JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,302
- 5,439
Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Singida, Manispaa ya Singida, Thomas Ngiracha, amesimamishwa kazi kwa muda usiojulikana kwa tuhuma za kujihusisha kimapenzi na mwanafunzi wa kidato cha nne (jina tunalihifadhi) wa shule hiyo.
Mkuu wa Shule hiyo, Joseph Shani na Mkurugenzi wa Shule, Matliga Makuza walithibitisha kuchukuliwa kwa hatua hiyo dhidi ya mwalimu huyo.
Mwalimu Ngiracha (mtuhumiwa) alipoulizwa kwa njia ya simu alikiri kusimamishwa kazi kutokana na kuhusishwa na tuhuma hizo na kwamba suala hilo linashughulikiwa na vyombo vingine vya sheria.
"Ni kweli suala la kunihusisha mimi na tukio hilo zipo, lakini kimsingi sio za kweli, kwa sasa linashughulikiwa na vyombo vingine vya sheria," alisema.
Naye, Mkuu wa Shule huyo, Shani amesema mwalimu huyo ambaye pia alikuwa Mwalimu wa Nidhamu alisimamishwa kazi Mei 28, 2022 baada ya kikao cha uongozi wa shule kilichofanyika Mei 27, 2022 ambacho alimshirikisha Mkurugenzi wa Shule.
Shani alisema uongozi wa shule ulipata malalamiko kutoka kwa mwanafunzi Mei 23, 2022, kwa kuandika barua kuelezea usumbufu anaoupata kutoka kwa mwalimu huyo ambaye alimlazimisha awe na uhusiano naye na kufanya naye mapenzi mara kadhaa.
Alisema baada ya barua hiyo, uongozi wa shule ulimuita mwanafunzi na wenzake kuwahoji kuhusu suala la mwalimu huyo kuwa na mahusiano ya mapenzi na mwenzao ambao walithibitisha jambo hilo.
"Nilivyopata malalamiko kwa maandishi kutoka kwa mwanafunzi tulikaa kikao na Mkurugenzi wa Shule tukaamua kumsimamisha kazi Mei 28, 2022," alisema.
Alisema suala hilo lilifikishwa hadi kwa Ofisa Elimu wa Mkoa, Jeshi la Polisi na Dawati la Jinsia ambao wanaendelea kulifanyia kazi kwa taratibu nyingine za kisheria.
Alisema uwezekano wa mwalimu huyo kurejea shule hapo kuendelea na kazi haupo kwa sababu tayari uongozi wa shule umeshachukua hatua za kuajiri walimu wengine ambao wameziba nafasi yake.
Taarifa zaidi kutoka katika shule hiyo inadaiwa awali mwanafunzi huyo baada ya kuwa amelalamikia kitendo anachofanyiwa na mwalimu huyo na uongozi wa shule kutochukua hatua, alilazimika kwenda ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida kupeleka malalamiko yake kwa Ofisa Elimu wa Mkoa.
Kabla ya taarifa kufikishwa mkoani, mwalimu anayetuhumiwa kufanya kitendo hicho alianza kumzushia makosa mwanafunzi huyo na kumpa adhabu kadhaa, ikiwa ni mbinu ya kumdhibiti asieleze suala la mahusiano yao kwa watu wengine.
"Mwalimu alianza sana kumwandama mwanafunzi (anatajwa jina) na kwa kumpa adhabu ya kulima majani, alimpiga hadi mkono ukavimba, visa vilikuwa haviishi," kilisema chanzo kimoja cha habari.
Taarifa zaidi zimedai kuwa mwanafunzi huyo aliitwa kwa mwalimu huyo usiku na kuamua kuwachukua wenzake ili washuhudie.
"Huyo mwanafunzi baada ya kuitwa kwa sababu aliona imekuwa kero alikwenda na wenzake wawili, mmoja alisimama dirishani na mwingine mlangoni, mwanafunzi alipoingia tu ofisini mwalimu alizima taa kwa hiyo mwanafunzi aliyekuwa mlangoni akagonga mlangoni na kujifanya ana shida ndipo mwalimu akaamua kuwasha taa na hakufanya lolote," kilieleza chanzo hicho.
Taarifa zaidi zimeeleza kuwa siku moja mwalimu huyo baada ya suala hilo kujulikana kwa kuwa alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya Shule, aliamua kuitisha kikao cha kamati yeye mwenyewe mtuhumiwa, lakini baada ya kugundua suala hilo halijakaa vizuri kwa upande wake aliamua kukiahirisha ghafla wakati kilikuwa kimeshaanza.
Chanzo: IPP
Mkuu wa Shule hiyo, Joseph Shani na Mkurugenzi wa Shule, Matliga Makuza walithibitisha kuchukuliwa kwa hatua hiyo dhidi ya mwalimu huyo.
Mwalimu Ngiracha (mtuhumiwa) alipoulizwa kwa njia ya simu alikiri kusimamishwa kazi kutokana na kuhusishwa na tuhuma hizo na kwamba suala hilo linashughulikiwa na vyombo vingine vya sheria.
"Ni kweli suala la kunihusisha mimi na tukio hilo zipo, lakini kimsingi sio za kweli, kwa sasa linashughulikiwa na vyombo vingine vya sheria," alisema.
Naye, Mkuu wa Shule huyo, Shani amesema mwalimu huyo ambaye pia alikuwa Mwalimu wa Nidhamu alisimamishwa kazi Mei 28, 2022 baada ya kikao cha uongozi wa shule kilichofanyika Mei 27, 2022 ambacho alimshirikisha Mkurugenzi wa Shule.
Shani alisema uongozi wa shule ulipata malalamiko kutoka kwa mwanafunzi Mei 23, 2022, kwa kuandika barua kuelezea usumbufu anaoupata kutoka kwa mwalimu huyo ambaye alimlazimisha awe na uhusiano naye na kufanya naye mapenzi mara kadhaa.
Alisema baada ya barua hiyo, uongozi wa shule ulimuita mwanafunzi na wenzake kuwahoji kuhusu suala la mwalimu huyo kuwa na mahusiano ya mapenzi na mwenzao ambao walithibitisha jambo hilo.
"Nilivyopata malalamiko kwa maandishi kutoka kwa mwanafunzi tulikaa kikao na Mkurugenzi wa Shule tukaamua kumsimamisha kazi Mei 28, 2022," alisema.
Alisema suala hilo lilifikishwa hadi kwa Ofisa Elimu wa Mkoa, Jeshi la Polisi na Dawati la Jinsia ambao wanaendelea kulifanyia kazi kwa taratibu nyingine za kisheria.
Alisema uwezekano wa mwalimu huyo kurejea shule hapo kuendelea na kazi haupo kwa sababu tayari uongozi wa shule umeshachukua hatua za kuajiri walimu wengine ambao wameziba nafasi yake.
Taarifa zaidi kutoka katika shule hiyo inadaiwa awali mwanafunzi huyo baada ya kuwa amelalamikia kitendo anachofanyiwa na mwalimu huyo na uongozi wa shule kutochukua hatua, alilazimika kwenda ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida kupeleka malalamiko yake kwa Ofisa Elimu wa Mkoa.
Kabla ya taarifa kufikishwa mkoani, mwalimu anayetuhumiwa kufanya kitendo hicho alianza kumzushia makosa mwanafunzi huyo na kumpa adhabu kadhaa, ikiwa ni mbinu ya kumdhibiti asieleze suala la mahusiano yao kwa watu wengine.
"Mwalimu alianza sana kumwandama mwanafunzi (anatajwa jina) na kwa kumpa adhabu ya kulima majani, alimpiga hadi mkono ukavimba, visa vilikuwa haviishi," kilisema chanzo kimoja cha habari.
Taarifa zaidi zimedai kuwa mwanafunzi huyo aliitwa kwa mwalimu huyo usiku na kuamua kuwachukua wenzake ili washuhudie.
"Huyo mwanafunzi baada ya kuitwa kwa sababu aliona imekuwa kero alikwenda na wenzake wawili, mmoja alisimama dirishani na mwingine mlangoni, mwanafunzi alipoingia tu ofisini mwalimu alizima taa kwa hiyo mwanafunzi aliyekuwa mlangoni akagonga mlangoni na kujifanya ana shida ndipo mwalimu akaamua kuwasha taa na hakufanya lolote," kilieleza chanzo hicho.
Taarifa zaidi zimeeleza kuwa siku moja mwalimu huyo baada ya suala hilo kujulikana kwa kuwa alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nidhamu ya Shule, aliamua kuitisha kikao cha kamati yeye mwenyewe mtuhumiwa, lakini baada ya kugundua suala hilo halijakaa vizuri kwa upande wake aliamua kukiahirisha ghafla wakati kilikuwa kimeshaanza.
Chanzo: IPP