Makonda awapa Ofisi CHADEMA. Awataka walipie pango la ofisi ya Makao Makuu kwani mwenye nyumba analalamika

pantheraleo

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
691
878
Habari wakuu,
1576762781541.png

Ofisi ambayo CHADEMA Makao Makuu wamezawaidiwa

Leo Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, amewagawia nyumba ambayo ni Ofisi ya CCM Wilaya ya Kinondoni. Amesema ameamua kuwagawia CHADEMA kwa sababu Makao Makuu ya CHADEMA Wamepanga na hawalipi Kodi hivyo, Mwenye nyumba kila siku anashinda Ofisini kwake kuomba amsaidie kudai deni la Nyumba. Alimwambia nikiwadai wataingiza mambo ya Siasa.
1576762817493.png

Hivyo nimeamua kuwajengea Ofisi mpya CCM Knondoni yenye gorofa moja ili ile ya zamani wawaachie chaadema Makao makuu. amesema atatumia Sh2.5 bilioni kujenga ofisi za Chama cha Mapinduzi (CCM) katika wilaya tano za Dar Kama asante yake kwa Wanaccm.

Watu Watahoji natoa wapi hela wengine eti naingia bajeti, Nataka wajiulize
1576762849378.png

Nmejenga Chumba cha mama na mtoto Amana. Nmejenga Chumba cha Upasuaji Mwananyamala nikiwa Mkuu wa Wilaya na siku ya Uzindunzi ndo nikaambiwa nimepata Ukuu wa Mkoa “wanaohoji kwamba fedha za Serikali zinatumika kujenga ofisi ya chama, wahoji kuhusu ofisi 73 za walimu zilizojengwa katika shule hapa Dar es Salaam, wahoji kuhusu watoto wanaopewa matibabu ya moyo na hospitali ya Chanika wahoji fedha zake zinatoka wapi.”

"Wapo wenye fikra potofu ambao wakiona ofisi hizi watadhani ubunge, nafasi hizi zipo kwa ratiba ya Mungu. Mkoa huu una majimbo mangapi?” Kaongeza nafasi nliyonayo ni zaidi ya Ubunge. Wabunge wote wa Dar wapo chini yangu na wakitaka kuzungumza lazima waniombe ruhusa.
1576763028666.png

Mwisho wa siku kaweka jiwe la msingi na akasema ujenzi ukiisha Ofisi ya Zamani wapewe CHADEMA Makao makuu wahamie hapo.Unajua hawa CHADEMA, Mimi nlimuombea kura Mbowe ili ashinde uchaguzi huu sababu Uwezo wake naujua, hana madhara kwa chama chetu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni amesema baadhi waliposikia Makonda ameahidi na ameamua kujenga ofisi hizo alihusianisha na uchaguzi wa mwaka 2020.

Katibu wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Zakaria Mwaisasu amewataka wanachama walioamua kukifanyia kazi chama chao wasiogope kelele ili mradi hawavunji kanuni na katiba ya chama hicho.
 
Makonda ana huruma sana

Amewajengea Bakwata ghorofa la makao makuu

Amewapa Yanga uwanja kigamboni

Amewalipia watoto zaidi ya 600 bima ya afya

Amewajengea CCM kinondoni ofisi za ghorofa

Amejenga ofisi za walimu Dsm yote

Amewapa Chadema ofisi zilizokuwa za CCM waweze kujisitiri

Hakika hakuna kiongozi wa CCM mwenye upendi kumzidi RC Makonda!
 
Makonda ana huruma sana

Amewajengea Bakwata ghorofa la makao makuu

Amewapa Yanga uwanja kigamboni

Amewalipia watoto zaidi ya 600 bima ya afya

Amewajengea CCM kinondoni ofisi za ghorofa

Amejenga ofisi za walimu Dsm yote

Amewapa Chadema ofisi zilizokuwa za CCM waweze kujisitiri

Hakika hakuna kiongozi wa CCM mwenye upendi kumzidi RC Makonda!
Tatizo lake anataka kuwafukuza ombaomba DAR wakati yeye kwenye ofisi za matajiri hatoki!
 
Kwenye nchi hii ukiwa madarakani unaweza kupata chochote ukitakacho, hata ukienda kwa matajiri unaweza kuwatishia upendevyo na kupata utakacho. Au Makonda aonyeshe alijenga majengo mangapi kabla ya kupata madaraka aliyonayo. Unaweza hata kuuza unga au kushirikiana na wauza unga ili kupata pesa za kusaka sifa za kisiasa.
 
Kwan ni Makonda au Bashite?
Kwenye nchi hkk ukiwa madarakani unaweza kupata chochote ukitakacho, hata ukienda kwa matajiri unaweza kuwatishia upendevyo na kupata utakacho. Au Makonda aonyeshe alijenga majengo mangapi kabla ya kupata madaraka aliyonayo. Unaweza hata kuuza unga au kushirikiana na wauza unga ili kupata pesa za kusaka sifa za kisiasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom