Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,886
- 6,883
Hapa ni moja ya majengo ambayo wapigania ukombozi barani Afrika walikuwa wakiishi akiwamo Marais Mugabe wa Zimbabwe na hayati Samora Machel wa Msumbiji kama ilivyokuwa makazi ya wapigania haki wa South Afrika pale Morogoro kilipo chuo cha Sokoine. Umbali wa km 34 toka Lindi mjini eneo lijulikanalo kama Farm 17.
Jambo la kushangaza serikali imeshindwa kubuni njia ya kuyaendeleza majengo haya na kubaki katika hali mbaya kwa kiwango hiki kwa sababu ya kuyatelekeza. Pamoja wanakijiji hapo kuamua kuanzisha shule ya sekondari lakini hali ya majengo hairidhishi, hali ni kama pichani inavyoonekana.
Gharama ya ujenzi wa majengo hayo siku ya leo ni mabilioni ya pesa, kwa nini kisianzishwe chuo kama ilivyofanyika Morogoro SUA kuyanusuri majengo na papo majengo yaweze kutunufaisha watanzania?