Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,879
- 16,311
Makamu Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Shekh Ally Kadogo ametangaza kujivua Uwanachama wa chama Cha demokrasia na Maendeleo Chadema kuanzia leo Juni 15, 2025 na kujivua nafasi yeke kama aliyonayo kwenye chama hicho.
Soma, Pia: Shehe Ally Mohamed Kadogoo achaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani
Akizungumza na Waandishi wa Habari amesema kuwa, amejiondoa CHADEMA na kuacha Siasa kabisa na si kwaajili ya kujiunga na chama kingine.
"Najivua, kwa maana ya kwamba sintojihusisha na siasa ya Chama, napumzika. Sitakuwa mwanachama wa chama chochote, napumzika. Hili liwekwe wazi asije mtu akafikiria sijui natoka hapa nakwenda wapi, napumzika kwa sababu nilichogundua katika maisha ya kawaida, siasa haina shukrani. Fanya utakavyofanya, inaweza ikatokea sehemu ukatukanwa bila ya sababu na watu hawazingatii kipi ulichokifanya nyuma. Na hili tumeliona takribani miezi sita, kwamba yupo mtu aliongoza chama takribani miaka 20 lakini leo ukija kuona mtu anatweet neno la Mungu baada ya kushindwa katika uchaguzi, yale maneno yanayokuja kushindiliwa mpaka unajiuliza hawa watu wameandika maneno haya wana kisasi naye? Kawachukulia dada zao au imekuwaje? Lakini ni mashambulizi mpaka unajiuliza hili limetokeaje."
"Ninachoahidi ni kwamba sitaandika kitabu cha kuisema vibaya Chadema, sitaandika kitabu cha nyuma ya pazia, mbele ya pazia ama katikati ya uvungu. Nitakachofanya ni kutulia na kuendelea na harakati zangu. Lakini pia itoshe kusema kwamba pamoja na kuacha kwangu siasa, bado nina nafasi kama Mtanzania ya kuweza kukosoa pale mambo yatakapoenda tofauti."
Soma, Pia: Shehe Ally Mohamed Kadogoo achaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani
Akizungumza na Waandishi wa Habari amesema kuwa, amejiondoa CHADEMA na kuacha Siasa kabisa na si kwaajili ya kujiunga na chama kingine.
"Najivua, kwa maana ya kwamba sintojihusisha na siasa ya Chama, napumzika. Sitakuwa mwanachama wa chama chochote, napumzika. Hili liwekwe wazi asije mtu akafikiria sijui natoka hapa nakwenda wapi, napumzika kwa sababu nilichogundua katika maisha ya kawaida, siasa haina shukrani. Fanya utakavyofanya, inaweza ikatokea sehemu ukatukanwa bila ya sababu na watu hawazingatii kipi ulichokifanya nyuma. Na hili tumeliona takribani miezi sita, kwamba yupo mtu aliongoza chama takribani miaka 20 lakini leo ukija kuona mtu anatweet neno la Mungu baada ya kushindwa katika uchaguzi, yale maneno yanayokuja kushindiliwa mpaka unajiuliza hawa watu wameandika maneno haya wana kisasi naye? Kawachukulia dada zao au imekuwaje? Lakini ni mashambulizi mpaka unajiuliza hili limetokeaje."
"Ninachoahidi ni kwamba sitaandika kitabu cha kuisema vibaya Chadema, sitaandika kitabu cha nyuma ya pazia, mbele ya pazia ama katikati ya uvungu. Nitakachofanya ni kutulia na kuendelea na harakati zangu. Lakini pia itoshe kusema kwamba pamoja na kuacha kwangu siasa, bado nina nafasi kama Mtanzania ya kuweza kukosoa pale mambo yatakapoenda tofauti."