Shindu Namwaka
JF-Expert Member
- Sep 22, 2014
- 4,911
- 3,080
Masikini kodi zetu zinatumika vibaya sana duhWeka link hapa ya blog yako uliyowasilisha hiyo kazi iliyowafanya watu wakulipie hadi Hong Kong!!!
Masikini kodi zetu zinatumika vibaya sana duhWeka link hapa ya blog yako uliyowasilisha hiyo kazi iliyowafanya watu wakulipie hadi Hong Kong!!!
Divide and ruleUAMUZI WA STAR TV NI USALITI KWA TAALUMA YA HABARIKwa muda wa wiki moja sasa kampuni ya Sahara Communications Limited, wamiliki wa Star TV na vyombo vingine vya habari kupitia mitandao ya kijamii wanasambaza taarifa kuwa watafanya mahojiano maalum na Mkuu wa Mkoa wa Dar ea Salaam, Paul Makonda, Jumatatu Mei 22, 2017.
Kusudio hilo la Star TV limekuja wakati kiongozi huyo akiwa amefungiwa na vyombo vya habari kwa uamuzi ulioitikiwa kwa pamoja baina ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) na kuungwa mkono na Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Nchini (MOAT) na taasisi nyingine za kihabari nchini. Uamuzi wa kumfungia Makonda uliotangazwa Machi 2017, ilitokana na kiongozi huyo kuvamia Kituo cha Utangazaji cha Clouds Madia, March 17, 2017 akiwa na askari wenye bunduki.
Uvamizi wa Clouds ulikuwa mwendelezo wa matukio ya RC Makonda kudhalilisha wanahabari, kutukana na kutoiheshimu taaluma ya habari. Katika tamko hilo, Makonda tulimpa masharti mepesi kurejesha uhusiano na tasnia ya habari, ambayo ni kuomba radhi waandishi wa habari kwa tukio la Clouds na matukio mengine kwa ujumla wake kama sehemu ya uungwana wa Kitanzania.
Tulisema katika tamko kwa yeyote atakayeshirikiana na Makonda naye tutamhesabu kama adui wa tasnia ya habari nchini. Kwa mantiki hiyo tunasema ikiwa Star TV wameamua kushirikiana na Makonda, basi ni wazi wameamua kwa hiyari yao wenye kujitangaza kama adui wa tasnia ya habari nchini.
Kila Mtanzania anajua jinsi ya kupambana na adui kwa namnaya kujilinda, na tasnia haitasita ku fanya hivyo. Kadhalika hivi sasa TEF tunafuatatilia kwa karibu uhusiano wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na vyombo vya habari kutokana na matukio ya mara kwa mara ya kudhalilisha wanahabari wanapokuwa kazini kwa amri yake. Matukio haya yakiendelea, tutalazimika kupitia uhusiano wa RC Gambo na vyombo vya habari nchini.
Mwisho, tunavipongeza vyombo vya habari, kwa maana ya magazeti, radio, televisheni na mitandao ya kijamii ndani na nje ya nchi kwa kutekeleza uamuzi wa kumfungia RC Paul Makonda kwa uaminifu uadilifu wa hali juu, licha ya vishawishi vya hapa na pale vinavyotolewa na wapambe wake.
Nguvu yetu ipo katika umoja wetu kama wanahabari. Tusiipoteze Mungu ibariki Tanzania.
Deodatusi Balile
Makamu Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania.
Mei 19, 2017
Pamoja na kujitosheleza kwa maelezo, lkn bado unataka ufafanuzi tuAcheni kuwapangia watu.au mliwasaidia kununua maspika?
Kama wameamua waacheni.
Ngoja nikuulize swali: Je, unakubaliana na kitendo ambacho alikifanya Makonda pale Clouds TV?! Unaamini alikuwa sahihi kabisa pale na hakuna kosa lolote alilofanya?!Sioni mantiki ya kumfungia RC mm nkiwa kama Mtanzania nafaidika nini ? na Mgomo huo Tatizo la Waandishi wa Habari nao Njaa Mbele kuliko kuzingatia Maslahi ya Watanzania Yakiwa kuta ndo mnataka Wananchi nao Tuwaunge Mkono!
Watz WOTE wakati mi sitaangalia?Siku hiyo watz wote watafungua startv kutaka kumsikiliza Makonda, sio ccm na cdm tu, hata hawa TEF na ndugu zao hawatobanduka kwny kioo. Achana na watz wanavyopenda habari motomoto bhana...
Nikae pembeni kivipi kuna sehemu nimeona kile ulichosema nadhani na Diallo mmemlisha SUMU ngoja tuone nani atapata madhara makubwa j3 issue sio kudeal na huyo member Mimi nakwambia ukweli naojua ili tatizo lakujifanya ukiwa ccm ndo UZALENDO ni upumbavu wa ajabu- Ungekaaa pembeni napigana na samaki mkubwa huyo kwa jina la bandia maana huyu amepata ujumbe atafikishia wenzake kuwa kumbe wanapoteza muda na mgomo hahahahahhaa
le Mutuz
Nimesema uongo upi?.Muogope Mungu mkuu Uongo ni dhambi