Makazi ya Mugabe, Samora yalivyotelekezwa Nachingwea

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,886
6,883
jengo_samora.jpg

Hapa ni moja ya majengo ambayo wapigania ukombozi barani Afrika walikuwa wakiishi akiwamo Marais Mugabe wa Zimbabwe na hayati Samora Machel wa Msumbiji kama ilivyokuwa makazi ya wapigania haki wa South Afrika pale Morogoro kilipo chuo cha Sokoine. Umbali wa km 34 toka Lindi mjini eneo lijulikanalo kama Farm 17.

Jambo la kushangaza serikali imeshindwa kubuni njia ya kuyaendeleza majengo haya na kubaki katika hali mbaya kwa kiwango hiki kwa sababu ya kuyatelekeza. Pamoja wanakijiji hapo kuamua kuanzisha shule ya sekondari lakini hali ya majengo hairidhishi, hali ni kama pichani inavyoonekana.

Gharama ya ujenzi wa majengo hayo siku ya leo ni mabilioni ya pesa, kwa nini kisianzishwe chuo kama ilivyofanyika Morogoro SUA kuyanusuri majengo na papo majengo yaweze kutunufaisha watanzania?
 
Mkuu!

Hizo ndiyo za serikali DHAIFU. Si unakumbuka ile meli ya samaki wa Magufuli ilivyo oza na kuibiwa kila kitu licha ya kuwepo ulinzi wa POLICECCM wa masaa 24. Hakuna wanalo liweza zaidi ya kujikita kwenye UFISADI. Hiyo nyumba wanaiona hailipi ndiyo maana wameitelekeza Mkuu. Labda tuwaombe Wana Msumbiji waje kuikarabati ili iwe jengo la historia kwao.
 
Hayo si mambo ya kipao mbele kwa CCM, Kule SUA walifanya kwa vile huwa wanapata misaada hivyo ilikuwa njia ya kujikomba kupata misada sasa hao wengine hawana uwezo kutoa misaada
 
Mkuu!

Hizo ndiyo za serikali DHAIFU. Si unakumbuka ile meli ya samaki wa Magufuli ilivyo oza na kuibiwa kila kitu licha ya kuwepo ulinzi wa POLICECCM wa masaa 24. Hakuna wanalo liweza zaidi ya kujikita kwenye UFISADI. Hiyo nyumba wanaiona hailipi ndiyo maana wameitelekeza Mkuu. Labda tuwaombe Wana Msumbiji waje kuikarabati ili iwe jengo la historia kwao.

Unaweza kushangaa serikali inavyoingia gharama kubwa kujenga vyuo wakati kuna majengo kama haya yanaweza kuwa chuo kikuu. Hata Waziri wa Mambo ya Nje Membe anayetokea huko huko, Mkapa, Salma na wengine wengi tu hawaoni uchungu na majengo haya ambayo yangeweza kupunguza gharama ya ujenzi wa vyuo vikuu? Angalia CCM sasa inaingia gharama kubwa kujenga chuo chao Dodoma, na serikali nayo inajenga vyuo vingi tu, kwa nini kimoja wapo kisiwe katika majengo haya ambayo yanahitaji tu renovation kisha mambo ni mdundo tu.

Miko ya Kusini huenda ni ya Mwisho kwa vyou vikuu nchini lakini wao wenyewe wa huko akina Mathias Chikawe wamelala tu na kufanya mikingamo ya kuua upinzani.
 
Hayo si mambo ya kipao mbele kwa CCM, Kule SUA walifanya kwa vile huwa wanapata misaada hivyo ilikuwa njia ya kujikomba kupata misada sasa hao wengine hawana uwezo kutoa misaada

Majengo labda yangekuwa Dar, Dodoma, Morogoro hapo yangechangamkiwa kwa vile ni karibu na Magogoni.
 
Serikali ya CCM kwa kujisahau hawajambo............

Natafuta uwezekano wa kumvaa Mkuchika au Membe watoe ufafanuzi kwa nini wimbi la ufunguaji vyuo vikuu nchini hauendi kwa kasi kama mikoa ya kusini wakati kuna majengo tayari kama haya ambayo yangewexa kutumika.
 
Natafuta uwezekano wa kumvaa Mkuchika au Membe watoe ufafanuzi kwa nini wimbi la ufunguaji vyuo vikuu nchini hauendi kwa kasi kama mikoa ya kusini wakati kuna majengo tayari kama haya ambayo yangewexa kutumika.
Ni kweli kuwa KUSINI ni yatima laini tegemea kupokea majibu rahisi sana kutoka kwa hawa watu maana huwa siamini kama wanauzalendo kivile wa kujali kule wanakotoka na wananchi wao wa huko
 
Kusini walitoa rais tukajua afadhari ndugu na jamaa zetu watasikika vilio vyao pamoja na kuwa na maendeleo makubwa kama ilivyo kuwa toka enzi za zamani enzi za kituo cha biashara duniani

Nikikumbuka kitabu nilicho soma kuh sehemu kuu ya biashara duniani ilikuwa uko kusini...Simanzi tupu
 
Ni kweli kuwa KUSINI ni yatima laini tegemea kupokea majibu rahisi sana kutoka kwa hawa watu maana huwa siamini kama wanauzalendo kivile wa kujali kule wanakotoka na wananchi wao wa huko

Nilikuwa natalii kwenye blog ya Mjengwa leo ambaye yuko huko Umachingani, ameonekana kushangaa kikubwa, kwani tatizo la wengi wetu tukishafanikiwa hatukumbuki tulikoanzia kuvaa lubega tukichunga ng'ombe na kondoo na kuona kueleza hayo ni aibu, kumbe ni dalili za jitihada tulizofikia na hivyo kurudi kuwahimiza wenzetu wafuate nyayo.

Nakumbuka picha kumbukumbu ya mtutu wa bomu pale mikindani unaolenga baharini silaha iliyotumiwa na wazungu enzi hizo kujilinda na maadui. Viongozi wetu wanaangalia tu visima vya chumvi vilivyo pale bondeni lakini kule kwenye kumbukumbu ya mambo ya kale umbali wa kuinua kichwa na kutupia jicho huku barabara kuu ikipita mita chache tu hakuna jitihada za kuhifandhi kumbukumbu hiyo. Ama kweli kwa waseremali utakosa kiti cha kukalia.
 
Kusini walitoa rais tukajua afadhari ndugu na jamaa zetu watasikika vilio vyao pamoja na kuwa na maendeleo makubwa kama ilivyo kuwa toka enzi za zamani enzi za kituo cha biashara duniani

Nikikumbuka kitabu nilicho soma kuh sehemu kuu ya biashara duniani ilikuwa uko kusini...Simanzi tupu

Ukibahatika kufika huko ndipo utakapojua kwamba mkombozi ni mmisionari, la sivyo leo tungekuwa tunaongea mengine kama ilivyotokea safari moja nilipoenda ziwa Tanganyika Km kadhaa hivi kutoka Kipili. Tulikuwa na gari dogo aina ya Landrover rangi nyeupe. Hiyo barabara ilikuwa mpya tu ilitengenezwa kwa jitihada za Mbunge Itara wa wakati huo kutokea Kate, Kitosi na kisha kuishia ziwa Tangabyika. Katika kumbukumbu yao huko ni greda lililokuwa linalima barabara. Gari iliyofuata ni chakavu landrover. Ya kwetu ingawa ilikuwa short chesis hard top na nyeupe, tulikuwa na ziada ya kuwazuia wasifuate maana ilikuwa ni mara yao ya kwanza kuona kitu kama hicho na wakawa wanasema ni bado mtoto anakua. Tuliwatahadhalisha wasilisogelee mno wakati linatembeza wanaweza pata ajali wao walisema mbona lina macho linaona? (kina macho kinaona). Mbaya saidi tulipofika mahala na kusimamisha gari wakawa wanachungulia kuona kama ni la kike au kiume. Basi ni vituko duniani kuna mambo. Kuna sehemu ambacho ni bado sana. Hiyo ilikuwa Miaka ya 90.
 
Mimi nikikumbuka maisha ya Tza wala sijalaumu kwa nini maishani mwangu sikuwa i kumpigia kura mpuuzi yeyote na sito fanya hivyo mpaka nijue kweli viongozi wetu hawajijali wao na familia zao....Unachoongea kuh Kusini ni kweli tupu japo sijafika
 
its about time we send these pics to these guys and hopeful they can come to invest!!!!
 
Ukibahatika kufika huko ndipo utakapojua kwamba mkombozi ni mmisionari, la sivyo leo tungekuwa tunaongea mengine kama ilivyotokea safari moja nilipoenda ziwa Tanganyika Km kadhaa hivi kutoka Kipili. Tulikuwa na gari dogo aina ya Landrover rangi nyeupe. Hiyo barabara ilikuwa mpya tu ilitengenezwa kwa jitihada za Mbunge Itara wa wakati huo kutokea Kate, Kitosi na kisha kuishia ziwa Tangabyika. Katika kumbukumbu yao huko ni greda lililokuwa linalima barabara. Gari iliyofuata ni chakavu landrover. Ya kwetu ingawa ilikuwa short chesis hard top na nyeupe, tulikuwa na ziada ya kuwazuia wasifuate maana ilikuwa ni mara yao ya kwanza kuona kitu kama hicho na wakawa wanasema ni bado mtoto anakua. Tuliwatahadhalisha wasilisogelee mno wakati linatembeza wanaweza pata ajali wao walisema mbona lina macho linaona? (kina macho kinaona). Mbaya saidi tulipofika mahala na kusimamisha gari wakawa wanachungulia kuona kama ni la kike au kiume. Basi ni vituko duniani kuna mambo. Kuna sehemu ambacho ni bado sana. Hiyo ilikuwa Miaka ya 90.
I am lost in between,to buy your story OR shove it back to you
 
jengo_samora.jpg

Hapa ni moja ya majengo ambayo wapigania ukombozi barani Afrika walikuwa wakiishi akiwamo Marais Mugabe wa Zimbabwe na hayati Samora Machel wa Msumbiji kama ilivyokuwa makazi ya wapigania haki wa South Afrika pale Morogoro kilipo chuo cha Sokoine. Umbali wa km 34 toka Lindi mjini eneo lijulikanalo kama Farm 17.

Jambo la kushangaza serikali imeshindwa kubuni njia ya kuyaendeleza majengo haya na kubaki katika hali mbaya kwa kiwango hiki kwa sababu ya kuyatelekeza. Pamoja wanakijiji hapo kuamua kuanzisha shule ya sekondari lakini hali ya majengo hairidhishi, hali ni kama pichani inavyoonekana.

Gharama ya ujenzi wa majengo hayo siku ya leo ni mabilioni ya pesa, kwa nini kisianzishwe chuo kama ilivyofanyika Morogoro SUA kuyanusuri majengo na papo majengo yaweze kutunufaisha watanzania?

Bodi ya Utalii na Watu wa makumbusho waingize katika kumbukumbu za maeneo ya kuhifadhiwa kwa ajili ya Utalii wa ndani na nje.
 
Bodi ya Utalii na Watu wa makumbusho waingize katika kumbukumbu za maeneo ya kuhifadhiwa kwa ajili ya Utalii wa ndani na nje.

Wazo lako lingekuwa na maana kwa viogozi wetu kama kungekuwa na aina ya utekaji mapato tokaka eneo hilo, la sivyo kazi bado.
 
Halmashauri au uongozi wa eneo husika kuweni wabunifu,hiki ni chanzo cha mapato!
Wengine mazingira mazuri mpate watalii kutoka nchi zilizokuwa na viongozi walioishi Wilayani kwenu.
Ombeni kibali ofisi ya Rais mfanye safari mkatangaze kivutio hiki,na ile ndege mpya ikifika ilete watalii kutoka nchi hizo!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom