Makofi ya leo bungeni, wabunge wapatiwe huduma ya kwanza

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,607
696,730
Sijui ni kuzidiwa na utamu? Au ni umafiki? Au ni sababu ya kupata ladha mpya!! Waitwao wabunge leo wa CCM na wale covid-19 walipigia makofi kila alichokisema mama
Kuna wakati hata hayakuhitajika lakini yalipigwa... Meza za bunge leo zimeipatapata na viganja vya waheshimiwa kama havijavilia damu sijui? Tutaona kesho kama kuna watakaoweza hata kushika kalamu
IMG-20210422-WA0161.jpg
 
Shujaa alikuwa anaweza kwenda pale Jitegemee-Mabibo akasema mbunge wa Ubungo, chapa kazi, maendeleo hayana chama, akatoka na msafara wake, akafika Kimara-Stop over akasema hawezi kujenga barabara kwa sababu walimchagua John Mnyika kutoka Chadema kuwa mbunge. Jamaa alikuwa ni mtawala anaeweza kujisahau ndani ya dakika 15 alichosema awali..... 😃
 
30 Reactions
Reply
Back
Top Bottom