Makerere University ‘ Vinara ‘ Afrika, SAUT ni ya ‘ Vipanga ‘ tupu na UDSM ni ya ‘ Hohe Hahe ‘ waliokubuhu

naomba kufahamu kwa uelewa wangu mdogo hv dv 3 point 13 mfano na dv one ya hkl na akachaguliwa kusoma udsm yupi kipanga ...
Hujanielewa Nadhani,sio kila kozi inayotolewa UDSM ina competition, unaweza ukawa una one HKL lakini Hukuomba kozi mfano inayohusu arts and heritage.wakati huo kuna mwenye division 3 ameaply hiyo,unadhani atakosa? Ndo hapo tunapokataa kuwa sio wote wanaosoma UDSM wana division 1
 
Huu Uzi ni kama una bifu au chuki binafsi na UDSM. Mi sijasoma udsm lakini naamini bado ni chuo bora east Africa. Labda kwenye Hivyo viwango udsm inashika namba ngapi kwa Africa ukilinganisha na SAUT!?
 
Ni kweli kabisa hakuna mtu sensible anaweza kusema chuo Fulani ni kizuri kuliko kingine hasa kwa sisi ambao tuko makazini wote tunapiga kazi vizuri bila kujali Nani amesoma chuo gani
hizi huwa ni mada za first year tuwasamehe maana kioindi hiki wanatambiana nani bora kuliko mwenzake , wengi wanatumaini kuchaguliwa chuo furani kunampatia kipaumbele zaidi ya mwingine lakini wanashindwa kutambua kwamba maisha sio black and white kama wanavyofikiria.
 
Dah mungu anisaide labda mtazamo wangu utabadilika, yaani tng ninekuwa na negative perception juu ya Genta nikiona nyuzi zake za sifa sifa nazipuiza kabisa, najikuta nasoma kwanza comments za watu kisha ndio narudi kusoma uzima, vinginevyo sitasoma kabisa huo Uzi!
 
Haahaaaahaaa mbavu zangu mie
Bahati mbaya sikusoma chuo hapa bongo but kihistoria na kiuhalisia chuo cha SAUT ni moja kati ya vyuo vya hovyo kabisa vinavyozoa takataka za kila aina kutoka Advance. Ni ukosefu wa adabu kuifananisha SAUT ya UDSM..labda uifananishe SAUT na wenzake kina IFM, TEKU, Mwl. Nyerere na vyuo vingine vya hovyohovyo
 
Katika hali inayoonyesha kwamba Uganda si tu kwamba ni Taifa lenye Wasomi walioiva kabisa bali kama hujasoma ama katika Shule zao za Msingi au Upili au Vyuo Vikuu vyao basi jua hujaiva Kichwani. Ni kwamba Chuo Kikuu cha Makerere kimetajwa kuwa Chuo Bora Namba Tano Barani Afrika huku kile ambacho Watanzania wengi wanakisifia cha UDSM kikiwa hohe hahe ( Kiubora ) Afrika Mashariki, Afrika, Duniani na hata Mbinguni pia.

Na Kuonyesha kwamba Waganda hawatanii Kielimu Taarifa / Ripoti rasmi iliyotolewa na The Times Higher Education World University Rankings 2020 imekitaja Chuo Kikuu cha Makerere kuwa ndiyo Chuo Kikuu bora Afrika Mashariki, Kati na Magharibi huku Kikipitwa tu na Vyuo Vikuu vya Afrika ambapo kwa Afrika nzima Chuo Kikuu cha Cape Town (UCT) Kinaongozwa japo na chenyewe kwa dunia nzima Kinaongozwa na Chuo Kikuu cha Oxford kilichopo nchini Uingereza.

Baada ya hapo Mimi kama Mtanzania sikukubali kabisa hivyo nikachukua jitihada zangu binafsi na Kuwauliza hawa ‘ Jamaa ‘ kwanini Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ( ambapo walisoma hapo wanajifanya wana Akili na Wameelimika kuliko wa Vyuo vingine nchini Tanzania ) hakipo katika Viwango bora jibu la haraka haraka nililojibiwa ni kwamba Wahitimu wa hapo ( Wanafunzi ) hawako ‘ Competent ‘ kabisa na wakiacha Kuibia ibia / Kuibiana Mitihani au Kufaulu kwa ‘ Magumashi ‘ basi wanaweza kidogo Kufikiriwa lakini kwa sasa UDSM siyo Chuo Kikuu bora tena.

Mwishoni kabisa nikamuuliza huyo Mtu sawa nimeshakubali kuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sasa ni ‘ Kwishnei ‘ Kitaaluma na Mimi kama An Eagle nakubalina nao kwa 100% kwani huwa nakutana mno na Watu pamoja na Wanafunzi waliosoma UDSM na wengi wao ‘ arguments ‘ zao ziko ‘ very illogical ‘ hadi utawaonea huruma. Nikamwomba aniambie angalau ni Vyuo Vikuu gani Afrika Mashariki ambavyo kwa sasa vinakuja kwa Kasi sana na vinaweza hata Kushindana na Makerere, UCT na Oxford akanitajia kwa Tanzania ni Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino kilichopo Mwanza, Chuo Kikuu cha Day Star kilichopo nchini Kenya na Chuo Kikuu cha Ndejje kilichopo nchini Uganda.

Kwa bahati mbaya An Eagle bado sijasoma sana na Kufika ngazi za Elimu ya Juu kama wengi wenu hapa JamiiForums ila kutokana na huu Utafiti basi nashawishika haraka sana nikitaka Kusoma Elimu ya Juu niende Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino ( SAUT ) Mkoani Mwanza na ule mpango wangu niliokuwa nao wa Kusoma Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ( UDSM ) nimeusitisha rasmi kwani na Mimi sitaki Kusoma katika Chuo ambacho hakikubaliki na ‘ Wataalam ‘ na hata katika Viwango bora duniani hakipo kabisa na kinatia tu aibu.

Kwa Utafiti huu ‘ Murua ‘ kabisa nadhani Wazazi wengi nchini Tanzania sasa mtakuwa mnajua ni wapi kuwapeleka Watoto wenu ili wakawe ‘ Vipanga / Werevu ‘ ambapo ni SAUT Mwanza na pia mmeshajua ni wapi hamtakiwi hata ‘ Mthubutu ‘ kuwapeleka Watoto wenu wakasome kwani watatoka huko ‘ Watupu / Hohe Hahe ‘ na mtajuta kabisa.


Hongereni sana Watafiti wa Elimu.

Wewe sio tu kwamabani mtu mjinga, lakini pia wewe ni mwovu sana. Tatizo kubwa zaidi huwezi pia kubadilika maana umepitwa na wakati
 
Dah mungu anisaide labda mtazamo wangu utabadilika, yaani tng ninekuwa na negative perception juu ya Genta nikiona nyuzi zake za sifa sifa nazipuiza kabisa, najikuta nasoma kwanza comments za watu kisha ndio narudi kusoma uzima, vinginevyo sitasoma kabisa huo Uzi!

Kumbe An Eagle ni geta? Nilikuwa sijui hilo. Endelea Kuamini hivyo hivyo na Akili zako hizo mbovu za ' Kipa Katoka / Kipumbavu ' na nahisi yawezekana hata mwenyewe huyo geta aliko anawadharau na kuwapuuzeni kuliko maelezo. Halafu kuna ' Tetesi ' kwamba na hii ID ya nipekidogo nayo ni yake? Je unaweza Kujitetea kwamba siyo yake ili Wadau hapa wakuamini / tukuamini Ndugu?
 
all in all hizi degeree zetu ni za ukarani tuuu no matter what , maana hakuana kitu cha maana wasomi tumefanya zaidi ya kulalamika tuu mara chuo flani sijui kipo juu kingine ni cha kata , all in all nadhani material yanatumika hayana tofauti sana na unaweza kuta hata hawa walimu wanashare , no matter wapi degereeee yako ya ukarani inatokea tunatakiwa kufanya changes in real life na kuacha hizo simulations za vyuoni.
 
Kweli ni mbovu, mwanafunzi alie hitimu hapa Tz kwenye shule ya st kayumba four 4, akienda Uganda anaweza kufundisha wanafunzi wa Uganda form six kabisa, elimu yetu iko juu sana Kenya wanajitahidi ila hawawezi kutufikia hata robo hapa Africa ni S.A. na Egypt ndo viwango vyetu......
Kenya ipi unayoizungumzia we we? Kwenye masuala ya elimu Kenya wametuzidi mbali narudia mbali hatuwafikii hata theluthi moja maahindano ya vyuo vikuu yaliyowahi kufanyika afrika fainali aliingia naijeria na Kenya sio udsm,sio mzumbe wrote hawakufua dafu
 
Ugonjwa wa inferiority complex ni mbaya sana unatibika dawa yake ni vidonge vinaitwa haloperidol au amitryptyline.Au kama ukizidiwa unapigwa sindano inaitwa injection modicate
 
Back
Top Bottom