Makhirikirhi na akli zetu kiuchumi!

utiyansanga

JF-Expert Member
May 19, 2010
214
7
Wale jamaa wa ngoma za kienyeji kitoka Botswana wameletwa tena! kutafuta fedha za Watanzania .Hiki ni kielelezo kingine cha uduni wa fikra zetu!Ukichunguza kwa makini kinachofanywa na hili kundi si lolote si chochote ukilinganisha na ngoma zetu za kienyeji ...Kinachotusumbua hapa ni uduni wa fikra na kutojitambua .Muziki wa Tanzania ni bora sana hebu angalia vikundi kama Parapanda ,au MRISHO mPOTO,sisi tambala na wengine...JAMANI KUJIAMINI NA KUPENDA UTAMADUNI WETU NI HATUA MUHIMU KUELEKEA KWENYE UKOMBOZI WA KWELI.WATANZANIA TUAMKE!
 
Unajua hata me huwa nashindwa kushangaa. Nimeshaona mara nyingi siku hizi kwenye sherehe au hafla mbalimbali tunaambiwa kuna kikundi kikakuja kucheza ngoma. Wakiingia wanacheza hizo ngoma za Makhirikhiri. Huwa najiuliza: hivi Tanzania hii ilivyo na utajiri wa ngoma kutoka kwenye makabila zaidi ya 120, hakuna ngoma ya kucheza ila hiyo ya Botswana? Kwa kweli tunatia aibu. Nadhani hata wao (watswana) na hata wengine wa nchi nyingine wanatucheka kama si kutuhurumia, tunapoonyesha kuhusudu ngoma za wenzetu wakati sisi tunazo kibao lakini hatuzithamini. Tubadilike jamani!
 
sawa kabisa nakubaliana na wewe.

Ila kuna tatizo sana pia kwenye ngoma zetu, huwa naona karibu vikundi vingi wanakata viuno tu, hamna style mpya!! sanaa kawaida huwa inauzika na kama watu watakuwa creative basi itajiuza sana.

Angalia hat miziki ya kizazi kipya, niambie ni nani anayeimba na kuwa ana kundi la kucheza style ambazo ni unique zenye kuvuta hisia za watu

kweli makhirikhiri sioni kitu hata nilivyoona kwenye mkanda wao ni wimbo mmoja tu mzuri,mingine bomu.

When we talk, eat, think about globalization hizi ni athari zake na tukubaliane ni haki ya mtu kuamua anataka au anamtaka nani ili afurahishwe ndio maana kila kukicha watu wanabishana kuhusu arsenal na man U, hata kukosoa makocha wao!!

Simply kuna tatizo sehemu fulani , halijaanza sasa, lakini kubwa ni kuwa hatuna utamaduni wetu...umepotea, umeacha room ya hawa watu kuja na kwa sababu kila kitu tunacopy kesho watakopy hapa Tz ,angalia miziki ya zaire ilivyomeza utamaduni wa kitanzania.

It is too late but not like that to restore our identity that is our culture.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom