Makofi wa! wa! wa! waaaaaaa

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
Tunayemsikiliza sasa ni mtu ambaye ninamuheshimu mno mno. Huyu ni mkurugenzi na mwanzilishi wa chuo cha mguu peku, Barefoot College, ndugu Bunker Roy.
Msikilize:
- nilipomaliza shule nilijiambia kuwa nataka kuanzisha chuo kwa ajili ya watu masikini, watu wasio na elimu hata kidogo
- alianzisha chuo katika kijiji cha Tilonia ambapo ni jangwa. Kuna wakati hawapati mvua kwa miaka 6
- Sababu ya kuita chuo "barefoot" ni kuwa watu wengi duniani wanaotembea bila viatu wana maarifa na uwezo mkubwa
- chuo hiki ni sehemu ambayo walimu na wanafunzi wanajifunza
- chuo hiki hakikubali watu wenye vyeti vya shule au vyuo lakini zaidi ni kuwa hata wanaohitimu chuo hiki hawapewi vyeti
-** Anatuonyesha nyumba zilizojengwa na mwanafunzi wa chuo hicho ambaye hajui kusoma wala kuandika
- paa la chuo hicho lilijengwa na wanawake kwa kutumia teknolojia ya India ambayo imekuwa ikitumika zaidi ya miaka 100
- kijiji cha Tilonia kimeshaingia karne ya 21: wana teknolojia ya mtandao usiwaya, wanauza bidhaa zao mtandaoni (Tilonia), n.k.
**anatuonyesha teknolojia ya kukusanya maji ya mvua.
- teknolojia hii inasaidia kuwapatia wanavijiji maji na hivyo kuwapa watoto muda wa kwenda shule (maana hutumia masaa mengi kutafuta maji) na pia kuwapa wazazi wao muda wa kufanya mambo mengine badala ya kutembea mwendo mrefu kutatufa maji. Baada ya kuanza kutumia teknolojia hii katika mashule vijijini, idadi ya watoto wanaokwenda shule iliongezeka!
- wahandishi wa kisasa ni wajinga sana...elimu yao imeshindwa kabisa kutatua matatizo makubwa ya masikini na watu vijijini
- alikwenda kwa waziri wa maji kumwambia kuwa serikali ijihusishe na mradi wa kukusanya maji ya mvua mlimani, waziri akasema: Hutaweza maana mhandishi mkuu amesema haiwezekani. Bunker akamwambia waziri: nipe ruhusu nijaribu. Mradi huo ulifanikiwa na sasa vijiji vingi vinatumia teknolojia hiyo
* Anatuonyesha picha ya vibao vinavyokusanya nishati ya jua. Teknolojia hii iliwekwa na inakarabatiwa na mtu ambaye amehudhuria shule kwa miaka 6 tu maishani mwake.
- tumevipa vijiji zaidi ya 6000 teknolojia ya nishati ya jua
- anatuonyesha picha ya mhandisi wa kwanza wa teknolojia ya nishati ya jua ambaye ni mwanamke wa nchini Afghanistan
- asilimia 60 ya watoto vijijini India hawaendi shule maana wanachunga mifugo. Lakini wana uwezo wa kwenda shule usiku, ila hakuna taa. Sasa tumetengeneza taa zinazotumia nishati ya jua kwahiyo kuna shule vijijini ambazo wanafunzi wanakwenda shule usiku
** anatuonyesha picha ya dakitari wa kijijini.
- huyu bwana mnavyomuona ni mlemavu na hakuwa na elimu hata kidogo. Tulikumta barabarani tukamsimamisha tukamwambia, "Twende chuoni kwetu na baada ya miezi sita utakuwa dakitari!" Hivi sasa anafanya kazi kwenye zahanati vijijini akipima watu damu, choo, anatoa dawa, n.k.
- anaseme kuna kijiji Ethiopia ambapo watoto wanatembea zaidi ya saa moja kwwenda shule wakiwa wamebeba maji kwa matumizi shuleni wakati kwa teknolojia rahisi sana shule hizo zinaweza kukusanya maji ya mvua
- wanafunzi wanaokubaliwa katika chuo chake lazima wawe wametoka vijijini, wachaguliwe na kijiji, na mafunzo wanayopata yanaendana na mahitaji ya kijiji wanachotoka na lazima warudi kijijini kwao
- moja ya sababu inayowafanya chuo hiki wasitoe vyeti ni kuwa ukishampa mtu cheti basi ujue atakimbilia mijini wakati nia ya chuo hiki ni kufunza wahandisi, wanasayansi, na wataalamu mbalimbali kwa ajili ya wakazi vijijini
- alipoanza kuishi kijijni baada ya kumaliza chuo wanakijiji walimuuliza kama amefanya kosa mjini na anawakimbia polisi. Wanakijiji walidhani hivyo maana mfumo wa elimu ya kisasa unawaondoa wasomi vijijini, wanakijiji hao hawakuamini kuwa Bunker amekwenda kijijini hapo kuishi nao. Ameishi hapo kwa miaka 35 sasa
- Anamaliza kwa nukuu toka kwa Mahtma Gandhi: Kwanza wanakudharau, kisha wakucheka, kisha wanapambana nawe, kisha unashinda!

Makofi wa! wa! wa! waaaaaaa
 
looh ,very encouragng news...tenx and hopin wil be the top story of the day...makofi wa wa wa w
 
The Following User Says Thank You to kilimasera For This Useful Post:

Elia (Today)​
 
The Following User Says Thank You to kilimasera For This Useful Post:

ezan
(Today)
 
noble initiative, waambie Keep it up! maybe na sisi tufikirie vitu kama hivyo
 
noble initiative, waambie Keep it up! maybe na sisi tufikirie vitu kama hivyo

kwa hapa bongo ni ngumu sana bwana Russian sijui labda kutokee mapinduzi ya ajabu ya kiuchumi yaani watu wa vijijini wamesahaulika kabisa!
 
Back
Top Bottom