Makinda ampinga Zitto hoja ya Kumuondoa Waziri Mkuu

Kama uliangalia bunge jana utakuwa ulimsikiliza vizuri Zitto na kuelewa mchakato anaotaka kuufanya.

Katika kuwasilisha hoja ya kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu, mwenye hoja anatakiwa kwanza awe na sahihi sabinni za wabunge, na ndicho alichosisitiza Zitto jana kwamba wabunge wote wenye uchungu na nchi hii kuanzia leo wajitokeze kusaini ili sasa kuanzia hapo hoja hiyo ipate kufikishwa kwa spika kwa ajili ya ufuatiliaji na utekelezaji.

Nadhani kuna watu wanajaribu kuipotosha hoja hii as if Zitto akishapata saini sabini tu, basi waziri mkuu ana step down. Tujitahidi kujiepusha na upotoshaji unaofanywa hapa, bila shaka kwa malengo maalum.

Hata alichoandika january makamba kwenye twitter yake ni katika kujipapatua tu, iko wazi kabisa kwamba Zitto ni mtu maarufu sana, hawezi kuhitaji public stunt katika hili, bali amewatega waosha vinywa wote wa ccm ili watanzania wajue ni mbunge yupi mzalendo na ni yupi domokaya.

wELL SAID mURRA

It is M4C:
  • Movement 4 Change
  • Movement 4 the Cause
  • Movement 4 our Children
  • Movement 4 our Country

The time has come!!
 
Kirobo kazini

Kwa ufupi hoja ya Zitto labda bunge lijalo siyo J3 tena amesema sio utaratibu na mambo ya hayo ni makandokando haikuwa ya msingi.

Kwa maana hiyo Mawaziri watapeta kama kawa na tutarajie chuki na kisasi ktk kipindi hiki cha madaraka na prove taaarifa ya kuwa ni mabadiriko ya baraza la mawaziri ndio litawatoa sio kura za bunge.

Na kulingana na kauli ya Kiroboto Zitto kasema kuwa tatizo si waziri mkuu bali mawaziri wake ndo hoja ya Zitto kwa maana nyingine watakao achia ngazi ni baadhi ua mawaziri si baraza zima na ikumbukwe kuwa Mrema kasema ni system yote ilitakiwa wote waondoke.

Tanzania tunasafari ndefuuuuuuu sana kufika
 
Anasema pia kuwa siku zilizobaki ni tatu na zinazohitajika ni 14, so mama anasema wakusanye tu lakini hoja hazina msingi
 
Hivi wanasheria wa CDM kina Lissu, Mdee etc hawakujua taratibu za kuwasilisha hoja ili kumshauri Zitto kabla hajaumbuka na hoja yake hii kama ilivyotokea sasa??

Pamoja na kwamba namsapoti Zitto (kama yeye), nalaumu magwanda kwa kutokuwa makini.
 
Zoezi Batili.......................
Thanl You Speaker...
Someni katiba.....
 
Ni kutoka bungeni muda huu na tusome katiba ya nchi vizuri na kanuni za bunge. Tufanye mambo mengine sasa na tuache jazba.
 
Dah! inaonyesha kweli mbio hizi zinaweza kwama ukutani maana kuna kipengele cha D kinasema hivi:-
(d) haijapita miezi tisa tangu hoja ya namna hiyo ilipotolewa Bungeni na Bunge likakataa kuipitisha.

 
anasema hoja ya Zitto haikubaliki kama wanataka wakusanye kwa ajiliya kuletwa kwenye bunge lijalo...ni kama Makamba anajiona shujaa vile kwa hii movie
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom