Makampuni yenye tenda za Usafi kwenye Taasisi kadhaa Yananyonya wafanyakazi wake

Inanambo

JF-Expert Member
Jun 26, 2011
3,985
2,770
Kuna tabia ya wizi na unyonyaji wa jasho la vijana wetu wanaopata kibarua kwenye kampuni za usafi. Kampuni hizi zilianza kutoa huduma ya usafi, Chakula na ulinzi katika taasisi mbali mbali baada ya kuondoa ajira ya Mesenja.Huajiri vijana kufanya usafi wa choo, nje na ndani ya majengo. Vijana hujituma kufanya kazi lakini huishia kulipwa 80000 hadi 100000 kwa mwezi.

Hawalipwi nauli wala chai au lunch ni kujitegemea. Huu ujira ni kidogo sana ukilinganisha na kazi vijana wanazofanya. Waajiri wao huwatumikisha tangu jumatatu saa 11:30 asubuhi -10:30 jioni hadi Jumamosi. Wakidai ujira zaidi wanafukuzwa. Ni haki kumlipa mtu elfu 3 kwa siku? Vyama vya wàfanyakazi mko wapi? Fuatilieni Unyonyaji huu.
 
Kuna tabia ya wizi na unyonyaji wa jasho la vijana wetu wanaopata kibarua kwenye kampuni za usafi. Kampuni hizi zilianza kutoa huduma ya usafi, Chakula na ulinzi katika taasisi mbali mbali baada ya kuondoa ajira ya Mesenja.Huajiri vijana kufanya usafi wa choo, nje na ndani ya majengo. Vijana hujituma kufanya kazi lakini huishia kulipwa 80000 hadi 100000 kwa mwezi. Hawalipwi nauli wala chai au lunch ni kujitegemea. Huu ujira ni kidogo sana ukilinganisha na kazi vijana wanazofanya. Waajiri wao huwatumikisha tangu jumatatu saa 11:30 asubuhi -10:30 jioni hadi Jumamosi. Wakidai ujira zaidi wanafukuzwa. Ni haki kumlipa mtu elfu 3 kwa siku? Vyama vya wàfanyakazi mko wapi? Fuatilieni Unyonyaji huu.
Ni hatari. hapa kwetu walinzi wanalipwa 130,000 kwa mwezi bila posho ya ziada. wakishakuzoea ukipita getini wanaomba buku, jero au chochote ulicho nacho. sasa huwa najiuliza hivi siku nikitoka na mali ya mwajiri huyu mlinzi atathubutu kunichukulia hatua wakati namtoa kwa buku karibu kila siku au kwa kumpa kazi ya kuosha magari ya wafanyakazi akimaliza lindo?

Hawa wa usafi nao hata kazi zao hawafanyi vizuri maana kuanzia saa 3 mpaka mchana wanafanya kazi ya kwenda kuleta vyakula kwa ujira wa 500 au 1000. mwishowe wanakuwa marafiki mpaka tunashindwa kuwaripoti.
 
Ndio maana akina dada wengi wanaofanya kazi hiyo huishia kuliwa na wafanyakazi wa taasisi ambazo kampuni zao zimepewa tenda
 
ndio maana akina dada wengi wanaofanya kazi hiyo huishia kuliwa na wafanyakazi wa taasisi ambazo kampuni zao zimepewa tenda
Kwa kweli inabidi wafanye hivyo ili kujikimu. Unaweza kuishi kwa shilingi elfu 3 kwa siku hapa Dar? Kazi nyingi ujira kidogo wenye makampuni wakinufaika. Kama mlivyochangia ofisini kwetu tunawatuma kwa ujira Wa mia 5 angalau tuchangie nauli moja. Bora kuwa House girl/boy kuliko kufanya kazi Na haya makampuni. House girl/boy utakula, kufua, kulala, chai, daladala kwa gharama ya mwajiri
 
Kuna tabia ya wizi na unyonyaji wa jasho la vijana wetu wanaopata kibarua kwenye kampuni za usafi. Kampuni hizi zilianza kutoa huduma ya usafi, Chakula na ulinzi katika taasisi mbali mbali baada ya kuondoa ajira ya Mesenja.Huajiri vijana kufanya usafi wa choo, nje na ndani ya majengo. Vijana hujituma kufanya kazi lakini huishia kulipwa 80000 hadi 100000 kwa mwezi. Hawalipwi nauli wala chai au lunch ni kujitegemea. Huu ujira ni kidogo sana ukilinganisha na kazi vijana wanazofanya. Waajiri wao huwatumikisha tangu jumatatu saa 11:30 asubuhi -10:30 jioni hadi Jumamosi. Wakidai ujira zaidi wanafukuzwa. Ni haki kumlipa mtu elfu 3 kwa siku? Vyama vya wàfanyakazi mko wapi? Fuatilieni Unyonyaji huu.
Kima cha chini ni ngapi? Total hours zao kwa wiki ni 30. Kwa kawaida masaa ya kazi bila overtime kwa wiki ni 40. Inawezekana wako ndani ya sheria. Hii ni biashara. Kama umeinvest pesa, muda, nk lazima upate return on your investment. Ukumbuke hawa wafanyakazi hawana elimu, hawana training. Ukiwa too generous, hufanikiwi katika biashara.

Naona nimekosea masaa: ni masaa 77 kwa wiki, hapo kuna breaks za chai na chakula, utapata masaa 67, ukitoa 40, masaa 9 na nusu ya jumamosi yatalipiwa Mara 2 ya mshahara kwa saa na overtime ya siku za kawaida ni Mara 1-1/2 ya mshahara kwa saa. Sijui kwa vibarua inakuwaje?
 
Kumbuka nayo ni biashara na yahitaji kupata faida, nyinyi mlipe 250,000 kwa kila mfanyakazi,
Wao watoe sabuni, walipe VAT, walipie ofisi na bado tena wataka faida kama biashara yoyote ile....
Ukitaka uone ugumu anzisha yako uwalipe hizo unazoona wanaonewa
 
Kumbuka nayo ni biashara na yahitaji kupata faida, nyinyi mlipe 250,000 kwa kila mfanyakazi,
Wao watoe sabuni, walipe VAT, walipie ofisi na bado tena wataka faida kama biashara yoyote ile....
Ukitaka uone ugumu anzisha yako uwalipe hizo unazoona wanaonewa
kwa hiyo wanafanya biashara kwa kunyonya Vijana wetu enhe na wewe unawalinda! basi ipo siku watakosa watu wa kuwanyonya kihivyo uone kama hawatafunga hizo kampuni. Sitaki wapewe mamilioni, lakini wangewafikiria hata kuwapa nauli au chai. Mtu anakufayia biashara yako kwa uaminifu toka saa 11:30 asubuhi hadi saa 10:30 jioni kwa ujira wa mkia wa mbuzi ni haki? wanafeka nyasi, wanalima, wananyesha maua, wanadeki, wanafagia, wanasafisha vioo, vyoo, masinki, wanabeba mizigo tena juani na kwenye mvua unatetea walipwe elfu 3 kwa siku? wengine wamepanga wana wake na watoto, TUCTA ione watakavyo wasaidia wahanga hawa.
 
Somesha watoto wako yasiwakute yanayokukuta wewe
Kwa hiyo waendelee kuwanyonya wanaowaingizia fedha. Wangesoma wote nani wangefanya hizo kazi? Nimeleta hapa kwa kuguswa na taabu ya hawa wafanyakazi ambazo kila kukicha wanashinda njaa huku mabosi wao wakipata Lunch Serena.
 
Nilishawahi kufanya hii kazi aiseee nilipomaliza forn six nilipata taabu kwanza hela ndogo, pili unaipata tarehe 50 yani shida tupu lakini yalikuwa mapito tu
 
Mkuu naungana na we haya makampini ni jipu ujungu aisee kiukweli wanawanyonya kama c binadamu wenzie nafananisha hii biashara kama ya utumwa utatumikishwa et kisha unaelimu ndo mtu umunyonye hiv jpm tunakuomba upangalie aisee naona hata awa chodau cjui uwa kunakitu uwa wanafanya
 
Usishangae Hao Tu Nenda MOHAMED INTERPRISES,BAKHERESA NK watu wanapgishwa kazi ngumu hatari na hawana mikataba na idara za kazi zipo tu hazifanyi chochote
 
Back
Top Bottom