Kwani hujui MD25?
Kama huji kaa kimya kaka usilazimike kuchangia hakuana amri ya polisi eti ni lazima kuchangia usipochangia utakamatwa au kushitakiwa siyo hivyo kabisa, tunatakiwa kuwapinga watu bila kuingilia utawala na mambo yao binafsi.
Kama mjinga mmoja alisema eti Mbunge fulani asichaguliwe kwa sababu hana mke SWALI: Mke wa mbunge au mume anakusaidia nini wewe mwananchi? Mayai ya huyo mtu yana faida gani kwako wewe na watanzania kwa ujumla? Elewa kuwa hakuna chuo wala shule ya ustaraarabu jiheshim tu kaka na usitumie lugha kali ambayo hata mama yako akisoma kwa hakika atasikitika japokuwa unatumia pen name, hatuendi hivyo JF inasomwa na watu wa rika zote kutumia lugha kama hizo wote tunaoingia humu tunaonekana wahuni.
Hata hivyo mada yenyewe ilihusu maslahi ya umma wewe ukaingiza masuala bianafsi sijui ulielewa mada au ulikuwa una maana gani!!!!!??????
Lugha za aina hii ndizo zinazotuharibia lafudhi ya JF. Falsafa ya wastaarabu ni kujadili hoja si kumjadili mtu. Inapotokea kumjadili mtu basi tujikite katika hoja ya msingi si kuingilia mambo binafsi ni kujidhalilisha na kumshalilisha mtu ambalo ni kosa la jinai.