TANZIA Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad afariki dunia

Hata Kama hatuipendi serikali lakini tusiisingizie kwa Jambo lisilo na uhakika naamini pamoja na changamoto za JPM hawezi kufanya huu upuuzi maana uwepo wa seif kwenye serikali ya umoja wa kitaifa ulikuwa unampa sifa yeye JPM na serikali yake. Kwa hili namtetea Magufuli.
Mkuu siasa kitu kibaya sana hata lisu na yeye angekubali kutibiwa Tanzania na yeye angekuwa tushamsahau walivyoona zanzibar mechi ngumu ikapelekwa taifa mechi maana marefa wao mungu awalaani wote waliohusika kwenye zoezi hili.

RIP MAALIM
 
Innalilah wainnailaihi rajiuun.
maalim hakuacha pengo ameacha mapengo,kubwa ambalo alikuwa akilipigania dhidi ya uhai wake ni kuwaweka pamoja WaZanzibari na hakuwacha kuwausia jambo hilo na kama amefanikiwa basi ameondoka Duniani akiwaachia WaZanzibar zawadi ndani ya umoja na mashikamano.

Tunaweza kusema kukubali kuingia kwake ndani ya serikali ya Umoja wa Kitaifa ni uwezo wa ALLAH kumtimizia ahadi yake aliyokuwa akiitamani muda wa uhai wake,Maalim ameondoka amewacha WaZanzibari ndani ya furaha na matumaini mapya.Amewaacha pale ambapo alitamani.
 
RIP mpambanaji..........kuna mwingine yuko njiani.....sio kwamba tunafurahi bali tuna huzuni.....misiba mitaani kila kona.......mshkaji damu wa jiwe kamfuta Maalim fasta......who netx??? Mungu pekee ajuae.....tunaomba po ee Mungu....
 
ninahisi huenda pasiwe na gari kabisa na watu wakausindikiza kwa miguu kutoka Airport mpaka Gombani kusaliwa na kutoka hapo mpaka kijijini kwake. Huu Mkusanyika utakuwa mkubwa kupita maelekezo na watu hawatakuwa na tahadhari yoyote. Na tunajua kuwa kuna watu wanabeba hivi virusi, kwenye umma huo watakuja kuumwa wengi mno ambao wengi wao watakuwa wazee na kuanza kuona idadi ya vifo ikikuwa kwa kasi ya ajabu sana. Kutokana na udogo wa visiwa hivi na watu kuwa karibu karibu bila tahadhari, haitoshangaza ikawa 80% ya wazanzibari wakajikuta wanaumwa na hii kitu.

Zanzibar ina Wizara yake ya Afya, wangefanya mazungumzo na S.A wakatupatia tu hio chanjo ilofeli kwao.
Wameshasema haifai huku kwetu ya nini tena.Hata hizo nyengine baada ya mwaka zitakuwa hazina maana tena kwani wanasema hicho kiddudu kinabadili sura kila siku.Bora tuchukue msimamo wetu huu huu na Mungu atatulinda.
 
Kwanza nashangaa nani aliyemshawishi atangaze ana corona.Na baadae raisi wa Zanzibar alipoulizwa akasema hawezi kutaja ugonjwa anaougua makamo wake.Halafu ni familia nzima kiasi kwamba ni rahisi kuelezwa wakati wa kifo chake hakukuwa na ndugu yoyote wa karibu kutokana na karantini.
Natamani nisikie maalim Seif kafufuka kabla kuzikwa leo jioni ili atupe mkanda wote wa kifo chake. Maeelezo yake baada ya kufufuka yanaweza kuwa kama hivi " Loo ! washenzi sana hawa. ...Niwaambia mimi niacheni hapa hapa nyumbani sina haja kwenda hospitali kwani sina tatizo la kupumua na hata homa ilishaacha. .Wakanibeba juu juu mpaka Mnazi mmoja na mimi na madaktari wangu tukakataa kuwekewa oksijen. Ikaendelea hivyo mpaka tarehe 9 waliponipandisha kwenye ndege usiku bila kufuatanishwa na ndugu yoyote mpaka Darisalama . Tangu siku hiyo ikawa tunavutana na kuminyana nami ili waniwekee mipira ya oksijen.Wale madaktari wa mwanzo wakaingiwa na huruma wakaondoka .Asubuhi yake wakaja wengine na hawa wa mwisho ndio wakanizidi nguvu mpaka nikazimia ..... Mumenifahamu sawa sawa ....".
Kwa hyo unataka kusema wamemuua na s ugonjwa?
 
Kama wanalitaka kumuuwa TL ujue kila aliekua mpinzani alikua yumo kwenye list ya kupotezwa ukiachia mbali hawa wakiowaweka ndani bila sababu, Mungu mnusuru Mdude na sindano za sumu kutoka kwa hawa magaidi Ccm
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom