Makocha, wachezaji wasio na vibali kutumika kabla ya Ligi Kuu kuanza

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Serikali imesema Vilabu vinaweza kuwatumia wachezaji, makocha na wafanyakazi wengine ambao ni raia wa kigeni katika kipindi hiki ambacho Ligi Kuu haijaanza.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Sera, Bunge na Kazi, Jenista Mhagama amesema Vilabu vinatakiwa kukamilisha taratibu za kisheria za kuwaombea vibali vya kazi raia hao.

Ametoa wito kwa waajiri wote wakiwemo wamiliki wa vilabu vya mpira kuhakikisha wanazingatia Sheria za Kazi na kufanya mashauriano na Ofisi hiyo wanapopata changamoto badala ya kukimbilia kwenye vyombo vya habari.
 

Attachments

  • TAARIFA KWA UMMA.pdf
    711.8 KB · Views: 7
Back
Top Bottom