walifanya hivyo baada ya kuona umuhimu wake!

Na jambo la muhimu kulifahamu ni kwamba, hata hiyo TAJA ni kundi la watu tofauti yake na TEF pamoja na MOAT ni muundo wake tu kisheria. Suala lililoko katika mjadala sio suala la kisheria, ni suala la uaminifu. Ni jambo linaloonekana dogo lakini lenye athari kubwa kijamii. Unapokuwa na wamiliki wa vyombo vya habari pamoja na wahariri wao "wasaliti" unatarajia nini?

Naomba unielewe mkuu Paskali. Maoni yangu yanazingatia iwapo tu wahariri wa Startv ni wanachama wa TEF, na Diallo amejiandikisha MOAT na amekuwa akinufaika kama membar wa MOAT.
 
Deodatusi Balile: popote ulipo, kama taarifa hiyo umeiandaa wewe mwenyewe, tambua kwamba wewe si mwana habari aliyekamilika. Rejea sifa na wajibu wa mwanahabari ambayo ni kuwahabirisha watu katika mazingira yoyote yale, hata ya hatari.

Kama hiyo taarifa inawakilisha tasnia ya habari, ni hakika kwamba Tanzania haina wanahabari bali wachumia tumbo. Mnainajisi tasnia ya habari.

Kipi kinachohatarisha mwanahabari hadi aache kutafuta na kutoa habari, iwapo hata vitani, wanahabari wanakuwepo!

Iwapo, mna ushahidi tosha kuhusu RC Makonda kuvamia CloudsTV (nukuu ya maandishi katika rangi nyekundu), njia sahihi si kususia kuaandika maswala ya RC Makonda, hata yanayohusu ofisi yake (Mkuu wa Mkoa), ila kumfikisha kwenye vyombo vya sheria. Naamini wanahabari wanao uwezo wa kuchunguza na kukusanya ushahidi wa kutosha, na ndiyo maana wengi hutegemea vyombo vya habari kupata taarifa ya kila tukio na masuala mbalimbali.

Deodatusi Balile: TOA BORITI JICHONI KWAKO KWANZA
Nadhani kinachogomba hapa ni uelewa tu. TEF wamejitenga na Daud Bashite ambaye ndiye RC wa Dar es Salaam. TEF hawajajitenga na ofisi ya RC wa Dar es Salaam wala hawana tatizo na utoaji wa habari zinazohusu mkoa wa Dar es Salaam. Si kazi ya TEF kumpeleka mahakamani Daud Bashite. Vyombo vinavyopaswa kufanya hivyo vipo nenda kawaulize hao. Waache TEF na mambo yao kwa kuwa inaonekana hata uelewa wako wa mambo uko low mno!
 
Nadhani kinachogomba hapa ni uelewa tu. TEF wamejitenga na Daud Bashite ambaye ndiye RC wa Dar es Salaam. TEF hawajajitenga na ofisi ya RC wa Dar es Salaam wala hawana tatizo na utoaji wa habari zinazohusu mkoa wa Dar es Salaam. Si kazi ya TEF kumpeleka mahakamani Daud Bashite. Vyombo vinavyopaswa kufanya hivyo vipo nenda kawaulize hao. Waache TEF na mambo yao kwa kuwa inaonekana hata uelewa wako wa mambo uko low mno!

Una ushahidi na ulichokiandika (maandishi mekundu) au ndio huo ushabiki wa habari za uzushi wa mitandaoni!

Au utakuja na jibu lako ati Si kazi ya TEF kumpeleka mahakamani Daud Bashite!

Kama kuna ushahidi usio na mashaka uwekeni wazi, kila raia auone na kushinikiza vyombo husika kuchukua hatua.

Kumbuka RC Makonda ni Kiongozi wa juu Kitaifa, hivyo hapaswi kutiliwa mashaka ya aina yoyote, maana CHEO NI DHAMANA.
 
Mbona nape mnamuita msaliti anapoenda kinyume na matakwa yenu
we shoga mimi sio ccm!!

usiwe na mawazo ila anayesupport cdm ni cdm au anayeipinga ccm ni mpinzani!! ebu kua na heshimu kuwa ili ni jukwaa!

haimaanishi kwa sababu mimi ni mwanaume tu, basi naweza kuwa baba yako
 
Back
Top Bottom