mkalamo
JF-Expert Member
- Sep 7, 2013
- 324
- 347
Muda huu watu waliojitambulisha kuwa ni maafisa wa jeshi la Polisi kutoka makao makuu, wamezingira ofisi ndogo ya makao makuu ya Chama cha ACT-Wazalendo yaliyopo Magomeni jijini Dar es Salaam kwa minajili ya kumkamata afisa wa Chama hicho Dotto Rangimoto, anayehusika na usambazaji wa Taarifa za Chama katika mitandao ya kijamii.
Awali maafisa hao walitaka kumchukua Rangimoto bila ya kuonyesha vitambulisho vyao hali iliyozua tafrani ya maneno baina yao na watu waliotaka wajitambulishe.
Mpaka sasa maafisa hao hawajaeleza ni makosa gani wanamuhusisha nayo, huku wakihimiza kutaka kukagua ofisi nzima ya chama hicho kwa madai ya kutafuta simu inayotumiwa na Rangimoto katika mitandao ya kijamii.
Hata hivyo maafisa hao wameshindwa kuonyesha kibali cha ukaguzi na kwa sasa wamewapigia wenzao kwa ajili ya kuongeza nguvu katika eneo hilo.
UPDATES;
=====
Arodia Peter, Afisa Habari.. Dotto Rangimoto Kijana afisa msaidizi kitengo cha habari na Afisa kampeni kimataifa, Dahlia Majid, Wamechukuliwa na Polisi. Dotto anashikiliwa kwa Makosa ya Kimtandao
UPDATES 26/09/2020
Awali maafisa hao walitaka kumchukua Rangimoto bila ya kuonyesha vitambulisho vyao hali iliyozua tafrani ya maneno baina yao na watu waliotaka wajitambulishe.
Mpaka sasa maafisa hao hawajaeleza ni makosa gani wanamuhusisha nayo, huku wakihimiza kutaka kukagua ofisi nzima ya chama hicho kwa madai ya kutafuta simu inayotumiwa na Rangimoto katika mitandao ya kijamii.
Hata hivyo maafisa hao wameshindwa kuonyesha kibali cha ukaguzi na kwa sasa wamewapigia wenzao kwa ajili ya kuongeza nguvu katika eneo hilo.
UPDATES;
=====
Arodia Peter, Afisa Habari.. Dotto Rangimoto Kijana afisa msaidizi kitengo cha habari na Afisa kampeni kimataifa, Dahlia Majid, Wamechukuliwa na Polisi. Dotto anashikiliwa kwa Makosa ya Kimtandao
UPDATES 26/09/2020