Makanisa ya kiroho yana mchango gani kwenye kusaidia jamii?

madawati kila mtu anatoa. changieni basi hata kujenga vyoo mashuleni jamaniiii
 
Utakuta muumini kafunga tai hatakama viatu vime toboka na shati limekwisha.
Yukoradhi alale na njaa lakini pesa yake kidogo ya akiba ampe mchungaji akale bager na maziwa fresh. Wachungaji hawana huruma kabisa.
Usiwajumlishe wote wapo wachungaji wa makanisa mengi ya kiroho wanaishi na watu wasio na makazi kama watoto wao.
 
Utakuta muumini kafunga tai hatakama viatu vime toboka na shati limekwisha.
Yukoradhi alale na njaa lakini pesa yake kidogo ya akiba ampe mchungaji akale bager na maziwa fresh. Wachungaji hawana huruma kabisa.

Ni utumwa wa fikra, unaacha kununua viatu upendeze, unampelekea mchungaji akanunue helkopta kisa Musa aliandika mpeleke sadaka kwenye madhabahu.
 
Makanisa ya kiroho ni ya kichawi,mtu anayeingia huko tayari kaisha rogwa.Na serikali ikitaka kufanikiwa ni kuyafunga na wachungaji wake wauwawe.
 
Nimekuwa nikisali kwenye makanisa haya ya Kiroho, lakini pamoja na kupata sadaka nyingi sana toka kwa Waumini ni vigumu kusikia mipango yao kuhusu kusaidia wenye shida katika jamii bali utasikia mipango ya kumnunulia Mchungaji Helikopta, Vogue n.k. Jamani wenye shida wasaidiwe na nani? Wakuu wa Wilaya? Ama?

Mie naona msaada mkubwa ni afya ya akili. Mtoto anapozaliwa katika hali ya kawaida afya yake ya akili inakuwa nzuri. Anapokua, anapata mafundisho mbalimbali ambayo yanamtia kwenye kifungo. Kwa hiyo makanisa ya kiroho yanasaidia watu kuzaliwa mara ya pili. Yaani kuwatoa kwenye fikra ambazo zinaharibu mfumo wa akili kwenda kwenye mfumo wa fikra ambao unaimarisha afya ya akili.

Anaefikia 'Enlightenment' anakuwa ameushinda mfumo wa fikra wa kiutumwa.
 
Shida ya makanisa mengi viongozi wake wametawaliwa na tamaa ya mali mno,saa ngapi atafikiria kusaidia wengine.Ndio maana viongozi wengi wa haya makanisa wanaishi maisha kitajiri sana wakati wahumini Wapo hoe hae
Na wafaidi wajinga.
 
Yapo baadhi yanasaidia jamii kwa kuwa na mfuko maalum wa yatima na wajane kv fpct,eagt na tag pia baadhi Yao wanasomesha watoto kwa gharama nafuu kwenye shule zao kama Tag,mengine sifahamu kama yanafanya kwa ajili ya jamii
Umetaja FPCT nimekumbuka hili kanisa
Wana shule nzuri sana za Sekondari kule Igunga; Kasulu, Sumbawanga na Ruo - Lindi; hospitali kubwa Nkinga karibu na Nzega; Hospitali kubwa pale Mchukwi Rufiji; kituo cha wenye ukoma Iduguta; Radio Studio Arusha; wana Mradi wa Walemavu, Tanga; vituo vya vijana Mwanza, Lindi, Mtwara, Kigoma, Singida na Shinyanga. Wanafanya vizuri.
 
Ndugu zangu Mimi nakumbuka nilipokuwa nasoma shule ya msingi kuna majamaa walikuwa wanafanyaga mazingaombwe saana shuleni kwetu ilikuwa kila siku ya ijumaa ivo,
Nikifuatilia saivi hiyo huduma haifanyiki tena mashuleni.
Ukienda kwenye makanisa haya ya kiroho kabisa huduma hii imehamia makanisani wachungaji waongo wanafanya vitu vya ajabu watu wanatoa PESA saana kwa kushuhudia tu mazingaombwe kanisani.
Ndo hawa YESU alisema nitawakana mbele ya baba
 
mtu anayehoji matumizi ya sadaka amekufa kiroho.Ujenzi wa huduma mbalimbali ni jukumu la serikali.Hata hao rc sijui kkkt na mengine hujenga kwa ajili ya kufanya biashara.kama unabisha nenda kasome bure ama katibiwe bure.Mipango ya kusaidia yatima hufanyika kila leo kwani hujaona vituo vingi vya kulelea watoto yatima?acheni tabia yakukashifu walokole kila siku nyie.
Swala ni kwamba mbona sadaka wanazitumia wao kununulia magari na ndege?, kujitajirisha wao tu
 
Back
Top Bottom