Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,601
- 217,991
Nimeona kwenye Gazeti la Mwananchi Ndugu Makonda akitambulishwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa ya Taifa Stars , huku katibu wa Kamati hiyo akitajwa kwa jina la Herisi Said , hivi hii kamati ya hamasa ina majukumu gani na iliteuliwa na nani kwa utaratibu upi ? inakuwaje watu wasio na mchango wowote kwenye soka wakapewa jukumu la uhamasishaji ?
Makonda mtu mwenye bifu kila mahali anawezaje kuwa mhamasishaji wa soka , mchezo ambao hajawahi kuucheza tangu azaliwe ? atamhamasisha nani ? Hakika mikosi ya Taifa stars inaletwa na mengi sana ! mtu aliyeshindwa kukomboa makontena yake ya biashara bandarini atahamasisha nini kwenye soka , mchezo unaohitaji pesa , umoja na mshikamano ?
Makonda mtu mwenye bifu kila mahali anawezaje kuwa mhamasishaji wa soka , mchezo ambao hajawahi kuucheza tangu azaliwe ? atamhamasisha nani ? Hakika mikosi ya Taifa stars inaletwa na mengi sana ! mtu aliyeshindwa kukomboa makontena yake ya biashara bandarini atahamasisha nini kwenye soka , mchezo unaohitaji pesa , umoja na mshikamano ?