Makapuku Forum

Dereva wa Bodaboda Rogers John Kesi (17) mkoani Kilimanjaro ameuwawa na Abiria aliemkodisha kwa ajili ya kumpeleka nyumbani kwake, RPC Amon Kakwale amethibitisha.

“Ilikua ni May 10 2021 saa kumi na mbili alfajiri Polisi tulipata taarifa za kuuwawa kwake, alikodiwa kituoni Kiborloni na Mteja kumpeleka kwenda nyumbani kwake Mnazi Shani Tours, baada ya kufika Abiria ambae ni Mtuhumiwa aliingia na Rogers nyumbani ili kumuonesha mzigo wa kuubeba”

“Wakati Rogers akiwa kwenye harakati za kuuchukua mzigo huo ambao ni meza, Abiria ambae ndiye Mtuhumiwa aitwae Sifaeli maarufu Godson (21) Mmasai alimtokea kwa nyuma na kumpiga nyundo kichwani kwake na Marehemu akadondoka chini”

“Baadae Sifaeli alichukua waya na kumnyonga nao na alipohakikisha kwamba Rogers amekata roho alimpigia simu Rafiki yake wakashirikiana kuubeba mwili na kuuweka kwenye mifuko ya sandarusi, wakauweka kwenye pikipiki hiyohiyo na kwenda kutelekeza kandokando ya barabara kuu ya Moshi -Himo” ——— RPC Kakwale.
20210513_044324.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amerejea nchini akitokea Uganda ambako mapema leo amehudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Uganda Yoweri Museveni.

Rais Museveni ameapishwa leo kuiongoza Uganda kwa muhula wa sita mfululizo, hii ni baada ya kushinda uchaguzi wa Jan 14, 2021 kwa kuwashinda wagombea wengine 10 katika nafasi ya Urais (akiwemo Robet Kyaluganyi maarufu Bobi Wine) kwa ushindi wa 58%
20210513_044854.jpg
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania, Mamlaka ya Bandari Tanzania na Mamlaka ya Serikali Mtandao kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuboresha utendaji wa Bandari ya Dar es Salaam, ameyasema hayo alipotembelea bandari hiyo kujionea utendaji.

“TPA endeleeni kuiimarisha bandari yetu, hii ni sura ya uchumi wa nchi yetu, zungumzeni lugha moja ya uwajibikaji, TRA muwepo maeneo yote yanayohitaji uwepo wenu na muda wote Wateja wetu wahudumiwe ili bandari yetu iendelee kuwa bora, Nchi nyingi zinatutegemea”

“Dosari zote za mfumo wa TANCIS zifanyiwe kazi, mfumo usituharibie, mnapoona kuna madhaifu fanyeni marekebisho ya haraka, tunataka Wateja waingie na kutoka kwa muda mfupi”

Vilevile Waziri Mkuu amemuagiza Kamishna Mkuu wa TRA apeleke Watumishi katika mizani ya TANROADS iliyopo Kurasini Dar es Salam ili kurahisisha ukaguzi wa ‘seal’ pale ambapo magari yamezidisha uzito na yanahitaji kukaguliwa.
20210513_125811.jpg
20210513_125835.jpg
20210513_125921.jpg
20210513_125936.jpg
 
UNAAMBIWA Mohamed Ayoub wa Myanmar aliwabeba Wazazi wake kwenye vikapu kama hivi na kutembea nao kwa miguu siku 15 akikimbia unyanyasaji na vita huko Rakhine ambako zaidi ya Watu 9000 waliuwawa huku zaidi ya 750000 wakikimbia makazi yao, hata hivyo Baba yake alifariki baadae.
20210513_130532.jpg
 
UNAAMBIWA Singapore kuna sheria inayokataza yeyote kutembea uchi bila nguo iwe hadharani, ndani ya nyumba yake au pengine, adhabu ni $ 2000 (Tsh. 4,638,000), Mtu akifanikiwa kukupiga picha hata kama ni ndani kwako unapigwa faini au jela miezi mitatu.
20210513_130628.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom