Makonda alichaguliwa na nani kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa ya Taifa Stars ?

Mkitaka mafanikio ya timu ya Taifa ifanikiwe muondoeni huyu Makonda kuishobokea hii timu , huu ni ujumbe wangu wa mwisho kwenu
 
Hizi chuki hazina maana.
Kwangu Taifa Star aongoze nani hakuna tofauti.
Bahati mbaya hata hamtaji mwenye bahati.
 
Chuki yako dhidi ya bwana Makonda imefika climax, you are better than that, kipi kikubwa kuwa RC dar au kuwa mwenyekiti kamati ya uhamasishaji?
Timu ya Taifa ni mali ya nchi na wananchi wake , haiwezekani watu wasio na mchango wowote kwenye soka letu wajipachike vyeo kwa malengo yaliyojificha .
 
Mkuu erthrocyte
Tuambie nani sasa awepo kwenye nafasi hiyo. Acha kuzunguka mbuyu
Kwani viongozi wa TFF kuna mwenye machungu na Mpira.
 
Mkuu erthrocyte
Tuambie nani sasa awepo kwenye nafasi hiyo. Acha kuzunguka mbuyu
Kwani viongozi wa TFF kuna mwenye machungu na Mpira.
Hakuna haja ya kuwa na hiyo kamati , kwanza imetokana na nini ? waacheni watanzania wenyewe waihamasishe timu yao
 
Nadhani jifunze kutofautisha Benchi la Ufundi na Uhamasishaji

Makonda hakachaguliwa kwenye Bench la ufundi Bali ni Mhamasishaji tu Jambo ambalo halihitaji kujua Mpira wala Kutojua Mpira, Sasa unaposema hajawahi kucheza mpira sijui umekusidia kuprove nini wakati Bakhressa hajawaji kucheza hata Chandimu na anamiliki timu ya Azam lakini wewe kwenye Uhamasishaji tu unaanza kukosoa.

Watu tunapenda ujuaji kweli.
Mkuu


Je bakhressa ana bifu kila kona???
 
Hawaruhusiwi wengine kupata kiki, ni hao wawili tu, jiwe na bashite mwingine ukikaribu tu, hawachelewi kukutumbua.
 
Nimeona kwenye Gazeti la Mwananchi Ndugu Makonda akitambulishwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Hamasa ya Taifa Stars , huku katibu wa Kamati hiyo akitajwa kwa jina la Herisi Said , hivi hii kamati ya hamasa ina majukumu gani na iliteuliwa na nani kwa utaratibu upi ? inakuwaje watu wasio na mchango wowote kwenye soka wakapewa jukumu la uhamasishaji ?

Makonda mtu mwenye bifu kila mahali anawezaje kuwa mhamasishaji wa soka , mchezo ambao hajawahi kuucheza tangu azaliwe ? atamhamasisha nani ? Hakika mikosi ya Taifa stars inaletwa na mengi sana ! mtu aliyeshindwa kukomboa makontena yake ya biashara bandarini atahamasisha nini kwenye soka , mchezo unaohitaji pesa , umoja na mshikamano ?
Ndio maana sisi wanakamati wa kamati ya roho mbaya tunafanya ibada kuomba Mungu asaidie hili litimu lifungwe magoli mia nane
 
Dogo anajua kutafuta publicity,
Niliona akiwa kwenye mkutano huku pembeni waziri mwakyembe akiwa kakaa kama vile yeye ndio mkuu wa mkoa,na Makonda ndio waziri mwenye dhamana.
Yaani RC anabehave kama yeye ndio mwenye dhamana ya mpira ndani ya jamhuri ya muungano kuliko waziri husika.
Yaani niliona Mwakyembe na ujeuri wake wote aliouonesha kipindi kile cha Richmond,kakaa anacheka cheka kwa kila jambo Makonda analoongea.
Katika hari ya kawaida,nilitegemea,waziri awe na uhusika mkubwa kuliko mwenyekiti wa kamati,lakini wapi!!hawa mawaziri mbele ya RC wa Dar,wanakuwa wapole,waoga waoga,wanakanyaga kanyaga!
Mawaziri pekee ambao wanajua nafasi zao vzr,na hawaruhusu Papaa Makonda,awavuruge,ni Jafo,Lukuvi,
 
Ujinga ujinga tu,wakati mashindano yaanza hatukujua kuwa tunahitaji kufuzu? J
Mtu kama makonda anaufahamu gani kuhusu mpira? Hatuwezi fanikiwa Kwa zima moto

Makonda anataka kutembelea nyota, aliona Haji alipata umaarufu Simba ilipojitutumua, sasa anataka nae apate mileage stars ikifanya vyema.

Sio jambo baya kama ataifanya hiyo kazi vyema ilete matunda.
 
WANAKAMATI SASA NI HAWA WAFUATAO.
WEMA SEPETU
STEVE NYERERE
JACKLINE WOLPER
AMBER RUTY
PIERE KONKI LIKWIDI
...........
Kumbuka kuwa wapo wachezaji wa zamani wa timu hiyo ya taifa, wapo viongozi walioongoza klabu na vyama vya soka kwa mafanikio makubwa lakini kamati ya uhamasishaji wanawekwa bongo movie na Paulo Makonda.

NASISITIZA TUSISITE KUIPONGEZA SERIKALI YA AWAMU HII YA TANO KWA KUSABABISHA HILO KUTOKEA. HAKIKA WANASTAHILI PONGEZI.
 
Dogo anajua kutafuta publicity,
Niliona akiwa kwenye mkutano huku pembeni waziri mwakyembe akiwa kakaa kama vile yeye ndio mkuu wa mkoa,na Makonda ndio waziri mwenye dhamana.
Yaani RC anabehave kama yeye ndio mwenye dhamana ya mpira ndani ya jamhuri ya muungano kuliko waziri husika.
Yaani niliona Mwakyembe na ujeuri wake wote aliouonesha kipindi kile cha Richmond,kakaa anacheka cheka kwa kila jambo Makonda analoongea.
Katika hari ya kawaida,nilitegemea,waziri awe na uhusika mkubwa kuliko mwenyekiti wa kamati,lakini wapi!!hawa mawaziri mbele ya RC wa Dar,wanakuwa wapole,waoga waoga,wanakanyaga kanyaga!
Mawaziri pekee ambao wanajua nafasi zao vzr,na hawaruhusu Papaa Makonda,awavuruge,ni Jafo,Lukuvi,
mkuu una jicho la Tai !
 
Back
Top Bottom