Makamu wa Rais Dkt. Mpango: Wabunge wa upande wa pili (CHADEMA, ACT na CUF) ni vema mkajiunga CCM ili kwa pamoja tujenge nchi

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
82,750
139,535
Makamu wa Rais Dkt. Mpango amesema wabunge wa upande wa pili akimaanisha Chadema ACT wazalendo na CUF ni vema wakajiunga na CCM ili kwa pamoja tuijenge mama Tanzania.

Dkt. Mpango amewashauri wabunge hao kwamba kama kuna ugumu wa wao kuhamia CCM basi wawe hata wanajenga hoja zenye kuleta maslahi ya kimaendeleo kwa mama Tanzania na siyo vinginevyo.

Chanzo: TBC.

Maendeleo hayana vyama!
 
Nimeona Lisu leo amejipanga kuchafua nchi .

Yani Mkenya PLO Lumumba amejipanga kuitetea Tanzania lakini mzaliwa wa Singida Tundu Lisu anajipanga kuchafua...
Lissu atasema ukweli kuhusu Mwendazake wakati PLO Lumumba atapiga propaganda ambayo ilikuwa inamwingiza "chaka" Mwendazake bila yeye kujitambua kwa maslahi ya Kenya.

Bahati mbaya Mwendazake alikubali sifa zaidi kuliko ukweli. Na wafuasi wake mkawa "wazalendo wa sifa za mtu" kuliko wazalendo wa nchi kwa kukumbatia ukweli unaoweka huru watu.
 
Lissu atasema ukweli kuhusu Mwendazake wakati PLO Lumumba atapiga propaganda ambayo ilikuwa inamwingiza "chaka" Mwendazake bila yeye kujitambua kwa maslahi ya Kenya.
Bahati mbaya Mwendazake alikubali sifa zaidi kuliko ukweli. Na wafuasi wake mkawa "wazalendo wa sifa za mtu" kuliko wazalendo wa nchi kwa kukumbatia ukweli unaoweka huru watu
Lissu ni mgonjwa wa akili na kilaza mkubwa.
 
Binamu tutakapokua na vyama vingi na vikawa vyama imara kweli CCM hawataonekana kuikataa demokrasia.

Tatizo wanaojiita upinzani nao magumashi tu.
Vyama magumashi ambavyo mnaamini havina uwezo wa kuwanyang'anya madaraka hamvitaki halafu bila aibu unasema mtakubali vyama vya upinzani vyenye uwezo wa kuwanyang'anya madaraka? Sijui Watanzania mnawaonaje.

Amandla...
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom